Msanii Jux Anyakua Tena Tuzo ya Jayli Nchini Ivory Coast

Msanii Jux Anyakua Tena Tuzo ya Jayli Nchini Ivory Coast

Msanii nyota wa Bongofleva, Juma Jux, ameendelea kudhihirisha ukubwa na ubora wake katika muziki wa Afrika Mashariki baada ya kutwaa kwa mara ya pili tuzo ya Jayli Awards nchini Ivory Coast. Kupitia mitandao ya kijamii, Jux ameonesha kufurahishwa na kutuzwa kama Msanii Bora wa Afrika Mashariki wa Mwaka, akitoa shukrani kwa waandaaji wa tuzo hizo pamoja na mashabiki wake. Lakini pia ameweka wazi kuwa ushindi huu anaumweka wakfu kwa mtoto wake, Rakeem, akionyesha upendo na fahari ya kuwa baba. Ushindi huo umeonekana kama uthibitisho wa kazi kubwa anayoweka katika muziki, huku nyimbo zake zikizidi kusikika ndani na nje ya Tanzania. Mashabiki na wadau mbalimbali wa muziki wameendelea kumpongeza, wakisema tuzo hiyo inadhihirisha mchango wake muhimu katika kukuza muziki wa Afrika Mashariki.

Read More
 Juma Jux na Mkewe Priscilla Wadokeza Mpango wa Kuhamia Kenya

Juma Jux na Mkewe Priscilla Wadokeza Mpango wa Kuhamia Kenya

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Juma Jux na mkewe kutoka Nigeria, Priscilla Ojo,wameibua msisimko mkubwa mtandaoni baada ya kudokeza mipango yao ya kuhamia nchini Kenya na kununua makazi mapya. Tetesi za wawili hao kuhama zilianza kusambaa baada ya kushiriki picha zenye mvuto na video fupi wakiwasili kwenye jumba la kifahari jijini Nairobi. Kitendo hicho kilizua uvumi na minong’ono mingi kuhusu hatua yao kubwa inayofuata kimaisha. Kuongeza chumvi kwenye habari hizo, kampuni ya usanifu wa mambo ya ndani ya Fine Urban Construction & Interiors pia ilichapisha picha za siri za jumba hilo la kifahari ambalo inadaiwa wawili hao wanalimezea mate. Hatua hii imefurahisha mashabiki wao, ambao sasa wanangoja kwa hamu kuthibitishwa rasmi kwa uamuzi huo wa Jux na Priscilla kuhamishia makazi yao makuu nchini Kenya.

Read More
 Juma Jux Ampongeza Diamond kwa Kufungua Milango ya Kimataifa kwa Wasanii wa Bongo

Juma Jux Ampongeza Diamond kwa Kufungua Milango ya Kimataifa kwa Wasanii wa Bongo

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Juma Jux, amempongeza Diamond Platnumz kwa mchango wake mkubwa katika kufungua njia za kimataifa kwa wasanii wa Tanzania. Akizungumza katika mahojiano na El Mando TZ, Jux amesema kuwa Diamond ameonyesha mfano wa kuigwa kupitia matamasha yake makubwa aliyoandaa nchini Uingereza, ikiwemo London, Manchester na Glasgow mwezi Julai, ambayo yalitoa fursa kwa muziki wa Tanzania kufika hadhira ya kimataifa. Jux amesisitiza kuwa hatua kama hizo ni muhimu katika kuinua tasnia ya muziki wa Bongo Fleva, hasa pale msanii mmoja anapowapa nafasi wenzao kupata exposure kupitia majukwaa ya kimataifa. Jux ametolea mfano wasanii wa Nigeria ambao wanapoenda kufanya maonesho barani Ulaya, kama vile katika ukumbi wa O2 Arena, huwa hawasahau kuwashirikisha wasanii wenzao wa nyumbani. Hata hivyo amesema kuwa ni muhimu kwa wasanii wa Tanzania pia kuendeleza utamaduni huo wa kusaidiana, ili kuhakikisha muziki wa Bongo Fleva unaendelea kupanuka na kushindana kimataifa.

