FOBY AUPONDA UWEZO WA MARIOO KWENYE MUZIKI WA BONGOFLEVA

FOBY AUPONDA UWEZO WA MARIOO KWENYE MUZIKI WA BONGOFLEVA

Msanii wa Bongofleva Foby amefunguka kuwa mkali wa ngoma ya “Beer tamu” Marioo hawezi kuvikwa taji la Ufalme wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania. Kupitia mahojiano aliyoyafanya hivi karibuni, mwanamuziki huyo amedai kwamba Marioo hawezi kuwa mfalme wa muziki wa Bongofleva ikiwa anaimba muziki wa Amapiano, kwani mfalme anatakiwa kukuza na kufanya mziki wao wa nyumbani na sio kuiga muziki kutoka mataifa mengine. HitMaker wa ngoma ya “Ode” amechukizwa na kitendo cha rapa Damian Sol kumkana hadharani kwamba hamfahamu kwa kusema kuwa rapa huyo amewavunjia heshima vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikipiga nyimbo zake ikizingatiwa kuwa wamekutana mara nyingi kwenye matamasha mbali mbali ya muziki. Ikumbukwe Foby kwa sasa anafanya vizuri kwenye Digital Platforms mbali mbali na EP yake iitwayo ME, MYSELF & 1 ambayo aliiachia rasmi mwishoni mwa mwaka wa 2021 ikiwa na jumla ya mikwaju 5 ya moto.

Read More
 BAHATI ATUHUMIWA KUIBA IDEA YA WIMBO WA JE UNANIFIKIRIA KUTOKA KWA MARIOO

BAHATI ATUHUMIWA KUIBA IDEA YA WIMBO WA JE UNANIFIKIRIA KUTOKA KWA MARIOO

Mkali wa muziki nchini Bahati ameingia tena katika mijadala kwenye mitandao nchini  baada ya kudaiwa kuiba  idea ya wimbo wa  β€˜For You’ wa msanii  wa Bongofleva Marioo Kulingana na ripoti inayosambaa mitandaoni, inadaiwa Bahati ametumia mdundo na ubunifu wa video wa wimbo huo kwenye wimbo wake mpya wa”Je unanifikiria”, hivyo kuibua maswali mengi miongoni mwa wadau wa muziki nchini ambao walienda mbali zaidi na kuhoji kuwa msanii huyo amekosa ubunifu kwenye muziki wake. Hata hivyo Bahati hajetoa tamko lolote kuhusiana na madai hayo yaliyoibuliwa na baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Read More
 MARIOO MBIONI KUJA NA “I’AM MARIOO TOUR”

MARIOO MBIONI KUJA NA “I’AM MARIOO TOUR”

Hitmaker wa Beer Tamu, Marioo ametangaza ujio wa tour yake nchini Tanzania aliyoipa jina la β€œI’am Marioo tour.” Marioo ameweka wazi ujio wa tour yake hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram huku akiwaachia mashabiki swali kupendekeza ni mkoa gani nchini Tanzania ambao asiache kukanyaga kwenye tour yake hiyo. Pamoja na kuweka wazi ujio wa tour yake hiyo marioo hajagusia endapo kuna wasanii wengine ambao anatarajia kushirikiana nao kwenye tour hiyo au atakuwa mwenyewe tu. Kauli ya marioo inakuja siku chache baada ya kuwatolea uvivu wasanii wa bongo fleva kwa kuwaita wanafiki pale linapokuja suala la kupeana michongo ya kufanikiwa kwenye muziki

Read More