Mbosso Aachia EP Mpya Room Number 3

Mbosso Aachia EP Mpya Room Number 3

Staa wa Bongo Fleva Mbosso ameanza ukurasa mpya katika muziki wake kwa kuachia EP yake ya tatu iitwayo Room Number 3, miezi michache baada ya kuondoka kwenye lebo ya WCB Wasafi. EP hiyo, ambayo ina nyimbo 7 bila collabo yoyote, tayari imechukua nafasi ya kwanza kwenye majukwaa makubwa ya muziki kama Apple Music na Spotify, hatua inayothibitisha kuwa Mbosso bado ni nguvu kubwa kwenye tasnia ya muziki wa Afrika Mashariki. Nyimbo zilizopo kwenye EP hiyo ni: Pawa, Nusu Saa, Tena, Merijaah, Siko Single, Aviola, na Asumani. Maudhui ya EP yanahusu mapenzi, maisha na hisia za kina, yakionyesha ubunifu wa Mbosso akiwa msanii huru. Kwa mashabiki wa muziki wa Kiswahili, Room Number 3 ni ishara ya mwanzo mpya kwa Mbosso, na sasa inapatikana kwenye majukwaa yote ya kidijitali.

Read More
 Mbosso anyosha maelezo kuhusu kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo.

Mbosso anyosha maelezo kuhusu kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo.

Msanii wa Bongo Fleva, Mbosso amefunguka kuhusu tatizo la ugonjwa wa moyo ambalo limemwandama tangu akiwa mtoto. Akizungumza katika mahojiano maalum Mbosso ambaye ni msanii wa lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) amesema kwamba ugonjwa huo unasababishwa na mafuta kuwa mengi kwenye mishipa ya damu ya kwenda kwenye moyo. Dalili alilozitaja za ugonjwa huo ni pamoja na maumivu upande wa kushoto wa kifua, viungo kupoteza hisia na kwake anatetemeka vidole. Hata hivyo Mbosso amesema tangu atambue kuwa ana ugonjwa huo wa moyo amekuwa akimtembelea daktari wake mara kwa mara na kuyafuata maagizo yake katika juhudi za kutaka kupo.

Read More
 Mbosso afunguka sababu za kusitisha tour yake nchini Marekani

Mbosso afunguka sababu za kusitisha tour yake nchini Marekani

Nyota wa muziki wa Bongofleva, Mbosso ambaye kwa sasa anafanya vizuri na EP yake mpya, amesitisha ziara (tour) yake ya muziki nchini Marekani hadi tarehe mpya zitakapotangazwa tena. Marekani ambayo ilitarajiwa kuanza Novemba 25 mpaka Desemba 16, 2022. Kupitia instastory ya Mbosso metoa sababu za Kusitisha Ziara yake ya kwa kusema kuwa Daktari amemtaka kutokusafiri au kukaa kwenye Ndege kwa zaidi ya Masaa nane. Mbali na hayo Mbosso ameahidi kuwa Tour hiyo itaendelea pindi atakapo pata ruhusa kutoka kwaa Daktari.. Itakumbukwa, ziara (tour) hiyo ya Mbosso ilitakiwa kuanza rasmi mwezi huu, tarehe 25 na kumalizika Desemba 16.

Read More
 Wimbo mpya wa Mbosso “Yataniua” wafutwa youtube kwa madai ya hakimiliki

Wimbo mpya wa Mbosso “Yataniua” wafutwa youtube kwa madai ya hakimiliki

Siku moja baada ya msanii kutoka lebo ya WCB, Mbosso kuzindua EP yake aliyoipa jina la KHAN katika ufukwe wa Bahari Beach jijini Dar es Salaam, moja kati ya nyimbo sita zilizomo kwenye EP hiyo imeondolewa Youtube. Ngoma iliyoondolewa, inaitwa Yataniua ambayo Mbosso ameimba na bosi wake, Diamond Platnumz na hivyo kufanya ngoma zilizosalia YOUTUBE kuwa tano, Asalaam, Wayo, Shetani, Pole na Huyu Hapa. Tangu kuzinduliwa kwa EP hiyo, kuliibuka mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii, Diamond akituhumiwa kuigilizia nyimbo mbili kwenye kipande alichoimba katika wimbo huo. Kipande cha kwanza anachodaiwa kukopi ni kutoka kwa msanii Asake wa Nigeria katika Wimbo wake wa Peace Be Unto You ambapo alichokibadilisha Diamond ni maneno tu lakini staili ya uimbaji inafanana kwa kila kitu na kipande hicho cha Asake. Kipande cha pili ambacho Diamond anadaiwa kukopi, ni kutoka kwenye ngoma ya Adiwele kutoka kwa msanii wa Afrika Kusini, Young Stunna akiwa amewashirikisha Kabza De Small na DJ Maphorisa. Bado haijafahamika ni nini sababu kubwa ya kuondolewa kwa ngoma hiyo ingawa gumzo kubwa kwenye mitandao ya kijamii ni kwamba huenda wenye nyimbo zao wameuripoti wimbo huo kwa kukiuka sheria za hati miliki. Licha ya kuondolewa Youtube, bado wimbo huo unaendelea kupatikana kwenye platforms nyingine kama Audiomack na Spotify.

