CINDY SANYU ATAJA CHANZO CHA MIGAWANYIKO MIONGONI MWA WASANII UGANDA

CINDY SANYU ATAJA CHANZO CHA MIGAWANYIKO MIONGONI MWA WASANII UGANDA

Nyota wa muziki kutoka nchini Uganda Cindy Sanyu amefunguka chanzo cha migawanyiko miongoni mwa wasanii nchini humo. Katika mahojiano yake hivi karibuni, Cindy amesema siasa imesabaratisha juhudi za kuunganisha wasanii nchini Uganda kwa kuwa baadhi ya wasanii wanafanya maamuzi yao kulingana na itakadi za kisiasa ya vyama wanavyoshabikia. Hata hivyo amesema licha ya yeye kuweka mikakati ya kuwaleta wasanii pamoja kupitia muungano wa UMA, imekuwa vigumu kwake kufanikisha jambo hilo kutokana na siasa, jambo ambalo amedai ni changamoto ambayo alikumbana kipindi anahudumu kama rais wa muungano huo. Cindy Sanyu atachuana na King Saha, Maurice Kirya kwenye kinyanganyiro cha kugombea urais wa muungano wa wasanii nchini uganda kwenye uchaguzi utakaofanyika hivi karibuni.

Read More
 CINDY SANYU MBIONI KUWAOMBA MSAMAHA WASANII ALIOWAKOSEA KIPINDI CHA NYUMA

CINDY SANYU MBIONI KUWAOMBA MSAMAHA WASANII ALIOWAKOSEA KIPINDI CHA NYUMA

Staa wa muziki nchini Uganda Cindy Sanyu ameweka wazi matamanio ya kumaliza tofauti zake na wasanii wanaohisi kuwa ana ubaya nao mara baada ya Bebe Cool kudai kwamba msanii huyo ni dikteta. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Cindy Sanyu amesema yeye sio dikteta kama jinsi ambavyo baadhi ya wasanii wanamchukulia ila mwaka jana alihamua kuwakandia wasanii waliokuwa wanamshambulia sana kutokana na utendekazi wake katika muungano wa wanamuziki nchini Uganda. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Local Man” amedai kuwa kabla hajateuliwa kuwa rais wa muungano huo kwa mara pili ana mpango wa kuomba msamaha wasanii wote aliwakosoa kipindi cha nyuma. Cindy ambaye anachuana na King Saha, Maurice Kirya pamoja na Daddy Andre kwenye wadhfa wa urais katika muungano wa wanamuziki ametoa wito kwa wanachama wa muungano huo kumpa kura zao kwenye uchaguzi ujao ili aweze kufanikisha mikakati aliyoanzisha kipindi anahudumu kama rais.

Read More
 CINDY SANYU AWACHANA WASANII WALIOTIA NIA YA KUGOMBEA URAIS WA MUUNGANO WA WANAMUZIKI UGANDA

CINDY SANYU AWACHANA WASANII WALIOTIA NIA YA KUGOMBEA URAIS WA MUUNGANO WA WANAMUZIKI UGANDA

Nyota wa muziki nchini Uganda Cindy Sanyu amewatolea uvivu wasanii ambao wametia nia ya kugombea wadhfa wa urais wa muungano wa wanamuziki nchini humo kwenye uchaguzi ambao utafanyika hivi karibuni. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Cindy ambaye kwa sasa ni rais wa muungano wa wanamuziki nchini Uganda amesema wasanii hao hawana vigezo vya kuongoza muungano huo na badala yake wamuachie nafasi akamilishe baadhi ya miradi ambayo alianzisha akiwa afisini kwa manufaa ya wanamuziki wote. Kauli ya Cindy imekuja mara baada ya kuchukua na kujaza fomu ya kumuidhinisha kugombea tena wadhfa wa urais wa muungano wa wanamuziki nchini Uganda mapema wiki hii. Utakumbuka wasanii kama Daddy Andre na King Saha wametangaza kuwania urais wa muungano wa wanamuziki nchini Uganda na sasa watachuana na cindy sanyu ambaye pia ametia nia ya kutetea wadhfa wake kwa mara ya pili.

Read More
 MUUNGANO WA WANAMUZUKI UGANDA KUFANYA UCHAGUZI KWA NJIA YA MTANDAO

MUUNGANO WA WANAMUZUKI UGANDA KUFANYA UCHAGUZI KWA NJIA YA MTANDAO

Muungano wa wanamuziki nchini Uganda ambao unajiandaa kufanya uchaguzi wa kuwachagua viongozi wapya mwezi huu wa Aprili umesema utafanya uchaguzi huo kwa njia ya mtandao. Katika mahojiano yake hivi karibuni Rais wa Muungano huo Cindy Sanyu amesema wamechukua hatua hiyo kwa sababu hawana fedha za kutosha kufanya uchaguzi kwa mfumo wa kawaida ambao unatoa nafasi kwa wanachama wao kupiga kura moja kwa moja kwa kujiwasilisha wenye kwenye vituo vya kupigia kura. “Fedha nyingi inahitajika kuandaa uchaguzi kwa njia ya kawaida na kwa sasa hatuna pesa za kutosha,” alisema Cindy. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Local Man” amesema muungano wa wanamuziki nchini Uganda umekosolea vibaya na wasanii kwa hatua yake ya kuendesha uchaguzi kwa njia ya mtandao huku akieleza kuwa wana mpango wa kuandaa uchaguzi wa kawaida kama watapata pesa kutoka kwa wahisani. “Ndio nafahamu watu wengi wanachukulia kupiga kura mtandaoni sio sahihi ila ndio njia pekee ambayo tuko nayo kwa sasa. Lakini ikitokea tumepata pesa kutoka kwa hisani na washirika wengine wa maendeleo, tutafanya uchaguzi kwa njia ya kawaida,” aliongeza Cindy. Cindy Sanyu alichaguliwa kuwa rais wa muungano wa wanamuziki nchini Uganda mwezi Machi mwaka wa 2021 kujaza nafasi ya Ykee Benda ambaye alijiuzulu. Utakumbuka Ykee Benda alichukua nafasi ya Sophie Gombya ambaye alijiuzulu pia na kujiunga na siasa.

Read More
 CINDY SANYU AREJELEA MAJUKUMU YAKE KAMA RAIS WA MUUNGANO WA WASANII UGANDA BAADA YA LIKIZO FUPI

CINDY SANYU AREJELEA MAJUKUMU YAKE KAMA RAIS WA MUUNGANO WA WASANII UGANDA BAADA YA LIKIZO FUPI

Staa wa muziki nchini Uganda Cindy Sanyu ametangaza rasmi kurejea kwenye majukumu yake kama rais wa chama cha wanamuziki nchini humo baada ya kuchukua mapumziko mafupi. Kupitia ukurasa wake amepost picha akiwa katika afisi za chama cha wasanii nchini uganda UMA huku akidokeza kuwa yupo tayari kwa ajili ya kuwasimamia wasanii na pia kuweka mikakati ya kuandaa uchaguzi wa chama hicho mwaka huu. Kauli ya Cindy imekuja mara baada ya kukamilisha likizo aliyochukua kwa ajili kumlea mtoto wake aliyepata mwaka huu na mume wake Joel Atiku. Utakumbukwa kabla miezi miwilli kabla ya kujifungua Cindy Sanyu aliruhusiwa kuchukua likizo fupi kama rais wa chama cha wasanii nchini uganda jambo ambalo lilimpelekea kusitisha kufanya shows kama njia ya kujiandaa kumpokea mtoto wake.

Read More