Mbosso Akanusha Vikali Kumkimbia Mkubwa Fella

Mbosso Akanusha Vikali Kumkimbia Mkubwa Fella

Msanii wa nyota wa Bongo Flava, Mbosso, amekanusha vikali madai yanayosambaa mitandaoni yanayodai kuwa amemkimbia meneja mkubwa Fella Sweet Fella katika kipindi ambacho meneja huyo anaumwa. Akizungumza kuhusu taarifa hizo, Mbosso amesema madai hayo si ya kweli, akiyataja kuwa ya kupotosha umma. Amesema amekuwa karibu na familia ya Mkubwa Fella, akiwatembelea mara kwa mara, pamoja na kutoa msaada wowote unaohitajika kadri ya uwezo wake. Mbosso amesisitiza kuwa anamthamini sana Mkubwa Fella kutokana na mchango mkubwa alioutoa katika safari yake ya muziki na hawezi kamwe kumsahau wala kumtelekeza kama baadhi ya walimwengu wanavyodai. Hata hivyo, hitmaker huyo wa Pawa, ameomba umma na mashabiki kupuuza taarifa zinazolenga kuchafua jina lake ikizingatiwa kuwa Mkubwa Fella alikuwa moja kati ya watu ya waliyoikuza kipaji chake na kumtambulisha kwa mashabiki wengi wa muziki ndani na nje ya Tanzania chini ya Yamoto Band.

Read More
 Mbosso Awajibu Wanaotilia Shaka Uandishi Wake Baada ya Mafanikio ya 2025

Mbosso Awajibu Wanaotilia Shaka Uandishi Wake Baada ya Mafanikio ya 2025

Msanii wa nyota wa Bongo Fleva Mbosso amewajibu wakosoaji wanaotilia shaka uwezo wake wa kuandika nyimbo baada ya mwaka wa 2025 kumwendea vyema kimuziki kwa kuachia kazi zilizopokelewa vizuri na mashabiki. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Mbosso ameonekana kuchoshwa na madai yanayosambaa mtandaoni kuwa anaandikiwa nyimbo zake, akiorodhesha maneno ambayo yamekuwa yakitumiwa kumdhalilisha kisanii. Hitmaker huyo wa Pawa, ametaja hoja mbalimbali ambazo zimekuwa zikitumiwa kumdhalilisha mtandaoni, zikiwemo madai kwamba ana talanta bila juhudi, anasaidiwa na nguvu za kishirikina, anategemea teknolojia ya AI na huwa anaandikiwa nyimbo na watu wengine. Kauli hiyo imechukuliwa na wengi kama ujumbe mzito kwa wakosoaji wake, hasa ikizingatiwa kuwa Mbosso amekuwa akisifiwa kwa uandishi wenye hisia nzito, mashairi yenye kugusa maisha halisi na uwezo wa kuwasilisha ujumbe kwa sauti ya inayovutia.

Read More
 Mbosso Afikisha Views Bilioni 1 YouTube

Mbosso Afikisha Views Bilioni 1 YouTube

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mbosso, ameandika historia mpya katika safari yake ya muziki baada ya kufikisha jumla ya watazamaji (views) bilioni 1 kwenye mtandao wa YouTube kupitia nyimbo zake zote. Mbosso alijiunga rasmi na YouTube tarehe 2 Novemba mwaka 2017, na tangu wakati huo amekuwa akitoa kazi zilizopokelewa vyema na mashabiki wake ndani na nje ya Afrika Mashariki. Mafanikio haya yanaonesha ukuaji mkubwa wa umaarufu wake pamoja na mvuto wa muziki wake katika soko la kimataifa. Kupitia hatua hii, Mbosso ameingia kwenye orodha ya mastaa wachache wa Tanzania waliowahi kufikisha views bilioni 1 YouTube, akijiunga na majina makubwa kama Diamond Platnumz, Zuchu, Harmonize na Rayvanny. Mafanikio ya Mbosso yanaendelea kuthibitisha mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa Bongo Fleva na kupeperusha bendera ya Tanzania kimataifa, huku mashabiki wake wakimpongeza kwa kazi nzuri na bidii kubwa tangu alipoanza safari yake ya muziki.

