Megan Thee Stallion Afunguliwa Kesi Mpya Mahakamani

Megan Thee Stallion Afunguliwa Kesi Mpya Mahakamani

Jaji katika Mahakama Kuu ya Los Angeles ameamuru kuwa rapa maarufu Megan Thee Stallion na kampuni yake ya usimamizi Roc Nation wakabiliane na kesi ya madai yaliyowasilishwa na mpiga picha wake wa zamani, Emilio Garcia. Mwezi Aprili 2024, Emilio Garcia alifungua kesi akidai kuwa alilazimika kushuhudia tendo la ngono lililotokea wakati Megan alikuwa kwenye ziara yake ya muziki (Tour). Aidha, Emilio anadai pia kutolipwa malipo yake kwa kazi za muda wa ziada alizofanya akiwa mpiga picha binafsi wa rapa huyo, ambapo alihudumu kati ya mwaka 2018 hadi Juni 2023. Kesi hiyo bado inaendelea mahakamani, huku mawakili wa Megan Thee Stallion na Roc Nation wakipinga vikali madai hayo. Wakili wa upande wa Megan amesisitiza kuwa madai ya Emilio Garcia ni ya uongo na yanatumiwa kama mbinu ya kumchafua jina la mteja wao. Hata hivyo, mahakama imeamua kuwa madai hayo ya Emilio yatalazimika kushughulikiwa kisheria huku pande zote zikitoa hoja zao mbele ya jaji. Kesi hii imevutia umakini mkubwa kutoka kwa vyombo vya habari na mashabiki wa rapa huyo, huku wengi wakisubiri kuona hatma ya kesi hii ambayo inaweza kuwa na athari kwa hadhi ya Megan Thee Stallion na kampuni yake.

Read More
 Wakili wa Megan Thee Stallion Amshambulia Tory Lanez Baada ya Kuzindua Tovuti ya Kujitetea

Wakili wa Megan Thee Stallion Amshambulia Tory Lanez Baada ya Kuzindua Tovuti ya Kujitetea

Mvutano kati ya Megan Thee Stallion na Tory Lanez unaendelea kuchukua sura mpya, huku wakili wa Megan akitoa tamko kali kupitia jarida la XXL baada ya timu ya mawakili wa Tory kuzindua tovuti mpya inayodai kuonyesha ushahidi wa kutetea  haki ya msanii huyo. Tovuti hiyo, iliyoanzishwa na timu ya Tory Lanez, inalenga kushawishi umma kuhusu kutokuwa na hatia kwake katika kesi ya kumpiga risasi Megan Thee Stallion, tukio ambalo lilitokea mwaka 2020 na kumweka Tory kwenye matatizo makubwa ya kisheria. Katika kujibu hatua hiyo, wakili wa Megan alikemea vikali juhudi za Tory Lanez kujaribu kuandika upya simulizi ya tukio la kumpiga risasi Megan mwaka 2020. Alisema kuwa tovuti hiyo ni jaribio la kuwapotosha mashabiki na kulifanya jambo hili kuwa la burudani badala ya kutafuta haki. Wakili huyo alisisitiza kuwa Tory tayari alikutwa na hatia kupitia mfumo wa sheria wa Marekani, na kwamba kuendelea kujaribu kujiosha kupitia mitandao na vyombo vya habari ni kudhalilisha wahanga wa ukatili na kuleta mkanganyiko kwa umma. “Ni aibu kuona mtu anayejaribu kugeuza maumivu ya mtu kuwa kampeni ya mtandaoni. Ukweli ulishasemwa mahakamani, na haki ilitendeka,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo. Kwa upande wa Tory Lanez, timu yake ya mawakili imeendelea kushikilia kuwa msanii huyo hakutenda kosa lolote, na wanasema tovuti hiyo ni jukwaa la kutoa taarifa walizoita “uhalisia wa tukio.” Wakati huu, Tory Lanez bado anahudumu kifungo baada ya kupatikana na hatia katika kesi hiyo. Hata hivyo, juhudi za timu yake za kupigania hadhi yake mbele ya macho ya umma zinaendelea kushika kasi, huku wafuasi wa pande zote wakiendelea kupambana mitandaoni kwa maoni na mitazamo tofauti.

