Rapa Cardi B Aahidi Kutii Sheria Zote za Saudi Arabia Kabla ya Show Riyadh

Rapa Cardi B Aahidi Kutii Sheria Zote za Saudi Arabia Kabla ya Show Riyadh

Rapa wa Marekani, Cardi B, amewatuliza wananchi wa Saudi Arabia baada ya mjadala mtandaoni kuhusu maadili na sheria za nchi hiyo kabla ya ziara yake inayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu jijini Riyadh. Katika mazungumzo yake kupitia Insta Live, Cardi B amesisitiza kuwa atatii kikamilifu sheria na taratibu zote za Saudi Arabia pindi atakapowasili kwa ajili ya onyesho lake. Pia amebainisha kuwa hana tabia ya kutumia pombe na anajitambua kama mwanamke mwenye maadili, hivyo hana sababu ya kwenda kinyume na kanuni za nchi hiyo. Cardi B anatarajiwa kutumbuiza kwenye moja ya matamasha makubwa ya mwisho wa mwaka, hafla inayotarajia kuvutia mastaa mbalimbali wa kimataifa.

Read More
 Cardi B Atinga Mitaani New York Kutangaza Albamu Yake Mpya

Cardi B Atinga Mitaani New York Kutangaza Albamu Yake Mpya

Msanii wa muziki wa hip-hop nchini Marekani, Cardi B, amewashangaza mashabiki na wachambuzi wa muziki baada ya kuonekana akizunguka mtaani ya New York akitangaza kwa mikono yake mwenyewe albamu yake mpya “Am I The Drama.” Tukio hilo lililoshuhudiwa na wapita njia na mashabiki wake limeibua mitazamo tofauti. Wapo wanaoona hatua hiyo kama mkakati wa kibunifu wa kumfanya msanii huyo aendelee kuwa karibu na mashabiki wake na kuonesha unyenyekevu katika tasnia ambayo mara nyingi hutegemea matangazo makubwa ya kibiashara. Hata hivyo, upande wa pili wa maoni unasema ni dalili za kukata tamaa na ishara kwamba mradi huo huenda unakumbwa na changamoto za kupenya sokoni kabla hata ya kutoka rasmi. Kwenye mitandao ya kijamii, mjadala umechacha. Wafuasi wake wanamsifu kwa ujasiri wa kwenda mitaani na kujibebea jukumu la kutangaza kazi yake badala ya kutegemea matangazo ya kibiashara pekee. Lakini wakosoaji wanadai hatua hiyo inadhihirisha presha anayokabiliana nayo, hasa katika soko la muziki lenye ushindani mkali ambapo wasanii wapya na wakongwe huachia miradi kila mara.

Read More
 Cardi B Aondolewa Mashtaka ya Shambulio na Ubaguzi

Cardi B Aondolewa Mashtaka ya Shambulio na Ubaguzi

Rapa maarufu wa Marekani, Cardi B, amekutwa hana hatia katika kesi ya madai yaliyofunguliwa na mlinzi wake wa zamani wa usalama, Emani Ellis. Ellis alikuwa amemshataki Cardi B kwa madai ya kumshambulia kwenye ofisi ya daktari wa wanawake huko Beverly Hills mwaka 2018. Mlinzi huyo alidai Cardi alimshambulia, kumtemea mate, na kumtolea maneno ya ubaguzi wa rangi, na kuomba fidia ya $24 milioni (takriban Ksh bilioni 3.1). Hata hivyo, ushahidi uliotolewa na mashahidi waliokuwa kliniki hiyo ulikanusha madai ya Ellis. Majaji wakachunguza ushahidi huu na hatimaye wakamua kusimama na Cardi B, wakimkuta hana hatia. Akizungumza nje ya mahakama, Cardi B amesema kuwa atapambana na mtu yeyote atakayefungua shauri la uongo dhidi yake, akionya kuwa safari hii mhusika atalazimika kugharamia uharibifu wowote atakaomsababisha. Cardi B pia alisisitiza kuwa kesi hii ilikuwa njama ya kutaka pesa, na alieleza kuwa hana hofu ya kudai haki yake mbele ya sheria. Uamuzi huu unamruhusu Cardi B kuendelea na maisha yake bila kuingiliwa na masuala ya kisheria yanayohusiana na tukio hilo la zamani, huku akiwakilisha mfano wa kushikilia haki binafsi na usalama wa heshima.