Read More
 Mbosso atangaza ujio wa ziara yake ya muziki nchini Marekani

Mbosso atangaza ujio wa ziara yake ya muziki nchini Marekani

Mwimbaji nyota kutoka lebo ya WCB, Mbosso ametangaza rasmi ujio wa ziara yake kimuziki ya kimatifa ya Marekani. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema ziara hiyo itaanza rasmi tarehe 25, mwezi Novemba hadi 16, mwezi Desemba. “King Khan Live in USA: Nov 25th – Dec 16th.”, Amaandika Mbosso. Mbosso ambaye ana zaidi ya streams Milioni 100 katika mtandao wa Boomplay, kwenye mahojiano yake na Dizzim Online mwishoni mwa wikiendi hii iliyoputa, aliweka wazi Oktoba 21, anaachia EP yake mpya ambayo ameitaja kuwa ndio project yake atakayoifungia mwaka.

Read More
 MBOSSO AFUNGUKA KUFANYA KAZI NA RAYVANNY

MBOSSO AFUNGUKA KUFANYA KAZI NA RAYVANNY

Hitmaker wa “Moyo”, Msanii Mbosso amefunguka uhusiano wake na Bosi wa Next Level Music Rayvanny. Katika mahojiano yake hivi karibuni Mbosso amesema licha ya Rayvanny kuondoka kwenye lebo ya WCB bado wana uwezo wa kufanya kazi pamoja kwani wao ni marafiki wakubwa. “Ni mwanangu, kwa hiyo inapokuja kazi ambayo natakiwa nifanye na Rayvanny lazima tufanye ni rafiki yangu, nakutana naye, anakuja ofisini tunapiga stori, yaani hakuna noma,” amesema Mbosso. Julai mwaka huu Rayvanny alijiondoa rasmi kwenye lebo ya WCB aliyoitumikia kwa miaka saba na kuelekeza nguvu zake katika lebo yake, Next Level Music ambayo inamsimamia msanii Mac Voice. Utakumbuka chini ya WCB Mbosso alimshirikisha Rayvanny katika wimbo wake uitwao Pakua kutoka kwenye albamu yake, Definition of Love huku Rayvanny akimshirikisha Mbosso kwenye ngoma yake, Zuena inayopatika kwenye albamu, Sound From Africa.

Read More
 ALBUM YA MBOSSO “DEFINITION OF LOVE”  YAFIKISHA STREAMS MILLIONI 55 BOOMPLAY

ALBUM YA MBOSSO “DEFINITION OF LOVE” YAFIKISHA STREAMS MILLIONI 55 BOOMPLAY

Album ya msanii Mbosso, “Definition Of Love” inaendelea kufanya vizuri kwenye digital platforms mbalimbali. Good news ni kwamba tayari imefikisha jumla ya Streams MILIONI 55 kwenye mtandao wa Boomplay. “Definition Of Love”, ndio album ya kwanza kwa mtu mzima Mbosso kuiachia tangu aanze safari yake ya muziki na pia alipojiunga na lebo ya WCB mwaka 2018. Album ya “Definition Of Love”, iliachiwa rasmi Machi 9, mwaka wa 2021 ikiwa na jumla ya nyimbo 12 za moto zenye maudhui ya mapenzi.

Read More
 MBOSSO ATHIBITISHA UJIO WA COLLABO YAKE NA PRODYUZA KRIZ BEATZ KUTOKA NIGERIA

MBOSSO ATHIBITISHA UJIO WA COLLABO YAKE NA PRODYUZA KRIZ BEATZ KUTOKA NIGERIA

Nyota wa muziki wa Bongofleva Mbosso ameunza mwaka 2022 kwa kuzitafuta ladha za kimataifa zaidi hii ni baada ya kuingia studio na mtayarishaji mkubwa wa muziki barani Afrika Kriz Beatz kutoka nchini Nigeria. Mbosso ambaye yupo nchini Nigeria na Diamond Platnumz amepost kupitia InstaStory yake akiwa studio na Kriz Beatz huku ikionesha wazi kabisa kuna kazi mpya wanaandaa. Kriz Beatz ni kati ya watayarishaji wakubwa wa muziki Barani Afrika waliotengeza nyimbo kali mbalimbali kama African Beauty ya Diamond Platnumz, 911 aliyowashirikisha Harmonize na Yemi Alade, Diana na Pana za Tekno.

