Mr. Seed Afunguka kwa Uchungu: “Polisi Sio Marafiki Zetu”

Mr. Seed Afunguka kwa Uchungu: “Polisi Sio Marafiki Zetu”

Msanii wa muziki nchini Kenya, Mr. Seed, ameungana na Wakenya wanaomwombea Boniface Kariuki, kijana aliyepigwa risasi na polisi na ambaye kwa sasa yuko ICU, kwa kutoa ujumbe mzito wa majonzi na hasira kupitia mitandao ya kijamii. Katika ujumbe wake wa wazi na wa kugusa hisia, Mr. Seed alisema kuwa hali ya usalama nchini inamfanya kujiuliza kama kweli polisi bado wanaweza kuaminika kama walinzi wa raia. Alieleza kuwa tukio hilo limemvunja moyo kiasi cha kufikiria kuwafundisha watoto wake kuwa polisi si marafiki, bali chanzo cha hofu kwa wananchi. “Nahisi kama ni lazima nifundishe watoto wangu kuwa polisi si marafiki zetu, si ndugu wala dada zetu… wanatuua na kutufanya maisha kuwa magumu,” aliandika kwa uchungu. Akiwa amejaa hasira na maumivu, Mr Seed aliongeza kauli kali ya kulaani ukatili wa polisi akimalizia ujumbe wake kwa maneno: “F** the popo!!”* Kauli hiyo, licha ya kuwa na hisia kali, imezua mjadala mkubwa mtandaoni, ambapo baadhi ya wananchi walionyesha kuungana naye kwa maumivu yanayotokana na ukatili wa maafisa wa usalama, huku wengine wakihimiza matumizi ya lugha ya staha kutokana na nafasi yake kama msanii. Mr. Seed ni miongoni mwa wasanii kadhaa waliotoa maoni yao kufuatia tukio la kupigwa risasi kwa Boniface, pamoja na Eric Omondi ambaye ametangaza kampeni ya kuvaa barakoa Ijumaa hii kama njia ya kumbukumbu na mshikamano kwa waathiriwa wa ukatili wa polisi. Wito wa haki kwa Boniface Kariuki unaendelea kushika kasi, huku mashirika ya haki za binadamu yakitaka uchunguzi wa haraka na hatua kali kuchukuliwa dhidi ya waliohusika. Huku hasira na huzuni zikiendelea kutanda nchini, sauti za wanamuziki na wasanii zinazidi kuwa sauti za wananchi, wakitaka mabadiliko ya kweli katika mfumo wa usalama wa taifa.

Read More
 Mr Seed atuhumiwa kukimbia majukumu ya kumlea mwanaye

Mr Seed atuhumiwa kukimbia majukumu ya kumlea mwanaye

Mzazi mwenza wa msanii Mr Seed, Liz Sonia amemtuhumu msanii huyo kwa kukimbia majukumu ya kumlea mwanaye. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Liz amesema Mr. Seed amekuwa akikwepa majukumu yake kama baba kwa kipindi cha miaka saba iliyopita. Aidha amesema kitendo cha Hitmaker huyo wa “Dawa ya Barida” kushindwa kutoa mahitaji ya msingi kwa motto wao ilimlazimu kujitolea kumhangaikia mwanaye ili aweze kukimu maisha yake. Mrembo huyo amekiri kuchoshwa kubeba majukumu ya Mr. Seed ambaye amekuwa jeuri kwa muda mrefu huku akimuonya abadili miendo yake vingnevyo atakuja kujutia siku za mbeleni.

Read More
 Mr Seed akanusha kuwa tapeli mtandaoni

Mr Seed akanusha kuwa tapeli mtandaoni

Msanii kutoka nchini Kenya Mr Seed amekanusha tuhuma za kuwalaghai watu mtandaoni. Akizungumza na Mungai Eve amesema madai hayo hayana ukweli wowote akisema kuwa yeye ni mfanyibiashara na mwekezaji wa sarafu ya bitcon. Msanii huyo amesema hana ufahamu wowote kuhusu mtandao wa Send Wave Platform ambao anadaiwa kutumia kuwatapeli watu pesa zao. Kauli yake imekuja mara baada ya baadhi ya wanawake kujitokeza na kudai Mr. Seed aliwaibia fedha zilizotengewa miradi ya uwekezaji wa nyumba.

