Femi One Aonyesha Fahari Yake Kufanya Kazi na Brand Kubwa ya Kimataifa

Femi One Aonyesha Fahari Yake Kufanya Kazi na Brand Kubwa ya Kimataifa

Rapa mkali kutoka nchini Kenya, Femi One, amezungumza kwa fahari kuhusu uzoefu wake wa kufanya kazi na kampuni kubwa ya vinywaji vya nishati, Monster Energy, akieleza kuwa ushirikiano huo ulikuwa hatua muhimu katika maisha na taaluma yake. Akizungumza katika mahojiano ya hivi majuzi, Femi One alifichua kuwa alikuwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kuteuliwa kuwa balozi rasmi wa bidhaa hiyo maarufu duniani. “I was the first African female Brand Ambassador for Monster Energy. Niko proud kuwa associated na brand kama Monster,” alisema kwa msisitizo. Kwa mujibu wa rapa huyo, fursa hiyo haikuwa tu hatua kubwa katika taaluma yake, bali pia ilikuwa nafasi ya kuvunja mipaka ya kijinsia katika sekta ya burudani na biashara. Alisema kuwa kupitia ushirikiano huo, alipata jukwaa la kimataifa kuonyesha kazi yake, kushirikiana na wabunifu mbalimbali, na kuwa kielelezo kwa wasichana wanaotamani kufanikisha ndoto zao katika tasnia tofauti. Femi One ambaye anaendelea kuwa sauti yenye ushawishi katika muziki wa Kenya na Afrika kwa ujumla, ameweka wazi kuwa ushirikiano na chapa kubwa kama Monster Energy ni uthibitisho wa jinsi wasanii wa Kiafrika wanavyozidi kutambuliwa na kuthaminiwa kimataifa. “Naamini hii ni mwanzo tu. Kuna nafasi nyingi kwa wasanii wa kike kuchukua nafasi katika brand kubwa, kama tukijiamini na kujituma,” aliongeza. Mashabiki wake na wanamuziki wenzake wameendelea kumpongeza kwa hatua hiyo muhimu, wakisema inatoa motisha kwa wasanii wa kike barani Afrika kuvunja mipaka na kutambulika kimataifa. Ushirikiano wake na Monster Energy ulihusisha kampeni za mitandaoni, matukio ya burudani, na shughuli za kuinua vipaji vya chipukizi.

Read More
 Rapa kutoka Kenya Femi One ashinda tuzo Afrimma 2022

Rapa kutoka Kenya Femi One ashinda tuzo Afrimma 2022

Rapper Femi One ameshinda kipengele cha rapper bora Afrika kwenye tuzo za Afrimma 2022 zilizokamilika wikiendi iliyopita huko Dallas nchini Marekani. Femi one ametumia mitandao yake ya kijamii kusherekea mafanikio kwa kushukuru uongozi wake pamoja na mashabiki kwa kumshika mkono kwenye safari yake ya muziki huku akiwahimizi marapa wa kike chipukizi kutia bidii katika kazi zao kwa kuwa wana nafasi zao kwenye tasnia ya muziki. “WE WON!!! Best Female Rapper In Africa . The first East African Female rapper to take it home , it’s such a big pat on the back for my team and I for all the work we’ve put in throughout the years . Truly consistency, patiency pays !!” “This should be an encouragement for all the up and coming Female rappers! There is a spot for you in this industry, keep building , keep doing it , they are watching . Thank you all so much for the continued support”, Aliandika. Femi one ambaye ni msanii wa kwanza wa kike kushinda tuzo ya Afrimma kwa upande wa muziki wa Hiphop anajiunga na Rayvanny, Diamond Platnumz  pamoja na Zuchu ambao walishinda tuzo ya msanii bora wa kiume Afrika mashariki, Best Live Act na msanii Bora wa kike Afrika Mashariki mtawalia. Femo One hakuwa Mkenya pekee aliyeteuliwa kuwania tuzo hizo, wengine ni pamoja na Khaligraph Jones- (Best Male East Africa), Otile Brown- (Best Male East Africa), Jovial- (Best Female East Africa), (Ssaru- Best Newcomer), Sauti Sol- (Best Live Act), na Fena Gitu- (Best Female Rap Act).

Read More
 Femi One aahidi kumnunulia gari King Kaka, amuambia achague lolote atakalo

Femi One aahidi kumnunulia gari King Kaka, amuambia achague lolote atakalo

Rapa wa kike nchini Femi One ameamua kurudisha fadhila kwa uongozi wake wa Kaka Empire ambao umemtoa kimuziki hadi kujulikana Afrika Mashariki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Femi One ametoa ametoa shukrani zake za dhati kwa mabosi wake King Kaka na Dennis Njenga kwa kumsaidia kufika alipo leo kwenye muziki ambapo ameenda mbali zaidi na kujitolea kuwanunulia wawili hao magari kama njia ya kuzawadi kwa kumshika mkono kisanaa. “Mapenzi na heshima nyingi sana kwa waungwana hawa wawili. Nikikumbuka safari yetu ya muziki huwa natabasamu tu ila wakati mwingine huwa nalia 😅 Moyo wangu umejaa shukrani nyingi King Kaka na Dennis Njenga ingieni showroom mchague magari mnayotaka!” Femi One alijiunga na lebo ya muziki ya Kaka Empire mwaka wa 2013 baada ya kuonesha uwezo wake kisanaa kupitia wimbo wa Ligi Soo Remix wake rapa King Kaka na tangu kipindi hicho amekuwa akiachia nyimbo kali mfululizo bila kupoa. Kando na muziki, Femi One pia mwaka 2021 aliandika historia ya kuwa Balozi wa Kwanza wa Kike kutoka barani Afrika wa Kinywaji cha Monster Energy.

