Daddy Owen Afunguka Kuhusu Tukio Lililomvunja Moyo Akiwa Kwenye Kilele cha Umaarufu

Daddy Owen Afunguka Kuhusu Tukio Lililomvunja Moyo Akiwa Kwenye Kilele cha Umaarufu

Msanii wa nyimbo za injili nchini Kenya, Daddy Owen, amesimulia kisa cha kusikitisha alichowahi kupitia akiwa kwenye kilele cha umaarufu kisanaa. Akiwa kwenye mahojiano hivi karibuni, Owen ameeleza jinsi alivyokuwa amialikwa kutumbuiza katika shule moja ya wasichana, lakini aliposhika jukwaa, wanafunzi wote walitoka ukumbini na kumwacha peke yake. Tukio hilo lilisababishwa na tetesi zilizokuwa zikienea wakati huo zikimhusisha na ibada za kishetani. Daddy Owen amesema kitendo hicho kilimuumiza, lakini kilimjenga na kumpa moyo wa kuendelea na huduma yake ya injili kupitia muziki. Ameongeza kuwa changamoto kama hizo ni sehemu ya safari ya imani na sanaa, akisisitiza umuhimu wa kusimama imara licha ya madai ya uongo. Kisa hicho kilitokea wakati msanii huyo alikuwa kwenye kilele cha muziki wake, ambapo vibao vyake maarufu kama System ya Kapungala na Tobina vilikuwa vikivuma sana na kumpa umaarufu mkubwa nchini. Licha ya changamoto hizo, Daddy Owen ameendelea kung’ara kama mmoja wa wanamuziki wa injili wenye ushawishi mkubwa nchini, akiwa na nyimbo nyingi zenye ujumbe wa matumaini na uvumilivu.

Read More
 Daddy Owen: “Ni Rahisi Kukubali Kifo Kuliko Talaka”

Daddy Owen: “Ni Rahisi Kukubali Kifo Kuliko Talaka”

Msanii wa nyimbo za injili Daddy Owen ameibua mjadala baada ya kutoa kauli yenye kugusa hisia kuhusu ndoa na changamoto za talaka. Akizungumza kwenye mahojiano, msanii huyo amesema kuwa kwa mtazamo wake, ni rahisi zaidi mtu kukubali kifo cha mpendwa wake kuliko kukabiliana na talaka, hasa pale ambapo kuna watoto. Kwa mujibu wa Daddy Owen, talaka huacha jeraha refu kwa sababu yule uliyeachana naye ataendelea kuwepo kwenye maisha yako kupitia majukumu ya malezi. Msanii huyo ameongeza kuwa hali huwa ngumu zaidi endapo bado kuna hisia za kimapenzi kwa mtu huyo, jambo linalomfanya aliyeachika kupata wakati mgumu zaidi kisaikolojia na kihisia. Kauli hiyo imepokelewa kwa mitazamo tofauti miongoni mwa mashabiki na wafuasi wake. Wapo waliomuunga mkono wakisema imani na uzoefu wake unaonyesha uhalisia wa maisha ya kifamilia, huku wengine wakihisi kuwa kulinganisha kifo na talaka ni jambo zito na tata. Daddy Owen amekuwa wazi mara kadhaa kuhusu changamoto za maisha yake ya kifamilia na imani yake katika dini, na mara nyingi hutumia hadithi zake binafsi kutoa mafunzo kwa jamii.

Read More
 Daddy Owen Atoa Ushauri kwa Wanaume: “Usioe kwa Sababu ya Mapenzi, Oa kwa Sababu ya Kusudi”

Daddy Owen Atoa Ushauri kwa Wanaume: “Usioe kwa Sababu ya Mapenzi, Oa kwa Sababu ya Kusudi”

