Cindy Sanyu Avunja Ukimya Kuhusu Pete ya Ndoa

Cindy Sanyu Avunja Ukimya Kuhusu Pete ya Ndoa

Mwanamuziki nyota kutoka Uganda, Cindy Sanyu, hatimaye amejibu tetesi zinazomzunguka kuhusu ndoa yake baada ya kuonekana mara kwa mara bila pete ya ndoa. Cindy, ambaye alifunga ndoa na muigizaji na mwongozaji wa filamu Prynce Joel Okuyo mwezi Desemba 2021, amesisitiza kuwa ndoa yake inaendelea vizuri na haina matatizo kama inavyodaiwa. Kwa mujibu wa Cindy, kutoonekana na pete ya ndoa imetokana na tukio ambapo shabiki mmoja aliichukua pete yake wakati wa mawasiliano ya karibu na mashabiki. Ameeleza kuwa kutovaa pete hiyo kumekuwa chanzo cha dhana potofu kuhusu ndoa yake, lakini ukweli ni kwamba uhusiano wake na mumewe unaendelea vizuri na kustawi. Aidha, amesema aliamua kutoanika hadharani tukio hilo ili kulinda ukaribu wake na mashabiki, akihofia kuwa kulizungumzia kungesababisha mpasuko au umbali na wafuasi wake. Kwa ufafanuzi huu, Cindy amewatoa wasiwasi wafuasi wake akisisitiza kwamba ndoa yake na Prynce Joel Okuyo inaendelea kwa mafanikio licha ya tetesi zilizokuwa zikienea.

Read More
 Cindy Sanyu Kutetea Wanamuziki wa Upinzani kwa Rais Museveni

Cindy Sanyu Kutetea Wanamuziki wa Upinzani kwa Rais Museveni

Rais wa Chama cha Wanamuziki Uganda (UMA), Cindy Sanyu, ametangaza mpango wa kuwasilisha rasmi malalamiko kwa Rais Yoweri Museveni kuhusu changamoto zinazowakumba wanamuziki wanaoamua pia kujihusisha na siasa za upinzani. Cindy amesema kuwa serikali mara nyingi imekuwa ikidhoofisha taaluma ya wasanii wanaoingia katika ulingo wa kisiasa, jambo analoliona kama kikwazo kwa maendeleo ya tasnia ya muziki nchini humo. Kwa mujibu wa mwanamuziki huyo, suala hilo atalibua katika kikao kijacho ambacho viongozi wa UMA wanatarajia kufanya na Rais Museveni. Amesisitiza kuwa hoja yake kuu itakuwa ni kutaka kuwepo na utofauti kati ya taaluma ya muziki na ile ya kisiasa, ili wanamuziki waweze kufanikisha malengo yao bila kudhalilishwa kwa misimamo yao ya kisiasa. Cindy, ambaye ni mmoja wa wanamuziki wakongwe na mashuhuri nchini Uganda, amesema nia yake ni kuhakikisha kuwa muziki hauchukuliwi kama kikwazo kwa yeyote anayeamua kujaribu siasa, bali kila taaluma ipewe heshima yake bila kuathiri nyingine.

Read More
 Cindy Sanyu Asema Hakujua Kuhusu Tamasha la Dax Vibes, Amshauri Aahirishe Kama Ana Hofu

Cindy Sanyu Asema Hakujua Kuhusu Tamasha la Dax Vibes, Amshauri Aahirishe Kama Ana Hofu

