Wakili wa Cardi B Ajibu Kesi ya Kipaza Sauti

Wakili wa Cardi B Ajibu Kesi ya Kipaza Sauti

Wakili wa rapa kutoka Marekani Cardi B, Drew Findling, ameibuka na kuikosoa vikali kesi mpya ya madai iliyofunguliwa dhidi ya mteja wake, akisema ni jaribio la kutaka kumpora pesa kwa kutumia jina lake maarufu. Kauli ya Findling imekuja kufuatia mwanamke mmoja, anayetambulika kama Jane Doe, kufungua kesi ya madai dhidi ya Cardi B kwa tuhuma za shambulio la mwili, uzembe na dhuluma ya kihisia, akidai kuwa alijeruhiwa baada ya kurushiwa kipaza sauti na rapa huyo wakati wa tamasha la Drai’s Beachclub huko Las Vegas mnamo Agosti 2023. Kwa mujibu wa maelezo ya Jane Doe, Cardi B alikuwa akitumbuiza katika hafla ya mchana iliyokuwa ikifanyika wakati wa joto kali, ambapo aliwaomba mashabiki wamwagie maji ili kupooza. Mwanamke huyo anasema alifanya hivyo kwa nia njema, lakini alichokutana nacho ni kurushiwa kipaza sauti kwa nguvu na Cardi B, kitendo ambacho sasa anadai kilimsababishia madhara ya kimwili na kiakili. Ingawa tukio hilo lilichukua sura kubwa mitandaoni wakati huo, uchunguzi wa polisi haukupelekea kufunguliwa kwa mashtaka yoyote ya jinai dhidi ya Cardi B. Polisi waliamua kufunga jalada hilo baada ya kukosa ushahidi wa kutosha, na kesi hiyo haikuwahi kufika kwa Mwendesha Mashtaka wa Kaunti. Hata hivyo, Jane Doe sasa ameamua kufungua kesi ya madai miaka miwili baadaye, akidai kuwa hata mnada wa kipaza sauti hicho kwa ajili ya shughuli za hisani ulimvuruga kisaikolojia na kumrudisha katika hali ya huzuni aliyoipitia baada ya tukio hilo. Mashabiki wa Cardi B wamejitokeza mitandaoni wakimtetea msanii huyo, wengi wakisema mwanamke huyo alitafuta kiki na sasa anajaribu kutumia tukio la zamani kujinufaisha kifedha. Hadi sasa, Cardi B hajatoa tamko la moja kwa moja kuhusu kesi hiyo mpya, lakini timu yake ya kisheria imeweka wazi kuwa wataipinga vikali hadi mwisho.

Read More
 Cardi B Kizimbani: Ashtakiwa kwa Kumrushia Shabiki Kipaza Sauti

Cardi B Kizimbani: Ashtakiwa kwa Kumrushia Shabiki Kipaza Sauti

Staa wa muziki wa Hip Hop Cardi B anakabiliwa na kesi ya kisheria kufuatia tukio la mwaka 2023 ambapo alinaswa kwenye video akimrushia shabiki wake kipaza sauti wakati wa onyesho moja jijini Las Vegas, Marekani. Kwa mujibu wa hati za mahakama zilizowasilishwa hivi karibuni, shabiki huyo ambaye jina lake halijawekwa wazi, anadai kuwa aliumia baada ya Cardi B kurusha kipaza sauti kwa hasira, kitendo kinachodaiwa kuwa ni shambulio, unyanyasaji wa mwili na uzembe. Tukio hilo lilitokea wakati wa onyesho la Cardi B mwezi Julai 2023, ambapo inasemekana msanii huyo alikasirishwa na kitendo cha shabiki kumrusha kinywaji akiwa jukwaani. Katika kile kinachoelezwa kuwa ni kisasi, Cardi alionekana akirusha kipaza sauti kwa nguvu kuelekea kwenye kundi la mashabiki. Ingawa hakukuwa na mashtaka ya jinai yaliyowasilishwa wakati huo, kesi hii mpya inaweza kumgharimu Cardi B fedha nyingi na kuathiri jina lake kwenye muziki. Wakili wa mlalamikaji anasema mteja wake alipata majeraha ya mwilini na pia mshtuko kutokana na tukio hilo.

