Jovial Aonya Wasichana Kuhusu Safari ya Uzazi

Jovial Aonya Wasichana Kuhusu Safari ya Uzazi

Nyota wa muziki kutoka Kenya, Jovial, amewapa changamoto mabinti wenye mioyo dhaifu kufikiria mara mbili kabla ya kuingia kwenye safari ya ujauzito na kujifungua. Kupitia Instastory, Jovial amefunguka kuhusu changamoto ambazo amekutana nazo wakati wa ujauzito na hata baada ya kujifungua, akisema kuwa ni safari yenye kuhitaji nguvu za mwili na akili. Amesema amekosa usingizi kutokana na usumbufu wa mtoto mchanga, hali ambayo imemfanya atambue kwa undani ugumu wa safari ya uzazi. Lakini pia kipindi hiki kimempa mtazamo mpya juu ya nguvu na uvumilivu unaohitajika na mama katika malezi ya mtoto. Kwa mujibu wake, pamoja na furaha kubwa ya kumpakata mtoto, hatua ya uzazi huambatana na changamoto ngumu kama uchovu wa mwili, mabadiliko ya homoni, na msongo wa mawazo unaoweza kuathiri afya ya mama. Hata hivyo amesema kuwa lengo lake si kuwatisha wasichana, bali ni kuwasisitizia umuhimu wa maandalizi ya kisaikolojia na kifedha kabla ya kuingia kwenye hatua ya uzazi.

Read More
 Jovial Afunguka Sababu ya Kutoanika Mtoto Wake Mitandaoni

Jovial Afunguka Sababu ya Kutoanika Mtoto Wake Mitandaoni

Mwanamuziki maarufu wa Kenya, Jovial, amefunguka kuhusu uamuzi wake wa kutoweka sura au jina la mtoto wake kwenye mitandao ya kijamii. Kupitia ukurasa wake wa Instastori, Jovial alisema kuwa hatua hiyo ni njia yake ya kumlinda mtoto wake dhidi ya madhara ya maneno na mitazamo hasi inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii. Alisisitiza kuwa, kama mzazi, jukumu lake la kwanza ni kuhakikisha usalama na utulivu wa mtoto wake. Kauli yake ilikuja baada ya shabiki mmoja kumuuliza kwa nini hadi sasa hajawahi kushirikisha mashabiki taarifa zozote kumhusu mtoto wake, tofauti na mastaa wengine ambao huanika familia zao hadharani. Jovial ameungana na orodha ya wasanii na watu mashuhuri ambao huchagua kutokuweka wazi maisha ya watoto wao, wakiamini kuwa faragha ni kinga muhimu katika ulimwengu wa kidijitali wenye changamoto nyingi.

Read More
 Jovial Atangaza Mapumziko ya Mitandao Baada ya Kujifungua

Jovial Atangaza Mapumziko ya Mitandao Baada ya Kujifungua

Mwanamuziki nyota wa Kenya, Jovial, ametangaza kuwa atachukua mapumziko kwenye mitandao ya kijamii baada ya kujifungua mtoto wake. Kupitia taarifa kwa mashabiki wake, msanii huyo amesema ataepuka shughuli za mitandaoni kwa muda ili kufurahia muda wa faragha na mtoto wake mchanga. Amesisitiza kuwa muda huu utamwezesha kujiweka sawa kimwili na kiakili kwa utulivu. Hata hivyo, Jovial amewahakikishia mashabiki wake kwamba mapumziko hayo hayatazuia kazi yake ya muziki. Amefichua kuwa tayari ana nyimbo mpya zilizokamilika na zitaachiwa wakati wa likizo yake ya uzazi. Tangazo hilo limepokelewa kwa pongezi na jumbe za kumtakia heri kutoka kwa mashabiki na wasanii wenzake, wengi wakimsifu kwa kuipa kipaumbele afya yake huku akiendeleza kipaji chake cha muziki.