Msanii maarufu wa Uganda, Cindy Sanyu, ametoa ufafanuzi kuhusu mgongano wa tarehe za matamasha kati yake na Dax Vibes, akieleza kuwa hakujua kuhusu tamasha lake hadi baada ya kutangaza tarehe ya onyesho lake mwenyewe. Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Cindy amesema hakuwa na nia ya makusudi kupanga tamasha lake siku hiyo, lakini anashauri Dax kuahirisha endapo anaona kushiriki tarehe hiyo ni changamoto.  “Sikujua kuhusu tamasha lake hadi nilipotangaza tarehe yangu. Kama anaogopa kushiriki tarehe hiyo na mimi, anaweza kuahirisha. Si jambo la ushindani,” alisema Cindy. Akiweka wazi uzito wa tukio hilo, Cindy alifichua kuwa tarehe 28 Agosti ina maana kubwa sana kwake kwani si tu siku ya kuzaliwa kwake kwa mara ya 40, bali pia inaadhimisha miaka 26 ya safari yake ya muziki. “Siku hiyo ni ya kihistoria kwangu – ni birthday yangu ya miaka 40 na miaka 26 kwenye muziki. Ni tamasha lenye maana ya kibinafsi sana,” aliongeza. Tofauti hiyo ya tarehe imesababisha gumzo mitandaoni, huku mashabiki wakitoa maoni tofauti. Wengi wamesimama na Cindy kwa msingi wa muda aliokaa kwenye tasnia ya muziki na alama ya mafanikio anayosherehekea. Wengine pia wanatoa wito kwa wasanii hao wawili kuonyesha mshikamano na kusaidiana badala ya kushindana. Kwa sasa, mashabiki wanaendelea kusubiri kuona iwapo Dax Vibes atazingatia ushauri huo au ataendelea na mpango wake wa tamasha katika tarehe ileile.

Read More
 Cindy Sanyu atangaza kurudi kwenye muziki baada ukimya wa miaka miwili

Cindy Sanyu atangaza kurudi kwenye muziki baada ukimya wa miaka miwili

Msanii mkongwe nchini Uganda Cindy Sanyu ametangaza kukamilika kwa likizo ya miaka miwili aliyochukua kwenye muziki wake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha taarifa hiyo kwa kusema kwamba ana mpango wa kuingia studio mwezi ujao kwa ajili ya kurekodi wimbo wake mpya. Hata hivyo amewataka mashabiki zake kupendekeza mada atakayoimba kwenye ngoma yake ijayo ambayo kwa njia moja au nyingine italeta tija kwenye maisha yao. “Naingia studio kurekodi wimbo mpya mwezi ujao. Una mada yoyote unayodhani ninapaswa kuzingatia ambayo itabadilisha maisha yako kama shabiki? #walkwithme,” aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram. Utakumbuka 2021 Cindy alitangaza kuchukua mapumziko mafupi kwenye muziki wake kwa ajili ya kupata muda mzuri wa kukaa na familia yake. Msanii huyo aliahidi mashabiki zake kuwa atarejea kwenye shughuli za kimuziki muda sahihi utakapowadia  na tangu kipindi hicho hajaachia wimbo wowote.

Read More
 Cindy Sanyu aikataa bei ya mapromota kwa wasanii wa Uganda

Cindy Sanyu aikataa bei ya mapromota kwa wasanii wa Uganda

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Cindy Sanyu amepuzilia mbali bei ya kufanya biashara na wasanii iliyotolewa na chama cha mapromota nchini humo akiitaja kuwa batili. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Cindy amewataka wasaniii kutoitikia wito wa mapromota hao wabinafsi huku akiitaka chama cha mapromota nchini Uganda kufanya kazi na wasanii watakaomudu gharama zao. “Kama huwezi kumudu msanii, usimpe kazi. Huwezi kumlazimisha msanii kujishusha kuendana na viwango vyako,” Cindy alisema. Mapema wiki hii Chama Cha Mapromota nchini Uganda (National Promoters Association) walitangaza pesa watakazowalipa wasanii wao kwenye shows mwaka 2023. Chama hicho kilieleza kuwa wamefanya utafiti na wameona umuhimu wa kuweka bei za wasanii wao ili kuendelea kufanya biashara na asiyefurahia malipo ya pesa walizowawekea wamewaruhusu kuandaa shows zao wenyewe.

