Eddy Kenzo Ataka Mazungumzo ya Amani na Azawi Kuondoa Mvutano wa Kisiasa

Eddy Kenzo Ataka Mazungumzo ya Amani na Azawi Kuondoa Mvutano wa Kisiasa

Msanii maarufu wa Uganda na Rais wa Umoja wa Wasanii (Uganda National Musicians Federation), Eddy Kenzo, ametangaza nia ya kuanzisha mazungumzo ya wazi na msanii mwenzake Azawi, ili kutatua tofauti zao za kisiasa ambazo zimeibua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wanamuziki nchini humo. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Kenzo amesema kuwa tofauti hizo hazipaswi kuendelezwa kwa njia ya mivutano ya mitandaoni bali kupitia mazungumzo ya moja kwa moja na ya wazi, akibainisha kuwa anathamini mchango wa Azawi katika tasnia na anataka suluhisho la kudumu. “Kama viongozi wa sanaa, ni jukumu letu kuonyesha mfano. Ningependa tuketi na kuzungumza hadharani ili tuweze kuelewana na kusaidia kuunganisha tasnia yetu,” alisema Kenzo. Wito huo wa Kenzo umepokelewa kwa hisia mseto mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakipongeza hatua hiyo kama ishara ya utu uzima na uongozi wa kweli, huku wengine wakimtaka aonyeshe vitendo zaidi badala ya maneno. Kwa sasa, bado haijajulikana iwapo Azawi atakubali mwaliko huo wa mazungumzo ya hadharani, lakini mashabiki wengi wana matumaini kwamba tofauti hizo zitatatuliwa kwa njia ya amani na kwa manufaa ya sekta ya muziki nchini Uganda. Taarifa hii inakuja baada ya Azawi kumkosoa hadharani mara kadhaa, akimtuhumu Kenzo kwa kushindwa kutumia nafasi yake ya uongozi kutetea masilahi ya wasanii na raia wa Uganda kwa ujumla. Azawi amekuwa akieleza kuwa Kenzo amekuwa kimya katika masuala muhimu yanayohitaji sauti ya msanii mwenye ushawishi kama yeye.

Read More
 Azawi Afichua Kuwekeza Milioni 24 Kurekebisha Meno

Azawi Afichua Kuwekeza Milioni 24 Kurekebisha Meno

Mwanamuziki wa Uganda, Azawi , amefunguka kuhusu uwekezaji mkubwa alioufanya kuboresha tabasamu lake, baada ya kupata mafanikio makubwa chini ya lebo ya Swangz Avenue. Akizungumza katika mahojiano na mtangazaji wa YouTube, Kasuku, Azawi alieleza kuwa alitumia kiasi cha shilingi milioni 24 za Uganda (UGX) kurekebisha tatizo la meno lililosababishwa na ajali aliyopata alipokuwa katika umri mdogo. Msanii huyo alisema alianguka na kuvunjika taya, hali iliyosababisha mapengo yaliyoathiri muonekano wake kwa muda mrefu.  “Sikuwa na uwezo wa kuyarekebisha zamani, lakini baada ya kupata mafanikio kupitia muziki wangu chini ya Swangz Avenue, niliamua kuweka hilo suala sawa. Ilikuwa ni hatua ya binafsi na ya muhimu kwangu,” alisema Azawi. Katika mahojiano hayo, Azawi pia aligusia maisha yake ya kimapenzi, akifichua kuwa awali alikuwa katika mahusiano ya muda mfupi, lakini sasa yuko tayari kutulia. Kwa utani, alieleza kuwa hupendelea wanaume warefu na wanene, akisema haavutiiwi na wanaume wenye misuli (six-packs). Azawi anaendelea kung’ara katika tasnia ya muziki Afrika Mashariki, na sasa si tu kwa sauti yake ya kipekee, bali pia kwa tabasamu linaloendana na jina lake kubwa. Swangz Avenue ilimsaini Azawi mwaka 2019 na kumtambulisha rasmi kwa umma tarehe 31 Oktoba mwaka huo. Tangu wakati huo, amejizolea umaarufu kwa nyimbo kama ‘Lo Fit’, ‘Masavu’, ‘Party Mood’, ‘Majje’, ‘Quinamino’, na ‘Ku Sure’.

Read More
 Azawi Kutumia Muziki Kupaza Sauti za Waganda Walionyimwa Haki

Azawi Kutumia Muziki Kupaza Sauti za Waganda Walionyimwa Haki

Mwanamuziki wa Uganda, Priscilla Zawedde maarufu kama Azawi, ameweka wazi dhamira yake ya kutumia muziki kama chombo cha kupaza sauti dhidi ya dhuluma na ukosefu wa haki nchini mwake. Hii ni baada ya takriban miaka miwili ya kuikosoa serikali hadharani kupitia majukwaa mbalimbali. Katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini Uganda, Azawi alieleza kuwa yupo mbioni kuingia studio kurekodi nyimbo za mapinduzi zenye ujumbe mzito unaoelezea machungu na hali halisi ya wananchi wa kawaida. “Nataka kuonesha maumivu ya Waganda wengi kupitia muziki wangu,” alisema Azawi. “Nafanya kazi juu ya hilo, na label yangu Swangz Avenue wanaheshimu maoni na mtazamo wangu.” Akiwa chini ya usimamizi wa lebo ya Swangz Avenue, Hitmaker huyo wa ngoma ya “Talking Stage” alisisitiza kuwa hana hofu ya kupoteza nafasi yake kwenye lebo hiyo, endapo msimamo wake wa kisanii hautaungwa mkono. “Ikiwa hawatataka kufanya kazi nami kwa sababu ya nyimbo hizo, ni sawa tu. Nitajiondoa,” alisema kwa msimamo thabiti. Azawi anaelekea kufungua ukurasa mpya wa muziki wenye uzito wa kijamii na kisiasa, hatua ambayo huenda ikamuweka kwenye mgongano na serikali au hata wasimamizi wake wa kazi za usanii lakini pia inaweza kumweka katika nafasi ya kipekee kama msanii anayesimama kwa ajili ya watu wake. Hata hivyo mashabiki wake wameonyesha msisimko mkubwa mtandaoni, wakimpongeza kwa ujasiri na nia ya kutumia muziki kama silaha ya kupigania haki na kuunganisha jamii.