Read More
 Amber Rose Aibua Mjadala Mpya Kuhusu Kesi ya Megan Thee Stallion

Amber Rose Aibua Mjadala Mpya Kuhusu Kesi ya Megan Thee Stallion

Mwanamitindo na mwanaharakati Amber Rose ameeleza hadharani sababu za kumtetea msanii Tory Lanez katika kesi ya kumpiga risasi Megan Thee Stallion mwaka 2020. Akizungumza kwenye mahojiano ya moja kwa moja katika kipindi cha Chris Cuomo kinachorushwa kupitia NewsNation, Rose alisema anaamini Lanez hana hatia na anastahili kusamehewa na Gavana wa California, Gavin Newsom. Katika mazungumzo hayo, Amber Rose alisisitiza kuwa ushahidi uliopo hauonyeshi moja kwa moja kuwa Tory ndiye alifyatua risasi. Alisema Lanez ameshathibitishwa kuwa hana uhusiano wa moja kwa moja na silaha iliyotumika, jambo linaloonyesha kuwa alipaswa kuachiliwa huru. Chris Cuomo, hata hivyo, aliibua hoja kuwa sampuli za DNA zilionyesha kuwa silaha hiyo ilikuwa inaweza kuguswa na watu wanne tofauti, lakini pia akaongeza kuwa Lanez alituma ujumbe wa kuomba msamaha baada ya tukio hilo, huku Megan Thee Stallion na rafiki yake Kelsey, waliokuwepo usiku huo, wakimtaja Lanez kama mtu aliyefyatua risasi. Amber Rose alijibu kwa kusema kuwa amesikia simulizi nzima kutoka kwa Tory Lanez mwenyewe, ambaye alimpigia simu moja kwa moja kutoka gerezani na kumueleza kile kilichotokea usiku huo. Kauli hii ya Amber Rose imezua maoni mseto mitandaoni, huku baadhi wakimtetea kwa kuonyesha huruma na kutaka haki ya kweli itendeke, huku wengine wakimtuhumu kwa kupuuza ushahidi wa upande wa Megan Thee Stallion. Haya yanakuja siku chache baada ya Amber Rose kuchapisha kipande cha video kinachomuonyesha Mwakilishi wa Bunge la Marekani, Anna Paulina, akimwambia Cuomo kuwa Tory Lanez hana hatia na kwamba kesi hiyo ililetwa kwake na Amber Rose mwenyewe.

Read More
 Tory Lanez Ahamishwa Gerezani Baada ya Kudaiwa Kuchomwa Kisu Mara 14

Tory Lanez Ahamishwa Gerezani Baada ya Kudaiwa Kuchomwa Kisu Mara 14

Rapa Tory Lanez, ambaye jina lake halisi ni Daystar Peterson, ameripotiwa kuhamishwa kutoka Gereza la California Correctional Institution lililopo Tehachapi, baada ya tukio la kushambuliwa na kuchomwa kisu mara 14. Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na tukio hilo, Lanez alivamiwa ndani ya gereza hilo na kushambuliwa katika tukio linalodaiwa kuhusiana na migogoro ya magenge ya uhalifu, hasa kundi la Bloods. Ingawa majeraha aliyoyapata hayakuwa ya kutishia maisha, shambulio hilo limezua hofu kubwa kuhusu usalama wake akiwa gerezani. Baada ya tukio hilo, rapa huyo alihamishiwa katika Gereza la North Kern State Prison, lililoko Delano, California, kwa lengo la kumlinda dhidi ya mashambulizi zaidi. Uhamisho huo unatajwa kufanyika haraka mara baada ya shambulio hilo. Tory Lanez anatumikia kifungo cha miaka 10 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumpiga risasi msanii mwenzake Megan Thee Stallion mwaka 2020, tukio ambalo lilizua gumzo kubwa katika tasnia ya burudani ya Marekani. Hata hivyo, Idara ya Magereza na Marekebisho ya Tabia ya Jimbo la California haijatoa taarifa rasmi kuthibitisha tukio hilo au sababu za uhamisho, ikitaja sababu za faragha na usalama wa wafungwa. Mashabiki na wafuasi wa rapa huyo sasa wanasubiri taarifa rasmi kuhusu hali yake ya afya na hatima ya kesi au uchunguzi wowote unaoweza kufunguliwa kutokana na tukio hilo la kushangaza.