Read More
 Jux Atoa EP Maalum Kuelezea Safari Yake ya Mapenzi na Mkewe Priscy

Jux Atoa EP Maalum Kuelezea Safari Yake ya Mapenzi na Mkewe Priscy

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Juma Jux, ameachia rasmi kazi yake mpya ya muziki, EP iitwayo “A Day To Remember”, kama kumbukizi maalum ya ndoa yake na mkewe mpendwa, Priscy. Kupitia mitandao ya kijamii, Jux ameeleza kuwa mradi huu si kazi ya kawaida, bali ni simulizi ya maisha yao ya upendo, kuanzia mwanzo wa safari yao ya mahaba hadi furaha waliyonayo sasa kama wanandoa. EP hiyo imejaa hisia, utamaduni na usanii wa hali ya juu, ikiwa imeshirikisha mastaa wawili wakubwa: Phyno kutoka Nigeria na D Voice kutoka Tanzania. Jux ameamua kuunganisha ladha ya Afrika Mashariki na Magharibi ili kuwasilisha ujumbe wa upendo unaovuka mipaka ya lugha na mataifa. Kati ya watayarishaji walioweka mikono yao kwenye kazi hii ni S2kizzy, Foxx Made It, na Aykbeats, huku kazi ya mixing na mastering ikifanywa na Lizer Classic, jina kubwa katika ubora wa sauti Afrika. Katika ujumbe wake, Jux hakusita kumshukuru mkewe Priscy kwa kuwa chanzo cha msukumo wa EP hii, pamoja na familia yake, timu nzima ya wasanii na wahusika waliounga mkono kazi hiyo, na mashabiki waliomfuatilia kwa miaka mingi. Amesisitiza kuwa baada ya harusi yao rasmi, atatoa wimbo wa kipekee kama zawadi ya kufunga sura hii mpya ya maisha. EP “A Day To Remember” itapatikana kuanzia usiku wa leo kwenye majukwaa yote ya kidijitali ya kusikiliza muziki. Mashabiki tayari wameonyesha hamasa kubwa, wakisubiri kwa shauku kusikia mchanganyiko wa upendo na sanaa katika kazi hii ya kipekee.

Read More
 Juma Jux kuzindua Album yake mpya Desemba 7 mwaka huu

Juma Jux kuzindua Album yake mpya Desemba 7 mwaka huu

Mwimbaji nyota wa BongoFleva Juma Jux ametangaza kusogeza mbele uzinduzi wa album yake mpya King Of Hearts ambapo sasa uzinduzi huo utafanyika Disemba 7. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Jux ameeleza kwamba amefikia maamuzi hayo ili kuhakikisha wasanii wote walioshiriki kwenye album yake wana perform siku ya uzinduzi ndani ya ‘The Super Dome’ Masaki, Jijini Dar es salaam. Lakini pia amebainisha kwamba, siku hiyo ya uzinduzi itajawa na surprise kibao na kuweka historia. “Siku ya tarehe 7 Disemba nataka iwe siku ya Industry nzima kuweka historia. Kuanzia ukumbi ambao itafanyika Show hii, Stage, Mavazi, Performance na kila kitu “, ameeleza Juma Jux.

Read More
 MWANAMUZIKI WA BONGOFLEVA  JUMA JUX ATUA KENYA KWA AJILI YA MEDIA TOUR

MWANAMUZIKI WA BONGOFLEVA JUMA JUX ATUA KENYA KWA AJILI YA MEDIA TOUR

Mwanamuziki Bongofleva, Juma Jux ametua nchini Kenya kwa ajili ya media tour pamoja na kuitangaza brand yake ya African Boy. Akiongea na waandishi wa habari, Jux amesema kuwa dhumuni lake kuu la kutembea Kenya ni biashara lakini pia atawapa mashabiki zake kwa kutumbuiza kwenye moja ya show yake hivi karibuni. “Kuna kazi nimekuja kufanya na pia nimekuja kwa media tour na pia kuna club appearances,” alisema Juma Jux. Utakumbuka kwa sasa Jux anafanya vizuri na wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la “I Love You” ambao ameshirikiana na Gyakie kutoka Ghana.

Read More