Read More
 Mume wa Cindy Sanyu akanusha tuhuma za kushindwa kufadhili harusi yao

Mume wa Cindy Sanyu akanusha tuhuma za kushindwa kufadhili harusi yao

Mwanamuziki Cindy Sanyu na mumewe, Prynce Okuyo juzi kati walitimiza mwaka mmoja wakiwa mke na mume baada ya kufanga ndoa mwishoni mwa mwaka 2021. Kufuatia uvumi kuwa Cindy ndiye alifadhili shughuli nzima ya harusi yao, mume wake Prynce Okuyo amejitokeza kwa mara ya kwanza na kukata mizizi ya fitina juu ya madai hayo. Okuyo ameeleza kuwa aliwekeza pesa zake nyingi kwenye harusi yao lakini pia alipokea michango kutoka kwa marafiki wao. “Je, uliona risiti yoyote kutoka kwake akikwambia alifadhili harusi pekee yake. Niliwekeza mamilioni ya pesa kuona hafla hiyo inafanikiwa. Hata marafiki zetu walitoa mchango mkubwa,” alisema katika mahojiano na televisheni moja nchini Uganda. Mpiga picha huyo pia alikanusha tuhuma za kulelewa na Cindy katika ndoa yao kwa kusema kuwa anatekeleza majukumu ya familia kama mume.

Read More
 Cindy ataka kukutana na Rais Yoweri Museveni

Cindy ataka kukutana na Rais Yoweri Museveni

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Cindy Sanyu amedokeza mpango wa kukutana na Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa ajili ya kuzungumzia sheria ya hakimiliki. Mwanamuziki huyo ameeleza kuwa amefanya mikutano na wabunge kuhusu utekelezwaji wa sheria ya hakimiliki lakini jitihada zake hazijazaa matunda yeyote. “Muswada huu ulisainiwa kuwa sheria lakini haujaleta mabadiliko kwenyemuziki. Tunaamini Mheshimiwa Rais atatusaidia kwa sababu tumetembea ofisi mbali mbali lakini ni machache yamefanyika. Tunataka kukutana na Rais mwenyewe,” alisema katika mahojiano na runinga moja nchini uganda. Cindy ni Rais wa Chama cha Wanamuziki Uganda (UMA), bodi inayowaleta pamoja wanamuziki tofauti nchini Uganda.

Read More
 UMA kuhakikisha wasanii nchini Uganda wanazikwa kwa heshima pindi wanapofariki

UMA kuhakikisha wasanii nchini Uganda wanazikwa kwa heshima pindi wanapofariki

Mwanamuziki Cindy Sanyu amedai kuwa chama cha wasanii nchini Uganda UMA itashirikiana na makampuni ya kutoa huduma ya mazishi nchini humo kuhakikisha wasanii wanazikwa kwa heshima pindi wanapofariki. Akizungumza kwenye hafla ya kuwaombea wasanii waliotangulia mbele za haki juzi kati, Cindy amesema wasanii wengi ambao walifariki miaka ya hapo nyuma hawakupokea upendo wa dhati kwenye mazishi yao licha ya kuacha alama kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Lakini pia amewashauri wasanii kujenga tabia ya kuweka akiba kama njia moja ya kuondokana na madeni wakati wa majanga. Miongoni mwa wasanii waliombewa kwenye hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na mastaa mbali mbali ni pamoja na Mowzey Radio, Sera, Martin Angume, Ak-47 na wengine kibao.

Read More
 CINDY SANYU AMKINGIA KIFUA EDDY YAWE KWA TUHUMA ZA KINGONO

CINDY SANYU AMKINGIA KIFUA EDDY YAWE KWA TUHUMA ZA KINGONO

Rais wa chama cha wasanii nchini Uganda Cindy Sanyu amedai kuwa hana uwezo wa kumsaidia msanii chipukizi Sumaiya Sheebah ambaye alidai kuwa alinyanyaswa kijinsia na Eddy Yawe. Cindy amesema mrembo huyo ana ushahidi wowote wa kuonyesha alidhulumiwa kingono na Eddy Yawe kwa kuwa hana mkataba wa kufanya kazi na msanii, hivyo itakuwa vigumu kumsaidia kisheria. Hitmaker huyo wa “Local Man” ametoa changamoto kwa wasanii kuhakikisha wanakuwa na mikataba ya kufanya kazi na wasanii wenzao kama njia ya kuwasaidia kisheria wakati wa matatizo. Utakumbuka juzi kati msanii chipukizi Sumaiya Sheebah aliibua madai kuwa Eddy Yawe amekuwa akimuitisha rushwa ya ngono ili waweze kufanya kazi ya pamoja, shutuma ambazo bosi huyo wa Dream Studios alikanusha vikali kwa kusema kwamba madai ya mrembo huyo hayana ukweli wowote kwani ni njia ya kuichafua brand yake ya muziki.

