Meta Yazindua Instagram Kwenye TV

Meta Yazindua Instagram Kwenye TV

Kampuni ya Meta imetangaza rasmi kuanza kuweka app ya Instagram kwa watumiaji wa televisheni. Hatua hii inalenga kuwapa watumiaji fursa ya kutazama video za Reels kupitia screen kubwa za TV, badala ya kutegemea simu pekee. Kwa mujibu wa Meta, utekelezaji wa mpango huu umeanza kwa kushirikiana na Amazon Fire TV, huku ikipangwa kupanua huduma hiyo na kuipeleka kwenye majukwaa mengine ya televisheni siku zijazo. Instagram kwenye TV itakuwa na muonekano wa Channels, unaowezesha watazamaji kufuatilia maudhui mbalimbali yakiwemo michezo, burudani na muziki. Meta imesema mfumo huo utaruhusu watu wengi kutazama kwa pamoja kwenye TV moja bila kuonyesha taarifa binafsi kama mazungumzo ya faragha au data za mtumiaji. Hatua hii inalenga kulinda faragha na kufanya matumizi yawe salama kwa familia, hali inayofanana na majukwaa ya YouTube na Netflix. Hatua ya Meta inafuatia mwelekeo wa mitandao ya kijamii kuingia kwenye soko la televisheni na video streaming. Ikumbukwe kuwa TikTok ilianza kupatikana kwenye TV tangu mwaka elfu mbili na ishirini.

Read More
 Instagram Yazindua Algorithm Mpya ya Kubinafsisha Maudhui

Instagram Yazindua Algorithm Mpya ya Kubinafsisha Maudhui

Instagram imezindua mfumo mpya wa algorithm unaowawezesha watumiaji kudhibiti maudhui wanayoona kwenye ukurasa wao wa nyumbani. Mfumo huu mpya unalenga kubinafsisha uzoefu wa kila mtumiaji kulingana na maslahi yake binafsi. Kwa mujibu wa maelezo ya Instagram, sasa watumiaji wanaweza kuunda algorithm zao wenyewe. Hii inamaanisha unaweza kuamua ni aina gani ya posts unazopendelea kuona ama ni michezo, filamu, comedy, masomo, sayansi, au mada maalum unayopenda. Mfumo mpya wa akili bandia (AI) wa Instagram utachambua posts zinazofanana na maudhui uliyoyachagua, kuhakikisha kwamba unapata zaidi ya kile unachokipenda. Kwa mfano, kama ukichagua filamu za aina ya comedy, algorithm itakuonyesha posts nyingi zinazohusiana na filamu hizo, ikiongeza uwezekano wa kupata taarifa na burudani zinazokidhi ladha yako. Watumiaji wanasema mfumo huu ni hatua muhimu katika kuboresha uzoefu wa mtumiaji, kwani sasa hakuna haja ya kupoteza muda kuangalia maudhui yasiyokufaa. Pia unatoa uhuru mkubwa kwa kila mtu kuunda feed yake ipasavyo. Instagram imesema mfumo huu mpya unaanza hatua kwa hatua na utazinduliwa rasmi kwa watumiaji wote ndani ya wiki chache zijazo.

Read More
 Instagram Yazindua Sehemu Mpya ya Kudhibiti Follow Requests

Instagram Yazindua Sehemu Mpya ya Kudhibiti Follow Requests

Mtandao maarufu wa kijamii Instagram umezindua kipengele kipya kinachowezesha watumiaji kudhibiti Follow Requests kutoka kwa akaunti ambazo tayari wanafuata. Kipengele hiki kinakusudia kurahisisha njia ya kudhibiti nani anayeweza kujiunga na mtiririko wa watumiaji, na kutoa udhibiti zaidi juu ya faragha ya akaunti. Kwa kutumia sehemu hii mpya, mtumiaji wa Private Accounts anaweza kukubali Requests kutoka kwa akaunti ambazo tayari wanazi-follow, bila taabu ya kukagua kila moja.. Kwa mfano, kama kuna akaunti ambayo unai-follow, akaunti hiyo inaweza kuku-follow automatically bila wewe kupata taabu ya kuiruhusu, mradi tu akaunti yako ni private. Kipengele hiki kinasaidia okoa muda na kurahisisha usimamizi wa Follow Requests, huku kikiweka watumiaji kwenye udhibiti zaidi wa faragha yao. Hatua hii inakuja wakati Instagram inajitahidi kuongeza udhibiti wa faragha na kutoa uzoefu bora zaidi kwa watumiaji wake duniani kote.

