Kim Kardashian akiri kupata ugumu kulea watoto na Kanye West

Kim Kardashian akiri kupata ugumu kulea watoto na Kanye West

Rapa Kanye West anampa wakati mgumu sana Baby Mama wake Kim Kardashian hasa kwenye malezi ya watoto wao baada ya kuachana. Kwenye mahojiano na Podcast ya Mtangazaji Angie Martinez, Kim amesema kushiriki kwenye suala la malezi na YE ni jambo gumu sana. “It’s hard. Co-parenting, it’s really fu**ing hard.”, Alisema kwa masikitiko. Aidha Kim Kardashian amedai kuwa hataki tofauti zake na Kanye West ziwaathiri watoto na namna wanavyomchukulia Baba yao. “Ninaweza kuwa napitia magumu mengi, lakini kama nipo kwenye gari ninawapeleka shule na wanataka kusikiliza nyimbo za Baba yao, haijalishi ni yapi tunapitia, inabidi nitabasamu na niweke nyimbo zake na nicheze kama hakuna kibaya kilichotokea. Nikiwashusha tu nakurudi nyumbani, naangua kilio.” alieleza Kim Kardashian

Read More
 Prodyuza Mike Dean atemana na Kanye West kisa sarakasi zake mtandaoni

Prodyuza Mike Dean atemana na Kanye West kisa sarakasi zake mtandaoni

Mtayarishaji na Mkandarasi (Engineer) wa muziki lakini pia rafiki wa muda mrefu wa rapa Kanye West aitwaye Mike Dean ametangaza kutemana na rapa huyo kufuatia mwenendo wake wa kila siku. Mike Dean ametoa ya moyoni kwa kusema Kanye amejikita kwenye kutafuta attention ya vyombo vya habari kuliko hata maisha yenyewe. Anasema YE amekuwa akifanya upuuzi ambao unapewa nafasi ya kuzungumzwa kwenye vyombo vya habari kiasi cha kuwanyima nafasi wanaofanya vizuri kisanaa na wanaostahili kuzungumzwa. Mike Dean amekuwa sehemu ya Kanye West kwenye muziki wake kwa kipindi kirefu akitayarisha Album zake na hata kuhusika kwenye matamasha yake mbali mbali upande wa sound.

Read More
 Kanye West ampatia Kim Kardashian nyumba baada ya mchakato wa talaka kukamilika

Kanye West ampatia Kim Kardashian nyumba baada ya mchakato wa talaka kukamilika

Rapa Kanye West amelazimika kumpatia Kim Kardashian nyumba ambayo aliinunua mwaka jana, ikiwa ni sehemu ya makubaliano yao ya Talaka ambayo yamefikia mwisho. Rapa huyo kutoka Marekani atahamisha umiliki wa nyumba hiyo kutoka kwenye jina lake kwenda kwa Kim. YE alinunua Jumba hilo Desemba 2021 kwa ($4.5 million) zaidi ya KSh. Milioni 551 likiwa pembeni ya makazi ya Kim Kardashian eneo la Hidden Hills ambapo alifanya hivyo kwa lengo la kuwa karibu na familia yake baada ya kuachana na mkewe.

Read More
 Kanye West na Kim Kardashian wafikia muafaka wa Talaka yao

Kanye West na Kim Kardashian wafikia muafaka wa Talaka yao

Rapa Kanye West na Kim Kardashian hatimaye wamefikia maridhiano ya Talaka na sasa YE atatakiwa kumlipa Kim Kardashian kiasi cha ($200k) zaidi ya Sh. Milioni 22 kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya watoto yaani Child support. Kubwa zaidi lililofikiwa muafaka ni haki sawa katika malezi ya watoto (equal access) ambapo awali ilikuwa ngumu kwa YE kupata nafasi ya hata kuwaona watoto wake. Japo imeelezwa kwamba watoto watatumia muda wao mwingi kwa Mama yao, jambo ambalo hata YE aliwahi kulipitisha. Itakumbukwa, Mwanamama Kim Kardashian mwezi Februari, mwaka jana alifungua shauri mahakamani la kudai Talaka baada ya kuwa kwenye ndoa kwa takribani miaka 7 na Kanye West.

