Breeder LW Aandika Wimbo wa Milioni 6 YouTube Akiwa Bypass!

Breeder LW Aandika Wimbo wa Milioni 6 YouTube Akiwa Bypass!

Rapper maarufu wa Kenya, Breeder LW, amewashangaza mashabiki wake baada ya kufichua kuwa aliandika na kurekodi wimbo wake maarufu “Dedi Dedilee” kwa dakika 10 tu,  akiwa kwenye Barabara ya Southern Bypass, Nairobi. Kupitia Insta Story yake, Breeder alisema kwamba aliuchana au freestyle wimbo huo mzima papo hapo, bila maandalizi maalum. Kulingana naye, hii ilikuwa moja ya nyimbo zilizokuja kwa haraka sana lakini zenye athari kubwa maishani mwake.  “Wrote this song in 10 minutes, I literally freestyled everything tukiwa Southern Bypass. One year later, this song changed our lives!!” Tangu kuzinduliwa kwake zaidi ya mwaka mmoja uliopita, “Dedi Dedilee” umevuma kwa kasi na kufikia mafanikio makubwa. Video rasmi ya wimbo huo kwenye YouTube imeshatazamwa zaidi ya 6.3 milioni hadi sasa, ikidhihirisha ukubwa wa ushawishi wa Breeder katika muziki wa kisasa wa Kenya. Wimbo huu umeibuka kuwa anthem ya mitaa, ukichochea mijadala, trends, na changamoto mbalimbali mitandaoni. Mtindo wake wa trap na drill, pamoja na chorus rahisi na ya kukumbukwa, umemfanya Breeder LW kujipatia umaarufu mkubwa. Mashabiki wengi wameelezea kuvutiwa na uwezo wa Breeder kuunda wimbo wa kiwango cha juu kwa muda mfupi, wakimpongeza kwa ubunifu wake wa asili. Kwa sasa, Breeder LW anaonekana kuendelea kung’ara katika game ya muziki huku akiahidi kuachilia kazi mpya hivi karibuni.

Read More
 Maandy azima tetesi za kutoka kimapenzi na Breeder LW

Maandy azima tetesi za kutoka kimapenzi na Breeder LW

Rapa Maandy kwa mara nyingine amekanusha madai yote kwamba yeye na msanii Breeder LW ni wapenzi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram akiwajibu mashabiki zake waliokuwa wakidhani kwamba wanachumbiana, Maandy amethibitisha kwamba madai hayo hayana ukweli wowote. Hitmaker huyo wa ‘Ni Wetu’ ameeleza kwa kina kwamba mwanamke aliyepiga picha na Breeder LW wakiwa kwenye mahaba mazito, siku moja baada ya kumbukizi ya kuzaliwa kwake sio yeye. Maandy amedai kwamba alipata taarifa ya kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na rapa huyo kupitia simu za marafiki zake, huku akiwataka mashabiki kuacha tabia ya kumhusisha kimapenzi na Breeder LW ikizingatiwa kuwa hakuna kitu kinaendelea kati yao.

Read More
 Rapa Breeder LW atangaza rasmi tarehe ya kuachia Vibes & Ting EP

Rapa Breeder LW atangaza rasmi tarehe ya kuachia Vibes & Ting EP

Rapa Breeder Lw anaendelea kutupasha kuhusu EP yake mpya ijayo aliyoipa jina la Vibes & Ting. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha kuwa EP hiyo itaingia rasmi sokoni Disemba 2 mwaka 2022 ambapo amewataka mashabiki kukaa mkao wa kula kupokea kazi hiyo ambayo ameitaja kuwa ni ya kitofauti. Vibes & Tings EP ina jumla ya. Nyimbo 8 za moto ambazo amezifanya mwenyewe bila kumshirikisha msanii yeyote. Kwa sasa mashabiki wanaweza kui-pre-order EP hiyo kupitia digital platforms mbali mbali za kupakua na kusikiliza muziki duniani ikiwemo Apple Music.