Read More
 MBOSSO MUHANGA WA KAZI ZILIZOPOTEA KWA PRODYUZA MOCCO GENIUS

MBOSSO MUHANGA WA KAZI ZILIZOPOTEA KWA PRODYUZA MOCCO GENIUS

Mwanamuziki kutoka WCB Wasafi Mbosso amekuwa moja wahanga waliopoteza kazi zao za muziki kwa prodyuza wa muziki wa Bongofleva Mocco Genius . Prodyuza huyo ambaye ametengeneza mikwaju mingi iliyofanya vizuri zikiwemo nyimbo za Zuchu, ametangaza kupoteza data muhimu zenye kazi za wasanii tofauti tofauti zaidi ya 500, ambapo Mbosso kupitia post ya mtayarishaji huyo kwenye mtandao wa Instagram aliacha ujumbe unao onyesha kuwa kazi zake 54 pia zimekwenda na maji. Tayari Mocco Genius ametangaza kumlipa kiasi chochote cha fedha mtu atakayemrudishia data hizo muhimu.

Read More
 MASAUTI AFUNGUKA KUFUKUZWA NA PROMOTA JUKWAANI MOMBASA

MASAUTI AFUNGUKA KUFUKUZWA NA PROMOTA JUKWAANI MOMBASA

Staa wa muziki nchini Masauti amevunja kimya chake baada ya kudaiwa kuwa alifukuzwa jukwaani kwenye tamasha la muziki lilofanyika Mombasa wikiendi iliyopita. Kupitia waraka aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa instagram Masauti amesema masaibu yake yalitokana na promota wa tamasha hilo huku akiwataka mashabiki kutomulaumu mbosso kwani hakuwa mhusika mkuu wa show hiyo. “Sijataka kuongelea issue ya show ya Mombasa lakini pia nimeona nivunje ukimya ili kuepuka unafki. Najua mashabiki zangu wanahofu kutaka kujua what exactly happened ndio singependelea mtu atumie jina langu kuelezea my side of the story. Nataka niwaombe tu kwanza tukio hili lilitokea lisitumike kumharibia rafiki yangu @mbosso_ jina wakati siye aliyeandaa show hii,” amesema Masauti Hitmaker huyo wa No Stress amesema kuna mwanadada ambaye alimkatiza akiwa jukwaani anatumbuiza jambo ambalo lilimlazimu Willy M Tuva kuingilia kati ndipo akapewa nafasi tena ya kutumbuiza. “Makosa yatupiwe waandalizi wa show hio mchwara tena sio wote ni dada mmoja tu ambaye singependa nimtaje jina😏Yeye ndo hakutaka kuheshimu kazi yangu na kunionyesha thamani kama msanii wa nyumbani. Lakini kama mpambanaji niliamua kueka kazi kwanza maana sipendi kueka hisia zangu mbele kwakua nina familia nyuma inayoniangalia mimi tu. Siku ile ya show walienda kinyume na mahitaji yangu kwenye rider lakini wala sikuvunjika moyo kwakua ni kijana ninayepambania sanaa yangu ili familia yangu ipate rizki😣Hakukua ata na usafiri wangu ili kufika sound check,” amesema Masauti . Hata hivyo amesema mapromota wa tamasha hilo hawakufadhili  usafiri wake kutoka na kwenda kwenye show licha ya kuwa na mkataba wa makubaliano. Baada ya kama nusu saa hivi, nikiendelea kuperfoem nikaona nyuma kuna mvutano unaendelea kati ya management yangu na watu kwenye stage. Yuleyule dada alitaka kunikatiza show katikati😒Vita hivo viliendelea kati yao na uongozi wangu ambao ulipinga hilo wazo lao la kusmamisha show katikati. Dj alismamisha show kwasababu yule dada alimtishia kutomlipa🤬 mvutano uliendelea akaja @mzaziwillytuva aliyeingilia kati na kukataa mziki ukatishwe namna hio. Aliungana nasi show ikaendelea. Nikaimba na mashabiki zangu hadi wakati wangu ukaisha ndo nikashuka kwenye stage,” ameeleza Masauti. Kauli ya masauti inakuja siku chache baada ya Nadia Mukami kufunguka namna ambavyo walidhulumiwa kwenye tamasha la muziki lilofanyika mjini mombasa wikiendi hii iliyopita.

Read More