Read More
 Femi One awajibu wanaowapinga wasanii kutumbuiza kwenye majukwaa ya kisiasa

Femi One awajibu wanaowapinga wasanii kutumbuiza kwenye majukwaa ya kisiasa

Rapa Femi One ambaye anafanya vizuri na wimbo wake mpya “Lip Service” amechukizwa na kitendo cha wakenya kuwakosoa wasanii wanapotumbuiza kwenye mikutano ya kisiasa. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Membo huyo amesema wasanii wanapoalikwa kufanya shows kwenye majukwaa ya kisiasa haimaanishi wanaunga mkono sera za viongozi wa mirengo fulani bali wameenda pale kwa ajili ya kujitafutia riziki. Utakumbuka Femi One ni moja kati ya wasanii waliotumbuiza kwenye majukwaa ya kisiasa hapa nchini Kenya msimu wa kampeini za uchaguzi mkuu uliokamilika, akiupigia upata mrengo wa Azimio la Umoja ambao ulishindwa na muungano wa Kenya Kwanza.

Read More
 Femi One adokeza ujio wa EP ya pamoja na Nyashinski

Femi One adokeza ujio wa EP ya pamoja na Nyashinski

Rapa Femi One ametangaza ujio wa EP yake mpya ambayo huenda akamshirikisha Nyashinsiki au Khaligraph Jones. Kwenye mahojiano na The Trend ya NTV rapa huyo ambaye anafanya vizuri na single yake mpya “Lip Service” amesema yupo mbioni kufanikisha hilo kwa kuwa tayari ameanza mazungumzo na marapa hao kuhusu mpango wa kufanya EP ya pamoja. Utakumbuka Femi One amefanya kazi ya pamoja na Nyashinski kupitia wimbo uitwao “Properly” na Khaligraph Jones kupitia ngoma inayokwenda kwa jina la “Blue Ticks”.

Read More
 FEMI ONE AFIKISHA STREAMS MILLIONI 5 BOOMPLAY

FEMI ONE AFIKISHA STREAMS MILLIONI 5 BOOMPLAY

Rapa kutoka Kenya, Femi One anaendelea kupokea upendo na support kubwa kutoka kwa mashabiki wake kiasi cha kufanya vizuri kwenye mtandao wa kupakua na kusikiliza muziki wa BoomPlay. Hadi kufikia sasa katika mtandao  wa Boomplay Kenya  Femi One amefanikiwa kufikisha  zaidi ya streams Million 5 kupitia nyimbo zake zote. Kupitia ukurasa wake wa instagram Femi One amewashukuru mashabiki zake kwa support wanayompa kila siku huku akiahidi kuendelea kuwapa burudani na ngoma kali zaidi. Ikumbukwe Album ya “Greatness” ambayo ndio albamu ya kwanza kwa femi one tangu aanze muziki wake imefanikiwa pia kufikisha  zaidi ya Streams millioni 1.2 kwenye mtandao wa Boomplay. Album ya Greatness iliachiwa rasmi mwezi Juni, 2 mwaka wa 2021 ikiwa na jumla ya mikwaju 14 ya moto huku  ikiwa na kolabo 9 pekee.

Read More
 PENZI LA PATORAKING WA NIGERIA LAMKOSESHA USINGIZI FEMI ONE

PENZI LA PATORAKING WA NIGERIA LAMKOSESHA USINGIZI FEMI ONE

Msanii wa muziki wa rap nchini Kenya, Femi One, ameshindwa kuficha mapenzi yake kwa nyota wa muziki wa Dancehall kutoka Nigeria, patoranking. Katika kikao cha Maswali na Majibu kupitia insta story yake kwenye mtandao wa instagram , hitmaker huyo wa ‘Utawezana” amesema anatamani kuolewa na nyota huyo wa Nigeria kwa sababu ana akili pia amekuwa akimfuatilia msanii huyo kwa muda mrefu. Hata hivyo watumiaji kwenye mitandao ya kijamii wameonekana kushangaza na kauli ya rapa huyo wengi wakihoji huenda femi one ana kazi ya pamoja na patoraking hivyo anatengeneza mazingira ya kuzungumuziwa kabla ya ujio wa ngoma yao mpya. Ikumbukwe Femi one tangu apate umaarufu kwenye tasnia ya muziki hajawahi weka wazi mahusano yake y kimapenzi lakini kutokana na ujumbe wake kwenye instagram page yake, inaonekana kuwa yuko tayari kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na patoraking.

Read More
 FENA GITU AWAPA SOMO MASHABIKI WANAOMFANANISHA NA RAPA FEMI ONE

FENA GITU AWAPA SOMO MASHABIKI WANAOMFANANISHA NA RAPA FEMI ONE

Female rapper kutoka Kenya Fena Gitu amechukizwa na kitendo cha mashabiki zake kushindwa kumtofautisha na msanii mwenzake Femi One. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Fena amewapa somo mashabiki ambao wamekuwa na mazoea ya kumuita Femi kwa kuwataka aacha tabia hiyo mwaka huu la sivyo wakome kumtaja kwenye shughuli zao. “Kama bado unaniita Femi 2022 wewe ni mzembe na sijali kabisa. Niite na jina langu kamili ama usinitaje kwenye shughuli zako.”  Ameandika Fena Gitu kupitia Twitter page yake. Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wameibuka na kumtolea uvivu fena gitu wakimtaka aache makasiriko kwani hawamfahamu kabisa na ndio maana wamekuwa wakimuita Femi One.

Read More