Read More
 Breeder LW atangaza ujio wa Extended Playlist yake mpya

Breeder LW atangaza ujio wa Extended Playlist yake mpya

Rapa kutoka nchini Kenya Breeder LW ametangaza kuja na Extended Playlist ‘EP’ yake mpya ambayo ameipa jina la ‘Vibes & Ting. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii Breeder amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula kuipokea EP yake hiyo ambayo kwa mujibu wake itaingia sokoni hivi karibuni. Hitmaker huyo wa “Gin ama Whiskey” amebainisha kuwa kwa sasa unaweza ukai Pre-Order “‘Vibes & Ting ” kupitia digital platforms mbalimbali ikiwemo Apple Music. ‘Vibes & Ting EP ina jumla ya nyimbo 8 za moto ambazo amezifanya mwenyewe bila kumshirikisha msanii yeyote.

Read More
 BREEDER LW ADOKEZA UJIO WA KOLABO YAKE NA KUNDI LA UNCOJINGJONG

BREEDER LW ADOKEZA UJIO WA KOLABO YAKE NA KUNDI LA UNCOJINGJONG

Baada ya kufanya vizuri na singo yake “Gin ama Whiskey” akiwa ameshirikiana na staa wa muziki nchini Mejja, Rapa Breeder LW amedokeza ujio wa kolabo nyingine akiwa na kundi la muziki linalokuja kwa kasi kwa sasa Uncojingjong. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Breeder LW amepost picha ya pamoja akiwa na wasanii wa kundi hilo ambapo amewataarifu mashabiki zake wakae mkao wa kula kupokea remix ya wimbo uitwao “Wanjapi” kutoka kwa Unco jing jong. “Piga Luku Kula Wanjapi@uncojingjong @litttlemaina_#BigBaba #bazengamentality #wanjapi”,Ameandika Breeder LW Kukazia hilo kundi la Unco jing jong limethibitisha kufanyika kwa Remix ya wimbo huo kupitia mitandao ya kijamii huku wakiambatanisha na video wakiwa studio na Breeder LW wakiimba sehemu ya wimbo wa ‘Wanjapi” “WANJAPI 2 LOADING Different artists different tastes…Tushaa skia wa East (@rapdokta & @is_bullet )…Acha tuskie wa West #wanjapi #ajingjongneverdie”..Uncojinjong wameandika kupitia Instagram. Kwa mujibu wa taarifa yao, Remix ya ‘Wanjapi’ itaingia rasmi sokoni wiki hii. Mpaka sasa wimbo wa ‘Wanjapi” kutoka kwa Unco jing jong unazidi kufanya vizuri kwenye majukwaa mbali mbali ya kupakua na kusikiliza mtandaoni kwani ndani ya miezi tisa imefanikiwa kufikisha zaidi ya views laki 2 youtube.

Read More
 BREEDER LW MBIONI KUACHIA COLLABO YAKE NA EXRAY TANIUA

BREEDER LW MBIONI KUACHIA COLLABO YAKE NA EXRAY TANIUA

Habari nzuri kwa mashabiki wa muziki nchini ni kwamba tutarajie muda wowote ujio wa Collabo kati ya Exray na Rapper Breeder LW. Breeder LW amethibitisha taarifa hiyo kwa mashabiki kupitia mahojiano yake ya hivi karibuni ambapo amewataka mashabiki kukaa mkao wa kula kupokea wimbo huo. Iwapo Breeder Lw na Exray wataachia collabo yao hiyo itakuwa ni kazi yao ya kwanza kufanya pamoja ikizingatiwa kuwa kipindi cha nyuma wamekuwa wakikutana kwenye kazi za wasanii wengine. Ikumbukwe Breeder Lw anafanya vizuri na singo yake mpya “Gin ama Whisky ambayo amemshirikisha Mejja na mpaka sasa video yake ina views million 1.2 kwenye mtandao wa youtube ndani kipindi cha wiki tatu.

