GUARDIAN ANGEL AWAJIBU WANAODAI MUZIKI WA INJILI HAUNA PESA

GUARDIAN ANGEL AWAJIBU WANAODAI MUZIKI WA INJILI HAUNA PESA

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Guardian Angel amewatolea uvivu wanaodai kuwa wasanii wa gospel wamefulia kiuchumi. Katika mahojiano yake hivi karibuni Guardian Angel amesema madai ya kuwa muziki wa injili hauna pesa hayana ukweli wowote ambapo ameenda mbali zaidi na kusema kuwa yeye ni moja kati ya wasanii ambao wana mkwanja mrefu  na hata ikitokea ameacha muziki pesa zake zitamsaidia kujikimu kimaisha. Katika hatua nyinngine amepinga madai kuwa Ringtone ameacha muziki wa injili kwa kusema kwamba haamini kabisa kama msanii huyo amekimbilia muziki wa kidunia kwani huenda anatumia jambo hilo kutengeneza mazingira ya kuzungumzia. Guardian Angel ametoa kauli hiyo baada ya walimwengu kuhoji kuwa tasnia ya muziki nchini kenya haina pesa na ndio maana wasanii wengi waliokuwa wanafanya muziki huo wamegeukia muziki wa kidunia.

Read More
 GUARDIAN ANGEL AKANUSHA KULELEWA NA ESTHER MUSILA

GUARDIAN ANGEL AKANUSHA KULELEWA NA ESTHER MUSILA

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Guardian Angel amekanusha madai yanayosambaa mtandaoni kuwa amekuwa akilelewa na mke wake Esther Musila. Katika mahojiano yake hivi karibuni Guardian Angel amenyosha maelezo kwa kusema kwamba madai hayo hayana msingi wowote kwa kuwa yeye ndiye huwa anagharamia mahitaji yote ya msingi kwa mke wake kama mume. “Hajawai kulipa bills za nyumba yangu kwa sababu mimi ndo bwana yake, mimi ndo nalipa bills zake. Na pia kama kuwekwa ni namna hiyo basi mimi sielewi. Na kama mtu anahisi hio ndo kuwekwa basi iko tu sawa. Si mimi ndo nawekwa, wewe unawashiwa nini,” Amesema. Hitmaker huyo wa Nadeka ameenda mbali zaidi na kusema kuwa kama kufurahia ndoa na kupendwa ndio imewaaminisha watu kuwa analelewa na mke wake Esther Musila, basi yupo radhi kufanya hivyo. “Kama hivi ndo kuwekwa inaonjaacha niwekwe milele wacha niwekwe zaidi, ni tamu. Because kama nimewekwa hata sifai kupost anything ya the lady I’m purported to be with. I have never said that she is my sugar mummy secondly, I have never lived in her house, it is her who came to my house, kwa hiyo mimi ndo mzee wa hiyo nyumba.” Amesisitiza Guardian Angel.

Read More
 GUARDIAN ANGEL AMTAMBULISHA MSANII WAKE MPYA CHINI YA SEVEN HEAVEN MUSIC

GUARDIAN ANGEL AMTAMBULISHA MSANII WAKE MPYA CHINI YA SEVEN HEAVEN MUSIC

Nyota wa muziki nchini Guardian Angel amemtambulisha rasmi msanii mpya ndani ya lebo yake ya muziki ya Seven Heaven Music. Katika mahojiano yake hivi karibuni Guardian Angel amesema msanii huyo kwa jina la DJ Kezz kenya atakuwa chini ya lebo ya  Seven Heaven Music  ambayo itasimamia kazi zake zote za muziki ambapo amewataka mashabiki zake wamkaribishe msanii huyo kwenye tasnia ya muziki nchini Hitmaker huyo wa ngoma ya “Deka” amesema ametumia kiasi cha shillingi milllioni 6 kutambulisha msanii huyo kwa mashabiki ikiwemo kutayarisha video za nyimbo zake tatu ambazo zitatoka karibuni. Kwa upande wake DJ Kezz kenya ambaye ni msanii wa kwanza kujiunga na lebo ya Seven Heaven Music, ameonyesha furaha yake kujiunga na familia ya  Seven Heaven Music kwa kusema kwamba  mashabiki wakae mkao wa kula kupokea nyimbo zake. Utakumbukwa kwa sasa  DJ Kezz kenya anafanya vizuri na wimbo wake mpya uitwao Jipende aliyomshirikisha bosi wake Guardian Angel ambao una zaidi ya views laki moja kwenye mtandao wa youtube ndani ya siku 4 tangu iachiwe rasmi.