Read More
 Kanye West amfukuza kazi mfanyakazi wake kisa Drake

Kanye West amfukuza kazi mfanyakazi wake kisa Drake

Rapa Kanye West ameripotiwa kumfukuza kazi mfanyakazi wake kwenye kampuni ya Yeezy kufuatia kupiga wimbo wa Drake ofisini. Hii ni kwa mujibu wa Rolling Stone. Utakumbuka juzi kati Drake alitapika nyongo kwenye “Circo Loco” ngoma ambayo inapatikana kwenye Album ya pamoja na 21 Savage, Her Loss. Drizzy alifunguka ya moyoni kwamba aliamua kupatana na Kanye West na kufanya onesho la pamoja (Free Larry Hoover Concert) Disemba 10, 2021 kwa sababu ya heshima tu ya godfather wake, J. Prince. “Linking with the opps, b*tch, I did that shit for J Prince. B*tch, I did it for the mob ties” – alichana Drizzy.

Read More
 Kanye West ashtakiwa kwa wizi wa wimbo

Kanye West ashtakiwa kwa wizi wa wimbo

Watu hawampumzishi Rapa KanyeWest kila siku wanampa msala mpya, Kampuni inayosimamia Kazi za B-Boy Records imedai kuwa Kanye West ameiba wimbo wa Boogie Down Productions wimbo unaitwa South Bronx ambao ulitoka Mwaka 1987. Kanye West anadaiwa kuiba wimbo huo na kutumia kwenye Wimbo wake wa Life Of The Party aliomshirikisha Andre 3000 Unaopatikana kwenye Album yake ya DONDA kama Bonus Track. Nyaraka zinasema kuwa hakukuwa na makubaliano yoyote baina ya Kampuni hiyo na Kanye West kutumia Kazi hiyo. Kupitia StepPlayer ya Kanye west ziliuzwa nakala 11000 ambapo inadaiwa YE aliingiza Mtonyo wa zaidi ya Dola Milioni 2 sawa na ziadi ya milioni 243 za Kenya.

Read More
 Drake amchana Kanye West na Megan Thee Stallion kupitia wimbo wa Circo Loco

Drake amchana Kanye West na Megan Thee Stallion kupitia wimbo wa Circo Loco

Rapa kutoka Marekani Drake ameamua kutapika nyongo kwenye “Circo Loco” ngoma ambayo inapatikana kwenye Album ya pamoja na 21 Savage, Her Loss. Drizzy amefunguka ya moyoni kwamba aliamua kupatana na Kanye West na kufanya onesho la pamoja (Free Larry Hoover Concert) Disemba 10, mwaka 2021 kwa sababu ya heshima tu ya godfather wake, J. Prince. “Linking with the opps, b*tch, I did that shit for J Prince. B*tch, I did it for the mob ties” – amechana Drizzy. Utakumbuka Drake pia kupitia hii single amemchana Megan Thee Stallion kufuatia madai yake ya kupigwa risasi na Tory Lanez kwa kusema kuwa alidanganya juu ya tukio hilo. “This b**ch lied about getting shot but she still a stallion. She don’t even get the joke but she still smiling.” amechana Drake.

Read More
 Adidas kuendelea kuuza bidhaa za Yeezy

Adidas kuendelea kuuza bidhaa za Yeezy

Kampuni ya mitindo na mavazi Adidas imetangaza kuendelea kuuza bidhaa za rapa Kanye West “Yeezy” bila kutumia jina hilo. Siku ya jana kampuni hio ilitangaza kuachana rasmi na rapa huyo, baada ya kauli zake za chuki dhidi ya watu wa jamii ya kiyahudi. “Bidhaa zote za Yeezy zitauzwa chini ya jina la Adidas na zitatambulika kama bidhaa za Adidas” – Chanzo kutokea Adidas. Kampuni ya Adidas imeripotiwa kuwa itapoteza takribani shillingi millioni 30 mwaka huu kufuatia kuvunja uhusiano wake Kibiashara na Kanye West.

