Cindy Sanyu Afunguka Kuhusu Mzozo wa Bebe Cool na Eddy Kenzo
Msanii nyota wa Uganda Cindy Sanyu amefunguka kuhusu mzozo unaoendelea kati ya wasanii, Bebe Cool na Eddy Kenzo, ambao wote wako kwenye msafara wa kampeni za Rais Yoweri Museveni. Cindy anasema mvutano huo hauna uhusiano wowote na masuala ya muziki. Kwa mujibu wake, chanzo cha migogoro kati ya wasanii hao wawili ni fedha na hamu ya kuwa karibu zaidi na Rais, kitu ambacho kimeibua ushindani mkali katika kampeni zinazoendelea. Hitmaker huyo wa Boom Party, anasisitiza kuwa mivutano hiyo ni ya muda tu na haitadumu. Anaamini kwamba pindi tu kampeni zitakapofika mwisho, Bebe Cool na Eddy Kenzo watasuluhisha tofauti zao, kwani madai yao hayahusiani na muziki bali mazingira ya kisiasa. Mvutano kati ya Eddy Kenzo na Bebe Cool umekuwa ukiongezeka tangu kampeni zianze mwezi Septemba, huku kila mmoja akipambana kuonekana au kupata nafasi za juu katika majukwaa la kisiasa.
Read More