Read More
 Video Mpya Yazima Uvumi: Cardi B na Stefon Diggs Wapo Bado Kwenye Mahaba

Video Mpya Yazima Uvumi: Cardi B na Stefon Diggs Wapo Bado Kwenye Mahaba

Tetesi kuwa uhusiano kati ya rapa maarufu Cardi B na mcheza mpira wa Marekani Stefon Diggs umeenea mitandaoni, lakini taarifa mpya zinaonyesha kuwa penzi lao bado lipo imara. Uvumi wa kuachana kwao ulianza baada ya mashabiki kubaini kuwa Cardi B alikuwa amefuta picha zote za Stefon Diggs kwenye akaunti yake ya Instagram, jambo lililoibua maswali mengi kuhusu mustakabali wa uhusiano wao. Hata hivyo, Cardi B alionekana kupuuzilia mbali uvumi huo kwa kuchapisha video kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), akionekana akiwa gym na Diggs wakifanya mazoezi pamoja. Video hiyo imechukuliwa kama jibu kwa waliodhani kuwa wawili hao tayari wameachana. Chanzo cha karibu na wawili hao kimeripotiwa kuiambia TMZ kwamba wapenzi hao bado wako kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanaendelea vyema, tofauti na taarifa zinazozunguka mtandaoni.

Read More
 Cardi B Aibua Sintofahamu Baada ya Kufuta Picha za Stefon Diggs

Cardi B Aibua Sintofahamu Baada ya Kufuta Picha za Stefon Diggs

Mashabiki wa rapa maarufu Cardi B wameibua hisia mseto mitandaoni baada ya kugundua kuwa msanii huyo amefuta picha zote za mpenzi wake mpya, Stefon Diggs, kutoka kwenye ukurasa wake wa Instagram. Hatua hiyo imezua tetesi kuwa huenda uhusiano wao umeingia matatizoni au hata kuvunjika kabisa. Wengi wa mashabiki walieleza mshangao na masikitiko, wakikumbuka jinsi penzi la Cardi na Stefon lilivyokuwa linaonekana kuwa la kipekee, lenye mapenzi ya dhati na hadhi ya juu. Wengine walitafsiri hatua hiyo kama njia ya Cardi kujilinda dhidi ya maisha ya umma, huku baadhi wakiamini ni dalili ya mgogoro wa kimapenzi unaoendelea kisiri. Penzi kati ya Cardi B na Stefon Diggs lilianza rasmi mwezi Juni 2025, walipoonekana kwa mara ya kwanza hadharani wakiwa kwenye boti ya kifahari, wakifurahia muda wao pamoja. Baadaye walihudhuria kwa pamoja Paris Fashion Week na mechi ya mpira wa vikapu jijini New York kati ya Knicks na Celtics, hali iliyothibitisha wazi kuwa walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi. Katika tamasha la Cannes, Cardi alionyesha upendo wake kwa Stefon kwa kuchora jina lake kwenye kucha zake, jambo lililozua gumzo mitandaoni. Mwisho wa mwezi Juni, wawili hao walikwenda mapumzikoni nchini Ufaransa ambapo Stefon alimkodishia Cardi kasri la kifahari kwa ajili ya likizo ya faragha. Hata hivyo, kufutwa kwa picha hizo kumezua hali ya sintofahamu kuhusu mustakabali wa uhusiano huo, hasa ikizingatiwa kuwa Cardi bado yuko katika mchakato wa talaka kutoka kwa mume wake wa zamani, Offset. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu taarifa rasmi kutoka kwa mmoja wao ili kufahamu hatima ya penzi hili lililoanza kwa kishindo.

