Harmonize Atoa Wito kwa Wasanii Watumie Singeli Kuelimisha Jamii

Harmonize Atoa Wito kwa Wasanii Watumie Singeli Kuelimisha Jamii

Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania, Harmonize, amewataka wasanii kutumia muziki wa Singeli kuibua mijadala ya kijamii na kupeleka ujumbe wenye maana kwa jamii badala ya kuishia kwenye burudani ya kawaida. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize alisema kuwa Singeli ni mtindo wa muziki wenye nguvu kubwa ya ushawishi na unastahili kutumiwa kuelimisha, kukuza maadili, na kuunganisha vizazi vyote kwa ujumbe wake. Harmonize, anayefahamika pia kwa jina la Konde Boy, alisisitiza kuwa kutumia Singeli kwa maudhui ya kijamii kutaongeza thamani ya muziki huo na kuufanya upokelewe na watu wa rika zote, si kundi moja tu. “Singeli ni mziki mkubwa sana. Wasanii tuutumie kuimba mambo ya msingi yenye maana, si kila siku kufurahisha tu,” aliandika msanii huyo katika ujumbe wake uliopata mapokezi makubwa mtandaoni. Katika hatua nyingine, Harmonize alidokeza kuwa anatarajia kuachia nyimbo mbili kubwa za kimataifa (International Bangers) usiku mmoja ndani ya mwezi Julai. Alisema kuwa ngoma hizo zitakuwa za kipekee na atawashirikisha wasanii wawili wakubwa wa kimataifa, ingawa hakuwataja majina yao. Hii imeongeza hamasa miongoni mwa mashabiki wake waliotamani kuona sura mpya ya kimataifa kutoka kwa bosi huyo wa Konde Gang. Singeli kwa sasa ni miongoni mwa mitindo ya muziki inayoshika kasi sana Tanzania. Julai 3, tulishuhudia msanii mkubwa wa Bongo Flava, Alikiba, akiachia wimbo wake wa kwanza wa Singeli uitwao Ubuyu, ambao mbali na kuburudisha, unatoa ujumbe mkali dhidi ya tabia zisizofaa katika jamii. Harmonize amepongeza mwelekeo huo, akiwahimiza wasanii wengine kuiga mfano huo kwa kutumia muziki kama chombo cha kuelimisha, kuonya, na kujenga.

Read More
 Akaunti ya Instagram ya Konde Gang Yafungwa Ghafla

Akaunti ya Instagram ya Konde Gang Yafungwa Ghafla

Akaunti rasmi ya Instagram ya lebo ya muziki ya Konde Gang, inayomilikiwa na msanii nyota Harmonize, imefungwa ghafla, jambo lililozua maswali mengi miongoni mwa mashabiki na wadau wa muziki. Mpaka sasa, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu sababu ya kufungwa kwa ukurasa huo, ambao ulikuwa na zaidi ya wafuasi milioni 2 na ulikuwa ukitumiwa kwa matangazo ya muziki, matukio ya lebo, pamoja na taarifa za wasanii walioko chini ya Konde Gang. Mashabiki wengi wameeleza mshangao na masikitiko yao kupitia mitandao mingine ya kijamii, wakitaka kufahamu kilichojiri. Wengine wamehisi huenda ni hitilafu ya muda kwenye Instagram, huku baadhi wakihisi huenda akaunti hiyo imefungwa kwa kukiuka masharti ya matumizi ya jukwaa hilo. Harmonize bado hajatoa tamko rasmi kuhusu hatua hiyo, lakini mashabiki wake wanatarajia kupata taarifa kutoka kwake au uongozi wa Konde Gang muda wowote. Kwa sasa, shughuli za lebo hiyo zinaendelea kupitia kurasa binafsi za wasanii na timu ya menejimenti.

Read More
 Harmonize Aendelea Kuumia Kimapenzi, Aandika Machungu Snapchat

Harmonize Aendelea Kuumia Kimapenzi, Aandika Machungu Snapchat

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Harmonize, anaonekana kupitia kipindi kigumu upande wa mahusiano licha ya kuwa na jina kubwa kwenye tasnia ya muziki na utajiri wa kutosha. Kupitia akaunti yake ya Snapchat, Harmonize amemwaga hisia zake kwa uchungu kuhusu mpenzi wake ambaye bado hajawa tayari kumkubali kikamilifu kwenye maisha yake. Katika ujumbe wake, Harmonize alieleza kwa wazi kwamba ana mapenzi ya dhati kwa mwanamke huyo, na kwamba siku atakayokubali kuwa naye rasmi, atamuoa papo hapo bila kuchelewa. Hata hivyo, kwa sasa ameamua kumpa nafasi ya kuendelea na maisha yake huku yeye akiendelea kumsubiri kwa subira. “Mimi ni mtu mzima, niko tayari. Siku akiamua tu, sihitaji hata kupanga… nitamuoa siku hiyohiyo,” aliandika Harmonize kwa hisia kali. Mashabiki wengi wameonesha hisia tofauti, wengine wakimpongeza kwa uvumilivu na upendo wa kweli, huku wengine wakimshauri asijidhalilishe kwa mapenzi yasiyolipwa kwa kiwango sawa. Hii si mara ya kwanza kwa Harmonize kulalamika kuhusu changamoto za kimapenzi, jambo ambalo limezua mijadala mitandaoni kuhusu maisha ya mahusiano ya wasanii mashuhuri.