Read More
 Instagram yazindua kipengele kipya cha kuchora ndani ya DM

Instagram yazindua kipengele kipya cha kuchora ndani ya DM

Kampuni ya Instagram imeweka mabadiliko mapya katika sehemu ya Direct Messages (DM), ambapo sasa watumiaji wote wanaweza kuchora moja kwa moja kwenye skrini ya mazungumzo. Kupitia mfumo huu mpya, mtumiaji anaweza kuchora au kuandika kwa mkono katika sehemu yoyote ya skrini ya DM, na mtu anayewasiliana naye ataweza kuona michoro hiyo papo kwa papo, bila kuchelewa. Kipengele hiki kipya kinapatikana kupitia alama ya (+) iliyopo chini ya skrini ya mazungumzo. Baada ya kubonyeza alama hiyo, mtumiaji ataona chaguo jipya lenye jina “Draw”, ambalo linamruhusu kuchora au kuandika alivyotaka moja kwa moja ndani ya DM. Instagram imesema maboresho haya yamelenga kuongeza ubunifu na njia za kujieleza kwa watumiaji wake, sambamba na kuboresha uzoefu wa mawasiliano binafsi. Kipengele hiki kinatarajiwa kuwafikia watumiaji wote duniani katika hatua za awali za masasisho mapya ya programu hiyo.

Read More
 Instagram Yaanzisha Mpangilio Mpya wa Tabs kwa Watumiaji

Instagram Yaanzisha Mpangilio Mpya wa Tabs kwa Watumiaji

Kampuni ya Meta imetangaza kuwa Instagram ipo mbioni kuanzisha mpangilio mpya wa tabs kwenye app hiyo maarufu, katika juhudi za kuboresha matumizi na kuongeza ufanisi kwa watumiaji. Katika mabadiliko hayo mapya, watumiaji wataweza ku-swipe kwenda kushoto au kulia kubadilisha tabs, ikiwa ni pamoja na sehemu za Home, Reels, DMs (Direct Messages), na Search. Mpangilio huu mpya unalenga kupunguza idadi ya mibofyo (clicks) na kufanya urambazaji ndani ya app kuwa wa haraka na wenye mtiririko rahisi zaidi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Instagram, style hii mpya inafanana kwa kiasi fulani na muundo wa TikTok, ambao umejizolea umaarufu kutokana na interface yake nyepesi na ya kisasa. Watumiaji wataweza kufikia sehemu wanazozitumia mara kwa mara kwa urahisi zaidi kama vile kutazama video fupi (Reels), kutuma ujumbe, au kufanya utafutaji ndani ya app. Mabadiliko haya yanakuja wakati Instagram ikiendelea kujiboresha kukabiliana na ushindani mkali kutoka kwa majukwaa mengine ya kijamii kama TikTok na Snapchat, huku ikilenga kuwapa watumiaji wake uzoefu wa kisasa, unaozingatia urahisi na kasi. Instagram haijatangaza rasmi tarehe ya kuanza kwa mabadiliko haya kwa watumiaji wote, lakini maboresho haya yanatarajiwa kuanza kutekelezwa hatua kwa hatua katika masasisho yajayo ya app.