Read More
 Cardi B Awashtua Mashabiki Kwa Tangazo La Albamu Mpya

Cardi B Awashtua Mashabiki Kwa Tangazo La Albamu Mpya

Rapa maarufu wa Marekani, Cardi B, ametangaza rasmi kuachia albamu yake mpya iitwayo “AM I THE DRAMA?”, itakayotolewa rasmi Septemba 19, 2025. Hii itakuwa albamu yake ya pili baada ya mafanikio makubwa ya albamu yake ya kwanza, “Invasion of Privacy”, iliyotolewa mwaka 2018, ambayo ilimpa tuzo ya Grammy kwa Best Rap Album na ikajizolea hits kadhaa kama Bodak Yellow na I Like It. Kupitia mtandao wa Instagram, Cardi B alieleza msisimko wake na kuahidi kuwa albamu hii mpya itaonyesha mabadiliko yake binafsi na kisanii, ikiwa ni pamoja na hadithi za maisha, changamoto, na mafanikio aliyopitia katika miaka ya hivi karibuni. Alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo zenye nguvu, uhalisia wa hali ya juu, na mtindo wake wa kipekee wa rap. Tangazo hilo limepokelewa kwa shangwe kubwa kutoka kwa mashabiki na wasanii wenzake, huku wengi wakitarajia kazi hiyo itatoa sauti mpya katika muziki wa rap na kuleta msisimko mpya sokoni. Albamu hii itakuja baada ya kipindi kirefu cha ukimya cha miaka saba, wakati Cardi B akiwa amejikita pia katika maisha ya kifamilia na shughuli za biashara. Kwa sasa, haijafahamika idadi kamili ya nyimbo au washiriki wa albamu hiyo, lakini inatarajiwa kuwa ni mojawapo ya albamu zilizotarajiwa zaidi mwaka huu katika muziki wa hip hop.

Read More
 Cardi B afunguka kuhusu msimamo wa mpenzi wake Stefon Diggs licha ya misukosuko

Cardi B afunguka kuhusu msimamo wa mpenzi wake Stefon Diggs licha ya misukosuko

Rapa maarufu Cardi B amefichua kuwa mchezaji wa NFL, Stefon Diggs, alimshauri aache kushiriki mambo ya faragha hadharani. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Cardi alisema kuwa Diggs alipendekeza awe na mipaka kwenye kile anachoweka mitandaoni au anachosema hadharani kuhusu maisha yao binafsi. Cardi B pia alieleza kuwa licha ya mahusiano yao, wawili hao huonana mara mbili tu kwa wiki kutokana na ratiba zao kuwa na shughuli nyingi. Hata hivyo, uhusiano wao umekumbwa na changamoto.  Hivi karibuni, video ilisambaa ikimuonyesha Diggs akiwa kwenye boti na wanawake wengine, jambo lililomfanya Cardi B kueleza hisia zake za kukerwa na tabia hiyo. Licha ya matatizo hayo, wawili hao walionekana pamoja hadharani kwa mara ya kwanza wakiwa wameshikana mikono katika mchezo wa NBA kati ya Boston Celtics na New York Knicks kwenye uwanja wa Madison Square Garden mnamo Mei 12, 2025. Kwa sasa, mashabiki wanaendelea kufuatilia maendeleo ya uhusiano wao, wakijiuliza ikiwa wataweza kushinda changamoto zilizopo na kuendeleza penzi lao.

Read More
 Cardi B Afichua Offset Hajatoa Msaada Wowote kwa Watoto Wao kwa Miezi 8