Msanii wa Injili nchini Kenya, Daddy Owen, ameibua mjadala mkubwa mtandaoni baada ya kutoa ushauri kwa wanaume kuhusu ndoa, akisisitiza kuwa msingi wa ndoa haupaswi kuwa mapenzi pekee, bali kuelewa kusudi la maisha. Kupitia chapisho lake la Instagram, msanii huyo alisema: “Kama mwanaume, usioe kwa sababu ya mapenzi. Oa kwa sababu ya kusudi. Nilifikiri ndoa ni kuhusu mapenzi, kumbe sio.” Msanii huyo alifafanua kauli yake kwa kusema kuwa wanaume wengi huingia kwenye ndoa wakiwa hawajajitambua wala kuelewa malengo yao ya maisha, hali inayochangia migogoro na kuvunjika kwa ndoa. “Kama kusudi lako halijajulikana, hiyo ni kama mabomu yanayosubiri kulipuka. Wanaume huoa chini ya kiwango chao kwa sababu hawajajua walipoelekea. Ukijua kusudi lako, mwanamke atajivuta kwenye hilo kusudi,” aliongeza. Kauli hii imepokewa kwa hisia tofauti kutoka kwa mashabiki wake, baadhi wakimsifu kwa mtazamo wa kiroho na msingi wa maisha yenye maono, huku wengine wakitofautiana naye, wakisema mapenzi bado yana nafasi kubwa katika ndoa yenye mafanikio. Daddy Owen, ambaye amepitia changamoto katika maisha yake ya ndoa hapo awali, anaonekana kutumia uzoefu wake kuwashauri vijana wanaopanga kuoa, akisisitiza umuhimu wa kujitambua kabla ya kuingia katika hatua hiyo muhimu ya maisha. Ujumbe wake umeendelea kuvutia mijadala kuhusu maana ya ndoa katika kizazi cha sasa, na umuhimu wa kuwa na msingi imara wa maisha kabla ya kuchukua jukumu la kifamilia.

Read More
 Daddy Owen akanusha kutoka kimapenzi na shabiki yake

Daddy Owen akanusha kutoka kimapenzi na shabiki yake

Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini Daddy Owen amekanusha madai ya kutoka kimapenzi na rafiki wake wa karibu Eve Maina. Kupitia instastory yake amesema hana uhusiano wowote wa kimapenzi na mrembo huyo huku akisema ukaribu wao ni wa kirafiki. Msanii huyo ambaye kipindi cha nyuma alitangaza kuwa anatafuta mke,amesema hatokuja kuweka wazi mahusiano yake kwa umma mtandaoni. “Hapo sijui, but ata kama nitaoa tena I would wish for something very very private,”Aliandika Kauli ya Daddy Owen inakuja mara baada ya shabiki kumuuliza kama anachumbiana na mrembo huyo.

Read More
 Daddy Owen akiri kutoshiriki tendo la ndoa kwa miaka miwili

Daddy Owen akiri kutoshiriki tendo la ndoa kwa miaka miwili

Mwimbaji wa nyimbo za Injili , Daddy Owen amefichua kuwa hajashiriki tendo la ndoa kwa miaka miwili. Katika mahojiano yake hivi karibuni, Owen amesema kuwa hajakuwa na hamu ya kufanya mapenzi tangu alipoachana na mke wake. “Sihitaji mwanamke, sijafanya mapenzi kwa miaka miwili, mwanamke ni wa kazi gani?” Owen alisema. Kauli yake imekuja mara baada ya kukiri kuwa hataki mwanamke kwenye maisha yake tena ikizingatiwa kuwa wiki kadhaa ilyopita alitangaza kuwa anatafuta mke. “Sitaki hata kupikiwa, nitakula hotelini, hata wageni wakija nyumbani kwangu tutanunua chakula, sitaki kuoa tena,” mwimbaji huyo alisema. Alisema kuwa ameridhika na maisha yake ya sasa na hatafuti mke wa kuoa kwani ana mambo mengi ya msingi ya kufanya. “Kwa sasa nafanya mambo mengi, sitafuti tena mke. Nitafute mke wa nini? Kama ni mtoto ninaye tayari, si bora kuwa na mtoto,” Owen alisema. Utakumbuka Daddy Owen na mkewe Farida Wambui walitengana mwaka 2020 baada ya kuwa kwenye ndoa kwa kipindi cha miaka minne.

