Gloria Ntazola Azua Gumzo kwa Kauli Kuhusu Ujauzito

Gloria Ntazola Azua Gumzo kwa Kauli Kuhusu Ujauzito

Socialite Gloria Ntazola ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kutoa kauli tata kuhusu suala la ujauzito. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Gloria alieleza wazi kuwa iwapo atapata mimba kwa sasa, ataichukua hatua ya kuitoa kwa sababu hana mpango wa kuzaa kwa wakati huu. Alisema hana mpango wa kulea mtoto kwa sasa na hakusita kusisitiza msimamo wake, akiongeza kuwa hata kejeli za watu haziwezi kumbadilisha maamuzi. Kauli hiyo imeibua hisia tofauti kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake, baadhi wakimtuhumu kwa kupuuza thamani ya maisha, huku wengine wakimtetea kwa kusema kila mtu ana haki ya kuchagua mustakabali wa maisha yake. Hii si mara ya kwanza Gloria Ntazola kuzua mjadala mtandaoni kupitia kauli zake zenye utata. Wengi wanamfahamu kwa mtindo wake wa maisha wa kifahari na tabia ya kuzungumza kwa uwazi bila kujali maneno ya wakosoaji. Kauli yake ya sasa imeendelea kugawanya mitazamo ya mashabiki, huku ikitarajiwa kuibua mjadala mpana zaidi kuhusu maadili, uhuru wa wanawake katika kufanya maamuzi ya uzazi, na nafasi ya mitazamo ya kijamii kwenye maisha binafsi.

Read More
 Gloria Ntazola Ajivunia Maisha ya Mpango wa Kando, Asema Anaishi kwa Furaha

Gloria Ntazola Ajivunia Maisha ya Mpango wa Kando, Asema Anaishi kwa Furaha

Mrembo wa mitandaoni Gloria Ntazola ameendelea kuzua gumzo baada ya kufichua wazi kwamba yeye ni mmoja wa wanawake walio mipango ya kando. Kwa mujibu wa maelezo yake, hatua hiyo imemletea furaha na amani kwa sababu amekuwa akipata kila kitu anachohitaji kutoka kwa mwanaume wake. Ntazola alifafanua kuwa mwanaume huyo amekuwa akimhudumia kikamilifu kwa kumpatia mahitaji ya msingi ikiwemo gari na matumizi ya kila siku. Anaeleza kuwa mara nyingi anapohisi hakupata anachotaka, humtishia mpenzi wake kwamba atamfichulia siri kwa mke wake, na ndipo hupokea alichokuwa akikitafuta. Mrembo huyo ameshauri wanawake wakubali hali ya kuwa mipango ya kando badala ya kupigania nafasi ya wake wa kweli kwa wanaume wao. Kwa mujibu wa kauli yake, Ntazola anasema wanaume wengi tayari wanatoka kimapenzi na wanawake zaidi ya mmoja, hivyo wanawake wasijisumbue kujipendekeza kuwa wao ndio wake halisi  ilhali ukweli ni kwamba uaminifu haupo. Kauli hiyo imewasha mitandao kwa kasi, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa ujasiri wa kusema ukweli wake, na wengine wakimshutumu vikali wakidai anahalalisha usaliti na kuvunja heshima ya ndoa. Mjadala unaoendelea umeibua maswali kuhusu maadili ya mahusiano ya kisasa, wengi wakijiuliza iwapo kauli ya Ntazola ni taswira halisi ya uhusiano wa sasa au ni mbinu yake ya kutafuta kiki mtandaoni.

Read More