Read More
 Mbosso Amuajiri Mume wa Shabiki Baada ya Ombi la Kazi Instagram

Mbosso Amuajiri Mume wa Shabiki Baada ya Ombi la Kazi Instagram

Staa wa muziki wa Bongo Fleva Mbosso Khan amegusa nyoyo za mashabiki wake baada ya kuonyesha moyo wa utu na kujali kwa kumsaidia shabiki aliyemuomba msaada wa kumpatia mume wake kazi ya udereva. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Mbosso amejibu ombi hilo lililoachwa kwenye sehemu ya maoni, ambapo shabiki huyo alieleza changamoto walizokuwa wakipitia yeye na mume wake kwa miaka mingi licha ya mume wake kuwa na ujuzi na uzoefu wa kuendesha magari. Shabiki huyo alimwomba msanii huyo amuunganishe mume wake na kazi ya udereva ili kuboresha maisha ya familia yao. Baada ya kuona ujumbe huo, Mbosso hakusita kuchukua hatua. Msanii huyo ameagiza timu yake kumtafuta shabiki huyo na kumsaidia kufanikisha ndoto ya kumuona mume wake akipata ajira ya udereva ndani ya timu yake. Hatua hiyo imepongezwa vikali na mashabiki pamoja na wadau wa muziki, wengi wakimwelezea Mbosso kama msanii mwenye moyo wa huruma na anayejali jamii inayomzunguka. Wengine wamesema kitendo hicho kinaonyesha kuwa umaarufu unaweza kutumika kubadilisha maisha ya watu kwa njia chanya.

Read More
 Mashabiki Kenya Wamkataa Mbosso Kisa Siasa

Mashabiki Kenya Wamkataa Mbosso Kisa Siasa

Mashabiki wa muziki nchini Kenya wameonyesha msimamo mkali dhidi ya nyimbo za msanii wa Tanzania, Mbosso, wakidai msimamo wake wa kisiasa hauendani na hisia zao. Tukio hili lilijitokeza wazi katika tuzo za Nganya jijini Nairobi, ambapo DJ aliyekuwa akicheza muziki alikumbana na upinzani baada ya kupiga wimbo Pawa na nyimbo nyingine za bongo flava. Badala ya kusherehekea, mashabiki walipaza sauti wakitaka muziki wa Kenya pekee, wakimtaja Toxic Lyrikali kama chaguo lao. Mbosso anadaiwa kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye alichaguliwa katika uchaguzi wa Tanzania uliokumbwa na utata. Mashabiki wa Kenya wanaonekana kuunga mkono wimbi linaloendelea nchini Tanzania, ambapo baadhi ya wananchi wameanzisha kampeni ya kuwaadhibu wasanii waliotumika kisiasa.

Read More
 Mbosso Kuachia Version Tatu za “Pawa” Kutoka Kenya, Tanzania na Rwanda

Mbosso Kuachia Version Tatu za “Pawa” Kutoka Kenya, Tanzania na Rwanda

Mwanamuziki nyota wa Bongofleva, Mbosso, ametangaza kuwa anajiandaa kuachia version tatu tofauti za wimbo wake “Pawa,”. Kila version itawashirikisha wasanii wakubwa kutoka ukanda wa Afrika Mashariki hasa mataifa ya Kenya, Tanzania na Rwanda Katika version ya Kenya, Mbosso amewashirikisha nyota wawili, Bien wa Sauti Sol na mfalme wa rap nchini Kenya, Khaligraph Jones.Toleo la Tanzania linakuja na nguvu ya Darassa, Billnass na Marioo, wasanii wanaosifika kwa uandishi, mitiririko na ubora wa midundo ya Bongo Fleva. Kwa upande wa Rwanda, Mbosso ameungana na The Ben, mmoja wa wanamuziki bora na wenye sauti yenye utamu katika ukanda huo. Mbosso amedokeza kuwa huenda akaachia version zaidi ya tatu, akiwashirikisha wasanii wengine kutoka Afrika Mashariki kutokana na mapokezi makubwa ya wimbo huo. “Pawa” ni wimbo uliopata mafanikio makubwa kutoka kwenye EP yake Room 3, na remix hizi zinatarajiwa kuufikisha mbali zaidi kimataifa.

