Magix Enga Aomba Msaada Kutimiza Ndoto ya Kuwa na Studio ya Kisasa

Magix Enga Aomba Msaada Kutimiza Ndoto ya Kuwa na Studio ya Kisasa

Mtayarishaji maarufu wa muziki nchini Kenya, Magix Enga, amefunguka na kuomba msaada wa kifedha kutoka kwa mashabiki wake na wadau wa muziki ili kuweza kujenga studio ya muziki yenye vifaa vya kisasa, itakayosaidia kukuza vipaji na kuboresha ubora wa muziki nchini. Magix Enga alisema kuwa ndoto yake ni kuwa na studio ya hali ya juu itakayotoa huduma za kisasa kwa wasanii wote, kutoka vipaji vipya hadi wasanii walioko kwenye viwango vya kimataifa, na hivyo kuchangia zaidi katika maendeleo ya tasnia ya muziki nchini. “Najivunia kazi yangu na wasanii wote niliowahi kushirikiana nao. Hata hivyo, ili kuendeleza muziki wa ubora wa kimataifa hapa Kenya, studio yenye vifaa bora ni lazima. Hali ya kifedha ni changamoto, hivyo naomba msaada wako ili tuweze kufanikisha hili,” alisema Magix Enga. Studio hiyo mpya itakuwa na vifaa vya kisasa vya kurekodi, kuchanganya na kusindika sauti, na itakuwa kitovu cha kuelimisha na kuendeleza vipaji vipya katika muziki. Mashabiki na wadau wa muziki wametakiwa kuungana na Magix Enga katika kampeni hii ya kufanikisha kuanzishwa kwa studio hiyo, huku baadhi yao tayari wakitoa michango kupitia majukwaa mbalimbali ya mtandaoni. Magix Enga ni mmoja wa watayarishaji wenye ushawishi mkubwa katika muziki wa Kenya, na studio hii itakuwa nyongeza kubwa katika kuboresha mazingira ya utayarishaji wa muziki nchini, na kusaidia wasanii wengi kufikia malengo yao.

Read More
 Magix Enga apata ukosoajii mkubwa mtandaoni kwa kujihusisha na kiki

Magix Enga apata ukosoajii mkubwa mtandaoni kwa kujihusisha na kiki

Prodyuza asiyeishiwa na matuko kila leo Magix Enga amejipata njia panda mtandaoni mara baada ya walimwengu kumshambulia kwa kuendekeza kiki kwenye sanaa yake. Purukushani ya wakenya na Magix ilianza pale ambapo prodyuza huyo aliposti picha akiwa kaunti ya Kilifi kwenye shughuli za kuinua vipaji siku chache baada ya video yake akiwa mlevi chakari kusambaa mtandaoni ambapo watu wengi walihuzunishwa na kisa hicho, wakitoa rai kwa wahisani kujitokeza na kumsaidia prodyuza kutokana na uraibu wa pombe ulioathiri maisha. Watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii wameonekana kukerwa na sarakasi za prodyuza huyo kwa kumshushia kila aina ya matusi huku wakimtaka aache kutengeneza kiki zisizo kuwa na mashiko kwa lengo la kutangaza kazi zake. Aidha baadhi wamehoji kuwa kitendo cha Enga kuishi maisha ya kuigiza mitandaoni itagharimu siku za mbeleni kwani watu wataanza kumchukulia poa ikitokea amepatwa na tatizo. Hii sio mara ya kwanza kwa Magix Enga kujihusisha na kiki zenye utata, miezi kadhaa iliyopita alikiri kuwa mwanachama wa dhehebu la IIlluminati, madai ambayo baadaye alikuja akajitenga nayo kwa kusema alikuwa anatafuta mazingira ya kuzungumziwa kwenye tasnia ya muziki nchini.

Read More
 Prodyuza Magix Enga azua gumzo mtandaoni baada ya kuonekana akiwa mlevi kupindukia

Prodyuza Magix Enga azua gumzo mtandaoni baada ya kuonekana akiwa mlevi kupindukia

Video ya mtayarishaji muziki nchini Kenya Magix enga akiwa katika hali mbaya imesambaa mitandaoni. Katika video hiyo, prodyuza huyo anaonekana akiwa amekaa chini ya mti katika mavazi yaliyochanika huku akiwa mlevi. Video ambayo awali ilisambaa kwa mara ya kwanza kwenye mtandao wa Tiktok ilizua taharuki mitandaoni, huku baadhi ya Wakenya wakiwataka wasamaria wema kumuokoa msanii huyo mwenye kipaji cha kipekee kutoka kwenye kadhia ya kubugia pombe kupindukia. Awali, magix enga alifichua kwamba alilazimika kujiunga na kituo cha matibabu ya watumiaji wa madawa, pombe na mihadarati ili kumsaidia kukabiliana na uraibu wake wa pombe. Baadaye aliruhusiwa kwenda nyumbani na tangu wakati huo alianza kufanya kazi na wasanii tofauti kama kawaida wakiwemo wasanii wa boondocks gang. Magix Enga ni miezi michache amegonga vichwa vya habari baada ya kukiri kwamba aliingia Illuminati kumbe ilikuwa kiki ya mziki.

