KING KAKA ATANGAZA UJIO WA ZIARA YAKE YA MUZIKI NCHINI MAREKANI
Rapa King Kaka ametangaza ujio wa ziara yake ya muziki nchini marekani kwa kuanika mkeka wa miji ambayo atafanya shows zake. Kupitia ukurasa wao rasmi wa Instagram king kaka, ameipa ziara hiyo jina la Coast To Coast Summer 2022 USA Tour ambapo amesema itafanyika ndani ya miji 13. Ziara hiyo ambayo anafanya kwa ushirikiano na Rarequest Music Group inatarajiwa kuzunguka kwenye miji mbalimbali nchini Marekani ikiwemo Boston, Chicago, Minnesota, Atlanta, Dallas, na Los Angeles. Hata hivyo hajaweka tarehe na mwezi ambayo ataanza tour yake hiyo ila king kaka amewataka mashabiki zake kufuatilia mitandao yake ya kijamii kwani yupo mbioni kuweka mambo sawa.
Read More