Read More
 Msanii Jovial Afunguka Kuhusu Safari Yake ya Ujauzito

Msanii Jovial Afunguka Kuhusu Safari Yake ya Ujauzito

Mwanamuziki maarufu wa Kenya, Jovial, ameweka wazi safari yake ya ujauzito ambayo anaiita kuwa mojawapo ya vipindi vigumu zaidi katika maisha yake ya hivi karibuni. Kupitia ujumbe aliouweka kwenye mitandao ya kijamii, Jovial ameeleza jinsi hali ya ujauzito ilivyomchosha na kumrudisha nyuma kiafya na kisaikolojia. Amesema wazi kuwa trimester ya kwanza (miezi mitatu ya mwanzo) ndiyo ilikuwa ngumu zaidi kwake, akifichua kuwa kulikuwa na wakati alikaa wiki nzima bila kuoga kutokana na uchovu na mabadiliko ya mwili. “Siwezi kudanganya, katika trimester yangu ya kwanza, niliishi wiki nzima bila hata kuoga. Nilikuwa nimechoka, sina hamu ya kitu chochote, mwili ulikuwa umelegea na akili ilikuwa mbali kabisa,” Aliandika Jovial Jovial, ambaye anajulikana kwa vibao kama Such Kinda Love na Jeraha, amesema alikuwa akipitia hisia kali ambazo zilimfanya ajihisi mnyonge na wakati mwingine kujiuliza kama hali hiyo ni ya kawaida kwa kila mwanamke mjamzito. Mashabiki wake wengi waliitikia kwa huruma na kumpa moyo, wakimtakia kila la heri katika safari yake ya uzazi. Wengine pia wamemsifu kwa kuwa mkweli na kueleza hadharani jambo ambalo wanawake wengi huwa wanapitia lakini huogopa kulizungumza. Jovial hajataja muda kamili wa kujifungua, lakini mashabiki wake wanaonekana kuwa na shauku ya kumuona mama mpya akiibuka tena na nguvu mpya katika muziki.

Read More
 Jovial Afunguka: Niliiba Taulo na Mashuka Ili Mtoto Apate Maziwa

Jovial Afunguka: Niliiba Taulo na Mashuka Ili Mtoto Apate Maziwa

Msanii nyota wa muziki nchini Kenya, Jovial, amefunguka kwa hisia kali kuhusu maisha magumu aliyowahi kupitia kabla ya umaarufu wake, akieleza kuwa aliwahi kuiba kwenye nyumba ya wageni (guest house) aliyokuwa akifanya kazi ili kumudu kulea binti yake mchanga. Kupitia Insta Story aliyochapisha jana kwenye mtandao wa Instagram, Jovial alisimulia kuwa wakati mmoja aliwahi kufanya kazi kama receptionist kwenye gesti moja huko Saba Saba, Mombasa, na kutokana na hali ngumu ya maisha, alilazimika kuiba mashuka na taulo kutoka gesti hiyo na kuyauza ili kupata pesa za kumtunza mwanawe aliyekuwa na umri wa miezi minne wakati huo. “Salo ilikuwa kidogo… a mother and child needed to survive. Tukibadilisha sheets na towels, usiku tunaiuza, tunagawanya hiyo doo Gai! Msinihukumu… Mungu hakutaka kuwe na CCTV juu singepata pesa ya maziwa ya mtoto.” aliandika Jovial. Jovial amesema kuwa, licha ya hayo yote, anakumbuka kwa shukrani hatua aliyopiga maishani na anajivunia kuwa mama ambaye hajawahi kata tamaa. Ameongeza kuwa kumbukumbu hizo humvunja moyo wakati mwingine, lakini pia humkumbusha kuwa bila matatizo hayo, hangejifunza kuwa imara na mwenye msimamo dhabiti kama alivyo leo. Jovial amewatia moyo mashabiki wake wanaopitia hali ngumu kwa sasa, akiwaambia wakae imara, kwani Mungu hutoa nafasi mpya kwa kila mmoja. “Cheki mtu akifanikiwa, usione kama hafai kuwa hapo… ni Mungu na yeye tu wanajua place ametoka!” Jovial alihitimisha kwa ujumbe kwa mashabiki na watu wanaopitia changamoto Kwa sasa Jovial anaendelea kufanya vizuri kwenye muziki, na simulizi yake imewagusa mashabiki wengi ambao wameonyesha heshima kubwa kwa ujasiri wake wa kusema ukweli kuhusu maisha yake ya awali.

