Offset Awasilisha Hati Mpya ya Talaka, Amuomba Cardi B Msaada wa Kifedha

Offset Awasilisha Hati Mpya ya Talaka, Amuomba Cardi B Msaada wa Kifedha

Rapa Offset ameibua mjadala mpya kwenye sakata lake la talaka na Cardi B baada ya kuwasilisha hati mpya mahakamani akitaka kulipwa msaada wa kifedha (spousal support) kutoka kwa mke wake wa zamani. Kulingana na ripoti mpya ya TMZ, Offset hajataja kiasi anachotaka hadharani, lakini imeelezwa wazi kuwa anahitaji malipo hayo kutoka kwa Cardi B. Hatua hii inaashiria mabadiliko makubwa katika mwelekeo wa talaka hiyo, ambayo ilianza kwa utulivu mnamo Agosti 2024 baada ya Cardi B kuwasilisha ombi la kuachana rasmi na rapa huyo. Lakini sasa, hatua ya Offset kudai msaada wa kifedha inaonyesha kuwa hana mpango wa kuondoka mikono mitupu katika mchakato huo. Licha ya ombi lake la msaada wa kifedha, Offset bado anataka malezi ya pamoja ya watoto wao watatu. Hili linaonyesha kwamba, pamoja na tofauti zao, bado anataka kuwa sehemu ya maisha ya watoto wao kwa karibu. Offset bado hajazungumza hadharani kuhusu ombi hilo jipya, lakini Cardi B alionekana kutoa ishara zisizo za moja kwa moja kupitia mitandao ya kijamii, ambapo alichapisha picha kadhaa kwenye Instagram instastory, hatua ambayo mashabiki wengi wameitafsiri kama majibu ya kimya kwa taarifa hiyo. Wakati mashabiki wakisubiri kauli rasmi kutoka kwa wawili hao, hali ya mvutano kati ya mastaa hawa wawili maarufu inaonekana kuongezeka, huku pesa na watoto vikibaki kuwa kiini cha mvutano huo wa talaka.

Read More
 Cardi B mbioni kuachia Album mpya

Cardi B mbioni kuachia Album mpya

Rapa Cardi B ataikata kiu yako ya muziki muda wowote kuanzia sasa baada ya ukimya wa miaka minne. Rapa huyo kutoka nchini Marekani ameonekana akiwa studio kwenye picha ambayo imesambaa kwenye mitandao leo. Mbali na picha hiyo, Cardi B ameifuata (follow) akaunti mpya iitwayo (Albumcb2) na kuashiria huenda ni ujio wa Album ya pili. Cardi B alitubariki na Album yake ya kwanza ‘Invasion of Privacy’ mwaka 2018 na hadi leo amekuwa akitutia kiu kikali kwa kuachia kazi kwa manati.

Read More
 Cardi B afunguka uoga kuathiri muziki

Cardi B afunguka uoga kuathiri muziki

Rapa Cardi B ameingiwa na hofu, na hiyo ndio sababu kuu ambayo inamfanya achelewe kuachia Album mpya kwa kipindi cha miaka mitatu sasa. Cardi B anasema amekuwa muoga kuachia ngoma kutokana na watu kumkosoa sana. “Kipindi cha kuanzia mwaka 2015 hadi 2018 nilikuwa napenda Muziki, lakini kwa sasa, kufanya muziki kwangu mimi imekuwa Kazi ambayo inanifanya niwe na wasiwasi. Kwa sababu kila mmoja anakosoa kila kitu ninachofanya. Wakati mwingine hupaswi kufanya kitu ambacho kinakufanya uwe na wasiwasi.” alisema Cardi B. Tangu alipoachia Album yake ‘Invasion of Privacy’ mwaka 2018, Cardi B amekuwa akirekodi nyimbo lakini haridhishwi na anachokifanya.