Read More
 CINDY SANYU AFUNGUKA KUHUSU KUSUSIA SHOW DUBAI

CINDY SANYU AFUNGUKA KUHUSU KUSUSIA SHOW DUBAI

Msanii nyota nchini Uganda Cindy Sanyu amefunguka sababu za kususia show yake nchini Dubai wikiendi iliyopita. Katika mahojiano yake Cindy amesema promota wa show hiyo aliingiwa na jeuri baada ya kushindwa kukamilisha malipo yake kabla ya kuingia jukwani kutumbuiza, jambo ambalo anadai lilimfanya kukataa kufanya performance yake. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Boom Party” ametoa changamoto kwa mapromota kuhakikisha wana pesa za kutosha kabla ya kuwapa wasanii mialiko ya kutumbuiza kwa show zao kwa sio kitendo cha kingwana kwa msanii kutumbuiza bila ys kulipwa haki yake. Hata hivyo amewaomba radhi mashabiki zake wa Dubai msamaha kwa kutotokea kwenye show yake kutokana mgogoro uliobuka kati yake na promota wa onesho hilo.

Read More
 CINDY SANYU AJITAPA NA UTAJIRI WAKE “MIMI KUFULIA? WATASUBIRI!

CINDY SANYU AJITAPA NA UTAJIRI WAKE “MIMI KUFULIA? WATASUBIRI!

Mwanamuziki kutoka Uganda  Cindy Sanyu amewajibu baadhi ya watu wanaodai kuwa anawania urais wa chama cha wanamuziki nchini humo kwa ajili ya kupata pesa. Katika kikao na wanahabari Cindy amesema ana utajiri mkubwa ambao aliupata kipindi anafanya kazi na makampuni mbali mbali. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Local Man” amesema lengo lake kuwania urais wa chama cha uma ni kuboresha tasnia ya muziki kwa faida ya vizazi vijavyo. Hata hivyo amesema hajawahi pokea mshahara wowote tangu akuwe rais wa chama cha wanamuziki nchini Uganda.

Read More
 BEBE COOL ABADILI MAWAZO DHIDI YA CINDY SANYU, AMUUNGA MKONO KUTWAA UONGOZI WA CHAMA CHA UMA

BEBE COOL ABADILI MAWAZO DHIDI YA CINDY SANYU, AMUUNGA MKONO KUTWAA UONGOZI WA CHAMA CHA UMA

Staa wa muziki kutoka nchini Uganda Bebe Cool ametangaza hadharani kumuunga mkono Cindy Sanyu kwenye azma yake ya kuongoza chama cha wanamuziki nchini humo licha ya kumkosoa kipindi cha nyuma. Katika mkao na wanahabari Bebe Cool amesema Cindy ndiye anafaaa kuwasimamia wasanii kwa kuwa ana uwezo mkubwa wa kushawishi wadau wa maendeleo pamoja na serikali kutoa pesa za kufadhilia miradi ya muziki lakini pia anazungumza lugha ya kiingereza kwa ufasaha tofauti na mpnzani wake King Saha. Hitmaker huyo “Gyenvudde” amesema Cindy ni kiongozi dhabiti asiye terereka na changamoto zozote ikizingatiwa kuwa kipindi cha corona alisimama kidete kuwatetea wasanii licha ya viongozi wengi wa wanamuziki nchini Uganda kukimbia majukumu yao. Kauli ya Bebe Cool imekuja mara baada ya kumkosoa cindy sanyu mwezi mmoja uliopita kwa kudai kuwa msanii huyo ana roho ya kulipiza kisasi lakini pia ana uwezo wa kustahimili ukosoaji kutoka kwa wapinzani kwa kuwa ni mtu mwenye hasira. Madai hayo ya Bebe Cool yalimuibua Cindy Sanyu na kusema kwamba ataanza mchakato wa kuwaomba msamaha wasanii wote aliowakosea kipindi cha nyuma kama njia moja ya kupata uungwaji kutoka kwa wanamuziki ambao wanapinga azma yake ya kutwaa uongozi wa urais katika chama cha wanamuziki  nchini Uganda.

Read More