Read More
 Msanii Jovial Atangaza Ujauzito Kupitia Wimbo Mpya “Chibaby”

Msanii Jovial Atangaza Ujauzito Kupitia Wimbo Mpya “Chibaby”

Msanii maarufu wa muziki wa Kenya, Jovial, ametangaza rasmi kuwa anatarajia mtoto na mchumba wake, Mike, kupitia wimbo wake mpya unaoitwa “Chibaby”, ambao tayari umeanza kuvuma mitandaoni. Taarifa hiyo ya kufurahisha ilifichuliwa kupitia video ya kipekee aliyopakia kwenye ukurasa wake wa Instagram, ambapo alionekana akiwa mwenye furaha tele, akicheza na kuimba kwa bashasha huku akionyesha wazi tumbo la ujauzito. Video hiyo iliwagusa mashabiki wake wengi, ambao walimiminika kwenye sehemu ya maoni kumpa pongezi na salamu za heri kwa hatua hiyo kubwa ya maisha. Katika wimbo wa Chibaby aliyomshirikisha msanii wa Biongofleva Ibraah, Jovial anasifia mapenzi ya dhati, amani ya ndoa, na furaha ya kutarajia mtoto. Mashairi ya wimbo huo yanadhihirisha hisia za shukrani na matumaini, huku akimtaja mchumba wake kama mshirika wa kwelin a mtoto wao kama zawadi ya maisha. Mtoto anayetarajiwa atakuwa wa kwanza kwa Jovial na Mike, na hatua hii imepokelewa kama mwanzo mpya katika safari yao ya kifamilia. Licha ya kuwa mmoja wa waimbaji walioweka alama katika muziki wa kisasa nchini Kenya, Jovial ameonyesha kuwa maisha ya wasanii hayahusu kazi pekee, bali pia kupanda na kushuka kwa maisha ya kawaida, ikiwemo uzazi na ujenzi wa familia. Mashabiki wanasubiri kwa hamu zaidi taarifa kutoka kwa msanii huyo kuhusu ujio wa mtoto na mipango yake ya baadaye, huku wengine wakimtaja kama mfano wa kuigwa kwa usawa wa kazi na maisha binafsi.  

Read More
 Wanaume wengi nchini Kenya wanaogopa ndoa – Jovial

Wanaume wengi nchini Kenya wanaogopa ndoa – Jovial

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Jovial amedai kwamba wanaume wengi siku hizi wanaogopa kuingia kwenye ndoa. Kupitia instastory yake ameandika ujumbe mrefu akisema kuwa wanaume wengi nchini wana afadhilisha kuzaa kwanza na wapenzi wao kabla ya kuhalalisha mahusiano yao kwa njia ya harusi. Msanii huyo anahoji kuwa wanaume wa karne hii hawaaminiki katika kuingia kwenye mahusiano ya kudumu kwani wengi wao wana kasumba ya kukatisha uchumba ghafla bila ya kutoa taarifa kwa wanawake wao. Jovial amesema kitendo cha watu kukimbia ndoa  kumpelekea maduka ya kuuza mavazi ya harusi kupungua sana nchini ikilinganishwa na mataifa ya nje, jambo ambalo anadai limewakosha wafanyibiashara fursa ya kuingiza kipato. Hata hivyo amedokeza mpango wa kutunga wimbo maalum kwa ajili ya wanaume wasiopenda masuala ya kufunga ndoa katika jamii.

Read More
 Jovial adokeza ujio wa EP yake mpya

Jovial adokeza ujio wa EP yake mpya

Mwimbaji nyota nchini, Jovial amethibitisha rasmi ujio wa EP yake mpya na ya kwanza katika safari yake ya muziki. Kupitia Instastory yake ameweka wazi mpango wake huo huku akisema kuwa amekamilisha mchakato wa kuiandaa EP hiyo. Lakini pia ameeleza kwamba, wimbo wa kwanza kutoka kwenye EP yake itaingia sokoni wiki mbili zijazo. Hata hivyo mrembo huyo bado hajaweka wazi jina na idadi ya nyimbo zitakazopatikana kwenye EP yake hiyo.