Read More
 Cardi B Amwaga Hasira kwa Paparazzi Mbele ya Kamera

Cardi B Amwaga Hasira kwa Paparazzi Mbele ya Kamera

Rapa maarufu wa Marekani, Cardi B, amekumbana na hali ya kutoelewana na paparazzi jana, akiwa nje ya Mahakama ya Alhambra, California. Paparazzi huyo aliuliza swali lisilo na adabu linalohusiana na uhusiano wake na mchezaji wa NFL, Stefon Diggs, mpenzi wake wa sasa, na pia aliyekuwa mume wake, Offset, ambaye hivi karibuni alionekana kujigamba kuhusu ujauzito wa mtoto wao wa nne. Cardi B, akiwa ameshtuka na kushikwa na hasira, alionyesha kukerwa kwake kwa kumnyanganya shabiki kalamu na kisha kumrushia paparazzi huyo. Rapa huyo aliweka wazi kuwa paparazzi wanapaswa kuwa na adabu na kumheshimu, akisisitiza kuwa wanawake wanastahili heshima wanapoulizwa maswali yenye hofu kama hayo. Hali hii imeonesha mara nyingine tena jinsi Cardi B anavyolinda maisha yake binafsi na jinsi anavyoshughulikia maswali yasiyo na heshima kutoka kwa waandishi wa habari.

Read More
 Cardi B Kortini! Akanusha Kumshambulia Mlinzi Akiwa Mjamzito

Cardi B Kortini! Akanusha Kumshambulia Mlinzi Akiwa Mjamzito

Rapa wa Marekani, Cardi B, amekanusha vikali madai kwamba alimshambulia mlinzi wa usalama mwaka 2018 wakati akiwa mjamzito. Akiwasili mahakamani mjini Alhambra, California siku ya pili ya kusikilizwa kwa kesi hiyo, jana, Cardi amesema hakuwahi kumgusa mlalamikaji Emani Ellis na kudai madai hayo hayana ukweli wowote. Msanii huyo amesisitiza kwamba Ellis ndiye aliyekuwa akimfuata na hata kujaribu kumrekodi bila ridhaa, jambo ambalo lilimfanya ahisi kuvamiwa faragha yake. Ellis, ambaye aliwasilisha ushahidi wake Jumatatu, anadai kuwa Cardi alimtukana, kumtupia mate, kumwekea kidole usoni na kuamuru walinzi wake kumshikilia katika ofisi ya daktari wa kina mama mwezi Februari mwaka 2018. Ellis amemshtaki Cardi kwa shambulio na kupiga, kusababisha msongo wa mawazo, uzembe na kizuizi cha kiholela. Kupitia kesi hiyo ya madai, Ellis anataka fidia ya gharama za matibabu, malipo ya mapato aliyopoteza na atakayopoteza siku zijazo, pamoja na adhabu ya kifedha na faini ya kiraia ya $25,000, kwa mujibu wa CourtTV.

