Amber Ray Afungua Ukurasa Mpya wa Maisha kwa Gari Jipya

Amber Ray Afungua Ukurasa Mpya wa Maisha kwa Gari Jipya

Mrembo maarufu mitandaoni nchini Kenya, Amber Ray, ameendelea kuthibitisha kwamba anajua kujitunza kwa jasho lake baada ya kujizawadia gari jipya la kifahari aina ya Range Rover. Kupitia ukurasa wake wa Insta Story, Amber alishiriki video na picha zikionyesha mchakato mzima wa gari hilo kusafirishwa kutoka bandarini hadi nyumbani kwake, ambapo ilipokelewa kwa shangwe na familia yake. Tukio hilo limejiri huku tetesi za kuvunjika kwa uhusiano wake na baba wa mtoto wake, Kennedy Rapudo, zikizidi kushika kasi. Hii ni baada ya Amber kuonekana mara kadhaa kwenye shughuli mbalimbali akiwa peke yake, hali iliyozua gumzo miongoni mwa mashabiki na wafuasi wake mitandaoni. Hata hivyo, Amber Ray hajazungumzia hadharani kuhusu uvumi huo, akionekana kuzingatia zaidi furaha na mafanikio yake binafsi. Gari hilo jipya limechukuliwa na wengi kama ishara ya kujipenda na kujiendeleza, licha ya changamoto za maisha ya mahusiano.

Read More
 Rapudo Amkingia Kifua Amber Ray Kufuatia Kashfa ya Obinna

Rapudo Amkingia Kifua Amber Ray Kufuatia Kashfa ya Obinna

Mfanyabiashara maarufu na mume wa sosholaiti Amber Ray,Kennedy Rapudo, amejitokeza hadharani kumtetea mkewe dhidi ya tuhuma alizoelekezewa na mwanahabari na mchekeshaji Oga Obinna. Kupitia video iliyosambazwa mitandaoni, Rapudo alieleza kutoridhishwa na jinsi Obinna alivyomkosoa Amber Ray hadharani. Rapudo alisema kuwa mke wake ni mwanamke anayejiheshimu na mchapakazi wa kweli, na kwamba hatakubali mtu yeyote kumvunjia heshima kwa misingi ya binafsi au ya kikazi. “Amber ni mke wangu na najua jinsi anavyojituma. Mtu yeyote anayemjua anajua kuwa anajiheshimu. Sitakubali mtu yeyote kumchafua hadharani,” alisema Rapudo kwa msisitizo. Kauli ya Rapudo ilikuja saa chache baada ya Oga Obinna kudai kuwa Amber Ray alifika kwenye shughuli ya kurekodi maadhui akiwa katika hali isiyofaa, akimtuhumu kuwa alikuwa amelewa kiasi na hivyo kuathiri utaratibu wa kazi. Obinna alidai kuwa hali hiyo ilisababisha ucheleweshaji na sintofahamu kazini. Amber Ray, kwa upande wake, alikanusha madai hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiyataja kama ya uongo na yenye lengo la kumharibia jina. Alisisitiza kuwa anajiheshimu na hajawahi kwenda kazini akiwa katika hali isiyo ya kitaaluma. Mvutano huu umeibua maoni tofauti miongoni mwa mashabiki wa burudani, huku baadhi wakiunga mkono msimamo wa Rapudo na Amber, na wengine wakitaka Obinna kutoa ushahidi wa madai yake au kuomba msamaha

Read More
 Amber Ray Aonekana na Rapudo Licha ya Tetezi za Kuvunjika kwa Ndoa

Amber Ray Aonekana na Rapudo Licha ya Tetezi za Kuvunjika kwa Ndoa

Sosholaiti maarufu wa Kenya, Amber Ray, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kushiriki video akiwa na mumewe Kennedy Rapudo, siku chache tu baada ya Rapudo kufuta akaunti yake ya Instagram, jambo lililoibua uvumi kwamba huenda kuna misukosuko katika ndoa yao. Katika video hiyo fupi iliyopakiwa kwenye Instagram Stories ya Amber Ray, wawili hao wanaonekana wakifurahia muda wao pamoja kwa bashasha, hali iliyotafsiriwa na wengi kama ishara kwamba huenda mambo bado ni shwari baina yao. Hapo awali, mashabiki walikuwa wameshtushwa na hatua ya Rapudo kujiondoa ghafla Instagram bila maelezo, hali iliyochochea maswali mengi mitandaoni. Hii si mara ya kwanza kwa wanandoa hao kujipata katikati ya minong’ono ya mitandaoni kuhusu uhusiano wao. Katika nyakati tofauti, wamekuwa wakiweka wazi maisha yao ya kifahari na familia, lakini pia hawajakosa migogoro ya hadharani ambayo huwavuta zaidi kwenye macho ya umma. Hadi sasa, Kennedy Rapudo hajarejesha akaunti yake ya Instagram, wala wawili hao hawajatoa tamko rasmi kuhusu kilichotokea. Hata hivyo, video hiyo imeonekana kuwatoa wasiwasi baadhi ya mashabiki waliokuwa na hofu kuhusu mustakabali wa ndoa yao. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu kuona iwapo kutakuwa na maelezo zaidi au hatua nyingine kutoka kwa wawili hao maarufu mitandaoni.