Read More
 Instagram Yaanza Kubadilisha Mwonekano wa Navigation Bar

Instagram Yaanza Kubadilisha Mwonekano wa Navigation Bar

Mtandao wa kijamii wa Instagram umeanza kufanya mabadiliko mapya katika mwonekano wa Navigation Bar ile sehemu ya chini ya programu ili kurahisisha matumizi na kuboresha uzoefu wa watumiaji. Katika mwonekano mpya, Instagram imepanga upya baadhi ya vipengele muhimu kama ifuatavyo: Sehemu ya DM (Direct Messages) itahamishwa chini, jambo litakaloiwezesha kuonekana kwa urahisi zaidi na kufikiwa haraka na watumiaji. Sehemu ya kuweka post mpya (+) sasa itakuwa juu kushoto badala ya kuwa katika Navigation Bar ya chini. Hii inamaanisha alama ya “+” haitakuwepo tena kwenye sehemu ya chini ya skrini. Logo ya Instagram itahamishwa kutoka upande wa kushoto na sasa itaonekana katikati ya skrini, ikitoa mwonekano wa kisasa zaidi. Watumiaji watakapofungua Home, badala ya kuona picha pekee, sasa wataanza kuona video za Reels, sawa na mfumo unaotumika kwenye TikTok. Sehemu ya Search itahamishwa chini, kwenye nafasi iliyokuwa inatumiwa na icon ya Reels, huku Reels zikihamishwa kwenda kwenye nafasi ya Search. Instagram imesema mabadiliko haya yanalenga kutoa kipaumbele zaidi kwa Reels kutokana na umaarufu wake mkubwa. Sehemu ya Notifications itabaki juu ya skrini kama ilivyokuwa awali, na haitaguswa na mabadiliko haya. Instagram imesema mabadiliko hayo yataanza kuonekana kwa watumiaji hatua kwa hatua duniani kote, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake za kuboresha mwingiliano wa watumiaji na kuongeza muda wa matumizi ya programu hiyo.

Read More
 Instagram Yaingia Kundi la Apps Zenye Watumiaji Bilioni 3

Instagram Yaingia Kundi la Apps Zenye Watumiaji Bilioni 3

Mtandao wa kijamii wa Instagram umetangaza rasmi kuwa sasa umefikisha wastani wa watumiaji bilioni 3 kwa mwezi, hatua kubwa inayoiweka kwenye orodha ya apps tatu pekee duniani kufikia kiwango hicho cha juu cha matumizi. Instagram sasa inaungana na Facebook na WhatsApp, ambazo pia zinamilikiwa na kampuni ya Meta, katika “chama cha Bil 3”, kundi la majukwaa ya kidijitali yanayotumika na zaidi ya watu bilioni 3 kila mwezi. Facebook ilikuwa ya kwanza kufikia idadi hiyo, ikifuatiwa na WhatsApp ambayo ilifikia watumiaji bilioni 3 mwezi Mei 2025. Kwa upande wake, Instagram ilikuwa na bilioni 2 Desemba 2021, na sasa imeongeza watumiaji bilioni moja zaidi ndani ya kipindi cha takribani miaka minne. Kufikia mafanikio haya makubwa, Instagram imeendelea kuvutia watumiaji kupitia huduma mpya kama Reels, maboresho kwenye Stories, na uhusiano wa karibu na biashara ndogondogo kupitia vipengele vya e-commerce. Kwa ujumla, mafanikio haya yanaonesha wazi nguvu ya kampuni mama ya Meta, ambayo sasa inadhibiti majukwaa makubwa matatu yenye ushawishi mkubwa zaidi duniani kwenye sekta ya mitandao ya kijamii na mawasiliano ya kidijitali.

