Ndugu wa Gloria Ntazola Apata Ajira Mpya Baada ya Kukataliwa na Familia

Ndugu wa Gloria Ntazola Apata Ajira Mpya Baada ya Kukataliwa na Familia

Ndugu ya socialite Gloria Ntazola, ambaye hivi karibuni aliomba msamaha hadharani na kuomba asaidiwe kuanzisha biashara, sasa amepata ajira mpya licha ya kukataliwa na familia yake. Mdau wa Burudani Obidan Dela amethibitisha taarifa hizo, akisema kijana huyo ameajiriwa kwenye moja ya maduka ya kuuza mavazi jijini Nairobi. Kwa mujibu wa Dela, uamuzi huo umekuja kama juhudi za kumsaidia kijana huyo kuanza upya maisha bila kutegemea familia. Hatua hii inakuja siku moja baada ya Gloria Ntazola kuapa waziwazi kwamba hataweza tena kumsaidia ndugu yake huyo, akidai aliumizwa sana kihisia kutokana na matendo yake ya awali. Gloria alisema kwamba licha ya kumsaidia mara kadhaa, tabia za kijana huyo na kukosekana kwa mabadiliko vilimfanya kuamua kutompa nafasi nyingine.

Read More
 Ndugu wa Gloria Ntazola Aomba Radhi Hadharani Baada ya Sakata la Familia

Ndugu wa Gloria Ntazola Aomba Radhi Hadharani Baada ya Sakata la Familia

Ndugu wa Socialite Gloria Ntazola ameomba radhi hadharani kufuatia sakata lililozua taharuki katika familia yao. Akipiga stori na mwanamitandao aitwaye 2Mbili, kijana huyo amekiri kusumbua familia na kuleta hali ya sintofahamu. Ameeleza kuwa anatamani kufunguliwa biashara ili kuanza upya na kujitegemea, akisisitiza kuwa hatua hiyo itamsaidia kurejesha imani ya familia na jamii. Kauli yake imekuja mara baada ya Gloria Ntazola kumfukuza kijana huyo nyumbani kwake kufuatia madai ya kumpiga mama yao mzazi na matumizi ya dawa za kulevya, jambo lililosababisha mzozo mkubwa wa kifamilia. Sakata hili linaendelea kuvutia hisia za mashabiki na wadau wa kijamii, huku wengi wakisubiri kuona kama familia ya Ntazola itakubali ombi hilo na kumsaidia kuanza upya.

Read More
 Gloria Ntazola Afunguka Baada ya Kumpa Ndugu Yake Msaada

Gloria Ntazola Afunguka Baada ya Kumpa Ndugu Yake Msaada

Mwanamitindo na mjasiriamali Gloria Ntazola amefunguka kwa uchungu kuhusu masaibu aliyopitia akijitolea kumsaidia ndugu yake aliyekuwa katika uraibu wa dawa za kulevya. Gloria anasema alitumia zaidi ya shilingi milioni mbili kumpeleka kijana huyo kwenye kituo cha Rehab ili kusaidiwa kuacha matumizi ya dawa hizo. Zaidi ya hapo, amekuwa akimlipia karo ya mtoto wake na kumsaidia kutafuta njia za kujitegemea. Hata hivyo, licha ya msaada huo wote, anadai kijana huyo alionyesha ukaidi, akakataa kufanya kazi, na tabia zake zikazidi kuwa changamoto. Tukio lililomuumiza zaidi, anasema, ni pale alipopiga mama yao mzazi, jambo lililomlazimu kumfukuza nyumbani kwa ajili ya usalama wa familia. Kauli ya Gloria imekuja mara baada ya kijana huyo kujitokeza mtandaoni akiomba msaada watu wamsaidie na makazi, madai ambayo Gloria mwenyewe ameyakana akisema kuwa familia yao ina majumba ya kutosha ya kifahari.

Read More
 Gloria Ntazola Afanya Upasuaji wa Urembo wa Shillingi Ksh Millioni 1.8

Gloria Ntazola Afanya Upasuaji wa Urembo wa Shillingi Ksh Millioni 1.8

Mrembo maarufu mtandaoni nchini Kenya, Gloria Ntazola, amefichua kuwa alitumia zaidi ya KSh 1.8 milioni kufanya upasuaji wa kuboresha mwili (cosmetic surgery) mjini Lagos, Nigeria. Akieleza safari yake ya upasuaji kupitia Instastory, Gloria ametaja kuwa kiasi hicho kilijumuisha gharama za taratibu za kitabibu, malazi ya hoteli, huduma za uangalizi baada ya upasuaji, pamoja na matibabu ya ziada aliyohitaji wakati wa kurejea katika hali yake ya kawaida. Hata hivyo, licha ya kushiriki uzoefu wake, mrembo huyo anayejulikana kama Kanjo Lady, ametoa tahadhari kwa wafuasi wake kuhusu hatari zinazohusiana na upasuaji wa aina hiyo. Gloria amesisitiza kuwa upasuaji wa kubadilisha mwonekano si jambo la mzaha na unaweza kuhatarisha maisha, akiwataka wanaofikiria kupitia njia hiyo kujiandaa kisaikolojia, kifedha na kimwili kabla ya kufanya uamuzi wowote.

