Konshens Afunguka Kuhusu Mvutano Wake na Mtayarishaji wa Muziki Rvssian

Konshens Afunguka Kuhusu Mvutano Wake na Mtayarishaji wa Muziki Rvssian

Msanii wa Dancehall kutoka Jamaica, Konshens, amezungumzia kwa mara ya kwanza mvutano wake na mtayarishaji maarufu wa muziki Rvssian, ambao umekuwa ukigonga vichwa vya habari. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Konshens amemtuhumu Rvssian kwa kusambaza taarifa potofu kuhusu mzozo wao na kufichua kuwa chanzo kikuu cha mgogoro huo ni masuala ya kifedha, siyo ukosefu wa uaminifu au urafiki. Katika ujumbe wake, Konshens ameeleza kuwa alimtaka Rvssian alipe sehemu ndogo ya fedha zilizokuwa zinadaiwa kutokana na ushirikiano wao wa awali. Hata hivyo, badala ya kushughulikia suala hilo kwa mazungumzo, Rvssian alimu-unfollow kwenye mitandao ya kijamii. Konshens amekiri kwamba aliwahi kutishia kumpeleka mahakamani, lakini amekanusha madai kuwa aliwahi kumshtaki rasmi, akisema walimaliza tofauti zao nje ya mahakama. Msanii huyo ameelezea kuwa hatua ya Rvssian kusambaza taarifa za uongo kwa umma ni usaliti mkubwa, akisisitiza kuwa alikuwa kama ndugu kwake. Licha ya mzozo huo, Rvssian bado anatajwa kuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Konshens. Wimbo wao wa pamoja wa mwaka 2016 “Privado”, una zaidi ya views milioni 294 kwenye mtandao wa YouTube, na kuwa mojawapo ya mafanikio makubwa zaidi ya Konshens katika jukwaa la kimataifa.

Read More
 Ngoma ya  Harmonize ‘Weed Language’ yarejeshwa Youtube

Ngoma ya Harmonize ‘Weed Language’ yarejeshwa Youtube

Ngoma ya ‘Weed language’ ya staa wa muziki wa Bongo Fleva , Harmonize imerejeshwa tena katika mtandao wa Youtube wa msanii Konshens masaa kadhaa yaliyopita. Harmonize jana kupitia ukurasa wake wa kijamii wa instagram aliahidi atauondoa wimbo huo kwenye mitandao yote ya kijamii baada ya kukiri kuwa maudhui ya wimbo huo yanakiuka maadili, mila na desturi pamoja na miongozo ya mamlaka za serikali nchini Tanzania. Hata hivyo Harmonize alioundoa katika mtandao wake wa Youtube ila kwa sasa unapatikana katika chaneli ya Konshens aliyemshirikisha katika ngoma hiyo.

Read More
 KRG THE DON ATHIBITISHA UJIO WA KOLABO YAKE NA MKALI WA DANCEHALL KUTOKA JAMAICA KONSHENS

KRG THE DON ATHIBITISHA UJIO WA KOLABO YAKE NA MKALI WA DANCEHALL KUTOKA JAMAICA KONSHENS

Habari nzuri kwa mashabiki wa muziki nchini ni kwamba tutarajie muda wowote ujio wa Collabo kati ya mwanamuziki KRG The Don na Star wa muziki wa dancehall duniani Konshens. Kupitia insta story ya KRG The Don kwenye mtandao wa Instagram ameshare taarifa hiyo nzuri kwa mashabiki na wadau wa muziki nchini kwa kuthibitisha kuwa tayari wawili hao wamefanya kazi ya pamoja. Endapo collabo hiyo itatoka itamfanya KRG The Don kuwa msanii wa pili nchini baada ya Ethic Entertainment kufanya kazi ya pamoja na mwanamuziki huyo nyota kutoka Jamaica. Itakumbukwa kwenye mkesha wa kuamkia mwaka mpya 2022 Konshens alipiga shoo ya kufa mtu kwenye onesho la NRG Wave Concert, shoo ambayo iliyoaacha wapenzi wa muziki mzuri wa dancehall wakitaka burudani zaidi kutoka mkali huyo

Read More