Read More
 Daddy Owen aahirisha hafla yake ya kila mwaka ya Malaika Disability Walk.

Daddy Owen aahirisha hafla yake ya kila mwaka ya Malaika Disability Walk.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Daddy Owen ameahirisha hafla yake ya kila mwaka ya Malaika Disability walk ambayo ilipangwa kufanyika tarehe 3 Desemba mwaka huu. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Owen alisema matembezi hayo hayatafanyika kutokana na kifo cha kusikitisha cha binamu yake Stephen Sunrise Osedo ambaye atazikwa siku hiyo, hivyo wamelazimika kusogeza mbele hadi Machi 4 mwaka 2023. “Kutokana na mazingira yasiyoepukika, tulilazimika kuahirisha MATEMBEZI YA WALEMAVU YA MALAIKA 2022 ambayo yalipangwa kufanyika tarehe 3 Desemba ambayo ni SIKU YA WALEMAVU DUNIANI! Mazishi yatakuwa tarehe hiyo hiyo (tarehe 3 Desemba)” “”Wakati huo huo shule nyingi za Msingi zimeomba ushiriki wa MATEMBEZI, hivyo tumebadilisha tarehe kuwa MACHI 4, 2023. Tunaomba msaada wenu kikamilifu na tunaomba radhi kwa wadau wote waliokuwa wamejitokeza kutuunga mkono.#MalaikaDisabilityWalk2023.”, Aliandika. Binamu yake Owen aliuawa kwa kupigwa risasi na afisa wa polisi huko Umoja, kaunti ya Nairobi wiki mbili zilizopita. Daddy Owen alianzisha hafla ya Malaika mwaka 2012 kwa lengo la kutambua mchango wa watu wenye changamoto ya ulemavu katika jamii.

Read More
 Daddy akanusha madai ya kutumia vyombo vya habari kutafuta mke

Daddy akanusha madai ya kutumia vyombo vya habari kutafuta mke

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini daddy owen amekanusha madai yanayotembea mtandaoni kuwa anatafuta mwanamke wa kuingia naye kwenye ndoa ikiwa ni siku chache zimepita toka alipoweka wazi vigezo anavyohitaji kutoka kwa mwanamke wà ndoto yake. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Daddy Owen amesema kauli yake ilinukuliwa vibaya na walimwengu huku akisema kama kweli angekuwa anatafuta mke angefanya hivyo bila kuwafahamishw watu ikingatiwa kuwa yeye bado ni mwanaume rijali ambaye ana uwezo mkubwa wa kutongoza mwanamke. Hitmaker huyo wa Vanity amewataka walimwengu kuacha kueneza propaganda mtandaoni kuwa anatafuta mke wa kuoa na badala yake wamuunge mkono kwenye muziki wake kwani ikitokea kuwa ameingia kwenye mahusiano ataweka wazi kwa mashabiki zake. Kauli ya Daddy Owen imekuja mara baada ya kuzua gumzo mtandaoni kuwa anatafuta mwanamke ambaye anatoka mashinani, na mcha mungu ili aweze kuingia naye kwenye ndoa ambapo alienda mbali zaidi na kuwataka wadada ambao wanatamani kutokana nae kimapenzi kutuma maombi kupitia mitandao yake ya kijamii.

Read More
 Pritty Vishy akata tamaa kwenye penzi la Daddy Owen.

Pritty Vishy akata tamaa kwenye penzi la Daddy Owen.