Read More
 GUARDIAN ANGEL AZINDUA JUKWAA LAKE LA KUSTREAM VIDEO ZA MUZIKI

GUARDIAN ANGEL AZINDUA JUKWAA LAKE LA KUSTREAM VIDEO ZA MUZIKI

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Guardian Angel na mke wake Esther musila wamezindua jukwaa lao la kustream video za muziki Jukwaa hilo liitwalo Solution.co.ke litatoa fursa kwa wasanii wa kenya na watengeneza maudhui kuingiza kipato kupitia maudhui wanayopakia kupitia mtandao kwa gharamu nafuu sana tofauti na majukwaa mengine kama Youtube Hata hivyo Guardian Angel amesema hivi karibuni atatoa muongozo wa namna ambavyo wanamuziki na wabunifu watakavyowasilisha kazi zao kwenye mtandao. Tayari couple hiyo imepakia video ya harusi yao na video ya wimbo mpya wa Guardian Angel uitwao money kwenye mtandao huo.

Read More
 GUARDIAN ANGEL AMVUA NGUO ANDREW KIBE KWA KUIKOSOA NDOA YAKE NA ESTHER MUSILA, AMUITA JINI SHETANI

GUARDIAN ANGEL AMVUA NGUO ANDREW KIBE KWA KUIKOSOA NDOA YAKE NA ESTHER MUSILA, AMUITA JINI SHETANI

Msanii wa nyimbo za injili nchini Guardian Angel amemtolea uvivu mwanahabari mwenye utata Andrew Kibe kwa madai ya kuikosoa ndoa yake na mke wake Esther Musila. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Guardian Angel amemtaka kibe aheshimu maamuzi yake na mke wake Esther Musila kuhalilisha ndoa kwa njia ya harusi ikizingatiwa kuwa wao ni watu wazima ambao upendo uliwaleta pamoja licha ya utofauti wa umri wao. “Maandiko matakatifu yanasema wakati mtu ameokoka aki-backslide, nini umu-happenia?…huwa anakuwa hatari zaidi kwani huwa anaingiliwa na shetani mara saba. Sina muda wa kupishana na shetani, vita vyetu ni vya kiroho my friend”..amesema kwenye mahojiano na Plug TV. Hitmaker huyo wa “Nadeka” ameenda mbali na kumshauri Kibe akome kuingilia maisha yao na badala yake aelekeze nguvu zake kwenye shughuli zitakazomuingizia kipato kwani anapoteza muda wake kuzungumzia jambo ambalo litamsaidia maishani. Kauli ya Guardian Angel imekuja mara baada ya Andrew Kibe kuonekana kukejeli ndoa yake na mke wake Esther Musila kwa kusema kwamba haoni ndoa hiyo ikidumu kwani msanii huyo aliwavunjia heshima vijana wa Kenya kwa hatua kumuoa mwanamke aliyemzidi kiumri.

Read More
 ALBUM YA GUARDIAN ANGEL “VICTORY” YAWEKA REKODI BOOMPLAY

ALBUM YA GUARDIAN ANGEL “VICTORY” YAWEKA REKODI BOOMPLAY

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Guardian Angel anazidi kufanya vizuri kupitia mauzo ya mtandaoni na Album yake ” Victory ” ambayo tayari ina takriban miezi miwili tangu itoke rasmi. Goods ni kwamba Album ya “Victory”  imefanikiwa kufikisha jumla ya Streams millioni moja kwenye mtandao wa kusikiliza na kupakua muziki wa Boomplay Kenya. Album ya “Victory” iliachiwa rasmi Novemba 11 mwaka 2021 ikiwa na jumla ya ngoma 10 ya moto na ni album ya pili kwa mtu mzima  guardian angel  tangu aanze safari yake ya muziki baada ya Thanks for Coming iliyotoka mwezi mei mwaka 2021  

Read More
 GUARDIAN ANGEL AFUNGA NDOA YA SIRI NA MCHUMBA WAKE ESTHER MUSILA

GUARDIAN ANGEL AFUNGA NDOA YA SIRI NA MCHUMBA WAKE ESTHER MUSILA

Nyota wa muziki wa injili nchini Guardian Angel ameripotiwa kufunga ndoa ya siri na mchumba wake Esther Musila  baada ya kuwa kwenye mahusiano kwa takribani mwaka mmoja. Kulingana na wajuzi mambo kwenye mitandao ya kijamii,Harusi hiyo ambayo inadaiwa kuwa ya siri imiefanyika leo jijini Nairobi na kuhudhuriwa na wageni wasiozidi 20, ikiwemo ndugu wa pande zote mbili za familia zao. Hata hivyo mashabiki wengi kwenye mitandao ya kijamiii wamefurahia kwa hatua ya wawili hao kuhalalisha mahusiano yao huku wengine wakiwa na mshangao kwanini ndoa hiyo imekuwa ya siri japokuwa ni jambo la kheri kwa kila mwanadamu Uhusiano wa kimapenzi wa hao ulianza mapema mwaka jana 2021, huku Guardian Angel akithibitisha mahusiano hayo rasmi baada ya ukaribu wake na mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 51 gumzo mtandaoni ambapo  wengi walishangazwa na hatua ya msanii huyo kutoka kimapenzi na mtu ambaye amemzidi umri.

Read More