Daddy Awashauri Wanaume Kutoziweka Hisia Zote kwa Wanawake

Daddy Awashauri Wanaume Kutoziweka Hisia Zote kwa Wanawake

Mwanamuziki wa Injili, Daddy Owen, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kutoa ushauri mkali kwa wanaume kuhusu namna wanavyopaswa kujihusisha kimapenzi na wanawake. Kupitia mitandao ya kijamii, Daddy Owen amewataka wanaume kutoziweka hisia zao zote kwa wanawake, akisema kufanya hivyo kunawafanya kuwa rahisi kudhibitiwa kihisia. Kwa mujibu wa ujumbe wake, wanaume wanaoweka mapenzi na hisia zao bila mipaka hujikuta wakitumia nguvu nyingi kupenda kuliko wanavyopendwa, hali ambayo huweza kuwafanya kuumizwa kwa urahisi. Msanii huyo, ameonya kuwa baadhi ya wanawake hutumia mapungufu hayo kama njia ya kuwapata na kuwadhibiti wanaume katika mahusiano. Kauli hiyo imezua mijadala mikubwa mtandaoni, baadhi ya watu wakikubaliana naye wakisema wanaume wengi huwa wanapoteza uthabiti wao pale wanapopenda kupita kiasi, huku wengine wakimkosoa kwa madai kuwa maoni yake yanachochea mgawanyiko katika mahusiano.

Read More
 Daddy Owen Awataka Wasanii Kuwajibika Baada ya Diamond Kufuta Picha za Kisiasa

Daddy Owen Awataka Wasanii Kuwajibika Baada ya Diamond Kufuta Picha za Kisiasa

Msanii wa muziki wa injili nchini Kenya, Daddy Owen, ametoa wito kwa wasanii barani Afrika kuwa na uwajibikaji mkubwa katika misimamo yao ya kijamii na kisiasa, akisisitiza umuhimu wa kusimama na wananchi badala ya mifumo ya kisiasa. Kupitia Instagram, Daddy Owen amesema kuwa tukio la Diamond kufuta machapisho ya kisiasa ni funzo kwa wasanii na watu mashuhuri kutambua kuwa sauti zao zina ushawishi mkubwa kwa jamii, hivyo ni muhimu kuzingatia misimamo yenye heshima na inayowakilisha ukweli wa wananchi. Ameongeza kuwa wasanii hawapaswi kutumia majukwaa yao kuunga mkono mamlaka bila kusikiliza hisia na matakwa ya mashabiki wao. Kwa mujibu wa Daddy Owen, jukumu la msanii ni kuleta matumaini, amani na mshikamano, si kugawanya jamii kupitia misimamo ya kisiasa. Kauli hiyo imekuja kufuatia hatua ya msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz, kufuta picha na video zote alizokuwa ameweka mtandaoni akimuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, baada ya wananchi nchini humo kupinga matokeo ya uchaguzi uliomalizika juzi na kuzua maandamano makubwa.

Read More
 Daddy Owen Aguswa na Video ya Raila Akiimba Jamaica Farewell

Daddy Owen Aguswa na Video ya Raila Akiimba Jamaica Farewell

Msanii wa nyimbo za injili, Daddy Owen, amefunguka namna kifo cha Raila Amollo Odinga kilivyomgusa baada ya kuona video inayomuonyesha kiongozi huyo akiimba wimbo wa “Jamaica Farewell” wa Harry Belafonte. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Daddy Owen amesema alipoamka asubuhi na kukutana na video hiyo, alihisi kuguswa kwa kina na mara moja akaingia YouTube kusikiliza wimbo huo mzima. Amesema alipofika kwenye sehemu ya maoni, aligundua kuwa karibu asilimia tisini ya maoni yalikuwa kutoka kwa Wakenya waliokuwa wakitoa heshima zao kwa Raila. Msanii huyo amesema tukio hilo lilimfanya kutafakari jinsi muziki unavyounganisha watu na kuvuka vizazi. Ameeleza kuwa ingawa wimbo huo ni wa miaka mingi iliyopita, umepata umaarufu upya miongoni mwa Wakenya kutokana na mapenzi ya Raila kwa muziki. Daddy Owen ametumia tukio hilo kutoa wito kwa wasanii chipukizi kutokata tamaa katika safari yao ya muziki, akisema muziki ni chombo chenye nguvu ya kuleta mabadiliko na kuishi hata baada ya msanii kuondoka duniani. Hata hivyo amehitimisha ujumbe wake kwa kusema kwamba Raila ataendelea kukumbukwa kama kiongozi aliyethamini sanaa na aliyetumia maisha yake kuleta matumaini na mshikamano miongoni mwa watu.

