META Yapiga Marufuku Wizi wa Maudhui Mitandaoni

META Yapiga Marufuku Wizi wa Maudhui Mitandaoni

Kampuni ya Meta, inayomiliki mitandao ya kijamii ya Facebook, Instagram, na Threads, imetangaza kuwa inaanza kuchukua hatua kali dhidi ya akaunti ambazo zinashiriki au kuchapisha upya (repost) maudhui ya akaunti nyingine bila ruhusa au kibali. Kupitia taarifa rasmi, Meta imesema kuwa sera hii inalenga kulinda haki miliki za watumiaji, kuhamasisha ubunifu wa asili, na kupunguza wizi wa maudhui mtandaoni. Akaunti zitakazobainika kukiuka sera hii zitawekewa vikwazo vya kufikia watumiaji wengine (reach restriction), kusimamishwa kwa muda, au hata kufungiwa kabisa. “Hii ni hatua ya kuhakikisha kuwa watu wanaotumia muda na juhudi zao kuunda maudhui wanapewa heshima na ulinzi wanaostahili,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo. Watumiaji sasa wanahimizwa kuhakikisha wanapata kibali kabla ya kushiriki tena maudhui ya wengine, hasa ya akaunti za kibiashara, wasanii, au waandishi wa habari. Hatua hii imepokelewa kwa hisia mseto, huku baadhi ya watumiaji wakiiunga mkono kwa kusema inalinda ubunifu, ilhali wengine wakieleza wasiwasi kuwa huenda ikapunguza usambazaji wa taarifa muhimu na burudani mtandaoni. Meta inatarajiwa kuanza kutekeleza hatua hizi kikamilifu katika siku chache zijazo, huku ikiwataka watumiaji kusoma na kuelewa masharti ya matumizi ya mitandao yao kwa kina.

Read More
 Instagram Yathibitisha Majaribio ya Kipengele Kipya cha Repost

Instagram Yathibitisha Majaribio ya Kipengele Kipya cha Repost

Kampuni ya Instagram imethibitisha kuwa ipo katika hatua za majaribio ya kipengele kipya kitakachowaruhusu watumiaji wake kushiriki tena (repost) machapisho ya wengine moja kwa moja kwenye wasifu wao. Katika taarifa rasmi, Instagram ilieleza kuwa kipengele hiki kinachojaribiwa kwa sasa na watumiaji wachache kinalenga kurahisisha usambazaji wa maudhui, bila kuhitaji kutumia mbinu za ziada kama screenshot au programu za watu wa tatu. Kipengele cha repost kitafanana kwa kiasi fulani na kile kinachopatikana kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), ambapo watumiaji wanaweza kushiriki tena machapisho ya wengine kwa kubofya tu. Kwa mujibu wa Instagram, repost zitakuwa zinaonekana kwenye tab maalum katika wasifu wa mtumiaji, tofauti na machapisho ya kawaida. Hatua hii imepokelewa kwa maoni tofauti mitandaoni. Baadhi ya watumiaji wamekaribisha mabadiliko hayo wakisema yataongeza ushirikiano na ueneaji wa maudhui, huku wengine wakihofia uwezekano wa maudhui ya watu kutumiwa vibaya bila ridhaa au muktadha sahihi. Instagram, ambayo ni chini ya kampuni mama ya Meta, imesisitiza kuwa lengo la kipengele hicho ni kusaidia watumiaji kushirikiana zaidi na kuonyesha maudhui yanayowavutia au kuwagusa kwa urahisi. Endapo majaribio yatafanikiwa, kipengele cha repost kinatarajiwa kuzinduliwa rasmi kwa watumiaji wote duniani katika miezi ijayo.

Read More
 Instagram Yaboresha DM kwa Kutafsiri Ujumbe wa Sauti na Kuongeza Muda

Instagram Yaboresha DM kwa Kutafsiri Ujumbe wa Sauti na Kuongeza Muda

Kampuni ya Meta imeendelea kuboresha huduma zake kwa watumiaji wa Instagram kwa kutangaza mabadiliko mapya katika sehemu ya ujumbe wa moja kwa moja (DM). Maboresho hayo yanahusisha uwezo wa kutafsiri ujumbe wa sauti kuwa maandishi (voice message transcription), pamoja na kuongeza muda wa ujumbe wa sauti kutoka dakika 1 hadi dakika 5. Kwa mara ya kwanza, watumiaji wa Instagram sasa wataweza kuona maneno ya ujumbe wa sauti kama maandishi, jambo linalowezesha mawasiliano kuwa rahisi hata pale ambapo mtu hawezi kusikiliza sauti moja kwa moja. Kipengele hiki kinatarajiwa kuwa msaada mkubwa kwa watumiaji walioko katika mazingira ya utulivu au wale wenye changamoto ya kusikia. Aidha, kwa muda mrefu, ujumbe wa sauti katika DM ulikuwa umewekewa kikomo cha dakika moja tu. Lakini kwa maboresho haya, watumiaji sasa wanaweza kutuma ujumbe wa sauti wa hadi dakika tano, jambo linalowapa uhuru zaidi wa kueleza na kuwasiliana bila kukatizwa. Mabadiliko haya ni sehemu ya juhudi za Meta kuboresha uzoefu wa watumiaji kwenye majukwaa yake, huku Instagram ikiendelea kushindana na majukwaa mengine ya mawasiliano kama WhatsApp, Telegram, na Signal.