Read More
 BREEDER LW AKIRI HADHARANI KUMZIMIA KIMAPENZI AZZIAD PAMOJA NA CARTOON COMEDIAN

BREEDER LW AKIRI HADHARANI KUMZIMIA KIMAPENZI AZZIAD PAMOJA NA CARTOON COMEDIAN

Rapa Breeder LW ameshindwa kuzuia hisia zake za mahaba kwa malkia wa tiktok Azziad pamoja na mchekeshaji Cartoon Comedian kwa kueleza wazi kuwa anawapenda sana. Breeder amefafanua kuwa ameamua kuwa mkweli na muwazi kwani warembo hao wana sifa zote anazozitafuta kwa mwanamke wa ndoto yake ambapo ameenda mbali zaidi na kusema kwamba yuko tayari kumuoa  mmoja kati yao endapo akikubali ombi lake. Rapa huyo ameweka wazi hayo alipokuwa akimjibu shabiki yake ambaye alitaka kujua ni warembo wagani hapa Kenya anatamani kuwa nao kwenye mahusiano ya kimapenzi katika kikao cha maswali na majibu kupitia mtandao wa Instagram.

Read More
 RAPPER BREEDER LW ATANGAZA UJIO WA KOLABO YAKE NA MEJJA

RAPPER BREEDER LW ATANGAZA UJIO WA KOLABO YAKE NA MEJJA

Habari nzuri kwa mashabiki wa muziki nchini ni kwamba tutarajie muda wowote ujio wa Collabo kati ya mejja na Rapper Breeder LW. Breeder LW amethibitisha taarifa hiyo kwa mashabiki kupitia insta story kwenye mtandao wa Instagram ambapo ameshare clip fupi ikimuonyesha akiwa location na mejja wakishoot video ya wimbo wao mpya ambayo kwa mujibu wake ni moto wa kuotea mbali. Hata hivyo mashabiki maonekana kuikubali ngoma hiyo ambapo wamemtaka rapa Breeder lw kuaharakisha mchakato wa kuachia audio pamoja na Video. Iwapo Breeder Lw na Mejja wataachia collabo yao hiyo itakuwa ni kazi yao ya kwanza kufanya kama wasanii wawili ikizingatiwa kuwa kipindi cha nyuma wamekuwa wakikutana kwenye kazi za wasanii wengine.

Read More
 BREEDER APOKEZWA TUZO YA SILVER PLAY BUTTON NA MTANDAO WA YOUTUBE

BREEDER APOKEZWA TUZO YA SILVER PLAY BUTTON NA MTANDAO WA YOUTUBE

Rapa kutoka nchini Kenya Breeder LW ametunukiwa tuzo ya silver play  button na mtandao wa youtube baada ya rapa huyo kufikisha jumla ya subscribers laki moja kwenye mtandao huo. Breeder LW ametumia ukurasa wake wa instagram kuwashukuru mashabiki zake kwa kumpa support kwenye muziki wake ambao unazidi kuonyesha mafanikio makubwa huku akiahidi kuendelea kuwapa muziki mzuri kwani tayari baadhi ya projects zimekamilika. Channel ya youtube ya Breeder LW ilifunguliwa rasmi Januari 14 mwaka wa 201y na mpaka sasa imefikisha zaidi ya watazamaji millioni 9.7 huku ikiwa na jumla ya subscribers 122, 000. Itakumbukwa tuzo ya silver play button huwa inatolewa kwa wanamuziki au watu maarufu kwenye mtandao wa youtube ambao hujizolea zaidi ya subcribers laki moja.    

Read More
 ALBUM YA RAPA BREEDER LW “BAZENGA MENTALITY” YAWEKA REKODI BOOMPLAY KENYA

ALBUM YA RAPA BREEDER LW “BAZENGA MENTALITY” YAWEKA REKODI BOOMPLAY KENYA

Album ya Rapa breeder Lw, Bazenga Mentality inaendelea kufanya makubwa kwenye mitandao ya kuuza na kusikiliza muziki duniani. Mpaka sasa imefikisha jumla ya streams MILIONI 1 kwenye mtandao wa kupakua na kusikiliza muziki wa Boomplay. Album hiyo  ya ” Bazenga Mentality ” iliachiwa rasmi Juni 30 mwaka wa 2021, ikiwa na jumla ya mizinga 15  za moto. Ikumbukwe Album ya “Bazenga Mentality” ni album ya pili kutoka kwa mtu mzima Breeder lw baada ya kabla kuosa iliyotoka mwaka wa 2008.

Read More