Mrembo asiyeishiwa na matukio kila leo Pritty Vishy amekata tamaa kwenye penzi la Daddy Owen ikiwa ni siku chache zimepita toka mwimbaji huyo wa injili amkatae hadharani. Mrembo huyo ambaye kwa wakati mmoja aliwahi kuwa penzini na msanii Stivo Simple Boy amemtaja Daddy Owen kama dikteta asiyekuwa na msimamo mara baada ya kusisitiza kuwa mwanamke wa ndoto yake lazima ajue kuzungumza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha lakini pia asiwe mtumiaji wa mtandao wa Tiktok. Hata hivyo amemalizia kwa kumshauri hitmaker huyo wa Vanity kutimukia nchini Uganda iwapo anataka kufanikisha mchakato wa kupata mke wa kuingia naye kwenye ndoa kwani wasichana wa Kenya hawana ufasaha wa lugha ya Kiingereza. “Nilikua namtaka lakini sasa penye inaelekea ni kama itabidi avuke Uganda. He’s like a dictator. Sijui hataki dem ako TikTok, anataka dem anajua Kizungu mingi. Ikifika mahali ya TikTok na Kizungu mingi avuke tu Uganda. Hapa Kenya tuko TikTok na tunaongea Kizungu ya kilami. Ugandans ndio wako bushy,” Alisema. Utakumbuka mara baada ya Daddy Owen kutangaza kuwa anatafuta mke wa kuingia naye kwenye ndoa mapema wiki iliyopita, amepokea zaidi ya maombi 10,000 kutoka kwa wanadada tofauti ambao wametia nia ya kumtaka kimahusiano.

Read More
 DADDY OWEN AWASHAURI MASTAA KUACHA KUISHI MAISHA YA KUIGIZA MTANDAONI

DADDY OWEN AWASHAURI MASTAA KUACHA KUISHI MAISHA YA KUIGIZA MTANDAONI

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Daddy Owen amewashauri mastaa kurudisha mkono kwa jamii kwa kutoa misaada kwa watu wenye uhitaji. Kupitia instagram Daddy Owen amesema hatua hiyo itawapa motisha wakenya kuwasaidia wakati matatizo badala ya kuisha maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii. Hitmaker huyo wa Yahweh amesema kipindi alijipata kwenye matatizo hakuna staa hata mmoja alijitokeza kumsaidia ila anamshukuru mungu mashabiki zake ndio walikuwa mstari wa mbele kumshika mkono hadi akarudi katika hali yake ya kawaida. Daddy Owen ametoa kauli hiyo akijibu swali la mchekeshaji Creative Terrence ambaye alitaka kufahamu ni kitu gani inawafanya wakenya kutowasaidii mastaa mbali mbali nchini wakati wana changamoto katika maisha. Swali la Terrence liliibua hisia mseto miongoni mwa wakenya mtandaoni ambao wamehoji kuwa wasanii wanaishi maisha ya kifahari kwenye mitandao ya kijamii jambo limewafanya wengi wake kutoamini kama kweli huwa wanapata maishani.

Read More
 DADDY OWEN AICHARUKIA JARIDA MOJA KWA KUCHAPISHA TAARIFA ZA UONGO KUHUSU UTAJIRI WAKE

DADDY OWEN AICHARUKIA JARIDA MOJA KWA KUCHAPISHA TAARIFA ZA UONGO KUHUSU UTAJIRI WAKE

Msanii wa nyimbo za injili Daddy Owen ameibuka na kukanusha taarifa za utajiri wake zilizoainishwa na jarida moja kuwa ana utajiri wa shilllingi millioni 938 za Kenya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema kuna watu walimfanyia mahojiano kwa njia ya  simu na walipomuuliza swali la utajiri alisusia lakini cha kushangaza alitumiwa taarifa kuwa ana utajiri dollar million 8 jambo ambalo amedai kuwa data hizo ni batili. “Someone called me for a phone interview, in the middle of the interview they asked me, how much are u worth? I said “pass” .. After a few minutes they sent me ths.. “, Ameandika Instagram. Msanii huyo amesema jarida hilo lilipaswa kufanya uchunguzi kwanza kabla ya kumuweka kwenye orodha ya mastaa ambao wana mkwanja mrefu. “Ngoja kwanza, before utoe calculator uanze kupiga hesabu ya $8M ni how much in Kshs. Mimi niko na swali tu moja, hawa watu walijuaje?? Nani aliwaambia?? Sasa nafaa “Amen” or “uongo”🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔😳😳😳😳😳😳😳 n btw.. I have just landed from Harare.. #ifyouknowyouknow😉”, Amekazia. Hii sio mara ya kwanza kwa mastaa kuwekewa utajiri usio wao, mapema mwaka jana Jarida la Forbes lilimweka Diamond Platnumz kwenye orodha ya wanamuziki tajiri Barani Afrika jambo ambalo lilimfanya msanii huyo kuijua juu jarida hilo kwa kuchapisha taarifa za uongo.