Read More
 Kanye West aondolewa kwenye orodha ya mabilionea

Kanye West aondolewa kwenye orodha ya mabilionea

Muda mfupi baada ya kampuni ya Adidas kutangaza kuachana na rapa Kanye West, jarida la Forbes limeibuka na kutangaza kuwa rapa huyo ameondelewa rasmi kwenye orodha ya mabilionea kutokana na thamani yake ‘net worth’ kushuka. Kanye West amejikuta akiingia katika wakati mgumu baada ya kutoa kauli za chuki dhidi ya jamii ya watu wa kiyahudi wiki kadhaa zilizopita, kitendo kilichopelekea kampuni mbalimbali kama Balenciaga na Adidas kuvunja naye mkataba. Mikataba aliyoisani rapa huyo na makampuni mbalimbali makubwa duniani iliongeza thamani yake mpaka kufikia hatua ya kuwa Bilionea, lakini baada ya makampuni hayo kuachana naye thamani yake imeshuka.

Read More
 Adidas yavunja mkataba na Kanye West

Adidas yavunja mkataba na Kanye West

Kampuni ya Adidas imeripotiwa kuvunja uhusiano wake wa kibiashara na Kanye West kufuatia kauli yake ya chuki dhidi ya Jamii ya Wayahudi. “Kampuni ya Adidas haivumilii hata kidogo maneno ya chuki na hatarishi kwa Umma yaliyotolewa na Kanye West. Kampuni imeamua kuvunja mkataba na Kanye West pamoja na kusitisha bidhaa zote zilizokuwa na ushirikiano pamoja na Yeezy” Imesomeka sehemu ya taarifa ya Adidas iliyotolewa kwa Umma. Itakumbukwa, tayari makampuni mengine kama Def Jam Records, Balenciaga na CAA yaliyokuwa yakifanya kazi na Kanye West, yashajiondoa kufanya nae kazi kufuatia sakata hilo la kauli za chuki.

Read More
 Kim Kardashian akasirishwa na kauli za Kanye West

Kim Kardashian akasirishwa na kauli za Kanye West

Mwanamitindo na aliyekuwa mke wa rapa Kanye West, Kim Kardashian ameonyesha kukasirishwa na kauli za aliyekuwa mume wake kuhusiana na tuhuma alizozitoa juu ya watu wenye asili ya kiyahudi. Kupitia ukurasa wake wa twitter Kim Krdashian ameandika “Hotuba ya chuki siyo sawa au yenye udhuru, Nasimama pamoja na jamii ya watu wa kiyahudi na naomba kauli hizo za kigomvi na zenye chuki kuelekea kwa wayahudi zifikie mwisho haraka” – Kim Kardshian Wiki iliyopita rapa Kanye West alitoa maneno ya chuki juu ya watu wenye asili ya kiyahudi huku akisema kuwa vyombo vya habari vya watu wa jamii ya kiyahudi vimekuwa vikitoa habari za kichonganishi zenye lengo la kuharibu jamii ya watu wa Marekani. Watu wa jamii ya kiyahudi wamekasirishwa na kauli hizo za rapa huyo, huku wengi wakitishia kufungua kesi dhidi ya Kanye West

Read More
 Balenciaga waachana na Kanye West

Balenciaga waachana na Kanye West

Mtandao wa Tmz umeripoti kuwa kampuni ya mitindo na mavazi kutokea Paris, Ufaransa imeamua kuvunja ushirikiano katika uzalishaji wa mavazi kati yao na rapa kutoka nchini Marekani, Kanye West. “Balenciaga haina mpango wa kuendelea na ushirikiano kati yetu na Kanye West”- Chanzo cha kuaminika kutokea Tmz Chanzo hicho hakijaweka wazi sababu ya kampuni hiyo kuachana na rapa huyo wakati wiki kadhaa zilizopita Kanye alikuwa mmoja wa washiriki katika onyesho kubwa la mavazi ya kampuni hiyo huko jijini Paris.

Read More