Tokyo 2025: Kipyegon Atetea Ubingwa, Dorcus Ewoi Aipatia Kenya Fedha

Tokyo 2025: Kipyegon Atetea Ubingwa, Dorcus Ewoi Aipatia Kenya Fedha

Mwanariadha anayeshikilia rekodi ya dunia Faith Kipyegon aliendeleza utawala wake katika mbio za mita 1500, aliposhinda taji yake ya nne mfululizo ya dunia katika siku ya nne ya Mashindano ya Riadha ya Dunia jijini Tokyo Japan. Kipyegon ambaye pia ni bingwa mara tatu wa Olimpiki alitumia muda wa dakika 3 na sekunde 52.15 na kujiongeza taji nyingine ya dunia. Alimaliza mbele ya mwenzake Dorcus Ewoi, ambaye alitumia muda wake bora wa dakika 3 na sekunde 54.92 kunyakua fedha, na Jess Hull wa Australia, aliyenyakua shaba kwa dakika 3 na sekunde 55.16. Kipyegon sasa mwanamke wa pili kushinda taji nne ya dunia katika mbio moja baada ya Shelly-Ann Fraser-Pryce ambaye ameshinda taji tano ya mbio za mita 100. Nelly Chepchirchir alimaliza wa nne kwa dakika 3 sekunde 55.25. Wakati huo huo, matumaini ya Kenya ya kunyakua medali zaidi katika Mashindano ya Riadha ya Dunia yaliboreshwa baada ya bingwa wa Olimpiki Emmanuel Wanyonyi na Kelvin Kimtai kufuzu kwa mbio za nusu-fainali ya mbio za mita 800. Kwa sasa Kenya inashikiliaa nafasi ya pili kwenye jedwali ya medali ikiwa na medali tano, 3 za dhahabu na moja ya fedha, nyuma ya Marekani, ambayo inaongoza kwa jumla ya nishani nane, zikiwemo sita za dhahabu.

Read More
 Kenya Yavizia Mataji ya Dunia Tokyo Kwa Uongozi wa Chebet na Kipyegon

Kenya Yavizia Mataji ya Dunia Tokyo Kwa Uongozi wa Chebet na Kipyegon

Macho yote yataelekezwa kwa wanariadha nyota Faith Kipyegon na Beatrice Chebet, wanaoshikilia rekodi za dunia, wakati Mashindano ya Riadha ya Dunia yatakapoanza leo katika Uwanja wa Kitaifa wa Japan, jijini Tokyo. Mwanariadha Beatrice Chebet, anayeshikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 5000 na mita 10,000, atashiriki kwa mara ya kwanza katika mbio za mita 10,000 kwenye mashindano haya, akiwa na azma ya kutwaa mataji mawili ya dunia msimu huu. Chebet tayari ameonyesha uwezo mkubwa katika majukwaa ya kimataifa, baada ya kunyakua nishani ya fedha na shaba katika mbio za mita 5000 kwenye Mashindano ya Dunia yaliyofanyika Eugene, Marekani (2022) na Budapest, Hungary (2023). Mwanariadha huyo atawaongoza wenzake wakiwemo Agnes Jebet Ngetich ambaye amekuwa akiandikisha matokeo bora katika mbio za kilomita 10 ambapo aliweka rekodi ya dunia ya dakika 28 na sekunde 46 jijini Valencia, na bingwa wa Afrika Janeth Chepngetich ambaye alishinda mbio za majaribio humu nchini. Mbio za mita 10,000 kwa wanawake zitaendelea kuwa kivutio kikuu, huku taji la dunia likishikiliwa kwa sasa na Gudaf Tsegay wa Ethiopia, ambaye pia anatarajiwa kutetea ubingwa wake.

Read More
 Faith Kipyegon Aweka Rekodi Mpya ya Dunia Paris Diamond League

Faith Kipyegon Aweka Rekodi Mpya ya Dunia Paris Diamond League

Bingwa wa dunia na Olimpiki kutoka Kenya, Faith Kipyegon, ameandika historia tena baada ya kuvunja rekodi ya dunia katika mbio za maili moja kwenye mashindano ya Paris Diamond League, kwa kukimbia kwa muda wa dakika 4:06.42. Muda huo mpya umevunja rekodi yake ya awali ya dunia ya 4:07.64 aliyoweka mwaka 2023 mjini Monaco, na unamuweka kwenye nafasi ya juu zaidi kama mwanamke wa kwanza kuwahi kukaribia kuvunja kizingiti cha dakika nne kwenye mbio za maili moja. Ingawa alishindwa kwa sekunde chache kufikia lengo la “sub-4 minute mile”, mafanikio hayo ni ya kihistoria. Muda huo mpya unasubiri kuthibitishwa rasmi na Shirikisho la Riadha Duniani (World Athletics). Ushindi huu unazidi kuimarisha nafasi ya Kipyegon kama malkia wa mbio za kati duniani, huku akiendelea na maandalizi kuelekea Michezo ya Olimpiki ya Paris 2024, ambako anatabiriwa kuwa mmoja wa wagombea wakuu wa dhahabu. Rekodi hii mpya ni ushahidi wa uwezo wake wa kipekee, juhudi kubwa na nidhamu ya hali ya juu, na inaongeza jina lake kwenye orodha ya wanariadha bora zaidi katika historia ya riadha ya wanawake duniani.

Read More