Read More
 Daddy Owen Afunguka Kuhusu Tukio Lililomvunja Moyo Akiwa Kwenye Kilele cha Umaarufu

Daddy Owen Afunguka Kuhusu Tukio Lililomvunja Moyo Akiwa Kwenye Kilele cha Umaarufu

Msanii wa nyimbo za injili nchini Kenya, Daddy Owen, amesimulia kisa cha kusikitisha alichowahi kupitia akiwa kwenye kilele cha umaarufu kisanaa. Akiwa kwenye mahojiano hivi karibuni, Owen ameeleza jinsi alivyokuwa amialikwa kutumbuiza katika shule moja ya wasichana, lakini aliposhika jukwaa, wanafunzi wote walitoka ukumbini na kumwacha peke yake. Tukio hilo lilisababishwa na tetesi zilizokuwa zikienea wakati huo zikimhusisha na ibada za kishetani. Daddy Owen amesema kitendo hicho kilimuumiza, lakini kilimjenga na kumpa moyo wa kuendelea na huduma yake ya injili kupitia muziki. Ameongeza kuwa changamoto kama hizo ni sehemu ya safari ya imani na sanaa, akisisitiza umuhimu wa kusimama imara licha ya madai ya uongo. Kisa hicho kilitokea wakati msanii huyo alikuwa kwenye kilele cha muziki wake, ambapo vibao vyake maarufu kama System ya Kapungala na Tobina vilikuwa vikivuma sana na kumpa umaarufu mkubwa nchini. Licha ya changamoto hizo, Daddy Owen ameendelea kung’ara kama mmoja wa wanamuziki wa injili wenye ushawishi mkubwa nchini, akiwa na nyimbo nyingi zenye ujumbe wa matumaini na uvumilivu.

Read More
 Daddy Owen: “Ni Rahisi Kukubali Kifo Kuliko Talaka”

Daddy Owen: “Ni Rahisi Kukubali Kifo Kuliko Talaka”

Msanii wa nyimbo za injili Daddy Owen ameibua mjadala baada ya kutoa kauli yenye kugusa hisia kuhusu ndoa na changamoto za talaka. Akizungumza kwenye mahojiano, msanii huyo amesema kuwa kwa mtazamo wake, ni rahisi zaidi mtu kukubali kifo cha mpendwa wake kuliko kukabiliana na talaka, hasa pale ambapo kuna watoto. Kwa mujibu wa Daddy Owen, talaka huacha jeraha refu kwa sababu yule uliyeachana naye ataendelea kuwepo kwenye maisha yako kupitia majukumu ya malezi. Msanii huyo ameongeza kuwa hali huwa ngumu zaidi endapo bado kuna hisia za kimapenzi kwa mtu huyo, jambo linalomfanya aliyeachika kupata wakati mgumu zaidi kisaikolojia na kihisia. Kauli hiyo imepokelewa kwa mitazamo tofauti miongoni mwa mashabiki na wafuasi wake. Wapo waliomuunga mkono wakisema imani na uzoefu wake unaonyesha uhalisia wa maisha ya kifamilia, huku wengine wakihisi kuwa kulinganisha kifo na talaka ni jambo zito na tata. Daddy Owen amekuwa wazi mara kadhaa kuhusu changamoto za maisha yake ya kifamilia na imani yake katika dini, na mara nyingi hutumia hadithi zake binafsi kutoa mafunzo kwa jamii.

Read More
 Daddy Owen Atoa Ushauri kwa Wanaume: “Usioe kwa Sababu ya Mapenzi, Oa kwa Sababu ya Kusudi”

Daddy Owen Atoa Ushauri kwa Wanaume: “Usioe kwa Sababu ya Mapenzi, Oa kwa Sababu ya Kusudi”

Msanii wa Injili nchini Kenya, Daddy Owen, ameibua mjadala mkubwa mtandaoni baada ya kutoa ushauri kwa wanaume kuhusu ndoa, akisisitiza kuwa msingi wa ndoa haupaswi kuwa mapenzi pekee, bali kuelewa kusudi la maisha. Kupitia chapisho lake la Instagram, msanii huyo alisema: “Kama mwanaume, usioe kwa sababu ya mapenzi. Oa kwa sababu ya kusudi. Nilifikiri ndoa ni kuhusu mapenzi, kumbe sio.” Msanii huyo alifafanua kauli yake kwa kusema kuwa wanaume wengi huingia kwenye ndoa wakiwa hawajajitambua wala kuelewa malengo yao ya maisha, hali inayochangia migogoro na kuvunjika kwa ndoa. “Kama kusudi lako halijajulikana, hiyo ni kama mabomu yanayosubiri kulipuka. Wanaume huoa chini ya kiwango chao kwa sababu hawajajua walipoelekea. Ukijua kusudi lako, mwanamke atajivuta kwenye hilo kusudi,” aliongeza. Kauli hii imepokewa kwa hisia tofauti kutoka kwa mashabiki wake, baadhi wakimsifu kwa mtazamo wa kiroho na msingi wa maisha yenye maono, huku wengine wakitofautiana naye, wakisema mapenzi bado yana nafasi kubwa katika ndoa yenye mafanikio. Daddy Owen, ambaye amepitia changamoto katika maisha yake ya ndoa hapo awali, anaonekana kutumia uzoefu wake kuwashauri vijana wanaopanga kuoa, akisisitiza umuhimu wa kujitambua kabla ya kuingia katika hatua hiyo muhimu ya maisha. Ujumbe wake umeendelea kuvutia mijadala kuhusu maana ya ndoa katika kizazi cha sasa, na umuhimu wa kuwa na msingi imara wa maisha kabla ya kuchukua jukumu la kifamilia.