Read More
 VINKA AKANUSHA KUWA KWENYE BIFU NA AZAWI

VINKA AKANUSHA KUWA KWENYE BIFU NA AZAWI

Msanii wa Swangz Avenue Vinka amekanusha madai ya kuwa kwenye ugomvi na msanii mwenzake Azawi. Katika mahojiano yake hivi karibuni vinka amesema madai hayo hayana msingi wowote kwa kuwa yanachochewa na baadhi ya watu wasiokuwa shughuli ya kufanya maishani. Hitmaker huyo wa ngoma ya “One Bite” amesema kuwa kama kweli angekuwa na ugomvi na azawi angemuunga mkono kwenye harakati zake za kutangaza onesho lake litakalofanyika hivi karibuni. Hata hivyo amesema yeye na Azawi ni marafiki wakubwa hivyo wameelekeza nguvu zao zote kwenye suala la kuupeleka muziki wa uganda kimataifa. Kauli ya Vinka imekuja mara baada ya uvumi kusambaa mtandaoni kuwa ana bifu na Azawi licha ya kwamba wote wamesainiwa kwenye lebo moja ya muziki.

Read More
 SPICE DIANA AKANUSHA BIFU LAKE NA MSANII MWENZAKE AZAWI

SPICE DIANA AKANUSHA BIFU LAKE NA MSANII MWENZAKE AZAWI

Nyota wa muziki kutoka nchini Uganda Spice Diana kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu suala la kuwa kwenye ugomvi na msanii mwenzake Azawi ambaye juzi kati ameshinda tuzo ya Janzi awards mwaka wa 2021. Hitmaker huyo wa “Upendo” amesema hana ugomvi na Azawi ambaye alishinda tuzo ya msanii bora wa kike kwenye tuzo za  Janzi Awards ila alikuwa anawakosoa waandaji wa tuzo hizo ambao walikuwa wanawatumia vibaya wasanii kwa maslahi yao binafsi. Spice Diana amesema ana furahia ushindi wa Azawi kwenye tuzo hizo kwani ni moja kati ya wadada ambao wameonyesha uwezo wa kipekee kwenye kazi zake za muziki. Ikumbukwe Spice Diana hakushinda tuzo hata moja kwenye tuzo za Janzi Awards licha ya kuwa na muendelezo mzuri wa kuachia kazi zake za muziki, jambo lilotafsiriwab na wajuzi wa mambo kuwa mrembo huyo ana machungu ya kutoshinda tuzo

Read More
 ALBUM YA AZAWI “AFRICAN MUSIC” YACHAPISHWA KWENYE BANGO LA NEW YORK TIMES

ALBUM YA AZAWI “AFRICAN MUSIC” YACHAPISHWA KWENYE BANGO LA NEW YORK TIMES

Nyota  wa muziki nchini Uganda Azawi anazidi kuchana mbuga kimataifa hii baada ya cover ya album yake mpya iitwayo “African Music” kutumika kama art work ya chati  ya new york times  billboard ya nchini Marekani. Kupitia ukurasa wake wa instagram Azawi amewatarifu mashabiki zake  taarifa hiyo njema kwa kushare picha ikionyesha picha yake ambayo ilikuwa imechapisha kwenye chati ya new york times square billboard huku akiwashukuru mashabiki zake ambao wamemshika mkono hadi akafikia mafanikio hayo. Hata hivyo Azawi anakuwa msaani wa pili  kutoka Uganda album yake kutumika kama cover kwenye chati hiyo kubwa ya muziki nchini marekani baada ya Eddy Kenzo. Mafanikio hayo yanakuja siku chache baada ya Azawi kutajwa kwamba atakuwa miongoni mwa wasanii nne wataowakilisha afrika kwenye mpango wa YouTube Black Voice Music  mwaka wa 2022 unaolenga kuhamasisha wasanii, waandishi wa nyimbo,na maprodyuza kote duniani kuhusu namna ya kuboresha kazi zao za sanaa. Ikumbukwe new york times square billboard wamekuwa na utaratibu wa kutumia picha za mastaa wa muziki ambao ngoma zao zinaongoza kwa mauzo kwenye mitandao mbali mbali ya kusikiliza muziki duniani.

Read More
 AZAWI AACHIA RASMI AFRICAN MUSIC ALBUM

AZAWI AACHIA RASMI AFRICAN MUSIC ALBUM

Mkali wa muziki kutoka nchini uganda Azawi ameachia rasmi album yake mpya inayokwenda kwa jina la African music.   African Music album imebeba jumla ya mikwaju 16 ya moto huku ikiwa na kolabo nne.   Azawi amewashirikisha wasani kutoka uganda ambao ni Eddy kenzo, A Pass, Fik Fameica na bosi wa lebo ya muziki ya swangz avenue Benon Mugumbya.   Album ya “African Music” ni album ya kwanza kutoka kwa Azawi baada ya kutubariki na EP yake iitwayo Lo-Fit iliyotoka mwaka wa 2020.   Hata hivyo Album hiyo inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya  kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile Apple music, Boomplay, na Spotify      

Read More