Instagram Yaingia Kundi la Apps Zenye Watumiaji Bilioni 3
Mtandao wa kijamii wa Instagram umetangaza rasmi kuwa sasa umefikisha wastani wa watumiaji bilioni 3 kwa mwezi, hatua kubwa inayoiweka kwenye orodha ya apps tatu pekee duniani kufikia kiwango hicho cha juu cha matumizi. Instagram sasa inaungana na Facebook na WhatsApp, ambazo pia zinamilikiwa na kampuni ya Meta, katika “chama cha Bil 3”, kundi la majukwaa ya kidijitali yanayotumika na zaidi ya watu bilioni 3 kila mwezi. Facebook ilikuwa ya kwanza kufikia idadi hiyo, ikifuatiwa na WhatsApp ambayo ilifikia watumiaji bilioni 3 mwezi Mei 2025. Kwa upande wake, Instagram ilikuwa na bilioni 2 Desemba 2021, na sasa imeongeza watumiaji bilioni moja zaidi ndani ya kipindi cha takribani miaka minne. Kufikia mafanikio haya makubwa, Instagram imeendelea kuvutia watumiaji kupitia huduma mpya kama Reels, maboresho kwenye Stories, na uhusiano wa karibu na biashara ndogondogo kupitia vipengele vya e-commerce. Kwa ujumla, mafanikio haya yanaonesha wazi nguvu ya kampuni mama ya Meta, ambayo sasa inadhibiti majukwaa makubwa matatu yenye ushawishi mkubwa zaidi duniani kwenye sekta ya mitandao ya kijamii na mawasiliano ya kidijitali.
Read More