Read More
 Mbosso Adai Nusra Atoe Uhai Akiwafurahisha Mashabiki Simba SC

Mbosso Adai Nusra Atoe Uhai Akiwafurahisha Mashabiki Simba SC

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Mbosso, amefunguka kuhusu namna alivyoweka nguvu kubwa kuhakikisha onyesho lake kwenye Simba Day linakuwa la kipekee, akieleza kuwa nusra ajitoe uhai wake ili kuwafurahisha mashabiki wa Simba Sports Club. Kupitia Instagram, Mbosso amesema alijiandaa kwa moyo wake wote na kuweka nguvu, muda na rasilimali nyingi kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Amebainisha kuwa mapenzi yake kwa Simba SC na mashabiki wake ndiyo yaliyomsukuma kufanya maandalizi ya hali ya juu, akisisitiza kuwa alijitolea zaidi ya kawaida ili burudani iwe ya kukumbukwa. Licha ya mafanikio makubwa ya perfomance yake, msanii huyo pia amewaomba mashabiki na viongozi wa Simba SC msamaha endapo kulikuwa na mapungufu yoyote katika utendaji wake wa Kazi, akisema yeye ni mwanadamu na hawezi kufanya kila kitu kwa ukamilifu. Simba Day hufanyika kila mwaka kwa ajili ya kuzindua msimu mpya wa klabu hiyo yenye mashabiki wengi, na mwaka huu Mbosso alipewa nafasi ya kuwa headliner, nafasi ambayo amesema itaendelea kubaki kuwa kumbukumbu muhimu katika maisha yake ya muziki.

Read More
 Mbosso Ajeruhiwa Akiwa Location ya Video Shoot

Mbosso Ajeruhiwa Akiwa Location ya Video Shoot

Msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Mbwana Yusuf Kilungi maarufu Mbosso, ameripotiwa kupata jeraha kwenye mguu wake wa kulia wakati wa shughuli za utayarishaji wa kazi yake mpya ya muziki. Tukio hilo lilitokea akiwa location akirekodi video, ambapo inadaiwa alidondoka ghafla baharini katika harakati za kuhakikisha mashabiki wake wanapata burudani ya kiwango cha juu. Ingawa haijafahamika ukubwa wa jeraha hilo, watu wa karibu na msanii huyo wamesema kuwa hali yake si ya kutia wasiwasi na anaendelea kupata matibabu. Mashabiki wake wameonyesha wasiwasi kupitia mitandao ya kijamii, huku wengi wakimtumia jumbe za kumtakia afueni ya haraka. Mbosso, anayejulikana kwa sauti yake ya kipekee na vibao kama Hodari na Fall, amekuwa akijiandaa na miradi mipya ya muziki, na tukio hili limekuja wakati mashabiki wakingoja kwa hamu kazi yake mpya.

Read More
 Mbosso Apata Views Nyingi Kenya Kuliko Tanzania Kwenye YouTube

Mbosso Apata Views Nyingi Kenya Kuliko Tanzania Kwenye YouTube

Mwanamuziki nyota wa Bongo Fleva, Mbosso, ameibua mjadala baada ya takwimu kuonyesha kuwa muziki wake unasikilizwa zaidi nchini Kenya kuliko nyumbani kwao Tanzania. Kwa mujibu wa ripoti ya takwimu za YouTube, nyimbo za Mbosso zimeangaliwa zaidi ya mara milioni 102 kutoka Kenya, ikilinganishwa na mara milioni 47 kutoka Tanzania. Hii inamaanisha kwamba takribani asilimia 68.5 ya watazamaji wake kutoka Kenya na Tanzania wanatoka Kenya pekee. Ufanisi huu unaonyesha namna Mbosso alivyojijengea mashabiki wakubwa nchini Kenya, huku muziki wake ukiendelea kushika nafasi kwenye redio, majukwaa ya kidijitali na mitoko ya burudani. Wachambuzi wa muziki wanasema hali hii inathibitisha nguvu ya soko la Kenya kwa wasanii wa Afrika Mashariki, na kwa Mbosso, inaweza kufungua milango ya ushirikiano zaidi na wasanii wa Kenya pamoja na kuongeza idadi ya shoo katika nchi hiyo.

Read More
 Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso

Marioo Adai Hajawahi Kuandikiwa Wimbo, Mashabiki Wahoji Bifu na Mbosso

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Marioo, amefunguka kuhusu safari yake ya muziki, akisema licha ya mafanikio makubwa aliyopata hajawahi kubebwa na lebo kubwa wala kuandikiwa wimbo na mtu yeyote. Kupitia Instastory, msanii huyo amesema kuwa yeye ndiye msanii pekee mwenye hits “back to back”, akiongeza kuwa tayari ameshinda mara kadhaa tuzo za Msanii Bora wa Mwaka (Bongo Fleva), jambo linaloashiria ukubwa wa mchango wake katika tasnia. Marioo, ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake “Dunia”, pia amewajibu mashabiki waliokuwa wakimtaka kutoa, “Global Song”, akiahidi kwamba wimbo huo utapatikana kwenye Deluxe Version ya albamu yake “The God Son”, iliyotoka rasmi mwezi Novemba 2024. Kauli hiyo ya Marioo imepokewa kwa mitazamo tofauti, huku baadhi ya mashabiki wakidai huenda ujumbe huo umemlenga aliyekuwa staa wa WCB, Mbosso, ambaye juzi kati Diamond Platnumz alidai kwamba ndiye aliyeandika wimbo wake maarufu “Pawa.” Hali hiyo imezidisha minong’ono ya uwepo wa bifu la chini kwa chini kati ya Marioo na Mbosso, hasa ikizingatiwa kuwa wote wanahesabika kati ya waimbaji wenye mashabiki wengi na nyimbo zinazotamba kwa sasa.