Read More
 Daddy Owen akanusha kutoka kimapenzi na shabiki yake

Daddy Owen akanusha kutoka kimapenzi na shabiki yake

Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini Daddy Owen amekanusha madai ya kutoka kimapenzi na rafiki wake wa karibu Eve Maina. Kupitia instastory yake amesema hana uhusiano wowote wa kimapenzi na mrembo huyo huku akisema ukaribu wao ni wa kirafiki. Msanii huyo ambaye kipindi cha nyuma alitangaza kuwa anatafuta mke,amesema hatokuja kuweka wazi mahusiano yake kwa umma mtandaoni. “Hapo sijui, but ata kama nitaoa tena I would wish for something very very private,”Aliandika Kauli ya Daddy Owen inakuja mara baada ya shabiki kumuuliza kama anachumbiana na mrembo huyo.

Read More
 Daddy Owen akiri kutoshiriki tendo la ndoa kwa miaka miwili

Daddy Owen akiri kutoshiriki tendo la ndoa kwa miaka miwili

Mwimbaji wa nyimbo za Injili , Daddy Owen amefichua kuwa hajashiriki tendo la ndoa kwa miaka miwili. Katika mahojiano yake hivi karibuni, Owen amesema kuwa hajakuwa na hamu ya kufanya mapenzi tangu alipoachana na mke wake. “Sihitaji mwanamke, sijafanya mapenzi kwa miaka miwili, mwanamke ni wa kazi gani?” Owen alisema. Kauli yake imekuja mara baada ya kukiri kuwa hataki mwanamke kwenye maisha yake tena ikizingatiwa kuwa wiki kadhaa ilyopita alitangaza kuwa anatafuta mke. “Sitaki hata kupikiwa, nitakula hotelini, hata wageni wakija nyumbani kwangu tutanunua chakula, sitaki kuoa tena,” mwimbaji huyo alisema. Alisema kuwa ameridhika na maisha yake ya sasa na hatafuti mke wa kuoa kwani ana mambo mengi ya msingi ya kufanya. “Kwa sasa nafanya mambo mengi, sitafuti tena mke. Nitafute mke wa nini? Kama ni mtoto ninaye tayari, si bora kuwa na mtoto,” Owen alisema. Utakumbuka Daddy Owen na mkewe Farida Wambui walitengana mwaka 2020 baada ya kuwa kwenye ndoa kwa kipindi cha miaka minne.

Read More
 Daddy Owen aahirisha hafla yake ya kila mwaka ya Malaika Disability Walk.

Daddy Owen aahirisha hafla yake ya kila mwaka ya Malaika Disability Walk.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Daddy Owen ameahirisha hafla yake ya kila mwaka ya Malaika Disability walk ambayo ilipangwa kufanyika tarehe 3 Desemba mwaka huu. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Owen alisema matembezi hayo hayatafanyika kutokana na kifo cha kusikitisha cha binamu yake Stephen Sunrise Osedo ambaye atazikwa siku hiyo, hivyo wamelazimika kusogeza mbele hadi Machi 4 mwaka 2023. “Kutokana na mazingira yasiyoepukika, tulilazimika kuahirisha MATEMBEZI YA WALEMAVU YA MALAIKA 2022 ambayo yalipangwa kufanyika tarehe 3 Desemba ambayo ni SIKU YA WALEMAVU DUNIANI! Mazishi yatakuwa tarehe hiyo hiyo (tarehe 3 Desemba)” “”Wakati huo huo shule nyingi za Msingi zimeomba ushiriki wa MATEMBEZI, hivyo tumebadilisha tarehe kuwa MACHI 4, 2023. Tunaomba msaada wenu kikamilifu na tunaomba radhi kwa wadau wote waliokuwa wamejitokeza kutuunga mkono.#MalaikaDisabilityWalk2023.”, Aliandika. Binamu yake Owen aliuawa kwa kupigwa risasi na afisa wa polisi huko Umoja, kaunti ya Nairobi wiki mbili zilizopita. Daddy Owen alianzisha hafla ya Malaika mwaka 2012 kwa lengo la kutambua mchango wa watu wenye changamoto ya ulemavu katika jamii.

