CAROL KATRUE AMKIA KIFUA MIRACLE BABY KWA KUKIMBIA UJA UZITO
Msanii wa Mugithi Carol Katrue amemkingia kifua mume wake Peter Miracle Baby kwenye sakata la kumpa uja uzito mrembo aitwaye Tash Baby. Kwenye mahojiano na Mungai Eve Katrue amekataa ombi la Tash Baby kutaka mume wake kufanya vipimo vya DNA kuthibitisha kama alizaa nae mtoto kwa kusema kuwa uja uzito wa mrembo huyo sio wa Miracle Baby bali ni wa jamaa aitwaye Lorenzo. Katika hatua nyingine amekanusha tuhuma za Peter Miracle Baby kumtelekeza baba yake mzazi kwa kusema kuwa wazazi wa mume wake huyo wanaisha maisha mazuri, hivyo stori za mwanaume aliyejitokeza juzi kati mtandaoni na kudai ni baba mzazi wa Peter Miracle Baby hazina ukweli wowote. Carol Katrue amesema stori za Baba Mzazi wa msanii huyo kuishi maisha ya taabu zilitungwa na ukurasa mmoja wa udaku kwenye mtandao wa Facebook kwa lengo la kujitafutia umaarufu.
Read More