Cardi B Afichua Offset Hajatoa Msaada Wowote kwa Watoto Wao kwa Miezi 8

Mwanamuziki maarufu wa Marekani, Belcalis Almanzar, Maarufu kama Cardi B, amefichua kuwa mzazi mwenzake na rapa wa kundi la Migos, Offset, hajatoa msaada wowote wa kifedha kwa watoto wao kwa kipindi cha miezi minane. Akiwa anajibu kauli ya Offset aliyoitoa katika mahojiano na The Breakfast Club, Cardi B alikanusha vikali madai kwamba yeye ni mzazi asiyejali, akieleza kuwa ndiye anayebeba majukumu yote ya kifamilia. Cardi alisema kuwa amekuwa akitumia hadi dola 50,000 kwa mwezi kwa ajili ya watoto wao, na kumshutumu Offset kwa kushindwa kuwajibika kama baba.  “Natumia dola elfu hamsini ($50,000) kila mwezi kwa ajili ya watoto wetu, Kutoka kwenye ada za shule, huduma za afya, chakula, usafiri, hadi walinzi binafsi. Mimi ndiye nafanya yote. Mtu aseme mimi ni deadbeat? Hapana.”, Alisema Cardi B kwa hasira. Cardi B pia alionesha wasiwasi kuhusu hali ya kiakili ya Offset, akimtaka atafute msaada badala ya kueneza tuhuma za uongo dhidi yake mitandaoni. “Nakupa pole na nafasi kwa sababu najua hauko sawa kiakili. Lakini usitumie hilo kunivunjia heshima mbele ya watoto wetu na hadhira ya dunia nzima,” aliongeza. Mgogoro huo umeibua hisia kali mitandaoni. Mashabiki wa Cardi B wamemsifu kwa uwazi wake na kujitolea kama mama, huku baadhi ya wafuasi wa Offset wakimtetea na kueleza kuwa anaweza kuwa anashughulika na changamoto za kiakili au presha kutoka kwa timu yake ya kisheria. Kauli hiyo ya Cardi B inajibu mahojiano ya hivi karibuni ambayo Offset alifanya na kipindi maarufu cha The Breakfast Club, ambapo alieleza kuwa mawakili wake walimshauri kuomba msaada wa kifedha kutoka kwa Cardi kama mkakati wa kisheria kwenye mchakato wa talaka yao. Offset alidai kuwa Cardi alitaka kila kitu katika mgawanyo wa mali, na kwamba maombi yake ni sehemu tu ya kujilinda katika taratibu za mahakama. Wawili hao, waliowana mwaka 2017, wamekuwa kwenye uhusiano wa uliojaa migogoro, na sasa wapo kwenye hatua za mwisho kukamilisha talaka yao. Wana watoto wawili pamoja Kulture Kiari na Wave Set.

Read More
 Offset Awasilisha Hati Mpya ya Talaka, Amuomba Cardi B Msaada wa Kifedha

Offset Awasilisha Hati Mpya ya Talaka, Amuomba Cardi B Msaada wa Kifedha

Rapa Offset ameibua mjadala mpya kwenye sakata lake la talaka na Cardi B baada ya kuwasilisha hati mpya mahakamani akitaka kulipwa msaada wa kifedha (spousal support) kutoka kwa mke wake wa zamani. Kulingana na ripoti mpya ya TMZ, Offset hajataja kiasi anachotaka hadharani, lakini imeelezwa wazi kuwa anahitaji malipo hayo kutoka kwa Cardi B. Hatua hii inaashiria mabadiliko makubwa katika mwelekeo wa talaka hiyo, ambayo ilianza kwa utulivu mnamo Agosti 2024 baada ya Cardi B kuwasilisha ombi la kuachana rasmi na rapa huyo. Lakini sasa, hatua ya Offset kudai msaada wa kifedha inaonyesha kuwa hana mpango wa kuondoka mikono mitupu katika mchakato huo. Licha ya ombi lake la msaada wa kifedha, Offset bado anataka malezi ya pamoja ya watoto wao watatu. Hili linaonyesha kwamba, pamoja na tofauti zao, bado anataka kuwa sehemu ya maisha ya watoto wao kwa karibu. Offset bado hajazungumza hadharani kuhusu ombi hilo jipya, lakini Cardi B alionekana kutoa ishara zisizo za moja kwa moja kupitia mitandao ya kijamii, ambapo alichapisha picha kadhaa kwenye Instagram instastory, hatua ambayo mashabiki wengi wameitafsiri kama majibu ya kimya kwa taarifa hiyo. Wakati mashabiki wakisubiri kauli rasmi kutoka kwa wawili hao, hali ya mvutano kati ya mastaa hawa wawili maarufu inaonekana kuongezeka, huku pesa na watoto vikibaki kuwa kiini cha mvutano huo wa talaka.