Read More
 MUONEKANO MPYA WA MAGIX ENGA WAZUA GUMZO MTANDAONI.

MUONEKANO MPYA WA MAGIX ENGA WAZUA GUMZO MTANDAONI.

Mionekano kwa wasanii si jambo la kuchukulia poa, bali ni kazi. Ni moja ya njia za branding na kujiweka machoni kwa mashabiki muda wote. Sasa Prodyuza wa muziki nchini Magix Enga ameamua kuzinyoa nywele zake zote aina dread kichwani mwake (Kipara). Kupitia ukurasa wake wa Instagram Magix Enga amechapisha video akiwa amenyoa nywele hizo na kusindikiza caption inayosomeka, “Kichwa safi kama balloon”. Prodyuzo huyo ambaye pia ni mwimbaji hajaweka wazi sababu za kuchukua maamuzi ya kuonyoa dread zake ila ameibua hisia mseto miongoni mashabiki zake pamoja na mastaa wenzake ambao walibaki na masuala ni kitu gani kilimpelekea kuchukua maamuzi hayo magumu. “Kuriathiatia mutwe?” kwa maana ya “Nini mbaya na kichwa chako?” msanii Odi wa Muarang’a aliuliza. Hata hivyo wasanii wengine kama Exray wamesema kuwa wana heshimu maamuzi yake huku wengine kama Bien wa Sauti Sol wakimpongeza kwa hatua kubwa aliyochukua. Kwa muonekano wake mpya wa Magix Enga imeonyesha ni jinsi gani amebadilika kwa kuwa muonekano wake huyo umezua hisia mseto miongoni mwa mashabiki zake ambao wameandika ujumbe unaosomeka “looking different but cute … uko tu fiti new beginning ,looking marvelous” “Hii stunt nayo imeeza. Hizo nywele sio zako. I know this is a scum”

Read More
 MAGIX ENGA AACHIA RASMI EP YAKE MPYA, “MAWAZO EP”

MAGIX ENGA AACHIA RASMI EP YAKE MPYA, “MAWAZO EP”

Msanii na prodyuza wa muziki nchini Magix Enga ameachi rasmi EP yake mpya inayokwenda kwa jina la Mawazo Ep hiyo ina jumla ya mikwaju nne ya moto huku zote akiwa amezifanya kama msanii wa kujitegemea. Mawazo EP ambayo ina nyimbo kama Mapenzi, Nakuwaza,Ma-presure na Nisamehe  kwa sasa inapatikana exclusive kupitia mtandao wa youtube. Hii ni EP ya pili kwa mtu mzima Magix Enga tangu aanze safari yake ya  muziki baada ya Reason EP iliyotoka mapema mwaka huu.

Read More
 MAGIX ENGA MBIONI KUACHIA EP YAKE MPYA

MAGIX ENGA MBIONI KUACHIA EP YAKE MPYA

Prodyuza wa muziki nchini Magix Enga ametangaza ujio wa EP yake mpya ambayo ana mpango wa kuachia ndani ya mwaka huu wa 2022. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Magix Enga amewataka mashabiki wake wakae mkao wa kula kuipokea EP yake hiyo ambayo kwa mujibu wak ameipa jina la Mawazo EP. Hata hivyo hajeweka wazi Idadi ya ngoma wala tarehe rasmi ambayo EP yenyewe itaingia sokoni ila ameachia nyimbo mbili kutoka kwenye EP ambazo ni Ma-Pressure na Nakuwaza. Hii inaenda kuwa EP ya pili kwa mtu mzima Magix Enga tangu aanze safari yake ya  muziki baada ya Reason EP iliyotoka mapema mwaka huu ikiwa na jumla ya nyimbo 5 za moto.