Read More
 Jovial atoa somo kwa wafanyibiashara wanaotumia picha za mastaa bila idhini yao

Jovial atoa somo kwa wafanyibiashara wanaotumia picha za mastaa bila idhini yao

Msanii nyota nchini Jovial ameshindwa kuwavumilia wafanyibiashara wanaotumia picha za mastaa kwenye matangazo bila ridhaa yao. Kupitia insta story kwenye mtandao wa Instagram mkali huyo wa sauti amewapa somo wafanyibiashara sampuli hiyo kwa kuwaita wabahili wa kutoa michongo kwa wasanii licha ya kuwa wanalipwa mkwanja mrefu na makampuni tofauti kufanikisha shughuli hiyo. Hitmaker huyo wa “Mi Amor” amehapa kumchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote atakayejaribu kutumia picha yake bila idhini kwenye matangazo ikizingatiwa kuwa ametumia pesa nyingi kuitengeneza brand au chapa yake. Hata hivyo amewataka walimwengu kuacha kasumba ya kutumia njia ya mkato kufanikisha michongo yao na badala yake amewaasa kutoa riziki kwa wenzao kutokana na uhitaji wa watu duniani kutaka kufanikisha ndoto zao maishani.

Read More
 Jovial akanusha uvumi wa kutoka kimapenzi na Willy Paul

Jovial akanusha uvumi wa kutoka kimapenzi na Willy Paul

Msanii wa kikw kutoka Kenya Jovial  kwa mara ya kwanza amevunja kimya chake kuhusu uvumi wa kutoka kimapenzi na msanii mwenzake Willy Paul. Akimjibu shabiki kupitia ukurasa wake wa Facebook, Jovial ameweka wazi kuwa Pozee sio mpenzi wake kama watu wanavyodai mitandaoni huku akisisitiza kuwa uhusiano wake na bosi huyo wa saldido ulikuwa wa kikazi tu na si vinginesvyo. “Je, Pozee ni mpenzi wako wa dhati?” Shabiki mmoja aliuliza. Jovial akamjibu “Itoshe! Pozee si mpenzi wangu! Ni rafiki tu, ilikuwa biashara ambapo sote tulipata faida! Kwa sasa tumerudi kwa maisha yetu ya kawaida,. Hitmaker huyo wa Mi Amor amesema ameamua kufichua hayo kwa kuwa ameshindwa kuvumilia maswali ya walimwengu wanaolazimisha uhusiano wake na Willy Paul wakati hakuna kitu inaendelea kati yao. “Nimekabwa na maswali yenu! Mungu anisaidie kwa yatakayofuata! Aiii! Mayooo!” ameandika Jovial. Utakumbuka wawili hao walihisiwa kutoka kimapenzi walipojiachia kimahaba Zaidi miezi kadhaa iliyopita wakati walikuwa watangaza wimbo wao wa pamoja uitwao “Lalala”

Read More
 Jovial aweka wazi sababu za kutofanya kazi na wasanii wa kike nchini Kenya

Jovial aweka wazi sababu za kutofanya kazi na wasanii wa kike nchini Kenya

Mwanamuziki nyota nchini Jovial amefunguka sababu ya kutoshirikiana na wasanii wa kike kwenye kazi zake za muziki. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Hitmaker huyo wa “Mi Amor” amesema kuwa wasanii wengi wa kike ni wanafiki na ndio maana amekuwa akifanya kolabo nyingi na wasanii wa kiume. Jovial amedai kwamba anapendelea sana kuwa na marafiki wa kiume kwa sababu ni watu ambao wana moyo wa kusaidia tofauti na wanawake huku akisema ubinafsi ambao wasanii wa kike wanao kwenye shughuli zao ndio imechangia muziki wa Kenya kuwa na wasanii wachache wanawake.

Read More
 Jovial akiri kukosa usingizi kisa kutongozwa na wanaume nyakati za usiku

Jovial akiri kukosa usingizi kisa kutongozwa na wanaume nyakati za usiku

Msanii nyota nchini Jovial amechukizwa na kitendo cha mwanaume mmoja kumkosesha amani nyakati za usiku kwa kumtaka kimapenzi. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram amesema mwanaume huyo ambaye kipindi cha nyuma aliagiza chakula kutoka kwake, amegeuka kuwa kero kwake kwa kumpigia simu kila mara jambo ambalo amedai limemkosesha usingizi. Hitmaker huyo wa “Mi Amor” ameenda mbali na kusema licha ya kuwa anashukuru kwamba jamaa huyo ni shabiki yake kimuziki, hatowavumilia watu sampuli hiyo ikizingatiwa kuwa anapenda kuishi maisha yake ya faraghani bila muingilio wa mtu yeyote. Hata hivyo ameutaka uongozi wake kuhamkikishia usalama kwavkubadilisha laini yake ya simu kwani amekuwa akipokea simu nyingi kutoka kwa watu wasiojulikana.

Read More