Amber Ray na Rapudo Waonekana Pamoja Tena, Video Yazua Gumzo
Mastaa wa mitandaoni, Amber Ray na Kennedy Rapudo, wameendelea kuvutia macho ya mashabiki baada ya kuonekana pamoja tena wikiendi hii, licha ya uvumi uliokuwa umesambaa kwamba wameachana. Kupitia video inayosambaa mitandaoni, Rapudo anaonekana akiogelea na binti yake kwenye bwawa la kuogelea huku Amber Ray akionekana kando akifurahia tukio hilo kwa bashasha. Tukio hilo limewafanya mashabiki wengi kuhoji kama kweli wawili hao walikuwa wameachana au tetesi hizo zilikuwa ni uvumi tu. Hapo awali, taarifa zilienea kwamba kila mmoja tayari alikuwa ameingia kwenye mahusiano mapya na hata kudaiwa kuwa Amber Ray aliuza baadhi ya vifaa vya nyumba walivyokuwa wamenunua wakiwa pamoja na Rapudo. Lakini picha hii mpya ya pamoja imeonekana kupinga madai hayo, au angalau kuonesha kuwa wawili hao bado wana ukaribu wa kifamilia. Mashabiki mitandaoni wameendelea kutoa maoni mseto; wengine wakifurahishwa na kuona familia hiyo ikijumuika tena, huku wengine wakisisitiza kuwa huenda wawili hao wanadumisha urafiki kwa ajili ya binti yao. Hadi sasa, hakuna yeyote kati yao aliyetoa kauli rasmi kuthibitisha hali halisi ya mahusiano yao.
Read More