BENSOUL NA TIFFANY MUIKAMBA WAPATA MTOTO WAO WA KWANZA

BENSOUL NA TIFFANY MUIKAMBA WAPATA MTOTO WAO WA KWANZA

Mrembo Tiffany Muikamba amethibitisha kuwa amejifungua mtoto wa kike. Muikamba ambaye aliwahi kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii wa Sol Generation Bensoul ameeleza furaha yake kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kujifungua salama. Ni hatua ambayo imepokelewa kwa furaha na mastaa wa muziki nchini pamoja na mashabiki ambao wamemtakia mrembo huyo pamoja na Bensoul salamu la pongezi kwa hatua hiyo kubwa maishani. Utakumbuka taarifa za Tiffany Muikamba kuwa na uja uzito wa Bensoul zilibuka mwaka jana baada ya mrembo huyo kuanika wazi namna ambavyo walikutana na msanii huyo huko Mombasa, kitendo ambacho karibu ivunje uhusiano wa Bensoul na mpenzi wake wa siku nyingi Noni Gathoni.

Read More
 BENSOUL ATANGAZA UJIO WA ALBUM YAKE MPYA

BENSOUL ATANGAZA UJIO WA ALBUM YAKE MPYA

Msanii wa Sol Generation Bensoul ametangaza ujio wa album yake mpya tangu aanze safari yake ya muziki. Katika mahojiano yake hivi karibuni Bensoul amewataka mashabiki zake kukaa mkao wa kula kuipokea album yake mpya ambayo kwa mujibu wake itaingia sokoni mwakani. Mbali na hayo hitmaker huyo wa ngoma ya “Medicine” amedokeza mpango kufunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi Noni Gathoni licha ya kutokuwa na maelewano mazuri kipindi cha nyuma baada ya taarifa kuibuka kuwa Bensoul amempa uja uzito mwanamke mwingine.

Read More
 MWANAMKE ALIYEPEWA UJA UZITO NA MSANII WA SOL GENERATION BENSOUL AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA

MWANAMKE ALIYEPEWA UJA UZITO NA MSANII WA SOL GENERATION BENSOUL AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA

Mwanamke aliyebebeshwa uja uzito na msanii wa sol Bensoul amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya Bensoul kukiri hadharani kuwa alimsaliti mpenzi wake Noni Gathoni kwa kumpa uja uzito mrembo huyo kutoka Mombasa. Kwenye kikao cha maswali na majibu na mashabiki kwenye mtandao wa instagram mwanamke huyo anayefahamika kwa jina la Tiffany amesema hakuwa na nia ya kuvunja uhusiano wa bensoul na mchumba wake kipindi alihamua kutoka  kimapenzi na msanii huyo ila ni jambo ambalo lilitokea bahati mbaya. Mrembo huyo amekanusha taarifa zinazotembea kwenye mitandao ya kijamii kuwa anatumia jina la Bensoul kujitafuta kiki kwa kusema kuwa hana haja na umaarufu ikizingatiwa kuwa ni kweli ana uja uzito wa Bensoul. Hata hivyo amempongeza Bensoul kwa kujitokeza hadharani na kukubali kuwa ana uja uzito wake kwani ni wanaume wachache ndio wana uwezo wa kufanya hivyo. Kauli ya mrembo huyo imekuja mara baaada ya bensoul na mchumba wake noni Gathoni kuonekana wakionyeshana mahaba mazito kwenye mtandao wa instagram licha ya kuwa bensoul aliripotiwa kumsaliti mpenzi wake huyo kwa kumpa mwanamke mwingine uja uzito kwenye moja ya performance yake mwaka wa 2021 huko Mombasa.

Read More
 BENSOUL AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA KUKIRI HADHARANI KUMSALITI MCHUMBA WAKE NONI GATHONI

BENSOUL AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA KUKIRI HADHARANI KUMSALITI MCHUMBA WAKE NONI GATHONI

Msanii wa Sol Generation Bensoul amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ishu ya kumsaliti mpenzi wake Noni Gathoni baada ya kudaiwa kuwa alimpachika uja uzito mwanamke mmoja kaunti ya Mombasa. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Nairobi” amekiri hadharani kuwa ni kweli kuna mwanamke ana uja uzito wake kaunti hiyo huku akisema kuwa ni makosa ambayo alifanya na mrembo mmoja aliyekutana nae kwenye performance yake huko Mombasa. Bensoul ameenda mbali na kusema kwamba alikuwa na mpango kuweka wazi habari hiyo kwa umma ila mwanablogu mwenye utata nchini Edgar Obare alimpiku na kuchapisha taarifa hiyo kabla hajafanya hivyo. Hata hivyo ameahidi kujitolea  kusimamia suala nzima la kutoa matunzo kwa baby mama wake huyo hadi pale atakapojifungua. Suala hilo limeibua hisia mseto miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii wengi wakihoji kuwa hawaamini kama Bensoul anaweza jihusisha na  udanganyifu kwenye mahusiano yake ikizingatiwa kuwa hajawahi patikana na skendo yeyote tangu aanze safari yake ya muziki.

Read More