Read More
 Instagram Yazindua App Rasmi kwa Watumiaji wa iPad

Instagram Yazindua App Rasmi kwa Watumiaji wa iPad

Instagram imetangaza rasmi kuanzisha programu maalum kwa watumiaji wa iPad, hatua inayokuja baada ya zaidi ya miaka 15 ya huduma hiyo kupatikana kwa watumiaji wa simu pekee. Tangu kuzinduliwa kwake mwaka 2010, Instagram haijawahi kuwa na toleo rasmi kwa iPad, hali iliyowalazimu watumiaji kutumia app ya iPhone ambayo haikuwa na muonekano unaoendana na skrini kubwa ya iPad. Katika toleo hili jipya, Instagram imefanya mabadiliko kadhaa ya kimtindo na kimuundo. Ukurasa wa mwanzo wa app ya iPad umejikita zaidi kwenye maudhui ya video fupi (Reels) badala ya picha na machapisho ya kawaida (Feeds), tofauti na ilivyo kwenye toleo la simu. Aidha, sehemu ya maoni sasa inaweza kusomwa bila kuvuruga uonyeshaji wa video, na watumiaji wataweza kufungua ujumbe wa moja kwa moja huku wakiendelea kuona orodha ya mazungumzo yao upande mwingine wa skrini. Ripoti za hivi karibuni zinaonesha kuwa watoto na vijana wengi hutumia iPad kwa matumizi ya burudani, hasa kupitia TikTok, ambayo tayari imewekeza katika matumizi ya iPad na Smart TV. Hatua ya Instagram kuzindua toleo hili inatazamwa kama njia ya kuingia rasmi kwenye ushindani wa jukwaa la maudhui ya video, likiwa linalenga kuvutia kundi hilo la watumiaji na kuongeza muda wa matumizi kwenye jukwaa hilo.

Read More
 Instagram Yazindua Kipengele Kipya cha Folders Katika DM

Instagram Yazindua Kipengele Kipya cha Folders Katika DM

Instagram imeanza kuweka sehemu mpya inayowezesha watumiaji kuongeza folders katika upande wa ujumbe wa moja kwa moja (DM). Hatua hii inalenga kurahisisha upangaji na upatikanaji wa ujumbe, hasa kwa wale wanaopokea jumbe nyingi kila siku. Kupitia maboresho haya, watumiaji sasa wanaweza kutenganisha jumbe kwa urahisi kulingana na makundi tofauti. Mfano, mtu anaweza kutenganisha jumbe za waliyojibu kupitia Instagram Stories, kuweka tofauti kati ya jumbe kutoka kwa Followers na wale ambao si Followers, kutenga jumbe za kibiashara, pamoja na jumbe kutoka kwa akaunti zilizo na alama ya kuthibitishwa (verified). Kipengele hiki kinatarajiwa kuwasaidia sana wafanyabiashara, wabunifu wa maudhui na watumiaji wenye ufuasi mkubwa ambao mara nyingi hukumbwa na changamoto ya kusimamia mawasiliano mengi kwa wakati mmoja. Kwa sasa Instagram inalisambaza kipengele hiki hatua kwa hatua, na katika muda mfupi ujao watumiaji wote duniani wataweza kufurahia urahisi huu mpya wa kusimamia ujumbe wao.

Read More
 META Yapiga Marufuku Wizi wa Maudhui Mitandaoni

META Yapiga Marufuku Wizi wa Maudhui Mitandaoni

Kampuni ya Meta, inayomiliki mitandao ya kijamii ya Facebook, Instagram, na Threads, imetangaza kuwa inaanza kuchukua hatua kali dhidi ya akaunti ambazo zinashiriki au kuchapisha upya (repost) maudhui ya akaunti nyingine bila ruhusa au kibali. Kupitia taarifa rasmi, Meta imesema kuwa sera hii inalenga kulinda haki miliki za watumiaji, kuhamasisha ubunifu wa asili, na kupunguza wizi wa maudhui mtandaoni. Akaunti zitakazobainika kukiuka sera hii zitawekewa vikwazo vya kufikia watumiaji wengine (reach restriction), kusimamishwa kwa muda, au hata kufungiwa kabisa. “Hii ni hatua ya kuhakikisha kuwa watu wanaotumia muda na juhudi zao kuunda maudhui wanapewa heshima na ulinzi wanaostahili,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo. Watumiaji sasa wanahimizwa kuhakikisha wanapata kibali kabla ya kushiriki tena maudhui ya wengine, hasa ya akaunti za kibiashara, wasanii, au waandishi wa habari. Hatua hii imepokelewa kwa hisia mseto, huku baadhi ya watumiaji wakiiunga mkono kwa kusema inalinda ubunifu, ilhali wengine wakieleza wasiwasi kuwa huenda ikapunguza usambazaji wa taarifa muhimu na burudani mtandaoni. Meta inatarajiwa kuanza kutekeleza hatua hizi kikamilifu katika siku chache zijazo, huku ikiwataka watumiaji kusoma na kuelewa masharti ya matumizi ya mitandao yao kwa kina.