Read More
 Gloria Ntazola Apuzilia Mbali Miito ya Kufanyiwa BBL

Gloria Ntazola Apuzilia Mbali Miito ya Kufanyiwa BBL

Mrembo maarufu mtandaoni nchini Kenya Gloria Ntazola, anayejulikana kama Kanjo Lady, ameweka wazi kuwa hana mpango wa kufanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio (Brazilian Butt Lift) licha ya mashinikizo kutoka kwa baadhi ya wafuasi wake mitandaoni. Gloria, ambaye hivi karibuni amefichua kuwa alifanyiwa upasuaji wa kuongeza maziwa na kuminya kiuno nchini Nigeria, amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakimshawishi afanye BBL ili kukamilisha umbo lake. Kwa mujibu wa maelezo yake, makalio yake ya asili tayari ni makubwa, na haoni sababu ya kuongeza au kubadilisha chochote katika eneo hilo. Mrembo huyo amesema anaamini katika kufanya marekebisho anayoona yanafaa kwake binafsi, lakini si kufuata presha ya mitandaoni. Kauli yake imezua mjadala mitandaoni, baadhi ya watu wakimuunga mkono kwa kusimama na maamuzi yake ya urembo, huku wengine wakiendelea kutoa maoni tofauti kuhusu mabadiliko ya mwili kwa njia ya upasuaji.

Read More
 Gloria Ntazola Awakosoa Wanaume wa Nairobi kwa Ubahili Kwenye Miadi

Gloria Ntazola Awakosoa Wanaume wa Nairobi kwa Ubahili Kwenye Miadi

Socialite anayesuasua mtandaoni, Gloria Ntazola ameibua mjadala mkali mtandaoni baada ya kuwakosoa wanaume wa Kenya hasa Nairobi kwa kile alichokitaja kama tabia ya kujibana wanapopeleka warembo kwenye miadi ya kimapenzi (Dates). Katika ujumbe wake uliosambaa mitandaoni, Gloria ameeleza kuwa wanaume wengi jijini Nairobi hawapendi kutumia pesa zao kununua chakula kizuri kwa wapenzi wao, badala yake hukimbilia vyakula vya bei rahisi kama chips na mayai. Mrembo huyo amesisitiza kuwa wanaume wanapaswa kuwa wakarimu zaidi na kujifunza kuwathamini wanawake wanaowaalika kwenye miadi mbalimbali. Hata hivyo ametoa changamoto kwa wanaume kukoma kuwaalika wanawake kwenye shughuli hizo kama hawana pesa za kutosha za kukimu mahitaji yao ya msingi. Gloria Ntazola amejizolea umaarufu kutokana na matamshi yake yenye utata kuhusu masuala ya mahusiano na mitindo ya maisha, na mara kadhaa amekuwa akizua mijadala mikubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Read More
 Gloria Ntazola Azua Gumzo kwa Kauli Kuhusu Ujauzito

Gloria Ntazola Azua Gumzo kwa Kauli Kuhusu Ujauzito

Socialite Gloria Ntazola ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kutoa kauli tata kuhusu suala la ujauzito. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Gloria alieleza wazi kuwa iwapo atapata mimba kwa sasa, ataichukua hatua ya kuitoa kwa sababu hana mpango wa kuzaa kwa wakati huu. Alisema hana mpango wa kulea mtoto kwa sasa na hakusita kusisitiza msimamo wake, akiongeza kuwa hata kejeli za watu haziwezi kumbadilisha maamuzi. Kauli hiyo imeibua hisia tofauti kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake, baadhi wakimtuhumu kwa kupuuza thamani ya maisha, huku wengine wakimtetea kwa kusema kila mtu ana haki ya kuchagua mustakabali wa maisha yake. Hii si mara ya kwanza Gloria Ntazola kuzua mjadala mtandaoni kupitia kauli zake zenye utata. Wengi wanamfahamu kwa mtindo wake wa maisha wa kifahari na tabia ya kuzungumza kwa uwazi bila kujali maneno ya wakosoaji. Kauli yake ya sasa imeendelea kugawanya mitazamo ya mashabiki, huku ikitarajiwa kuibua mjadala mpana zaidi kuhusu maadili, uhuru wa wanawake katika kufanya maamuzi ya uzazi, na nafasi ya mitazamo ya kijamii kwenye maisha binafsi.

Read More
 Gloria Ntazola Ajivunia Maisha ya Mpango wa Kando, Asema Anaishi kwa Furaha

Gloria Ntazola Ajivunia Maisha ya Mpango wa Kando, Asema Anaishi kwa Furaha

Mrembo wa mitandaoni Gloria Ntazola ameendelea kuzua gumzo baada ya kufichua wazi kwamba yeye ni mmoja wa wanawake walio mipango ya kando. Kwa mujibu wa maelezo yake, hatua hiyo imemletea furaha na amani kwa sababu amekuwa akipata kila kitu anachohitaji kutoka kwa mwanaume wake. Ntazola alifafanua kuwa mwanaume huyo amekuwa akimhudumia kikamilifu kwa kumpatia mahitaji ya msingi ikiwemo gari na matumizi ya kila siku. Anaeleza kuwa mara nyingi anapohisi hakupata anachotaka, humtishia mpenzi wake kwamba atamfichulia siri kwa mke wake, na ndipo hupokea alichokuwa akikitafuta. Mrembo huyo ameshauri wanawake wakubali hali ya kuwa mipango ya kando badala ya kupigania nafasi ya wake wa kweli kwa wanaume wao. Kwa mujibu wa kauli yake, Ntazola anasema wanaume wengi tayari wanatoka kimapenzi na wanawake zaidi ya mmoja, hivyo wanawake wasijisumbue kujipendekeza kuwa wao ndio wake halisi  ilhali ukweli ni kwamba uaminifu haupo. Kauli hiyo imewasha mitandao kwa kasi, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa ujasiri wa kusema ukweli wake, na wengine wakimshutumu vikali wakidai anahalalisha usaliti na kuvunja heshima ya ndoa. Mjadala unaoendelea umeibua maswali kuhusu maadili ya mahusiano ya kisasa, wengi wakijiuliza iwapo kauli ya Ntazola ni taswira halisi ya uhusiano wa sasa au ni mbinu yake ya kutafuta kiki mtandaoni.

Read More