Read More
 Mr. Seed akerwa na kitendo cha Eric Omondi kuwakimbia wasanii waliotumbuiza kwenye hafla ya Jimmy Wanjigi

Mr. Seed akerwa na kitendo cha Eric Omondi kuwakimbia wasanii waliotumbuiza kwenye hafla ya Jimmy Wanjigi

Staa wa muziki Mr. Seed ameonekana kutofurahishwa na mienendo ya mchekeshaji Eric Omondi ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa akipigania maslahi ya muziki wa Kenya. Kwenye mahojiano na Presenter Ali, Mr. Seed amekerwa na kitendo cha Omondi kuwatumia vibaya wasanii waliotumbuiza kwenye hafla ya mwanasiasa jimmy wanjigi kwa kushindwa kuwatetea walipwe pesa zao licha ya kuwa karibu na mwanasiasa huyo. Hitmaker huyo wa ngoma ya dawa ya baridi amesema licha kumueleza Omondi masaibu yake na wasanii wengine waliotumbuiza kwenye hafla ya mwanasiasa huyo amekuwa jeuri kwenye suala la kuwasilisha malalamiko yao kwa Jimmy Wanjigi kwani amekuwa akitoa ahadi za uongo ambazo mpaka sasa hajaweza kutimiza. Utakumbukwa hii sio mara ya kwanza kwa Jimmy Wajingi kukosa kuwalipa watoa huduma kwenye shughuli zake kwani kipindi cha nyuma alituhumiwa pia kukwepa kulipa madeni ya wanamitindo wa mavazi waliyompa huduma.

Read More
 Mr. Seed mbioni kuachia Black Child Deluxe Album Edition

Mr. Seed mbioni kuachia Black Child Deluxe Album Edition

Mwanamuziki kutoka Kenya Mr. Seed ametusanua kuwa anakuja na Black Child Deluxe Album version, mara baada ya album hiyo kufanya vizuri mtandaoni. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema ataongeza nyimbo 5 kwenye ‘Deluxe edition’ ya album hiyo iliyotoka Oktoba 5 mwaka Jana ikiwa na nyimbo 11. Aidha amesema kwa yupo mbioni kufanya maandalizi ya listen party itakayohudhuriwa na wageni waalikwa pekee kabla ya Album hiyo kuingia sokoni rasmi. Mfumo huo wa deluxe version’ hufanywa na msanii katika album husika kwa kuongeza baadhi ya remix, au nyimbo mpya ambapo harmonize ametaja kuiongeza ngoma ya Dawa ya Baridi Remix ambayo kwa sasa inafanya vizuri.

Read More
 Mr. Seed afunguka chanzo cha kumaliza ugomvi wake na Bahati

Mr. Seed afunguka chanzo cha kumaliza ugomvi wake na Bahati

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Seed amefichua kuwa waliamua kumaliza ugomvi wao na Bahati kwa manufaa ya watoto wao. Kwenye mahojiano na World IS, Mr. Seed amesema watoto wao walikuwa wakishambuliwa kila mara kwenye mitandao ya kijamii kutokana na utofauti wao kimuziki, kitendo kilichowalazimu kukutana na kuweka kando uhasama wao ambao ungeathiri ukuaji wa watoto wao katika siku za mbeleni. “Nilikuwa nikiposti picha za mtoto wangu Gold na mashabiki wenye roho chafu walikuwa na mazoea ya kumlinganisha na mtoto wa Bahati Majesty. Hilo pia lilitokea kwa upande wa Bahati na watoto wetu wangeishia kutusiwa,” Alisema. Mr. Seed na Bahati ambao walikuwa marafiki wa karibu, walitofautiana mwaka 2018 baada ya wake zao Diana Marua na Nimo Gachuiri kukosa maelewano katika hafla ya mkesha wa mwaka mpya. Kwa mujibu wa mashuhuda, Diana alipinga wazo la Nimo la kuuza kahawa na vitafunio kwenye sherehe hiyo na aliishia kuwapigia simu polisi kumuondoa Nimo ambaye kwa wakati huo alikuwa mjamzito mzito.