Read More
 AMBER RAY AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA MWALA

AMBER RAY AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA MWALA

Soshalaiti maarufu mtandaoni Amber Ray amekanusha vikali kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na muigizaji maarufu nchini Mwala Kupitia youtube channel yake ameeleza kuwa amechoshwa kuzushiwa taarifa za uongo mitandaoni ambapo amesema hapendi kuhusishwa na Mwala kwani hana ukaribu wowote naye. ” No, I have never had anything sexual. We are not even friends. He had come to my house and taken a photo with Gavin. I took pictures with Otile and Ali Kiba sop I don’t know why they chose to say that am dating Mwala.” Amesema. Kauli yake imekuja mara baada ya walimwengu kudai kuwa Mwala amekuwa akifadhili maisha yake ya kifahari kufuatia hatua ya muigizaji huyo kuchapisha picha mtandaoni akiwa na mtoto wa Amber Ray aitwaye Gavin.

Read More
 AMBER RAY AZINDUA RECORD LABEL YAKE NA KUMTAMBULISHA MSAINI WAKE MPYA

AMBER RAY AZINDUA RECORD LABEL YAKE NA KUMTAMBULISHA MSAINI WAKE MPYA

Mwanamintindo na mfanyibiashara, Amber Ray, amezindua  lebo ya muziki iitwayo Rich Baddness Record ambapo amemtambulisha msanii wake wa kwanza aitwaye Shifuu ambaye ameachia rasmi video ya ngoma yake iitwayo ‘Monica’ Akizungumza na waandishi wa habari, Amber Ray amesema lengo la kuanzishwa lebo hiyo ni kusaidia vijana wenye vipaji kujitangaza kupitia muziki na pia kuifanya sanaa ya muziki nchini izalishe pato la taifa. Mrembo huyo ambaye ametamba kwenye mitandao ya kijamii kwa miaka mingi amesema baada ya kumtambulisha msanii wake Shifuu ana mpango pi kutanua wigo wa lebo hiyo kwa kuwaongeza wasanii wengine wenye vipaji nchini. Hata hivyo ameomba mashabiki wa muziki nchini kumuunga mkono ili aweze kusonga mbele maana kwa sasa amekuwa na watu kadhaa ambao wamekuwa wakimtegemea katika kufanya sanaa ya muziki. Rich Baddness Record inakuwa ni lebo ya kwanza nchini Kenys kuanzishwa na kusimamiwa na mwanamitindo, ikilinganishwa na lebo kadhaa ambazo zilikuwa zikisimamiwa na wadau waliokuwa katika tasnia ya sanaa na burudani.

Read More
 SOCIALITE MAARUFU NCHINI KENYA AMBER RAY AGEUKIA MUZIKI

SOCIALITE MAARUFU NCHINI KENYA AMBER RAY AGEUKIA MUZIKI

Socialite maarufu nchini Amber Ray amegeukia kufanya muziki ikiwa ni katika kutimiza ndoto zake za kuwa mwiimbaji. Amber Ray amesema ndoto za kuimba alikuwa nazo kabla ya kuanza kuwa mwanamitindo, hivyo anafurahia kuzikikamilisha kwa sasa. Amber Ray ambaye ametamba kwenye mitandao ya kijamii kwa miaka mingi ameshirikishwa kwenye wimbo uitwao “Monica” wa msanii Shifuu. Hata hivyo ngoma hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa walimwengu kwenye mitandao ya kijamii ambao wameonekana kumkatisha tamaa asigeukia muziki kwani hana kipaji cha kuimba huku wengine wakimpongeza kwa hatua ya kuonesha upande wake mwingine kando na ucheshi. Amber Ray anajiunga kwenye orodha ya mastaa ambao hapo awali walitambulika kama washawishi wakubwa kwenye mitandao ya kijamii na baadae wakageukia kufanya muziki.

Read More