Read More
 CARDI B AMKINGIA KIFUA MUMEWE OFFSET KWA UGOMVI WA BURNA BOY NA WIZKID

CARDI B AMKINGIA KIFUA MUMEWE OFFSET KWA UGOMVI WA BURNA BOY NA WIZKID

Rapa Cardi B ameibuka na kumkingia kifua mume wake Offset baada ya kusambaa kwa post ambayo inaonesha Offset akisema kwamba tayari ana ngoma na Burna Boy. Hii ni kufuatia kushindwa kumpata Wizkid kutokana na kutoza pesa nyingi kwenye kolabo ikilinganishwa na Burna Boy. Sasa baada ya wengi kuliiwekea post hiyo mashaka Cardi B ameibuka na kupuzilia mbali madai hayo kwa kusema kwamba hayana ukweli wowote kwani haitajatoka kwa Offset. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Cardi B ameandika “Fake As F*ck” na kisha kuifuta Tweet hiyo. Utakumbuka baada ya post  inayodaiwa kuwa ya Offset akimzungumzia Wizkid na Burna Boy kusambaa mtandaoni, taswira mbaya ilijengeka miongoni mwa walimwengu wengi wakihoji kuwa Burna Boy ni msanii wa kawaida kifedha ukimlinganisha na Wizkid.

Read More
 RAPA CARDI B AKIRI KUTESWA NA UMAARUFU

RAPA CARDI B AKIRI KUTESWA NA UMAARUFU

Rapa kutoka Marekani Cardi B amefunguka wazi kuwa amechoka kuwa maarufu, hii ni baada ya kumalizika kwa onesho la Met Gala 2022 Jijini New York Jumatatu wiki hii. Cardi B ameutumia ukurasa wake wa Instagram kwenda live na kusema kwamba umaarufu si kitu kizuri kwa upande wake huku kuwataka watu wasitamani umaarufu bali watamani kuwa matajiri. “Ninauchukia umaarufu, nachukia kuwa maarufu. Nachukia sana. Acha niwaambie kitu kimoja, kama umewahi kutamani kuwa tajiri na maarufu, usitamani kuwa maarufu, tamani kuwa tajiri.” Amesikika akiwa Instagram live. Hii sio mara ya kwanza kwa Cardi B kuonesha hautaki umaarufu, aliwahi kuufuta ukurasa wake wa Twitter kwa kueleza tatizo hilo.

Read More
 CARDI B APIGA CHINI DILI YA MABILIONI YA PESA, AJITOA KWENYE UHUSIKA WA FILAMU YA “ASSISTED LIVING”

CARDI B APIGA CHINI DILI YA MABILIONI YA PESA, AJITOA KWENYE UHUSIKA WA FILAMU YA “ASSISTED LIVING”

Rapa wa kike kutoka Marekani Cardi B amelipiga chini dili nono lenye thamani ya shilling billion 3.2 za Kenya kwa kujiondoa kwenye nafasi ya uhusika mkuu wa filamu ya ucheshi iitwayo ‘Assisted Living’ ambayo inatayarishwa chini ya kampuni ya Paramount Movies. Kwa mujibu wa tovuti ya Deadline, Cardi anatajwa kuchukua maamuzi hayo kutokana na kuzidiwa na ratiba zake. Cardi B amejiondoa kwenye nafasi hiyo ikiwa ni wiki mbili tu kuelekea siku ya kuanza uzalishaji (production) wa filamu hiyo. Kuondoka kwake kumeleta athari kubwa kwani kampuni ya Paramount Movies imebidi kuahirisha utengenezaji wa filamu hiyo. Hata hivyo wanasema hawajafungua mashtaka kwani wanaamini Cardi B anaweza kurejea tena siku za usoni.

Read More
 CARDI B ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DUNIA KUTAFUTA MWARUBAINI WA MZOZO UNAOSHUHUDIWA KATI YA URUSI NA UKRAINE

CARDI B ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DUNIA KUTAFUTA MWARUBAINI WA MZOZO UNAOSHUHUDIWA KATI YA URUSI NA UKRAINE

Female Rapper kutoka Marekani Cardi B ametoa maoni yake kuhusu nchi ya Urusi na ameshauri viongozi wakubwa duniani watafute suluhisho kwa usalama wa raia. Hii inakuja baada uwepo wa machafuko ya kisiasa yanayoendelea kati ya Ukraine na Urusi. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Cardi B anasema inabidi waanze kufikiria namna ambavyo raia wanaathirika kutokana na maamuzi yao. Lakini pia amesema kutokana na dunia kukumbwa na majanga kadhaa, viongozi hao wasiyape kipaumbele masuala ya kuwekeana vikwazo, vita, na kuvamiana.

