CAROL KATRUE AMKIA KIFUA MIRACLE BABY KWA KUKIMBIA UJA UZITO

CAROL KATRUE AMKIA KIFUA MIRACLE BABY KWA KUKIMBIA UJA UZITO

Msanii wa Mugithi Carol Katrue amemkingia kifua mume wake Peter Miracle Baby kwenye sakata la kumpa uja uzito mrembo aitwaye Tash Baby. Kwenye mahojiano na Mungai Eve Katrue amekataa ombi la Tash Baby kutaka mume wake kufanya vipimo vya DNA kuthibitisha kama alizaa nae mtoto kwa kusema kuwa uja uzito wa mrembo huyo sio wa Miracle Baby bali ni wa jamaa aitwaye Lorenzo. Katika hatua nyingine amekanusha tuhuma za Peter Miracle Baby kumtelekeza baba yake mzazi kwa kusema kuwa wazazi wa mume wake huyo wanaisha maisha mazuri, hivyo stori za mwanaume aliyejitokeza juzi kati mtandaoni na kudai ni baba mzazi wa Peter Miracle Baby hazina ukweli wowote. Carol Katrue amesema stori za Baba Mzazi wa msanii huyo kuishi maisha ya taabu zilitungwa na ukurasa mmoja wa udaku kwenye mtandao wa Facebook kwa lengo la kujitafutia umaarufu.

Read More
 MKE WA MIRACLE BABY CAROL KATRUE KUMFUNGULIA MASHTAKA BABY MAMA WA MSANII HUYO TASH BABY

MKE WA MIRACLE BABY CAROL KATRUE KUMFUNGULIA MASHTAKA BABY MAMA WA MSANII HUYO TASH BABY

Mke wa msanii Peter Miracle Baby, Carol Katrue amehapa kumfungulia mashataka baby mama wa msanii huyo kwa madai ya kuwakodisha watu wawaribie brand yao. Katika mahojiano yake amesema baby mama huyo aitwaye Tash Baby amekuwa akiwalipa watu wawaribie jina kitu ambacho kimewapelekea kupoteza dili la shillingi millioni 1 kutokana na skendo ambazo zimekuwa zikiwafuata katika siku za hivi karibuni. Kauli ya Carol Katrue imekuja mara baaada ya mrembo aitwaye Bree aliyedai kuwa ana uja uzito wa Peter Miracle Baby kujitokeza kwenye moja ya interview na kudai kuwa alilipwa shilling 3,500 na Tash Baby adanganye kuwa ana uja uzito wa msanii huyo

Read More