ALI KIBA NA SHILOLE WAMALIZA UGOMVI WAO MBELE YA MASHABIKI

ALI KIBA NA SHILOLE WAMALIZA UGOMVI WAO MBELE YA MASHABIKI

Mastaa wa Muziki wa Bongofleva Ali Kiba na Shilole wamethibitisha kumaliza tofauti zao. Wawili hao wameonesha kumaliza tofauti zao Mkoani Kigoma nchini tanzania mbele ya Mashabiki Baada ya alikiba kumpandisha jukwaani Shilole na Kuthibitisha kuwa hawana utofauti. Kwenye video Shilole anaseema “Tunaishi kwa kusapotiana, Alikiba namkubali, ila twende tukawatoe watu utata ulisema hukunialika na Alikiba alikubali kwamba amemualika”. Kutokuelewana kwao kulianza Mwaka jana mwezi Oktoba mara baada ya Ali Kiba kumkataa Shilole kuwa hakumualika kwenye Hafla yake ya Uzinduzi wa Album ya ONLY ONE KING licha ya kuwa Shilole Aliudhuria katika hafla hiyo.

Read More
 ALI KIBA AVUNJA KIMYA CHAKE BAADA YA NDOA YAKE KUFIKA MAHAKAMANI

ALI KIBA AVUNJA KIMYA CHAKE BAADA YA NDOA YAKE KUFIKA MAHAKAMANI

Hitmaker wa ngoma ya “Utu” Msanii Ali Kiba amefunguka kwa mara ya kwanza tangu kuripotiwa kwa taarifa ya mke wake Amina Khalef kufika mahakamani kwa ajili ya kesi ya kuomba talaka. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ali Kiba ameandika ujumbe unao ashiria huzuni kufuatia ndoa yake hiyo iliyodumu kwa miaka mitatu kuelekea ukingoni, kwa kumtakia heri mtoto wake Keyaan katika kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa;  “Halizuki jambo bila Mwenyezi Mungu kutaka yote Kheri, Happy birthday Son nakupenda sana, Usinisahau” Juzi kati taarifa kutoka kwenye magazeti makubwa nchini Kenya zilidai, Mkewe Ali kiba, Amina Khalef amewasilisha kesi katika mahakama ya Kadhi mjini Mombasa kutaka kutengana mume wake. Alieleza kuwa sababu kuu ya kuvunja ndoa yake na mwanamuziki huyo, ni kuwa na msongo wa mawazo na kutelekezwa na mumewe, huku akidai kuwa Ali kiba hatekelezi majukumu kama mume. Taarifa zilidai kwa sasa Amina anataka talaka na zaidi ya Shillingi laki 2 kila mwezi kwa ajili matunzo ya watoto. Mahakama imempa Alikiba siku 15 kujibu vinginevyo mchakato wa talaka utaendelea bila yeye kuwepo.

Read More
 MKE WA ALI AKIBA AWASILISHA OMBI LA KUDAI TALAKA KUTOKA KWA MWANAMUZIKI HUYO WA BONGOFLEVA

MKE WA ALI AKIBA AWASILISHA OMBI LA KUDAI TALAKA KUTOKA KWA MWANAMUZIKI HUYO WA BONGOFLEVA

Mke wa mwanamuziki Ali Kiba, Amina Khalef amewasilisha kesi mahakamani ya kutaka kutengana na mume wake. Amina anatajwa kuwasilisha kesi hiyo ya talaka katika mahakama ya kadhi mjini Mombasa mwezi uliopita baada ya kudumu kwa miaka mitatu  kwenye ndoa huku shauri hilo la talaka likitaka Ali Kiba ampe Amina kiasi cha shillingi laki 2 za Kenya kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya watoto wao wawili. Inaelezwa kuwa miongoni mwa sababu za kuvunja ndoa ya Amina na Ali Kiba ni kuwa na msongo wa mawazo pamoja na mwanamuziki huyo kutotekeleza majukumu yake kama mume. Hata hivyo Ali Kiba amepewa siku 15 awe ametoa majibu katika mahakama ya kadhi mjini Mombasa. Wawili hao walioana mwaka wa 2018, kwa sheria za Kiislamu ambapo waliandaa sherehe kubwa iliandaliwa mji Mombasa huku sherehe hiyo akitajwa kama harusi ghali zaidi Afrika Mashariki.

