Guardian Angel Aanzisha Kampeni Dhidi ya Unyanyasaji wa Mtandaoni

Guardian Angel Aanzisha Kampeni Dhidi ya Unyanyasaji wa Mtandaoni

Msanii wa muziki wa injili nchini Kenya, Guardian Angel, ameanzisha kampeni maalum ya kuhamasisha mashabiki na jamii kwa ujumla kuhusu athari za unyanyasaji wa mtandaoni (cyber bullying), Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Guardian Angel ametoa wito wa kusitisha kabisa vitendo vya unyanyasaji wa mtandaoni, akieleza kuwa tatizo hilo linaelekea kuwa miongoni mwa changamoto kubwa zaidi za mtandaoni kwa sasa. Msanii huyo amebainisha kuwa cyber bullying tayari inaathiri hadi asilimia 53 ya watoto, jambo linalotia wasiwasi mkubwa kwa wazazi na jamii kwa ujumla. Guardian Angel na mke wake Esther Musila wamekuwa miongoni mwa waathiriwa wakubwa wa cyber bullying, hali iliyowasababishia maumivu ya kihisia kiasi cha kutishia kuchukua hatua za kisheria, ikiwemo kuwafungulia mashitaka wahusika wanaowatusi mtandaoni

Read More
 Mke wa Guardian Angel Afunguka Sababu ya Kiapo Chao cha Ndoa kuwa Tofauti

Mke wa Guardian Angel Afunguka Sababu ya Kiapo Chao cha Ndoa kuwa Tofauti

Mwanamama Esther Musila amefunguka na kueleza sababu iliyowafanya yeye na mume wake, mwimbaji wa muziki wa injili Guardian Angel, kuamua kutumia maneno ya “for richer” pekee katika viapo vyao vya ndoa, na kuacha kipengele cha “for poorer” ambacho huonekana mara nyingi katika viapo vya kawaida vya ndoa. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Musila amesema waliamua kufanya hivyo kwa makusudi kwa sababu hawakutaka kutamka au kuingiza maneno yanayohusu umasikini au magumu katika ndoa yao, akisema kuwa maneno yana nguvu na yanaweza kuathiri mwelekeo wa maisha ya ndoa. Esther Musila ameongeza kuwa uamuzi huo haukumaanisha kupuuza changamoto za maisha, bali ni kuchagua kuanza ndoa yao kwa matumaini, imani na malengo mema, huku wakimtegemea Mungu kuwaongoza katika kila hatua. Kauli ya mwanamama huyo ambaye ndoa yake imepitia misusuko ya kupingwa na walimwengu, inakuja wakati anasherekea miaka minne ya ndoa yao na miaka sita ya kuwa pamoja tangu waanze uchumba wao.

Read More
 Guardian Angel Awasisimua Mashabiki kwa Kumsuprise Mkewe kwa Lunch Maalum

Guardian Angel Awasisimua Mashabiki kwa Kumsuprise Mkewe kwa Lunch Maalum

Msanii wa muziki wa Injili, Guardian Angel, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kuamua kumpa mke wake, Esther Musila, suprise ya kipekee kwa kumpeleka kwenye lunch maalum wakati walipokuwa jijini Kisumu kwa shughuli za kikazi. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Guardian ameposti video inayoonesha safari yao pamoja na nyakati za furaha walizoshiriki katika mkahawa mmoja huko Kisumu. Kwenye video hiyo, wawili hao wanaonekana wakifurahia vyakula mbalimbali huku wakicheka na kubadilishana mazungumzo ya upendo, hali iliyowavutia mashabiki wengi. Hatua hiyo imefasiriwa na wengi kama ujumbe mzito kwa wanaume wa Kenya kuhusu umuhimu wa kuthamini na kuenzi wake zao, bila kujali mazingira au maoni ya watu wengine. Guardian Angel pia anaonekana kupuuza kabisa ukosoaji uliowahi kujitokeza kuhusu kuoa mke aliyemzidi kiumri kwa kudhihirisha kuwa mapenzi ya kweli hayapimwi kwa umri bali kwa heshima, uelewano na upendo wa dhati.