Read More
 Wakili wa Cardi B Ajibu Kesi ya Kipaza Sauti

Wakili wa Cardi B Ajibu Kesi ya Kipaza Sauti

Wakili wa rapa kutoka Marekani Cardi B, Drew Findling, ameibuka na kuikosoa vikali kesi mpya ya madai iliyofunguliwa dhidi ya mteja wake, akisema ni jaribio la kutaka kumpora pesa kwa kutumia jina lake maarufu. Kauli ya Findling imekuja kufuatia mwanamke mmoja, anayetambulika kama Jane Doe, kufungua kesi ya madai dhidi ya Cardi B kwa tuhuma za shambulio la mwili, uzembe na dhuluma ya kihisia, akidai kuwa alijeruhiwa baada ya kurushiwa kipaza sauti na rapa huyo wakati wa tamasha la Drai’s Beachclub huko Las Vegas mnamo Agosti 2023. Kwa mujibu wa maelezo ya Jane Doe, Cardi B alikuwa akitumbuiza katika hafla ya mchana iliyokuwa ikifanyika wakati wa joto kali, ambapo aliwaomba mashabiki wamwagie maji ili kupooza. Mwanamke huyo anasema alifanya hivyo kwa nia njema, lakini alichokutana nacho ni kurushiwa kipaza sauti kwa nguvu na Cardi B, kitendo ambacho sasa anadai kilimsababishia madhara ya kimwili na kiakili. Ingawa tukio hilo lilichukua sura kubwa mitandaoni wakati huo, uchunguzi wa polisi haukupelekea kufunguliwa kwa mashtaka yoyote ya jinai dhidi ya Cardi B. Polisi waliamua kufunga jalada hilo baada ya kukosa ushahidi wa kutosha, na kesi hiyo haikuwahi kufika kwa Mwendesha Mashtaka wa Kaunti. Hata hivyo, Jane Doe sasa ameamua kufungua kesi ya madai miaka miwili baadaye, akidai kuwa hata mnada wa kipaza sauti hicho kwa ajili ya shughuli za hisani ulimvuruga kisaikolojia na kumrudisha katika hali ya huzuni aliyoipitia baada ya tukio hilo. Mashabiki wa Cardi B wamejitokeza mitandaoni wakimtetea msanii huyo, wengi wakisema mwanamke huyo alitafuta kiki na sasa anajaribu kutumia tukio la zamani kujinufaisha kifedha. Hadi sasa, Cardi B hajatoa tamko la moja kwa moja kuhusu kesi hiyo mpya, lakini timu yake ya kisheria imeweka wazi kuwa wataipinga vikali hadi mwisho.

Read More
 Cardi B Kizimbani: Ashtakiwa kwa Kumrushia Shabiki Kipaza Sauti

Cardi B Kizimbani: Ashtakiwa kwa Kumrushia Shabiki Kipaza Sauti

Staa wa muziki wa Hip Hop Cardi B anakabiliwa na kesi ya kisheria kufuatia tukio la mwaka 2023 ambapo alinaswa kwenye video akimrushia shabiki wake kipaza sauti wakati wa onyesho moja jijini Las Vegas, Marekani. Kwa mujibu wa hati za mahakama zilizowasilishwa hivi karibuni, shabiki huyo ambaye jina lake halijawekwa wazi, anadai kuwa aliumia baada ya Cardi B kurusha kipaza sauti kwa hasira, kitendo kinachodaiwa kuwa ni shambulio, unyanyasaji wa mwili na uzembe. Tukio hilo lilitokea wakati wa onyesho la Cardi B mwezi Julai 2023, ambapo inasemekana msanii huyo alikasirishwa na kitendo cha shabiki kumrusha kinywaji akiwa jukwaani. Katika kile kinachoelezwa kuwa ni kisasi, Cardi alionekana akirusha kipaza sauti kwa nguvu kuelekea kwenye kundi la mashabiki. Ingawa hakukuwa na mashtaka ya jinai yaliyowasilishwa wakati huo, kesi hii mpya inaweza kumgharimu Cardi B fedha nyingi na kuathiri jina lake kwenye muziki. Wakili wa mlalamikaji anasema mteja wake alipata majeraha ya mwilini na pia mshtuko kutokana na tukio hilo.

Read More
 Video Mpya Yazima Uvumi: Cardi B na Stefon Diggs Wapo Bado Kwenye Mahaba

Video Mpya Yazima Uvumi: Cardi B na Stefon Diggs Wapo Bado Kwenye Mahaba

Tetesi kuwa uhusiano kati ya rapa maarufu Cardi B na mcheza mpira wa Marekani Stefon Diggs umeenea mitandaoni, lakini taarifa mpya zinaonyesha kuwa penzi lao bado lipo imara. Uvumi wa kuachana kwao ulianza baada ya mashabiki kubaini kuwa Cardi B alikuwa amefuta picha zote za Stefon Diggs kwenye akaunti yake ya Instagram, jambo lililoibua maswali mengi kuhusu mustakabali wa uhusiano wao. Hata hivyo, Cardi B alionekana kupuuzilia mbali uvumi huo kwa kuchapisha video kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), akionekana akiwa gym na Diggs wakifanya mazoezi pamoja. Video hiyo imechukuliwa kama jibu kwa waliodhani kuwa wawili hao tayari wameachana. Chanzo cha karibu na wawili hao kimeripotiwa kuiambia TMZ kwamba wapenzi hao bado wako kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanaendelea vyema, tofauti na taarifa zinazozunguka mtandaoni.