Read More
 MAGIX ENGA AELEZA JINSI UKOSEFU WA SUPPORT UMEATHIRI PAKUBWA TASNIA YA MUZIKI NCHINI KENYA

MAGIX ENGA AELEZA JINSI UKOSEFU WA SUPPORT UMEATHIRI PAKUBWA TASNIA YA MUZIKI NCHINI KENYA

Prodyuza na mwanamuziki Magix Enga ameibuka na kudai tasnia ya muziki nchini Kenya ni mbovu ikilinganishwa na mataifa mengine. Kupitia instagram page yake Enga amesema kiwanda cha muziki nchini kinaangazia sana taarifa mbaya za wasanii badala ya kuwapa support wasaniii kwenye muziki wao ili waweze kuingiza kipato ambacho kitawainua kiuchumi. Hitmaker huyo “Kale” amesema  wasanii wengi wakongwe wanaishi kwenye lindi la umaskini kutokana na kukosa mazingira mazuri ya kutumia sanaa yao kuboresha maisha yao. Hata hivyo watumiaji wengi kwenye mitandao ya kijamii wameonekana kumuunga mkono kwa kauli yake hiyo huku wakitoa shime kwa washikadau wa masuala ya sanaa nchini kutatua changamoto zinazowakwamisha wasanii kutopata pesa za kuwasaidia kimaisha kupitia kazi zao za muziki. Utakumbukwa juzi kati Magix Enga alishika headlines za habari za burudani nchini baada ya kukiri hadharani kwamba stori yake ya kuwa muumini wa dhehebu la illuminati ilikuwa batili kitu kilichowakasirisha sana walimwengu kwenye mitandao ya kijamii.      

Read More
 WALIMWENGU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII WAMVUA NGUO MAGIX ENGA BILA UHURUMA

WALIMWENGU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII WAMVUA NGUO MAGIX ENGA BILA UHURUMA

Msanii na Prodyuza wa muziki nchini Kenya Magix Enga amejipata pabaya kwenye mitandao ya kijamii baada ya kudai kuwa yuko tayari kumlipa mchekeshaji Jalang’o shillingi millioni  2 za Kenya kila mwezi ili aachane azma yake ya kujiunga na siasa. Kauli hiyo ya Magix Enga imeonekana kuwakera watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii ambao wamedai kuwa Prodyuza huyo ana matatizo ya kiakili huku wakimtaka aache suala la kujigamba kuwa ana pesa nyingi wakati anaishi maisha ya uchochole. Baadhi wameenda mbali zaidi na kuhoji kuwa hatua ya Magix Enga kudai kuwa ni muumini wa dhehebu la illuminati ilikuwa njia ya kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa kwenye tasnia ya muziki nchini. Ikumbukwe juzi kati Magix Enga aliibuka na kudai kuwa alipata mali nyingi alipojiunga na  dhehebu la illuminati lakini alipookoka mambo yalianza kumuenda murama hadi akafilisika kiuchumi.

Read More
 MAGIX ENGA AKIRI KUWA MUUMINI WA DHEHEBU LA KISHETANI LA ILLUMINATI

MAGIX ENGA AKIRI KUWA MUUMINI WA DHEHEBU LA KISHETANI LA ILLUMINATI

Mtayarishaji wa muziki kutoka kenya Magix Enga amefunguka na kukiri kuhusu yale aliyopitia baada ya kujiunga na dini ya kishetani. Kwenye mahojiano na Plug TV, Magix amekiri kwamba umaskini ulimshinikiza kukubali kujiunga na dhehebu hiyo baada ya mwanadada mmoja wa kizungu kujitolea kumsaidia kujipatia utajiri mkubwa kutokana na  taaluma yake. “Kila mwezi nilikuwa napokea pesa. Kuna gari fulani ilikuwa inakuja kila mwezi naambiwa niingie. Nilikuwa nakalia kiti cha nyuma lakini sikuwa naangalia ni nani alikuwa anaendesha. Ningechukua pesa zangu kisha narudi studioni. Nilikuwa napata pesa  nyingi.” amesema Magix Enga Mtayarishaji huyo ameweka wazi kwamba hakuna karatasi zozote ambazo alitia saini na hakuna mtu yeyote ambaye alitoa kafara ila walikuwa wakitoa damu yake kwa kumtoboa kwenye tumbo. Licha ya manufaa yote ya kifedha ambayo alikuwa akiyapata Magix ameeleza kuwa alifikia uamuzi wa kuachana na dini hiyo ya kishetani baada ya kuanza kupatiwa maagizo ambayo hangeweza kutimiza huku akiweka wazi kwamba kwa sasa hayuko tena katika dhehebu hiyo na tayari amemkubali yesu na kuokoka licha ya kundelea kuwindwa na wanachama wa madhehebu ya illuminatti.

Read More