Read More
 Wanasheria wa Megan Thee Stallion Wakanusha Ushahidi Mpya Katika Kesi ya Tory Lanez

Wanasheria wa Megan Thee Stallion Wakanusha Ushahidi Mpya Katika Kesi ya Tory Lanez

Wakili wa rapa maarufu Megan Thee Stallion wametoa taarifa rasmi wakikanusha madai ya kambi ya Tory Lanez kuwa kuna ushahidi mpya ambao unaweza kumuondolea hatia kwenye kesi ya kumpiga risasi Megan mwaka 2020. Katika ripoti yenye kurasa 31 iliyotolewa wiki hii, timu ya sheria ya Megan imeeleza kuwa madai hayo yanayosambazwa ni ya kupotosha na hayana msingi wowote wa kisheria. Wameyataja kama “hadithi za uongo” zinazoenezwa na kile walichokiita “watesi wajinga.” “Hakuna ushahidi mpya kutoka Ring camera kama inavyodaiwa, na shahidi anayetajwa hajawahi kuwa eneo la tukio, wala kutoa ushahidi wowote hadharani au mahakamani,” alisema wakili Alex Spiro. Megan Thee Stallion pia aliunga mkono msimamo huo mapema wiki hii, akitoa kauli zinazosisitiza kuwa juhudi za kudhoofisha ukweli ni sehemu ya mateso yanayoendelea dhidi yake kama mhanga wa tukio hilo. Kesi hiyo iliibua hisia kali za kijamii na mitandaoni, na licha ya hukumu ya mahakama, juhudi za upande wa Tory Lanez kutaka kesi ifunguliwe upya au hukumu ipunguzwe zimeendelea kuchochea mijadala. Hata hivyo, timu ya Megan inasisitiza kuwa hakuna msingi wa kisheria au ushahidi wowote mpya wa kuanzisha mwelekeo tofauti wa kisheria. Kwa sasa, Tory Lanez anatumikia kifungo gerezani kufuatia hukumu hiyo ya kumpiga risasi Megan, na kesi hiyo inaendelea kuibua mazungumzo kuhusu haki kwa waathirika wa vurugu za silaha, na pia athari za upotoshaji wa umma kwenye kesi nyeti.

Read More
 Megan Thee Stallion Aonyesha Hasira kwa Mashabiki wa Tory Lanez Walio na Mashaka Kuhusu Kesi ya Risasi

Megan Thee Stallion Aonyesha Hasira kwa Mashabiki wa Tory Lanez Walio na Mashaka Kuhusu Kesi ya Risasi

Rapa maarufu kutoka Marekani, Megan Thee Stallion, ameamua kupambana hadharani na mashabiki wa Tory Lanez ambao bado wanakanusha ukweli kwamba mwanamuziki huyo alimpiga risasi licha ya uamuzi wa mahakama ya juri mjini Los Angeles kuthibitisha hilo. Kupitia ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, Megan ameonesha kuchoshwa na mashambulizi ya mfululizo kutoka kwa baadhi ya watu wanaoendeleza kampeni ya kumdhalilisha, huku akimtaja Tory Lanez kama shetani anayeendelea kumletea mateso hata baada ya hukumu. “Muda umefika muache kunitesa. Mlikuwa na nafasi ya kusema mliyotaka mahakamani. Mnaendelea tu na uongo  ni kama mapepo,” Megan alisema kwa hasira. Megan ambaye anaendelea na kazi yake ya muziki, ameweka wazi kuwa bado anapitia changamoto za kiakili kutokana na matukio hayo, hasa kutokana na mashambulizi ya mfululizo kutoka kwa baadhi ya watu mitandaoni. Ameongeza kuwa bado anaumizwa na namna watu wanavyopuuza ukweli na kumshambulia yeye badala ya kumwajibisha Tory. “Mahakama ilizungumza. Ukweli ulidhihirika. Lakini bado naandamwa kana kwamba mimi ndiye mwenye makosa.” aliongeza. Kauli hiyo imeibua mjadala mkali mtandaoni huku mashabiki wake wakimtetea vikali na kuitaka jamii kumheshimu kama manusura wa tukio la vurugu. Wengine, hususan wafuasi wa Tory, bado wanaonekana kushikilia imani tofauti, jambo linalozua sintofahamu kubwa. Tory Lanez tayari anatumikia kifungo gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kumpiga Megan risasi mwaka 2020, tukio lililotokea baada ya sherehe usiku. Huu ni mwendelezo wa mvutano kati ya Megan na Tory ambao umegusa si tu mashabiki wao, bali pia wasanii na wanaharakati wa haki za wanawake kwenye tasnia ya muziki duniani.