Read More
 DADDY OWEN ATOA WITO KWA WAHISANI KUWASAIDIA WATOTO WENYE UGONJWA WA CLUB FOOT.

DADDY OWEN ATOA WITO KWA WAHISANI KUWASAIDIA WATOTO WENYE UGONJWA WA CLUB FOOT.

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Daddy Owen ametoa wito kwa wahisani kuwasaidia watoto wenye matatizo ya ugonjwa wa  mguu kifundo kwa maana ya Club Foot. Kupitia Instagram Page Daddy Owen amesema watoto wengi ambao wameathiriwa na ugonjwa wa Club Foot katika jamii wameshindwa kuafikia ndoto zao kutokana na unyanyapa. Hitmaker huyo ngoma ya “Vanity” ametoa changomoto kwa mashirika ya kijamii na wahisani wengine kujitokeza na kuwanusuru  watoto wanaosumbuka na maradhi hayo kwa kuwapa matibabu. Daddy Owen ametoa kauli hiyo alipomtembelea mwanafunzi mmoja wa kike huko visiwa vya Rusinga ambaye alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa Club Foot lakini habari njema ni kuwa amefanyiwa upasuaji na anatembea vizuri.

Read More
 RUFFTONE AOMBA RADHI BAADA YA KUTOA KAULI TATA DHIDI YA DADDY OWEN

RUFFTONE AOMBA RADHI BAADA YA KUTOA KAULI TATA DHIDI YA DADDY OWEN

Mwimbaji wa nyimbo za Injili ambaye pia ni mwaniaji wa kiti cha useneti kaunti ya Nairobi, Rufftone, amejitokeza na kuomba radhi kakake Daddy Owen na Wakenya kwa ujumla kutokana na kauli ya chuki aliyoitoa juzi kati dhidi ya kakake. Rufftone amekiri kwamba alikuwa chini ya shinikizo na akaishia kumtumia kakake kueleza ni kwa nini alifikiri chama cha ODM kimekuwa kikihusishwa na uhuni. Mwanasiasa huyo ametetea matamshi yake akisema alinukuliwa vibaya na watumiaji wa mitandao ambao walisambaza kauli yake hiyo. Amesisitiza kuwa madai kuwa kakake alimtishia kwa panga yalilenga tu kuonyesha namna ambavyo Daddy Owen alivyokuwa na hasira wakati walitofautiana kimawazo mwaka 2007. “Nilichomaanisha kumleta Daddy Owen ni kuwafanya Wakenya watambue kwamba siasa zinaweza kujipenyeza kati ya familia na ndiyo maana nikatumia mfano wa familia kwa sababu ndicho Wakenya wanaelewa zaidi, “Rufftone alisema. “Samahani kwa nilichosema … nachukua jukumu kamili, ilikuwa bahati mbaya sana. “Maoni niliyotoa yalikuwa jukwaa langu la kwanza la kisiasa katika runinga, kwa hivyo ninaomba Wakenya wanisamehe,” akaongeza. Kwa upande wake msanii Daddy Owen pia amekiri kwamba alikuwa na shauku wakati wa uchaguzi wa mwaka 2007 lakini hajawahi kufanya vurugu. “Nilipenda sana siasa 2007 na ODM iliposhindwa nilivunjika moyo sana lakini ninachojua ni kwamba sikuwahi kubeba panga na sijawahi kuwa na vurugu kwa sababu ya siasa. Nadhani kaka yangu alikuwa chini ya shinikizo wakati huo na ilibidi atoe mfano akitumia jina langu,” Daddy Owen alisema.

Read More