Read More
 HARMONIZE AMTAKA ALI KIBA KUTUMBUIZA KATIKA SIKU YAKE YA UCHUMBA

HARMONIZE AMTAKA ALI KIBA KUTUMBUIZA KATIKA SIKU YAKE YA UCHUMBA

Mwanamuziki Maarufu nchini Tanzania, Harmonize ameonesha heshima kwa mwanamuziki mwenzake Alikiba kwa kumpongeza kwa kazi nzuri anayofanya kwenye tasnia ya Muziki wa Bongofleva. Kupitia ukurasa wake wa instagram, Harmonize alichapisha video fupi iliyokuwa ikicheza wimbo mpya wa Alikiba unaoitwa ‘Utu’ huku akiambatinisha na ujumbe kwamba siku ya kuvisha pete mpenzi wake lazima King Kiba atumbuize mashabiki wake. “Mtu amwambie mkongwe, mfalme Ali Kiba lazima aimbe kwenye usiku wa kumvisha pete mchumba wangu, huu muziki mzuri sana,” Harmonize aliandika. Utakumbuka juzi kati wanamuziki hao walionekana wakisafiri kwenye ndege pamoja jambo ambalo liliteka mazungumzo mtandaoni kwa muda

Read More
 ALI KIBA ADOKEZA UJIO WA ALBUM YAKE MPYA MWAKA WA 2022

ALI KIBA ADOKEZA UJIO WA ALBUM YAKE MPYA MWAKA WA 2022

Hitmaker wa ngoma ya Utu’ msanii Ali Kiba amegusia uwezekano wa kuachia album yake nyingine ifikapo mwakani 2022. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Msanii huyo wa Bongofleva amesema anafikiria kuachia album nyingine mwaka ujao hii ni baada ya album yake mpya Only One King aliyoiachia mwaka huu kufanya vizur kupitia digital platforms mbali mbali. “Thinking of releasing another album 2022!!!”..ameandika Ali Kiba kupitia ukurasa wake wa Twitter. Mpaka sasa Ali Kiba ameshaingiza sokoni album tatu na endapo ataachia album mpya mwaka 2022 itakuwa ni album ya nne tangu aanze safari yake ya muziki

Read More
 ONLY ONE KING ALBUM YA ALI KIBA NDANI YA TIMES SQUARE,NEW YORK.

ONLY ONE KING ALBUM YA ALI KIBA NDANI YA TIMES SQUARE,NEW YORK.

Album mpya ya msanii Ali kiba “Only One King” inazidi kuweka historia mara baada ya cover la album hiyo kuonekana katika Screen za eneo maarufu Times Square huko Jijini New York, nchini Marekani. Album hiyo ambayo ina siku tatu tangu iachiwe, ina kuwa kazi ya kwanza Kwa Ali kiba kuonekana Times Square sehemu ambayo matangazo makubwa duniani huonekana. Sanjari na hilo “Only One King” album imefanikiwa kufikisha jumla ya Streams Milioni 1 katika mtandao wa BoomPlay tangu iachiwe rasmi Oktoba 7. Album hiyo ambaye ni ya tatu kwa mtu mzima Ali Kiba ina nyimbo 16 alizoshirikisha wasanii kutoka Tanzania, Kenya na Nigeria. Miongoni mwa nyimbo zilizoko ni Utu, Let me, Niteke, Bwana mdogo, Happy, na nyingine nyingi.

Read More