Read More
 Instagram Yathibitisha Majaribio ya Kipengele Kipya cha Repost

Instagram Yathibitisha Majaribio ya Kipengele Kipya cha Repost

Kampuni ya Instagram imethibitisha kuwa ipo katika hatua za majaribio ya kipengele kipya kitakachowaruhusu watumiaji wake kushiriki tena (repost) machapisho ya wengine moja kwa moja kwenye wasifu wao. Katika taarifa rasmi, Instagram ilieleza kuwa kipengele hiki kinachojaribiwa kwa sasa na watumiaji wachache kinalenga kurahisisha usambazaji wa maudhui, bila kuhitaji kutumia mbinu za ziada kama screenshot au programu za watu wa tatu. Kipengele cha repost kitafanana kwa kiasi fulani na kile kinachopatikana kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), ambapo watumiaji wanaweza kushiriki tena machapisho ya wengine kwa kubofya tu. Kwa mujibu wa Instagram, repost zitakuwa zinaonekana kwenye tab maalum katika wasifu wa mtumiaji, tofauti na machapisho ya kawaida. Hatua hii imepokelewa kwa maoni tofauti mitandaoni. Baadhi ya watumiaji wamekaribisha mabadiliko hayo wakisema yataongeza ushirikiano na ueneaji wa maudhui, huku wengine wakihofia uwezekano wa maudhui ya watu kutumiwa vibaya bila ridhaa au muktadha sahihi. Instagram, ambayo ni chini ya kampuni mama ya Meta, imesisitiza kuwa lengo la kipengele hicho ni kusaidia watumiaji kushirikiana zaidi na kuonyesha maudhui yanayowavutia au kuwagusa kwa urahisi. Endapo majaribio yatafanikiwa, kipengele cha repost kinatarajiwa kuzinduliwa rasmi kwa watumiaji wote duniani katika miezi ijayo.

Read More
 Instagram Yaboresha DM kwa Kutafsiri Ujumbe wa Sauti na Kuongeza Muda

Instagram Yaboresha DM kwa Kutafsiri Ujumbe wa Sauti na Kuongeza Muda

Kampuni ya Meta imeendelea kuboresha huduma zake kwa watumiaji wa Instagram kwa kutangaza mabadiliko mapya katika sehemu ya ujumbe wa moja kwa moja (DM). Maboresho hayo yanahusisha uwezo wa kutafsiri ujumbe wa sauti kuwa maandishi (voice message transcription), pamoja na kuongeza muda wa ujumbe wa sauti kutoka dakika 1 hadi dakika 5. Kwa mara ya kwanza, watumiaji wa Instagram sasa wataweza kuona maneno ya ujumbe wa sauti kama maandishi, jambo linalowezesha mawasiliano kuwa rahisi hata pale ambapo mtu hawezi kusikiliza sauti moja kwa moja. Kipengele hiki kinatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa watumiaji walioko katika mazingira ya utulivu au wale wenye changamoto ya kusikia. Aidha, kwa muda mrefu, ujumbe wa sauti katika DM ulikuwa umewekewa kikomo cha dakika moja tu. Lakini kwa maboresho haya, watumiaji sasa wanaweza kutuma ujumbe wa sauti wa hadi dakika tano, jambo linalowapa uhuru zaidi wa kueleza na kuwasiliana bila kukatizwa. Mabadiliko haya ni sehemu ya juhudi za Meta kuboresha uzoefu wa watumiaji kwenye majukwaa yake, huku Instagram ikiendelea kushindana na majukwaa mengine ya mawasiliano kama WhatsApp, Telegram, na Signal.

Read More