Harambee Stars Yacharazwa 8–0 na Senegal Uturuki

Harambee Stars Yacharazwa 8–0 na Senegal Uturuki

Timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, imepata matokeo mabaya zaidi katika historia ya mechi zake za kirafiki baada ya kulala 8–0 dhidi ya miamba wa Afrika Senegal, kwenye mchezo uliopigwa jana usiku nchini Uturuki. Mchezaji nyota wa Al-Nassr na zamani wa Liverpool, Sadio Mane, aling’ara kwa kufunga hat-trick, huku mshambulizi wa Bayern Munich Nicolas Jackson akiongeza mabao mawili. Mabao mengine yalifungwa na Malik Diouf wa West Ham United, Ibrahim Mbaye wa PSG, pamoja na Cherif Ndiaye wa Samsunspor. Huu unakuwa mchezo wa pili mfululizo Harambee Stars kupoteza ndani ya siku nne, baada ya kukubali kichapo cha 1–0 dhidi ya Equatorial Guinea katika mechi nyingine ya kirafiki. Kwa upande wa Senegal, ushindi huu ulikuwa dawa ya kurejesha morali baada ya kukosa kufunga dhidi ya Brazil katika mchezo wao uliopita ambao walishindwa mabao 2–0. Stars wanacheza mechi zenye ushindani mkubwa kama sehemu ya maandalizi kuelekea fainali za AFCON 2027, ambazo zitafanyika kwa mara ya kwanza katika Afrika Mashariki, zikiandaliwa kwa ushirikiano na Kenya, Uganda na Tanzania.

Read More
 Harambee Stars Kuchuana na Senegal Leo Kwenye Mchezo wa Kirafiki

Harambee Stars Kuchuana na Senegal Leo Kwenye Mchezo wa Kirafiki

Timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, itakutana na Senegal leo jioni katika mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayochezwa katika Uwanja wa Mardan hapa Uturuki. Mchuano huu utakuwa wa pili wa kirafiki wa kimataifa kwa Stars mwezi huu, baada ya kufungwa bao moja kwa nunge na Equatorial Guinea Ijumaa iliyopita. Historia inaonyesha kuwa timu hizo zimekutana mara nne, ambapo Senegal imeandikisha ushindi mara tatu na kutoka sare mara moja. Mechi ya mwisho ya Harambe Stars dhidi ya Senegal ilikuwa mwaka 2019 katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, ambapo Stars ilipoteza mabao matatu kwa nunge. Mechi ya leo itakuwa fursa muhimu kwa Stars kujipima nguvu dhidi ya wapinzani wao wenye viwango vya juu huku ikijinoa kabla ya mechi zijazo za ushindani. Kocha na wachezaji wanatarajiwa kutumia mchezo huu kuimarisha mikakati na kuimarisha mawasiliano uwanjani kabla ya mashindano makubwa yajayo.

Read More
 Harambee Stars Wapoteza Mechi Tatu za Kufuzu Kombe la Dunia 2026

Harambee Stars Wapoteza Mechi Tatu za Kufuzu Kombe la Dunia 2026

Timu ya taifa ya soka, Harambee Stars, ilipoteza mechi yake ya tatu katika michuano ya kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026, baada ya kufungwa mabao 3-1 na Gambia uwanjani Kasarani. Kipigo hicho ni pigo kubwa kwa Harambee Stars, ambayo sasa haijaweka wazi nafasi yake ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazoandaliwa mwaka ujao katika mataifa ya Marekani, Canada, na Mexico. Harambee Stars imeshinda mechi moja tu kati ya saba zilizochezwa hadi sasa katika awamu ya kufuzu, na inashikilia nafasi ya tano kwenye kundi F ikiwa na alama 6, alama 12 nyuma ya vinara wa kundi hilo, Gabon. Aidha, Stars sasa itacheza dhidi ya Ushelisheli katika mechi ijayo itakayofanyika tarehe 9 mwezi huu, kabla ya kumaliza mashindano haya kwa kucheza na Burundi na Kodivaa mwezi Oktoba mwaka huu. Fainali za Kombe la Dunia 2026 zitaanza rasmi tarehe 11 Juni na kuhitimishwa tarehe 19 Julai.

Read More