Read More
 CARDI B AMZAWADI OFFSET CHEQUE YA SHILLINGI MILLIONI 226

CARDI B AMZAWADI OFFSET CHEQUE YA SHILLINGI MILLIONI 226

Wakati ukichukulia poa kumbukizi ya kuzaliwa kwa mpenzi wako, huko nchini Marekani rapa Cardi B hakuwa na jambo dogo kwa Baby Daddy wake OffSet , Hitmaker huyo wa “WAP” amemsurprise mume wake Offset kwa cheque nzito ya dollar million 2 za Kimarekani kama zawadi ya Birthday yake ambayo ilikuwa Disemba 14. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa instagram Offset ametoa shukrani za dhati kwa mke wake Cardi B kwa zawadi hiyo ya kitofauti ambayo hakuitegemea, sambamba na kuonyesha mkoba huo pamoja na bei kupitia risiti ya manunuzi. “Wow Asante mpenzi (Cardi B). Mara nyingi unaniletea vitu vya kitofauti nakupenda na nakuheshimu sana”. Aliandika Offset kupitia ukurasa wake wa Instagram. Hii sio mara ya kwanza kwa Cardi B kumpa mumewe zawadi kubwa  kwani mwaka 2020 wakati Offset aliposherehekea kutimiza miaka 29, Cardi B alimsurprise na ndinga kali,aina ya  Lamborghini Aventador SVJ.

Read More
 CARDI B ATANGAZA KUACHIA RASMI ALBUM YAKE MWAKA WA 2022

CARDI B ATANGAZA KUACHIA RASMI ALBUM YAKE MWAKA WA 2022

Rapa Cardi B kutoka Marekani ameendelea kuwa mtu wa ahadi kwa mashabiki wa muziki wake juu ya ujio wa album yake mpya baada ya miaka mitatu sasa. Jana kupitia Instagram LIVE, Cardi B amesema watu watarajie album mpya wakati wowote kuanzia mwaka 2022. Sababu kuu ya kuchelewa kuachiwa kwa album hiyo ni muda, Cardi B amedai kwamba amekuwa na muda finyu ukizingatia kwa sasa ana watoto wawili. Invasion of Privacy ya mwaka 2018 ndio album pekee ambayo Cardi B amewabariki mashabiki zake tangu atie mguu kwenye muziki.

Read More
 KESI YA CARDI B KUWASHUSHIA KICHAPO WAHUDUMU WA CLUB KUSIKILIZWA LEO

KESI YA CARDI B KUWASHUSHIA KICHAPO WAHUDUMU WA CLUB KUSIKILIZWA LEO

Rapa kutoka Marekani Cardi B  yuko hatarini kufungwa miaka minne  jela kufuatia mashtaka mawili yanayomkabili,ya kuwapiga na kuwafanyia fujo wahudumu wawili wa club iitwayo Angels-Strip-Club Mwaka 2018 Cardi B alikamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa makosa hayo mawili lakini mwaka wa 2019 alikanusha kwenye mahakama kuu ya queens akiwa kizimbani kwa kumwambia hakimu kuwa hana hatia Inadaiwa Cardi B alitoa maelekezo kwa wasaidizi wake kuwapiga wahudumu hao wawili wa klabu hiyo  na baadaye yeye pia alishiriki kutembeza kipigo, kurusha viti na kupasua chupa mara baada ya kusikia kuwa mmoja kati yao alitoka kimapenzi na mumewe Offset. Hata hivyo usikilizaji wa kesi hiyo umepangwa kufanya oktoba 25, mwaka huu na endapo rapa huyo atakutwa na hatia ya makosa yote mawili basi kifungo cha miaka minne  jela kitamhusu

Read More
 CARDI B AJIWEKA PEMBENI NA MAMBO YA SIASA, ATAJA CHANZO

CARDI B AJIWEKA PEMBENI NA MAMBO YA SIASA, ATAJA CHANZO

Rapa Cardi B alikuwa anapaza sauti yake kwenye mijadala mbali mbali ya siasa za nchini Marekani, lakini kuna muda alikuwa hasikiki tena na watu kuanza kujiuliza maswali. Akijibu swali hilo ambalo aliulizwa na shabiki mmoja kupitia ukurasa wake wa Twitter, Cardi B amesema aliamua kukaa kimya kutokana na kunyanyaswa na kambi ya chama cha Republican ambacho kilikuwa kinaongozwa na Rais Donald Trump. Lakini pia, alikuwa akipokea ukosoaji mkubwa kutoka kwa watu ambao alikuwa akiwapigania kwenye siasa.

Read More