Read More
 Guardian Angel Atoa Onyo Kali Kwa Wanaoeneza Chuki Mitandaoni

Guardian Angel Atoa Onyo Kali Kwa Wanaoeneza Chuki Mitandaoni

Msanii wa muziki wa Injili, Guardian Angel, ametoa onyo kali kwa watumiaji wa mitandao wanaoeneza chuki na kuwakandamiza wengine kupitia maneno ya kashfa na matusi. Kupitia ujumbe wake mtandaoni, Guardian Angel amesema kuwa watu wengi wanaumizwa na maudhui ya chuki yanayoenezwa bila kujali hisia zao, akibainisha kuwa wengi wao hupitia mateso makubwa kimya kimya kutokana na maneno ya ukatili yanayorushwa dhidi yao bila huruma. Amesisitiza kuwa wale wanaotumia mitandao kuumiza wengine kwa lugha za kudhalilisha watawajibika siku moja, akisema hakuna atakayeweza kutoroka matokeo ya matendo yake. Guardian Angel amewataka watumiaji wa mitandao kutumia majukwaa yao kwa ajili ya kujenga na kuhamasisha upendo, badala ya kutumika kama chanzo cha chuki, majeraha ya kiakili na machafuko ya kijamii.

Read More
 Guardian Angel Amtia Moyo Oga Obinna Baada ya Kukosolewa Mitandaoni

Guardian Angel Amtia Moyo Oga Obinna Baada ya Kukosolewa Mitandaoni

Staa wa nyimbo za injili nchini Kenya, Guardian Angel, amemtaka mtangazaji Oga Obinna kupuuza ukosoaji wa watu na kuendelea kusaidia vijana kupitia jukwaa lake, akisisitiza umuhimu wa kufanya mema bila kuathiriwa na maneno ya chuki. Akizungumza katika hafla ya kumuaga marehemu Shalkido hapo jana, Guardian amemtia moyo mtangazaji huyo, akimhimiza kutokata tamaa licha ya wimbi la ukosoaji alioupokea mitandaoni Hitmaker huyo wa Kimya, amempongeza Obinna kwa moyo wake wa kusaidia watu na kumtaka aendelee na juhudi zake za kuinua jamii licha ya upinzani na ukosoaji anaokutana nao. Guardian ameongeza kuwa mara nyingi watu wanaojituma kufanya mazuri ndio hukosolewa zaidi, lakini kinachojalisha ni athari chanya wanayoacha katika jamii. Guardian Angel, alikuwa miongoni mwa waombolezaji waliouthuria mazishi ya msanii wa miondoko ya Gengetone, Shalkidoh, yaliyofanyika jana katika kijiji cha Kimbo Matangi, Kaunti ya Kiambu.

Read More
 Guardian Angel Afunguka Kuhusu Shinikizo la Kupata Mtoto na Esther Musila

Guardian Angel Afunguka Kuhusu Shinikizo la Kupata Mtoto na Esther Musila

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Guardian Angel ameweka wazi msimamo wake kufuatia shinikizo kutoka kwa baadhi ya mashabiki wanaomtaka yeye na mkewe Esther Musila kupata mtoto. Akipiga stori na Plugtv, amesema hana wasiwasi kuhusu suala hilo, akifafanua kuwa uhusiano wao haukujengwa kwa msingi wa watoto bali kwa upendo wa dhati kati yao. Kwa mujibu wake, maagano yao yalitoa kipaumbele kwa upendo, na watoto ni kama nyongeza tu katika maisha yao. Hitmaker huyo wa Kimya, ameongeza kuwa kama watapata mtoto, watamshukuru Mungu kwa baraka hiyo, na endapo hilo halitatokea bado wataendelea kufurahia maisha yao kwa amani na furaha. Msanii huyo pia ameonyesha kutoridhishwa na shinikizo kutoka kwa watu wanaoingilia maisha yao ya kifamilia, akisema haelewi lengo la wale wanaowataka wapate mtoto kwa lazima. Guardian Angel na Esther Musila wameendelea kudumisha ndoa yao kwa upendo mkubwa licha ya ukosoaji kutoka kwa baadhi ya watu mitandaoni. Wawili hao wameonyesha kwamba upendo wa dhati haupimwi kwa umri, watoto au matarajio ya watu bali kwa maelewano na kuheshimiana.