Read More
 Ombi la Kumtaka Gavana Newsom Kumsamehe Tory Lanez Lavuka Saini 250,000

Ombi la Kumtaka Gavana Newsom Kumsamehe Tory Lanez Lavuka Saini 250,000

Msanii maarufu wa muziki wa Hip Hop, Tory Lanez, ameendelea kupata uungwaji mkono mkubwa mtandaoni kupitia ombi lililowekwa kwenye mtandao wa Change.org, likimtaka Gavana wa California, Gavin Newsom, amsamehe. Kwa siku tatu mfululizo, ombi hilo limekuwa namba moja kwa kupendwa na kusainiwa zaidi kwenye jukwaa hilo, na kufikisha zaidi ya saini 250,000. Ombi hilo linataka msamaha rasmi kwa Tory Lanez kufuatia kifungo alichopokea baada ya kupatikana na hatia ya kumjeruhi rapa Megan Thee Stallion kwa risasi. Juhudi hizo zimeungwa mkono na watu maarufu kutoka tasnia ya burudani nchini Marekani, akiwemo Drake, Amber Rose, na Ty Dolla Sign. Wanaounga mkono ombi hilo wanadai kuwa hukumu dhidi ya Tory ilikuwa na upendeleo na kwamba anastahili kupewa nafasi ya pili. Hata hivyo, kuna kundi linalopinga hatua hiyo, likisema kuwa kila mtu anapaswa kuwajibika kwa matendo yake bila kujali umaarufu. Hadi kufikia sasa, ofisi ya Gavana Newsom haijatoa tamko rasmi kuhusu ombi hilo au uwezekano wa msamaha. Hali ikiendelea kuchacha, mjadala kuhusu haki, sheria, na nafasi ya watu maarufu mbele ya vyombo vya sheria unaendelea kushika kasi.

Read More
 Mwanasheria wa Megan Thee Stallion Avunja Ukimya Kufuatia Madai Mapya ya Timu ya Tory Lanez

Mwanasheria wa Megan Thee Stallion Avunja Ukimya Kufuatia Madai Mapya ya Timu ya Tory Lanez

Mwanasheria wa mwanamuziki maarufu wa Marekani, Megan Thee Stallion, Alex Spiro, amejitokeza kutoa kauli kali kufuatia taarifa zilizotolewa jana na timu ya mawakili wa Tory Lanez kuhusu kesi ya kumpiga risasi Megan. Kupitia taarifa kwa jarida la XXL Magazine, Spiro amejibu madai yaliyotolewa katika mkutano wa waandishi wa habari uliandaliwa na mawakili wa Lanez, ambapo walidai kuwa rafiki wa Megan, Kelsey Harris, ndiye aliyempiga risasi msanii huyo – na siyo Tory Lanez kama ilivyodaiwa awali. Spiro amekanusha vikali madai hayo, akisisitiza kuwa hukumu iliyotolewa dhidi ya Tory Lanez ilifuata mchakato halali wa kisheria.  “Tory Lanez alishtakiwa na kutiwa hatiani na wenzake, na kesi yake ilipitia katika mfumo sahihi wa mahakama. Hili si suala la kisiasa – hii ni kesi ya shambulio la kikatili ambalo lilisikilizwa na kuamuliwa kwa mujibu wa sheria,” alisema Spiro. Kesi hiyo, ambayo ilivuta hisia za watu wengi kote duniani, ilimalizika kwa Tory Lanez kupatikana na hatia ya kumshambulia Megan kwa kutumia silaha ya moto, tukio lililotokea Julai 2020. Hukumu hiyo ilileta mgawanyiko mkubwa mtandaoni kati ya mashabiki wa pande zote mbili. Kwa sasa, bado haijabainika kama ushahidi mpya uliodaiwa na timu ya Tory Lanez utawasilishwa rasmi mahakamani kwa ajili ya rufaa au mapitio ya kesi.

