YouTube Yazindua Aina Mpya ya Matangazo ya “Peak Points” kwa Kutumia Akili Bandia

YouTube Yazindua Aina Mpya ya Matangazo ya “Peak Points” kwa Kutumia Akili Bandia

Mtandao wa YouTube umeanzisha mfumo mpya wa matangazo unaoitwa Peak Points, ambao hutumia teknolojia ya akili bandia ya Gemini inayomilikiwa na Google katika juhudi za kuboresha ufanisi wa matangazo ya mtandaoni. Mfumo huu wa kisasa una lengo la kuweka matangazo mara tu baada ya sehemu yenye mvuto mkubwa zaidi kwenye video yaani, pale ambapo watazamaji wamezama zaidi katika maudhui. Teknolojia hii ya Peak Points inalenga kutumia mbinu mpya inayojulikana kama emotion-based targeting, ambapo tangazo linawekwa katika wakati ambao watazamaji wanakuwa na hisia kali au shauku kubwa kutokana na kilichotokea kwenye video. Wataalamu wa masoko wanaamini kuwa hisia hizi huongeza uwezo wa kukumbuka tangazo, hivyo kuongeza athari ya uuzaji wa bidhaa au huduma. Mfumo huu una uwezo wa kutambua kilele cha usikivu wa watazamaji kama vile sehemu ya kushtua, kuchekesha, au kusisimua na kuweka tangazo baada ya tukio hilo ili kuvutia na kuathiri watazamaji kwa njia yenye nguvu zaidi. Ingawa mbinu hii inaonekana ya kibunifu na inalenga kuongeza thamani ya matangazo kwa waendeshaji wa biashara, baadhi ya watazamaji wameonyesha wasiwasi. Wengine wanasema matangazo haya yanaweza kuonekana kama usumbufu, hasa wakati mtazamaji amejikita kwenye hadithi au tukio muhimu la video. Kwa upande mwingine, wachambuzi wa masoko mtandaoni wanasema kuwa hatua hii inaonyesha mwelekeo wa siku zijazo wa matangazo yanayozingatia tabia na hisia za mtumiaji, kwa kutumia akili bandia. Wakati teknolojia ya Peak Points inaweza kuboresha uzoefu wa watangazaji kwa kupata wakati bora wa kufikisha ujumbe wao, bado kuna mjadala kuhusu usawa kati ya ubunifu wa biashara na faragha au raha ya mtazamaji.

Read More
 RAPA NAS NA KAMPUNI YA GOOGLE WAWEKEZA MABILLIONI YA PESA NIGERIA

RAPA NAS NA KAMPUNI YA GOOGLE WAWEKEZA MABILLIONI YA PESA NIGERIA

Rapa wa Marekani Nas akishirikiana na kampuni ya Google wamewekeza kiasi cha shillingi billioni 2.3 za Kenya kwenye kampuni ya Kiafrika iitwayo Carry1st ambayo inahusika na kutengeneza Mobile Games. Kwa mujibu wa The Hollywood Reporter, kiasi hicho cha fedha kitakwenda kusaidia kampuni hiyo kutanua wigo wa maudhui na pia kusaidia timu ya Wahandisi (engeeners) CEO na mwanzilishi wa Carry1st Bwana Cordel Robbin-Coker amesema wawekezaji hao wapya sio tu wameleta ahueni upande wa fedha lakini pia wameongeza kiwango cha maarifa kwa kuleta wataalamu ambao watasaidia kampuni hiyo kukua. Kampuni ya Carryfirst ina makazi yake nchini Nigeria.

Read More