Read More
 Cardi B Aibua Sintofahamu Baada ya Kufuta Picha za Stefon Diggs

Cardi B Aibua Sintofahamu Baada ya Kufuta Picha za Stefon Diggs

Mashabiki wa rapa maarufu Cardi B wameibua hisia mseto mitandaoni baada ya kugundua kuwa msanii huyo amefuta picha zote za mpenzi wake mpya, Stefon Diggs, kutoka kwenye ukurasa wake wa Instagram. Hatua hiyo imezua tetesi kuwa huenda uhusiano wao umeingia matatizoni au hata kuvunjika kabisa. Wengi wa mashabiki walieleza mshangao na masikitiko, wakikumbuka jinsi penzi la Cardi na Stefon lilivyokuwa linaonekana kuwa la kipekee, lenye mapenzi ya dhati na hadhi ya juu. Wengine walitafsiri hatua hiyo kama njia ya Cardi kujilinda dhidi ya maisha ya umma, huku baadhi wakiamini ni dalili ya mgogoro wa kimapenzi unaoendelea kisiri. Penzi kati ya Cardi B na Stefon Diggs lilianza rasmi mwezi Juni 2025, walipoonekana kwa mara ya kwanza hadharani wakiwa kwenye boti ya kifahari, wakifurahia muda wao pamoja. Baadaye walihudhuria kwa pamoja Paris Fashion Week na mechi ya mpira wa vikapu jijini New York kati ya Knicks na Celtics, hali iliyothibitisha wazi kuwa walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi. Katika tamasha la Cannes, Cardi alionyesha upendo wake kwa Stefon kwa kuchora jina lake kwenye kucha zake, jambo lililozua gumzo mitandaoni. Mwisho wa mwezi Juni, wawili hao walikwenda mapumzikoni nchini Ufaransa ambapo Stefon alimkodishia Cardi kasri la kifahari kwa ajili ya likizo ya faragha. Hata hivyo, kufutwa kwa picha hizo kumezua hali ya sintofahamu kuhusu mustakabali wa uhusiano huo, hasa ikizingatiwa kuwa Cardi bado yuko katika mchakato wa talaka kutoka kwa mume wake wa zamani, Offset. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu taarifa rasmi kutoka kwa mmoja wao ili kufahamu hatima ya penzi hili lililoanza kwa kishindo.

Read More
 Cardi B Awashtua Mashabiki Kwa Tangazo La Albamu Mpya

Cardi B Awashtua Mashabiki Kwa Tangazo La Albamu Mpya

Rapa maarufu wa Marekani, Cardi B, ametangaza rasmi kuachia albamu yake mpya iitwayo “AM I THE DRAMA?”, itakayotolewa rasmi Septemba 19, 2025. Hii itakuwa albamu yake ya pili baada ya mafanikio makubwa ya albamu yake ya kwanza, “Invasion of Privacy”, iliyotolewa mwaka 2018, ambayo ilimpa tuzo ya Grammy kwa Best Rap Album na ikajizolea hits kadhaa kama Bodak Yellow na I Like It. Kupitia mtandao wa Instagram, Cardi B alieleza msisimko wake na kuahidi kuwa albamu hii mpya itaonyesha mabadiliko yake binafsi na kisanii, ikiwa ni pamoja na hadithi za maisha, changamoto, na mafanikio aliyopitia katika miaka ya hivi karibuni. Alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo zenye nguvu, uhalisia wa hali ya juu, na mtindo wake wa kipekee wa rap. Tangazo hilo limepokelewa kwa shangwe kubwa kutoka kwa mashabiki na wasanii wenzake, huku wengi wakitarajia kazi hiyo itatoa sauti mpya katika muziki wa rap na kuleta msisimko mpya sokoni. Albamu hii itakuja baada ya kipindi kirefu cha ukimya cha miaka saba, wakati Cardi B akiwa amejikita pia katika maisha ya kifamilia na shughuli za biashara. Kwa sasa, haijafahamika idadi kamili ya nyimbo au washiriki wa albamu hiyo, lakini inatarajiwa kuwa ni mojawapo ya albamu zilizotarajiwa zaidi mwaka huu katika muziki wa hip hop.