Read More
 Familia ya Rapa Tory Lanez yamsameha Megan Thee Stallion

Familia ya Rapa Tory Lanez yamsameha Megan Thee Stallion

Familia ya rapa Tory Lanez imeweka wazi kumsamehe rapa Megan Thee Stallion. Baba mzazi wa rapa Tory Lanez, Sostar Peterson amethibitisha hilo kufuatia sakata la mwanae kukutwa na hatia ya makosa ya kumpiga risasi ya mguu rapa huyo Julai, mwaka 2020.. Kauli ya mzee huyo imekuja wiki chache baada ya kutoridhishwa na uamuzi wa Mahakama juu ya mwanae ambapo aliishtumu label ya Roc Nation ya Jay Z kuhusika katika uamuzi huo wa Mahakama. Ikumbukwe, Tory Lanez alikutwa na hatia ya makosa yote matatu na kwa sasa yupo rumande akisubiri hukumu yake kusomwa Februari 28, mwaka 2023 akitazamia kifungo cha miaka 22 jela.

Read More
 Baba mzazi wa Rapa Tory Lanez amshtumu Jay Z kwa kuhujumu kesi inayomkabili mwanaye

Baba mzazi wa Rapa Tory Lanez amshtumu Jay Z kwa kuhujumu kesi inayomkabili mwanaye

Baba mzazi wa Rapa Tory Lanez ameonekana kutoridhishwa na maamuzi ya mahakama kumkuta na hatia mwanaye kwenye shtaka la kumpiga risasi Megan Thee Stallion ambapo huenda akahukumiwa kifungo cha zaidi ya miaka 20 gerezani. Akiwa nje ya Mahakama, mzee huyo Sonstar Peterson, amemshtumu rapa Jay-Z pamoja Roc Nation kuwa wamehusika nyuma ya pazia kwenye maamuzi hayo. Familia nzima ya Tory Lanez imeonesha kuwa na hasira na Jay-Z pamoja na Beyonce wakidai kufanyiwa mchezo mchafu na familia hiyo. Jay-Z anatajwa kuhusika hadi kwenye kulipa gharama za kuendesha kesi hiyo. Ikumbukwe mwezi Juni mwaka 2022, Jay-Z alitangaza kumsaini Megan Thee Stallion ndani ya Roc Nation.

Read More
 Tory Lanez afunguka baada ya mahakama kumpata na hatia ya kumjeruhi Megan Thee Stallion

Tory Lanez afunguka baada ya mahakama kumpata na hatia ya kumjeruhi Megan Thee Stallion

Rapa Tory Lanez, amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya mahakama kumpata na hatia kwenye shtaka la kumpiga risasi Megan Thee Stallion, Julai mwaka 2020. Kwa mujibu wa L.A Times, rapa huyo amekaririwa akisema kuwa amesikitishwa na uamuzi wa mahakama lakini anaamini kila jambo katika maisha lina sababu zake. Tory Lanez atabaki rumande akingoja hukumu yake kusomwa Januari 27, mwaka 2023 baada ya kukutwa na hatia kwenye mashtaka matatu ikiwemo kumshambulia Megan kwa kutumia silaha lakini pia kubeba silaha iliyopakiwa risasi na ambayo pia haijasajiliwa. Hata hivyo timu ya Tory Lanez imeonekana kutoridhishwa na maamuzi ya mahakama, hivyo wakili wake George Mgdesyan anapanga kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo kwani hakuna ushahidi uliojitosheleza.

Read More
 Tory Lanez akutwa na hatia ya kumpiga risasi Megan Thee Stallion

Tory Lanez akutwa na hatia ya kumpiga risasi Megan Thee Stallion

Mahakama ya jiji la Los Angeles imemkuta na hatia rapa Tory Lanez kwa makosa matatu ikiwemo la kumshambulia na kumjeruhi kwa risasi aliekuwa mpenzi wake mwanamuziki Megan Thee Stallion. Tukio hilo lilitokea baada ya mabishano yaliyosababishwa na utani ambapo inadaiwa Tory Lanez alikasirika na kufyatua risasi zilizomjeruhi miguuni Megan Thee Stallion. Mara baada ya maamuzi ya mahakama Lanez aliondoka mahamani hapo chini ya ulinzi mkali kuelekea gereza la Los Angeles kusubiri kuanza kutumikia adhabu yake. Tory Lanez ambaye jina lake ni Daystar Peterson anaweza kuhukumiwa kifungo cha mpaka miaka 22 jela katika hukumu inayotarajiwa kusomwa Januari 25.

Read More