Read More
 Daddy akanusha madai ya kutumia vyombo vya habari kutafuta mke

Daddy akanusha madai ya kutumia vyombo vya habari kutafuta mke

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini daddy owen amekanusha madai yanayotembea mtandaoni kuwa anatafuta mwanamke wa kuingia naye kwenye ndoa ikiwa ni siku chache zimepita toka alipoweka wazi vigezo anavyohitaji kutoka kwa mwanamke wà ndoto yake. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Daddy Owen amesema kauli yake ilinukuliwa vibaya na walimwengu huku akisema kama kweli angekuwa anatafuta mke angefanya hivyo bila kuwafahamishw watu ikingatiwa kuwa yeye bado ni mwanaume rijali ambaye ana uwezo mkubwa wa kutongoza mwanamke. Hitmaker huyo wa Vanity amewataka walimwengu kuacha kueneza propaganda mtandaoni kuwa anatafuta mke wa kuoa na badala yake wamuunge mkono kwenye muziki wake kwani ikitokea kuwa ameingia kwenye mahusiano ataweka wazi kwa mashabiki zake. Kauli ya Daddy Owen imekuja mara baada ya kuzua gumzo mtandaoni kuwa anatafuta mwanamke ambaye anatoka mashinani, na mcha mungu ili aweze kuingia naye kwenye ndoa ambapo alienda mbali zaidi na kuwataka wadada ambao wanatamani kutokana nae kimapenzi kutuma maombi kupitia mitandao yake ya kijamii.

Read More
 Pritty Vishy akata tamaa kwenye penzi la Daddy Owen.

Pritty Vishy akata tamaa kwenye penzi la Daddy Owen.

Mrembo asiyeishiwa na matukio kila leo Pritty Vishy amekata tamaa kwenye penzi la Daddy Owen ikiwa ni siku chache zimepita toka mwimbaji huyo wa injili amkatae hadharani. Mrembo huyo ambaye kwa wakati mmoja aliwahi kuwa penzini na msanii Stivo Simple Boy amemtaja Daddy Owen kama dikteta asiyekuwa na msimamo mara baada ya kusisitiza kuwa mwanamke wa ndoto yake lazima ajue kuzungumza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha lakini pia asiwe mtumiaji wa mtandao wa Tiktok. Hata hivyo amemalizia kwa kumshauri hitmaker huyo wa Vanity kutimukia nchini Uganda iwapo anataka kufanikisha mchakato wa kupata mke wa kuingia naye kwenye ndoa kwani wasichana wa Kenya hawana ufasaha wa lugha ya Kiingereza. “Nilikua namtaka lakini sasa penye inaelekea ni kama itabidi avuke Uganda. He’s like a dictator. Sijui hataki dem ako TikTok, anataka dem anajua Kizungu mingi. Ikifika mahali ya TikTok na Kizungu mingi avuke tu Uganda. Hapa Kenya tuko TikTok na tunaongea Kizungu ya kilami. Ugandans ndio wako bushy,” Alisema. Utakumbuka mara baada ya Daddy Owen kutangaza kuwa anatafuta mke wa kuingia naye kwenye ndoa mapema wiki iliyopita, amepokea zaidi ya maombi 10,000 kutoka kwa wanadada tofauti ambao wametia nia ya kumtaka kimahusiano.

Read More
 DADDY OWEN AWASHAURI MASTAA KUACHA KUISHI MAISHA YA KUIGIZA MTANDAONI

DADDY OWEN AWASHAURI MASTAA KUACHA KUISHI MAISHA YA KUIGIZA MTANDAONI

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Daddy Owen amewashauri mastaa kurudisha mkono kwa jamii kwa kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji. Kupitia instagram Daddy Owen amesema hatua hiyo itawapa motisha wakenya kuwasaidia wakati matatizo badala ya kuisha maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii. Hitmaker huyo wa Yahweh amesema kipindi alijipata kwenye matatizo hakuna staa hata mmoja alijitokeza kumsaidia ila anamshukuru mungu mashabiki zake ndio walikuwa mstari wa mbele kumshika mkono hadi akarudi katika hali yake ya kawaida. Daddy Owen ametoa kauli hiyo akijibu swali la mchekeshaji Creative Terrence ambaye alitaka kufahamu ni kitu gani inawafanya wakenya kutowasaidii mastaa mbali mbali nchini wakati wana changamoto katika maisha. Swali la Terrence liliibua hisia mseto miongoni mwa wakenya mtandaoni ambao wamehoji kuwa wasanii wanaishi maisha ya kifahari kwenye mitandao ya kijamii jambo limewafanya wengi wake kutoamini kama kweli huwa wanapata maishani.

Read More