CARDI B APIGA CHINI DILI YA MABILIONI YA PESA, AJITOA KWENYE UHUSIKA WA FILAMU YA “ASSISTED LIVING”

CARDI B APIGA CHINI DILI YA MABILIONI YA PESA, AJITOA KWENYE UHUSIKA WA FILAMU YA “ASSISTED LIVING”

Rapa wa kike kutoka Marekani Cardi B amelipiga chini dili nono lenye thamani ya shilling billion 3.2 za Kenya kwa kujiondoa kwenye nafasi ya uhusika mkuu wa filamu ya ucheshi iitwayo ‘Assisted Living’ ambayo inatayarishwa chini ya kampuni ya Paramount Movies. Kwa mujibu wa tovuti ya Deadline, Cardi anatajwa kuchukua maamuzi hayo kutokana na kuzidiwa na ratiba zake. Cardi B amejiondoa kwenye nafasi hiyo ikiwa ni wiki mbili tu kuelekea siku ya kuanza uzalishaji (production) wa filamu hiyo. Kuondoka kwake kumeleta athari kubwa kwani kampuni ya Paramount Movies imebidi kuahirisha utengenezaji wa filamu hiyo. Hata hivyo wanasema hawajafungua mashtaka kwani wanaamini Cardi B anaweza kurejea tena siku za usoni.

Read More
 CARDI B ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DUNIA KUTAFUTA MWARUBAINI WA MZOZO UNAOSHUHUDIWA KATI YA URUSI NA UKRAINE

CARDI B ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DUNIA KUTAFUTA MWARUBAINI WA MZOZO UNAOSHUHUDIWA KATI YA URUSI NA UKRAINE

Female Rapper kutoka Marekani Cardi B ametoa maoni yake kuhusu nchi ya Urusi na ameshauri viongozi wakubwa duniani watafute suluhisho kwa usalama wa raia. Hii inakuja baada uwepo wa machafuko ya kisiasa yanayoendelea kati ya Ukraine na Urusi. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Cardi B anasema inabidi waanze kufikiria namna ambavyo raia wanaathirika kutokana na maamuzi yao. Lakini pia amesema kutokana na dunia kukumbwa na majanga kadhaa, viongozi hao wasiyape kipaumbele masuala ya kuwekeana vikwazo, vita, na kuvamiana.

Read More
 CARDI B AMZAWADI OFFSET CHEQUE YA SHILLINGI MILLIONI 226

CARDI B AMZAWADI OFFSET CHEQUE YA SHILLINGI MILLIONI 226

Wakati ukichukulia poa kumbukizi ya kuzaliwa kwa mpenzi wako, huko nchini Marekani rapa Cardi B hakuwa na jambo dogo kwa Baby Daddy wake OffSet , Hitmaker huyo wa “WAP” amemsurprise mume wake Offset kwa cheque nzito ya dollar million 2 za Kimarekani kama zawadi ya Birthday yake ambayo ilikuwa Disemba 14. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa instagram Offset ametoa shukrani za dhati kwa mke wake Cardi B kwa zawadi hiyo ya kitofauti ambayo hakuitegemea, sambamba na kuonyesha mkoba huo pamoja na bei kupitia risiti ya manunuzi. “Wow Asante mpenzi (Cardi B). Mara nyingi unaniletea vitu vya kitofauti nakupenda na nakuheshimu sana”. Aliandika Offset kupitia ukurasa wake wa Instagram. Hii sio mara ya kwanza kwa Cardi B kumpa mumewe zawadi kubwa  kwani mwaka 2020 wakati Offset aliposherehekea kutimiza miaka 29, Cardi B alimsurprise na ndinga kali,aina ya  Lamborghini Aventador SVJ.

Read More
 CARDI B ATANGAZA KUACHIA RASMI ALBUM YAKE MWAKA WA 2022

CARDI B ATANGAZA KUACHIA RASMI ALBUM YAKE MWAKA WA 2022

Rapa Cardi B kutoka Marekani ameendelea kuwa mtu wa ahadi kwa mashabiki wa muziki wake juu ya ujio wa album yake mpya baada ya miaka mitatu sasa. Jana kupitia Instagram LIVE, Cardi B amesema watu watarajie album mpya wakati wowote kuanzia mwaka 2022. Sababu kuu ya kuchelewa kuachiwa kwa album hiyo ni muda, Cardi B amedai kwamba amekuwa na muda finyu ukizingatia kwa sasa ana watoto wawili. Invasion of Privacy ya mwaka 2018 ndio album pekee ambayo Cardi B amewabariki mashabiki zake tangu atie mguu kwenye muziki.

Read More
 KESI YA CARDI B KUWASHUSHIA KICHAPO WAHUDUMU WA CLUB KUSIKILIZWA LEO

KESI YA CARDI B KUWASHUSHIA KICHAPO WAHUDUMU WA CLUB KUSIKILIZWA LEO

Rapa kutoka Marekani Cardi B  yuko hatarini kufungwa miaka minne  jela kufuatia mashtaka mawili yanayomkabili,ya kuwapiga na kuwafanyia fujo wahudumu wawili wa club iitwayo Angels-Strip-Club Mwaka 2018 Cardi B alikamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa makosa hayo mawili lakini mwaka wa 2019 alikanusha kwenye mahakama kuu ya queens akiwa kizimbani kwa kumwambia hakimu kuwa hana hatia Inadaiwa Cardi B alitoa maelekezo kwa wasaidizi wake kuwapiga wahudumu hao wawili wa klabu hiyo  na baadaye yeye pia alishiriki kutembeza kipigo, kurusha viti na kupasua chupa mara baada ya kusikia kuwa mmoja kati yao alitoka kimapenzi na mumewe Offset. Hata hivyo usikilizaji wa kesi hiyo umepangwa kufanya oktoba 25, mwaka huu na endapo rapa huyo atakutwa na hatia ya makosa yote mawili basi kifungo cha miaka minne  jela kitamhusu

Read More
 CARDI B AJIWEKA PEMBENI NA MAMBO YA SIASA, ATAJA CHANZO

CARDI B AJIWEKA PEMBENI NA MAMBO YA SIASA, ATAJA CHANZO

Rapa Cardi B alikuwa anapaza sauti yake kwenye mijadala mbali mbali ya siasa za nchini Marekani, lakini kuna muda alikuwa hasikiki tena na watu kuanza kujiuliza maswali. Akijibu swali hilo ambalo aliulizwa na shabiki mmoja kupitia ukurasa wake wa Twitter, Cardi B amesema aliamua kukaa kimya kutokana na kunyanyaswa na kambi ya chama cha Republican ambacho kilikuwa kinaongozwa na Rais Donald Trump. Lakini pia, alikuwa akipokea ukosoaji mkubwa kutoka kwa watu ambao alikuwa akiwapigania kwenye siasa.

Read More