Read More
 Ibraah Atangaza Kuondoka Rasmi Konde Gang Baada ya Kikao na BASATA

Ibraah Atangaza Kuondoka Rasmi Konde Gang Baada ya Kikao na BASATA

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Ibrahim Abdallah maarufu kama Ibraah, ametangaza rasmi kuondoka kwenye lebo ya Konde Music Worldwide baada ya kikao cha mwisho kilichowahusisha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na uongozi wa lebo hiyo. Kupitia mahojiano baada ya kikao hicho, Ibraah amethibitisha kuwa wamefikia mwafaka wa kumaliza tofauti zao na uongozi wa Konde Gang. Hata hivyo, ameeleza kuwa bado hajakabidhiwa baadhi ya vitu muhimu vinavyohusiana na kazi yake ya muziki, ikiwemo akaunti zake za digital platforms kama YouTube, Boomplay, na Spotify. Kwa upande wao, uongozi wa Konde Gang kupitia Sandra, ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa lebo hiyo, wamethibitisha kuwa Ibraah atakabidhiwa rasmi akaunti hizo kabla ya mwisho wa leo. Aidha, Sandra amemtakia kila la heri Ibraah katika safari yake mpya ya muziki nje ya Konde Gang, akisisitiza kuwa hakuna uadui kati yao bali ni mabadiliko ya kawaida katika tasnia ya sanaa. Kuondoka kwa Ibraah kunakuja baada ya muda mrefu wa tetesi na hali ya sintofahamu kuhusu mustakabali wake ndani ya Konde Gang. Mashabiki wake sasa wanangoja kwa hamu kuona ni wapi atapeleka kipaji chake na iwapo ataendelea kung’ara kama msanii huru. Hii ni miongoni mwa migogoro ya kimikataba inayozidi kuibuka katika tasnia ya muziki Tanzania, huku mashirika kama BASATA yakihimiza mazungumzo ya kidiplomasia kama njia ya kutatua mizozo kati ya wasanii na lebo zao. Ibraah alikuwa msanii wa kwanza kusainiwa Konde Music mwaka 2020, na ametoa nyimbo kadhaa zilizotikisa chati za muziki Afrika Mashariki, kama vile One Night Stand, Nani, na Dharau akiwa chini ya lebo hiyo.

Read More
 Harmonize Atamani Kuwa Baba, Aonyesha Mradi Mkubwa wa Ujenzi

Harmonize Atamani Kuwa Baba, Aonyesha Mradi Mkubwa wa Ujenzi

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Harmonize, ameonesha hatua nyingine kubwa katika maisha yake ya kifedha na ya binafsi baada ya kuposti kwenye Instagram Story picha ya mjengo mkubwa unaoendelea kujengwa, ishara ya mafanikio na uthibitisho wa ndoto alizowahi kuzielezea huko nyuma. Picha hiyo, iliyopambwa na maneno “My future so bright, I need a son now”, imetoa ujumbe wenye maana pana: si tu kuhusu mafanikio ya sasa, bali pia taswira ya ndoto za baadaye. Harmonize anaonesha kuwa sasa anawaza si tu kuhusu kujenga majumba, bali pia kuanzisha familia na kupata mrithi wa jina lake. Kauli hiyo imeibua mijadala mitandaoni, wengi wakitafsiri kama ishara ya utulivu wa kisaikolojia na kifamilia, huku mashabiki wake wakimpongeza kwa hatua hiyo kubwa ya maisha. Wengine wamekuwa wakitaka kujua iwapo msanii huyo tayari ana mipango ya ndoa au mtoto kwa wakati huu. Harmonize, ambaye amepitia mengi katika maisha yake ya muziki na mahusiano, anaonekana sasa kuelekea kwenye ukurasa mpya unaochochewa na maono ya urithi, utulivu, na mafanikio ya muda mrefu.

Read More
 KILLY AWAOMBA MASHABIKI WA KENYA WAMSAIDIE KUPATA ALIYEONDOA VIDEO YA WIMBO WAKE YOUTUBE

KILLY AWAOMBA MASHABIKI WA KENYA WAMSAIDIE KUPATA ALIYEONDOA VIDEO YA WIMBO WAKE YOUTUBE

Msanii wa Bongofleva, Killy amewaomba mashabiki wake waliyopo nchini Kenya kumsaidia kumpata Mutisya Munyithya ambaye ndiye ameipiga copy right YouTube video ya wimbo wake, Ni Yeye ambao amemshirikisha Harmonize. Mwimbaji huyo wa Konde Music Worldwide amewaomba mashabiki wanaomfahamu wawasiliane naye kwa namba +255 65 289 2317. “Mashabiki zangu pendwa poleni sana kwa maumivu ya kuondolewa kwa video yetu pendwa ya Ni Wewe. Hii ni moja ya changamoto tu katika kazi zetu japo inaumiza sana ila hatuna budi kuwa na subira”. “Ni changamoto ambayo ipo nje wa uwezo wangu ila Menejimenti ina shughulikia hilo na video yetu Ni Wewe itarudi tu soon, love you all my fans” amesema Killy. Hadi inaondolewa YouTube video hiyo ilikuwa na views zaidi ya milioni 2.

Read More