Read More
 Guardian Angel Atangaza Mpango wa Kujenga Kanisa Bila Msaada wa Mashabiki

Guardian Angel Atangaza Mpango wa Kujenga Kanisa Bila Msaada wa Mashabiki

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Guardian Angel ametangaza mipango mikubwa ya kujenga kanisa lake kabla ya kumalizika kwa mwaka huu, akisema ni njia yake ya kumrudishia Mungu shukrani kwa wema wake. Kupitia ujumbe alioweka mtandaoni, Guardian Angel amesema kuwa Mungu amekuwa mwema kwake kwa namna isiyoelezeka, na kwa sababu hiyo ameamua kujitolea kujenga nyumba ya ibada kama ishara ya shukrani na imani thabiti kwa muumba wake. Msanii huyo amesisitiza kuwa hatua hiyo siyo ya kibiashara wala mradi wa kutafuta misaada, bali ni jukumu la kiroho alilopokea kwa moyo wa unyenyekevu. Hata hivyo ameweka wazi kuwa hahitaji fedha wala michango kutoka kwa mashabiki wake, bali bali anawaomba maombi pekee ili Mungu aendelee kumpa nguvu na mwongozo katika kutimiza azma hiyo.

Read More
 Guardian Angel: Natumia Milioni 1.5 Kila Mwezi!

Guardian Angel: Natumia Milioni 1.5 Kila Mwezi!

Msanii wa muziki wa injili nchini Kenya, Guardian Angel, amefichua kiwango kikubwa cha fedha anachotumia kila mwezi kugharamia mahitaji yake ya msingi. Akipiga stori na podcast ya Mwakideu live, Guardian Angel amesema kuwa matumizi yake ya kila mwezi ni zaidi ya Shillingi milioni 1.5. Kwa mujibu wa msanii huyo, kiasi hicho kinahusisha gharama za maisha, miradi ya muziki, pamoja na majukumu mengine ya kifamilia na kijamii anayobeba. Amebainisha kuwa licha ya muziki wa injili kutoonekana kama sekta yenye mapato makubwa, yeye ameweza kujipanga kimaisha kuhakikisha anadumisha kiwango chake cha maisha. Kauli yake imezua mjadala mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakisifia uaminifu na uthubutu wake wa kuweka wazi hali yake ya kifedha, huku wengine wakishangazwa na ukubwa wa gharama hizo.

Read More
 Guardian Angel athibitisha mapenzi hayachagui umri, ampongeza mkewe kwa maneno ya kutia moyo

Guardian Angel athibitisha mapenzi hayachagui umri, ampongeza mkewe kwa maneno ya kutia moyo

Msanii maarufu wa nyimbo za Injili nchini Kenya, Guardian Angel, amemiminia mkewe, Esther Musalia, ujumbe mtamu wa mapenzi huku akimsherehekea kwenye siku yake ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 55. Kupitia mitandao ya kijamii, Guardian Angel aliandika ujumbe wenye hisia kali akimtaja Esther kama baraka kubwa katika maisha yake. “Kukupenda kulikuwa uamuzi bora zaidi wa maisha yangu. Namshukuru Mungu kila siku kwa kunibariki kwa kukupa wewe. Heri ya siku ya kuzaliwa, malkia wangu,” aliandika Guardian Angel kwenye ukurasa wake wa Instagram, akiambatanisha na picha wakiwa pamoja kwa furaha. Wawili hao wamekuwa kwenye uhusiano wa karibu na wa kudumu, licha ya tofauti kubwa ya umri kati yao, na wamekuwa wakivutia wengi kwa jinsi wanavyopendana na kushikilia ndoa yao kwa imani thabiti. Mashabiki na wafuasi wao wamejitokeza kwa wingi mtandaoni kuwatakia heri, huku wengi wakimsifu Guardian kwa kumuenzi mkewe hadharani na kuvunja mitazamo ya kijamii kuhusu ndoa zenye tofauti kubwa ya umri. Guardian Angel, anayejulikana kwa nyimbo maarufu kama Nadeka, Swadakta na Uskonde, ameendelea kuwa miongoni mwa wasanii wa Injili wanaoheshimika zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki, si tu kwa kipaji chake, bali pia kwa misimamo yake kuhusu ndoa, imani na familia.