Read More
 Avril afunguka sababu ya kuitosa Kolabo ya Mr. Seed

Avril afunguka sababu ya kuitosa Kolabo ya Mr. Seed

Mwanamuziki Avril amefunguka madai ya kuitosa kolabo ya msanii mwenzake Mr. Seed mwaka wa 2021. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Avril amesema hakuweza kufanya kazi ya pamoja na msanii huyo kwa sababu kipindi hicho alikuwa ameshikika na masuala ya kuitayarisha album yake ya Spirit. Hitmaker huyo wa “Chokoza” ameahidi kufanikisha kolabo yake na Mr. Seed hivi karibuni pindi tu ratiba zao zitakapokuwa sawa. Kauli yake imekuja mara baada ya mr. Seed kudai kuwa Avril amekuwa akikwepa kufanya nae kazi kwa muda wa miaka minne sasa licha ya kumkumbusha kila mara. Haikushia hapo alienda mbali zaidi na kudai kuwa wimbo wake wa ndoa alipaswa kumshirikisha Avril lakini kilichotokea na kumvunja moyo ni kitendo cha msanii huyo kuanza kumchunia kwa kutojibu meseji zake, hivyo akaamua kurekodi wimbo huo na mwigizaji Kate the Actress.

Read More
 MR SEED ADOKEZA KOLABO NA GUCHI KUTOKA NIGERIA

MR SEED ADOKEZA KOLABO NA GUCHI KUTOKA NIGERIA

Mwimbaji nyota nchini Mr. Seed licha ya kuwa anaendela kufanya vizuri na wimbo wake “Pressure”, mkali huyo hataki kupoa, ametumia wikiendi hii iliyopita kurekodi ngoma mpya. Mr. Seed amepost misururu ya picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa studio na Guchi wakiwa wanarekodi, hali inayoashiria kuwa wawili hao wapo mbioni kuachia wimbo wa pamoja. Guchi amekuwa nchini kwa ajili ya tamasha lakr la kimuziki ambalo limekamilika wikindi iliyopita.

Read More
 MR. SEED MBIONI KUACHIA DAWA YA BARIDI REMIX

MR. SEED MBIONI KUACHIA DAWA YA BARIDI REMIX

Nyota wa muziki nchini Mr. Seed ameweka wazi kuachia remix ya smash hit yake iitwayo “Dawa ya Baridi”. Wimbo ambao bado unaendelea kufanya vizuri kupitia majukwaa mbalimbali ya ku-stream muziki mtandaoni. Mr Seed ametangaza uwepo wa remix hiyo kupitia mahojiano yake na nicholas kioko ambapo amedokeza mpango wa kumshirikisha mbosso kutoka WCB kwenye remix ya wimbo wa dawa ya Baridi. Katika hatua nyingine amethibitisha pia kujikita zaidi katika suala la kufanya kolabo na wasanii mbali mbali ndani ya mwaka huu tofauti na mwaka jana alipokuwa anajishugulisha na kazi zake za muziki kama msanii wa kujitegemea. Utakumbuka kwa sasa Mr. Seed anafanya vizuri na wimbo wake mpya uitwao Pressure aliyomshirikisha Nviiri the story teller ambao una zaidi ya views laki 2 youtube ndani  ya wiki moja.