Read More
 Mbosso Ajibu Madai ya Diamond Platnumz Kuhusu Deni na Uandishi wa Nyimbo

Mbosso Ajibu Madai ya Diamond Platnumz Kuhusu Deni na Uandishi wa Nyimbo

Mzozo kati ya Diamond Platnumz na msanii wake wa zamani Mbosso umeendelea kuchukua sura mpya baada ya wawili hao kufichua mambo ya ndani ya Label ya WCB Wasafi. Baada ya Diamond kudai kuwa ameandika nyimbo nyingi za Mbosso na kumkopesha zaidi ya shilingi milioni 323 ambazo hakulipwa, Mbosso naye amejibu kwa kueleza kuwa yeye pia amekuwa akishiriki kuandika nyimbo za Diamond, ingawa hataki kuzitaja. Amesema tangu enzi zake akiwa Yamoto Band, Diamond alikuwa akimuita nyumbani kwake au studio kushiriki katika kazi hizo. Kupitia Instastories, Mbosso amekanusha madai kwamba anamwonea wivu Diamond, akibainisha kuwa kuna watu wa kati wanaojaribu kuwapandikizia uhasama. Amesema wazi kuwa huenda Diamond alikuwa na jambo moyoni kwa muda mrefu na sasa ameona wakati umefika wa kulitoa hadharani. Hata hivyo, licha ya mkanganyiko huo, Mbosso amesema ataendelea kumheshimu Diamond kwa mchango wake mkubwa katika maisha yake ya muziki. Kwa upande wake, Diamond amesisitiza kuwa Mbosso aliachwa na deni kubwa alipoondoka WCB, lakini aliamua kumsamehe bila malipo yoyote. Aidha, Diamond amedai kuwa wakati Rayvanny anaondoka WCB, Mbosso alimshawishi asifanye kazi naye, akimpinga kushirikiana naye kwenye nyimbo. Hata hivyo, Diamond amesema alikataa kuingiwa na chuki, akisisitiza kuwa kuondoka kwa msanii kwenye Label hakupaswi kuwa chanzo cha ugomvi.

Read More
 Mbosso Amtaka Diamond Kuvunja Ukimya Kuhusu Kauli za Baba Levo

Mbosso Amtaka Diamond Kuvunja Ukimya Kuhusu Kauli za Baba Levo

Mwanamuziki Mbosso ameibuka na kuweka wazi msimamo wake kufuatia mvutano unaoendelea mitandaoni kati yake, Diamond Platnumz, na Baba Levo, kuhusu tuhuma za kushirikiana kumchafua kwa jina au kazi zake. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Mbosso amesema kwa uwazi kuwa hana ukaribu wowote na Baba Levo, na hivyo hawezi kushirikiana naye kwa jambo lolote, tofauti na madai yanayoenezwa. Amefafanua kuwa yeye si mtu wa migogoro, na kwamba anamuheshimu Diamond kama kiongozi na kama msanii mkubwa aliyechangia ukuaji wa muziki wake. Hata hivyo, Mbosso amesisitiza kuwa ni wajibu wa Diamond kuzungumza hadharani kumkemea Baba Levo, kwani ukimya wake unaweza kutafsiriwa kama kukubaliana au kuunga mkono vitendo vya matusi na kejeli vinavyotolewa hadharani na Baba Levo. Kauli ya Mbosso imekuja muda mfupi baada ya Baba Levo kumuomba msamaha na Diamond Platinumz akidai kuwa hana ajenda yoyote na Mbosso ya kumchafulia brand yake. “Mzee Lukuga, sina Agenda yoyote na Mbosso na wala siwezi kupanga njama yoyote na Mbosso, nisamehe mzee wangu” Aliandika Instagram. Ikumbukwe jana kulizuka sintofahamu kati ya Mbosso na Baba Levo baada ya Baba Levo kudai kuwa ngoma ya Pawa imetungwa na Diamond Platnumz, ambapo Mbosso alikasirika na kudai huenda WCB inamfanyia figisu wakati aliondoka salama na anaheshimu sana mchango wao kwenye muziki na mara zote amekuwa akiwashukuru.

Read More