Read More
 Guardian Angel ataka kanisa kuunga mkono wasanii wa nyimbo za injili

Guardian Angel ataka kanisa kuunga mkono wasanii wa nyimbo za injili

Mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka Kenya Guardian Angel ametoa changamoto kwa makanisa kuanza kuunga mkono kazi za wasanii wa nyimbo za injili nchini humo. Kupitia ukurasa wa Instagram amesema wasanii wengi huenda wakaacha kujihusisha na muziki huo kabla mwaka 2023 haujaisha na kugeukia muziki wa kidunia kama hawatapata uungwaji mkono kutoka kwa wakristo. Hata hivyo amesisitiza kuwa iwapo makanisa yataitikia wito huo hakuna msanii wa nyimbo za injili ataacha muziki huo kwa kuwa wengi wao wanatapitia mazingira magumu kwenye masuala ya kuingiza riziki kupitia muziki wao. “2023 THE CHURCH MUST BEGIN TO SUPPORT KENYAN GOSPEL MUSICIANS…Otherwise things will be tough. Most of them might close down before the End of the Year:” “Hakuna msanii wa GOSPEL ataacha gospel tena sababu anaimba akiteseka….Choose what to do with This information”, Aliandika.

Read More
 Guardian Angel aachia rasmi album yake mpya “Arise and Shine”

Guardian Angel aachia rasmi album yake mpya “Arise and Shine”

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini  Guardian Angel ameachia rasmi album yake mpya inayokwenda kwa jina la  Arise and Shine. Victory imebeba jumla ya mikwaju 10 ya moto huku  ikiwa na kolabo 3 pekee kutoka kwa wasanii kama Miracle, DJ Kezz na Kamuhunjia. Album hiyo ambayo ndio kazi ya mwisho ya Guardian Angel kwa mwaka 2022, inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya  kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile Boomplay,Spotify na Apple Music Album ya ” A rise and Shine ” ni album ya tatu kwa mtu mzima  Guardian Angel  tangu aanze safari yake ya muziki baada ya Victory na Thanks for Coming zilizotoka mwaka 2021.

Read More
 ESTHER MUSILA ATOA WITO KWA WANAWAKE KUWAWEKA WAUME ZAO KWA MAOMBI

ESTHER MUSILA ATOA WITO KWA WANAWAKE KUWAWEKA WAUME ZAO KWA MAOMBI

Mke wa msanii Guardian Angel,Esther Musila ametoa changamoto kwa wanawake walio kwenye ndoa kujenga tabia ya kuwaweka waume zao kwenye maombi. Akipiga stori na SPM BUZZ Musila amesema maombi yana nguvu kubwa sana katika maisha ya ndoa kwa kuwa inaleta familia pamoja lakini pia inawasaidia wanandoa kufanikisha baadhi ya mipango yao. Mwanamama huyo wa miaka 52 amesema amekoshwa sana na mienendo ya mama taifa Bi Rachel Ruto ya kumtanguliza Mungu kwa kila jambo ambapo amehapa kwamba atafuata nyayo zake kuhakikisha mume wake Guardian Angel anafanikisha ndoto zake katika maisha. Utakumbuka Guardian Angel na mke wake Esther Musila ni miongoni mwa wasanii watakao toa burudani Septemba 13 katika hafla ya kuapishwa kwa Rais mteule wa Kenya Dkt. William Samoe Ruto kwenye uga wa kamataifa wa Kasarani.

Read More