Read More
 MR. SEED AKERWA NA KITENDO CHA JIMMY WANJIGI KUKWEPA DENI LAKE

MR. SEED AKERWA NA KITENDO CHA JIMMY WANJIGI KUKWEPA DENI LAKE

Staa wa muziki nchini Mr. Seed ameonekana kutofurahishwa na miendo ya mfanyibiashara aliyeugikia  siasa Jimmy Wanjigi. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Mr. Seed ameandika ujumbe wa masikitiko kwenda kwa wanjigi akisema kwamba mwanasiasa huyo ameshindwa kumlipa pesa zake licha ya kutoa huduma kwenye hafla yake ya siasa majumaa kadhaa yaliyopita. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Dawa ya Baridi” amesema Wanjigi amekuwa jeuri kwenye suala la kumlipa deni lake kwani kila mara akimuulizia kuhusu deni lenyewe amekuwa akitoa ahadi za uongo ambazo mpaka hajaweza kutimiza. Hata hivyo suala hilo limeibua maswali mengi miongoni mwa Wakenya kwenye mitandao ya kijamii ambapo wameonekana kumlaumu Mr. Seed kwa kukubali kufanya kazi na mwanasiasa bila ya kuwa na mkataba wa maelewano. Utakumbukwa hii sio mara ya kwanza kwa Jimmy Wajingi kukosa kuwalipa watoa huduma kwenye shughuli zake kwani kipindi cha nyuma alituhumiwa pia kukwepa kulipa madeni ya wanamitindo wa mavazi waliyompa huduma.

Read More
 MR. SEED AFUNGUKA MAZITO KUHUSU UKARIBU WAKE NA BAHATI

MR. SEED AFUNGUKA MAZITO KUHUSU UKARIBU WAKE NA BAHATI

Msanii nyota nchini Mr Seed amemuandika waraka mrefu msanii mwenzake Bahati baada ya hitmaker huyo wa ngoma ya Adhiambo kuweka wazi azma yake ya kuwania ubunge wa Mathare kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Kupitia waraka huo ambao aliuandika kupitia ukurasa wake wa Instagram Mr. Seed ameeleza namna alivyokula maisha ya taabu na bahati wakiwa wanaishi mathare, kipindi ambacho walikuwa wanajaribu kupenya kwenye kiwanda cha muziki nchini. Kulingana na Hitmaker huyo wa ngoma ya “Around”, umaskini ulikuwa sehemu ya maisha yao na haikuwazuia kuwaza mambo makubwa ambayo walikuwa wanatamani kufanikisha katika maisha yao. Mr. Seed ambaye ni bosi wa lebo y muziki ya Starbon ametangza kumuunga mkono bahati kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka wa 2022 ambapo amemtaja msanii huyo kama kiongozi ambaye anawafaa wakaazi wa eneo hilo. Itakumbukwa mapema mwaka wa 2019 mr seed waliingia kwenye bifu na bahati baada msanii huyo kuigura lebo ya muziki ya EMB ambako alikuwa amesainiwa kwa kipindi cha miaka miwili. Lakini ilikuja ikabainika baadae kuwa bifu ya wawili hao ilisababishwa na ugomvi ulioibuka kati ya wake zao.

Read More
 MR SEED AMZAWADI MAMA YAKE MZAZI KIPANDE CHA ARDHI

MR SEED AMZAWADI MAMA YAKE MZAZI KIPANDE CHA ARDHI

Msanii nyota nchini Mr. Seed anazidi kujipakulia baraka ya wazazi wake mara baada ya kumzawadi mama yake mzazi kipande cha ardhi ambacho ana mpango wa kumjengea mjengo wa kifahari. Kupitia video aliyoiposti kwenye ukurasa wake wa Instagram Bosi huyo wa lebo ya muziki ya Starborn Empire ametusanua kuwa shamba hilo aliyomnunulia mama yake lipo eneo la Matuu, Kaunti ya Machakos. Hakuishia hapo ameenda mbali zaidi na kutoa ushuhuda wa ndani ya maisha yake kwa kusema kwamba kuna kipindi familia yake ilipitia maisha magumu kiasi cha kukosa chakula kila siku. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Ndoa” amewahimiza vijana na mastaa wenzake kukumbuka  wazazi wao wanapofanikiwa kimaisha kwa kuwanunulia vitu vya thamani kwani bila wao wasingeweza kufanikisha baadhi ya malengo yao. Utakumbuka mwaka wa 2018 Mr. Seed alimzawadi mama yake mzazi gari mpya aina Toyota Audi kwa kuwa mama bora kwake lakini pia mwaka wa 2021 aliingia kwenye headlines nchini alipomnunulia mke wake Nimo gari mpya aina ya Mazda Demio kwa kusimama nae kipindi ambacho alikuwa amefulia kiuchumi.

Read More