Read More
 Cardi B afunguka kuhusu msimamo wa mpenzi wake Stefon Diggs licha ya misukosuko

Cardi B afunguka kuhusu msimamo wa mpenzi wake Stefon Diggs licha ya misukosuko

Rapa maarufu Cardi B amefichua kuwa mchezaji wa NFL, Stefon Diggs, alimshauri aache kushiriki mambo ya faragha hadharani. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Cardi alisema kuwa Diggs alipendekeza awe na mipaka kwenye kile anachoweka mitandaoni au anachosema hadharani kuhusu maisha yao binafsi. Cardi B pia alieleza kuwa licha ya mahusiano yao, wawili hao huonana mara mbili tu kwa wiki kutokana na ratiba zao kuwa na shughuli nyingi. Hata hivyo, uhusiano wao umekumbwa na changamoto.  Hivi karibuni, video ilisambaa ikimuonyesha Diggs akiwa kwenye boti na wanawake wengine, jambo lililomfanya Cardi B kueleza hisia zake za kukerwa na tabia hiyo. Licha ya matatizo hayo, wawili hao walionekana pamoja hadharani kwa mara ya kwanza wakiwa wameshikana mikono katika mchezo wa NBA kati ya Boston Celtics na New York Knicks kwenye uwanja wa Madison Square Garden mnamo Mei 12, 2025. Kwa sasa, mashabiki wanaendelea kufuatilia maendeleo ya uhusiano wao, wakijiuliza ikiwa wataweza kushinda changamoto zilizopo na kuendeleza penzi lao.

Read More
 Cardi B Afichua Offset Hajatoa Msaada Wowote kwa Watoto Wao kwa Miezi 8

Cardi B Afichua Offset Hajatoa Msaada Wowote kwa Watoto Wao kwa Miezi 8

Mwanamuziki maarufu wa Marekani, Belcalis Almanzar, Maarufu kama Cardi B, amefichua kuwa mzazi mwenzake na rapa wa kundi la Migos, Offset, hajatoa msaada wowote wa kifedha kwa watoto wao kwa kipindi cha miezi minane. Akiwa anajibu kauli ya Offset aliyoitoa katika mahojiano na The Breakfast Club, Cardi B alikanusha vikali madai kwamba yeye ni mzazi asiyejali, akieleza kuwa ndiye anayebeba majukumu yote ya kifamilia. Cardi alisema kuwa amekuwa akitumia hadi dola 50,000 kwa mwezi kwa ajili ya watoto wao, na kumshutumu Offset kwa kushindwa kuwajibika kama baba.  “Natumia dola elfu hamsini ($50,000) kila mwezi kwa ajili ya watoto wetu, Kutoka kwenye ada za shule, huduma za afya, chakula, usafiri, hadi walinzi binafsi. Mimi ndiye nafanya yote. Mtu aseme mimi ni deadbeat? Hapana.”, Alisema Cardi B kwa hasira. Cardi B pia alionesha wasiwasi kuhusu hali ya kiakili ya Offset, akimtaka atafute msaada badala ya kueneza tuhuma za uongo dhidi yake mitandaoni. “Nakupa pole na nafasi kwa sababu najua hauko sawa kiakili. Lakini usitumie hilo kunivunjia heshima mbele ya watoto wetu na hadhira ya dunia nzima,” aliongeza. Mgogoro huo umeibua hisia kali mitandaoni. Mashabiki wa Cardi B wamemsifu kwa uwazi wake na kujitolea kama mama, huku baadhi ya wafuasi wa Offset wakimtetea na kueleza kuwa anaweza kuwa anashughulika na changamoto za kiakili au presha kutoka kwa timu yake ya kisheria. Kauli hiyo ya Cardi B inajibu mahojiano ya hivi karibuni ambayo Offset alifanya na kipindi maarufu cha The Breakfast Club, ambapo alieleza kuwa mawakili wake walimshauri kuomba msaada wa kifedha kutoka kwa Cardi kama mkakati wa kisheria kwenye mchakato wa talaka yao. Offset alidai kuwa Cardi alitaka kila kitu katika mgawanyo wa mali, na kwamba maombi yake ni sehemu tu ya kujilinda katika taratibu za mahakama. Wawili hao, waliowana mwaka 2017, wamekuwa kwenye uhusiano wa uliojaa migogoro, na sasa wapo kwenye hatua za mwisho kukamilisha talaka yao. Wana watoto wawili pamoja Kulture Kiari na Wave Set.

Read More