Read More
 INSTAGRAM YAWEKA UTARATIBU WA KUHAKIKI UMRI WA WATUMIAJI WAKE

INSTAGRAM YAWEKA UTARATIBU WA KUHAKIKI UMRI WA WATUMIAJI WAKE

Instagram ni app ambayo inataka watumiaji wote wawe na umri wa miaka 13 na kuendelea. Akaunti za watoto ambao wana umri chini ya hapo zitakuja kudhibitiwa. Instagram ina utaratibu maalum kwa watumiaji wa Miaka 13 mpaka 17: Akaunti zao ni lazima ziwe Private na hazina matangazo. Kampuni ya Meta imetoa ufafanuzi kuhusu utaratibu mpya wa kuhakiki umri wa watumiaji. Katika utaratibu mpya ambao umeanza kwa baadhi ya nchi, watumiaji watalazimika kuthibitisha umri kwa kujipiga Video ya Selfie huku ukiwa unageuka pande zote kuonyesha uso wako. Kisha baada ya kuchukua video ya selfie, utaituma Instagram na itakaguliwa kuthibitisha umri wako. Majibu ya kuthibitisha umri wako yanatoka kuanzia baada ya dakika 20. Instagram imeshirikiana na kampuni ya Yoti; ambayo ni kampuni kubwa duniani inayohusika na kuhakiki umri na details za mtu kwa kutumia picha. mfumo wake unakagua bila kufahamu picha ya mtu, bila kuhifadhi picha ambazo zinahakikiwa na safe katika kutunza data zake. Hatua nyingine ni kupiga picha kitambulisho au cheti za kuzaliwa. Na njia nyingine ni Vouching; ambapo unaweza kuomba mtu mzima athibitishe kuwa wewe ni mtoto. Akaunti ya mtu anayethibitisha hairuhusiwi kuthibitisha mtu zaidi ya mmoja              

Read More
 INSTAGRAM KUWEKA SEHEMU YA KUPOST KATIKA TOVUTI YAKE

INSTAGRAM KUWEKA SEHEMU YA KUPOST KATIKA TOVUTI YAKE

Mtandao wa Instagram unatarajiwa kuweka uwezo wa kupost kwa kutumia tovuti ya Instagram katika kompyuta. Watumiaji wa kompyuta watakuwa na uwezo wa ku-upload videos na picha katika akaunti za Instagram kwa kupitia website ya Instagram. Hii ni feature ambayo watu wengi sana wanaihitaji hasa Account Managers na watu ambao wanatumia kompyuta katika shughuli mbalimbali. Badala ya ku-copy content kwenye simu ili utumia app ya Instagram katika simu, watu watakuwa na uwezo wa kutumia kompyuta kupost Instagram. Feature hii imechelewa sana kuwekwa kwa kampuni ya facebook imekuwa iki-promote app ya Instagram. Facebook imekuwa na full-features katika tovuti  yake lakini bado haikuweka feature ya kupost katika tovuti ya Instagram. Feature hii inaanza kutoka wiki hii kwa baadhi ya watumiaji  ila itatoka taratibu kwa watumiaji wote wa tovuti ya Instagram.

Read More
 INSTAGRAM KULETA FEATURE MAALUM YA KUTOA TAARIFA ZA MATATIZO YA KIUFUNDI YANAYOJITEKEZA

INSTAGRAM KULETA FEATURE MAALUM YA KUTOA TAARIFA ZA MATATIZO YA KIUFUNDI YANAYOJITEKEZA

Kufuatia taharuki ambayo imekuwa ikijitokeza kwa watumiaji pale ambapo mtandao wa Instagram unakuwa umekumbwa na matatizo ya kiufundi, sasa mtandao huo umeanza majaribio ya ‘feature’ mpya ambayo itakuwa ikitoa taarifa pale linapojitokeza tatizo hilo. Taarifa hiyo itakuwa ikitokea kwa mfumo wa notification kwenye ukurasa wa mtumiaji wa mtandao huo kumjulisha kuwa limejitokeza tatizo la kiufundi.

Read More
 INSTAGRAM YAONDOA IGTV

INSTAGRAM YAONDOA IGTV

Mtandao wa Instagram umetangaza kuunganisha IGTV (video ndefu) na video za Feeds (video za posts za kawaida) ambapo zote zitaitwa Instagram Video.   Instagram imeondoa jina la IGTV na video ndefu zitabaki kama kawaida lakini hazitaitwa IGTV. Video za feeds ambazo huwa na urefu wa sekunde 60, zote zitaitwa Instagram Video huku Reels zikibaki kuwa video fupi ambazo zitakuwa na style ya video za TikTok.   Katika profile za watumiaji wa Instagram, itabaki tab ya Feeds ambayo itakuwa na posts za picha, Reels, na Instagram Videos na app ya IGTV itaitwa Instagram TV.            

Read More