Read More
 Cardi B mbioni kuachia Album mpya

Cardi B mbioni kuachia Album mpya

Rapa Cardi B ataikata kiu yako ya muziki muda wowote kuanzia sasa baada ya ukimya wa miaka minne. Rapa huyo kutoka nchini Marekani ameonekana akiwa studio kwenye picha ambayo imesambaa kwenye mitandao leo. Mbali na picha hiyo, Cardi B ameifuata (follow) akaunti mpya iitwayo (Albumcb2) na kuashiria huenda ni ujio wa Album ya pili. Cardi B alitubariki na Album yake ya kwanza ‘Invasion of Privacy’ mwaka 2018 na hadi leo amekuwa akitutia kiu kikali kwa kuachia kazi kwa manati.

Read More
 Cardi B afunguka uoga kuathiri muziki

Cardi B afunguka uoga kuathiri muziki

Rapa Cardi B ameingiwa na hofu, na hiyo ndio sababu kuu ambayo inamfanya achelewe kuachia Album mpya kwa kipindi cha miaka mitatu sasa. Cardi B anasema amekuwa muoga kuachia ngoma kutokana na watu kumkosoa sana. “Kipindi cha kuanzia mwaka 2015 hadi 2018 nilikuwa napenda Muziki, lakini kwa sasa, kufanya muziki kwangu mimi imekuwa Kazi ambayo inanifanya niwe na wasiwasi. Kwa sababu kila mmoja anakosoa kila kitu ninachofanya. Wakati mwingine hupaswi kufanya kitu ambacho kinakufanya uwe na wasiwasi.” alisema Cardi B. Tangu alipoachia Album yake ‘Invasion of Privacy’ mwaka 2018, Cardi B amekuwa akirekodi nyimbo lakini haridhishwi na anachokifanya.

Read More
 CARDI B AMKINGIA KIFUA MUMEWE OFFSET KWA UGOMVI WA BURNA BOY NA WIZKID

CARDI B AMKINGIA KIFUA MUMEWE OFFSET KWA UGOMVI WA BURNA BOY NA WIZKID

Rapa Cardi B ameibuka na kumkingia kifua mume wake Offset baada ya kusambaa kwa post ambayo inaonesha Offset akisema kwamba tayari ana ngoma na Burna Boy. Hii ni kufuatia kushindwa kumpata Wizkid kutokana na kutoza pesa nyingi kwenye kolabo ikilinganishwa na Burna Boy. Sasa baada ya wengi kuliiwekea post hiyo mashaka Cardi B ameibuka na kupuzilia mbali madai hayo kwa kusema kwamba hayana ukweli wowote kwani haitajatoka kwa Offset. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Cardi B ameandika “Fake As F*ck” na kisha kuifuta Tweet hiyo. Utakumbuka baada ya post  inayodaiwa kuwa ya Offset akimzungumzia Wizkid na Burna Boy kusambaa mtandaoni, taswira mbaya ilijengeka miongoni mwa walimwengu wengi wakihoji kuwa Burna Boy ni msanii wa kawaida kifedha ukimlinganisha na Wizkid.

Read More
 RAPA CARDI B AKIRI KUTESWA NA UMAARUFU

RAPA CARDI B AKIRI KUTESWA NA UMAARUFU

Rapa kutoka Marekani Cardi B amefunguka wazi kuwa amechoka kuwa maarufu, hii ni baada ya kumalizika kwa onesho la Met Gala 2022 Jijini New York Jumatatu wiki hii. Cardi B ameutumia ukurasa wake wa Instagram kwenda live na kusema kwamba umaarufu si kitu kizuri kwa upande wake huku kuwataka watu wasitamani umaarufu bali watamani kuwa matajiri. “Ninauchukia umaarufu, nachukia kuwa maarufu. Nachukia sana. Acha niwaambie kitu kimoja, kama umewahi kutamani kuwa tajiri na maarufu, usitamani kuwa maarufu, tamani kuwa tajiri.” Amesikika akiwa Instagram live. Hii sio mara ya kwanza kwa Cardi B kuonesha hautaki umaarufu, aliwahi kuufuta ukurasa wake wa Twitter kwa kueleza tatizo hilo.

Read More