Remix ya “Pawa” Yamletea Nyota Ndogo Zawadi ya KSh100,000 Kutoka kwa Khaligraph Jones

Remix ya “Pawa” Yamletea Nyota Ndogo Zawadi ya KSh100,000 Kutoka kwa Khaligraph Jones

Mwanamuziki wa Pwani, Nyota Ndogo, amejipatia zawadi ya shilingi laki moja kutoka kwa rapa Khaligraph Jones, hatua inayohusishwa moja kwa moja na kampeni yake ya hivi karibuni ya kumtetea Papa Jones aingizwe kwenye remix ya wimbo “Pawa” wa Mbosso. Nyota Ndogo amefichua kupitia Instagram kuwa alishtuka alipokea ujumbe wa malipo (M-PESA) kutoka kwa Khaligraph, akieleza kuwa rapa huyo alimwambia zawadi hiyo ilikuwa ni ishara ya kumshukuru kwa kusimama upande wake kwenye mjadala wa remix hiyo. Wiki kadhaa zilizopita, Nyota Ndogo alitumia mitandao ya kijamii kushinikiza wasanii na mashabiki kuona umuhimu wa Khaligraph kushirikishwa katika remix ya Pawa. Alisisitiza kuwa iwapo rapa huyo angepewa nafasi, remix ya Mbosso ingezidi kupata nguvu na mvuto mkubwa katika soko la muziki wa Afrika Mashariki. Kitendo cha Khaligraph kimepongezwa na mashabiki mitandaoni, wengi wakikitafsiri kama heshima kubwa kwa msanii huyo wa Pwani na pia kuthibitisha jinsi rapa huyo anavyoweza kuthamini wale wanaomuunga mkono. Kwa sasa, bado haijathibitishwa rasmi iwapo Khaligraph atashirikishwa kwenye remix ya Mbosso, lakini tukio hili limezua mjadala mpana kuhusu ushirikiano wa wasanii wa Tanzania na Kenya, na jinsi sapoti ya wasanii wenzao inaweza kubadilisha mwelekeo wa muziki.

Read More
 Nyota Ndogo Amsikitikia Mrembo Aliyedai Hataki Kuolewa Wala Kuzaa

Nyota Ndogo Amsikitikia Mrembo Aliyedai Hataki Kuolewa Wala Kuzaa

Mwanamuziki kutoka Kenya, Nyota Ndogo, ameonyesha masikitiko yake kufuatia kauli ya mrembo wa mtandaoni kwa jina la Lydia Wanjiru, aliyesema hadharani kuwa hataki kuolewa wala kuzaa, akidai ndoa ni mzigo na watoto ni kero maishani. Kupitia ujumbe alioweka kwenye ukurasa wake wa Instagram, Nyota Ndogo amesema kuwa kila mtu ana haki ya kuamua namna anavyotaka kuishi, lakini akaonya kuwa mitazamo ya aina hiyo inapochapishwa hadharani inaweza kuwa na athari kwa vijana na wafuasi wanaochukulia kauli hizo kama mwongozo wa maisha. Msanii huyo amesisitiza kuwa watoto ni baraka ya kipekee inayomletea mzazi furaha na msaada mkubwa maishani. Ameongeza kuwa mara nyingi watoto huwa nguzo muhimu hasa katika uzee, kipindi ambacho marafiki na watu wengine huanza kujitenga. Hata hivyo, Nyota Ndogo amemwonya Lydia kwamba anaweza kujutia uamuzi wake huo baada ya miaka mingi, akisisitiza kuwa jamii bado inathamini familia na nafasi ya mzazi ni ya kipekee isiyoweza kuchukuliwa na mtu mwingine. Kauli ya Nyota Ndogo imezua mjadala mitandaoni, huku baadhi ya wafuasi wakimtetea kwa kusimamia maadili ya kifamilia, ilhali wengine wakisisitiza kuwa uhuru wa mtu binafsi unapaswa kuheshimiwa.

Read More
 Nyota Ndogo Atoa Onyo kwa Wasichana wa Ughaibuni

Nyota Ndogo Atoa Onyo kwa Wasichana wa Ughaibuni

Msanii Nyota Ndogo ametoa ujumbe mzito kwa wasichana wa Kiafrika wanaofanya kazi katika mataifa ya Kiarabu, akiwataka kuwa waangalifu na mahusiano ya mtandaoni. Kupitia Instgram yake, ameeleza kuwa mabinti wengi hujikuta wakitumika kihisia na kifedha na wanaume wasiowajali, huku wakiteseka kazini kwa masharti magumu. Nyota Ndogo amesema kuwa baadhi ya wanaume huwatumia wanawake walioko nje ya nchi kama chanzo cha fedha, wakiwadanganya kwa maneno matamu ya mapenzi. Amesema wapo wanaume wanaowalazimisha wanawake kuwatumia pesa za kodi, miradi au matumizi ya kila siku, huku wao wakifaidika kwa urahisi bila kuchangia chochote. Akiwa na uzoefu binafsi wa kufanya kazi ya ndani akiwa na umri wa miaka 17, Nyota amesema anafahamu vyema uchungu wa maisha ya ughaibuni. Alisisitiza kuwa wanawake wengi hujikuta wakibeba mzigo mara mbili kazi ngumu na mahusiano yenye mateso ya kihisia. Hitmaker huyo wa Watu na Viatu, ameonya kuwa tabia hii imewafanya baadhi ya wanaume kuwa wavivu wa maisha, kwa sababu wanategemea msaada kutoka kwa wanawake walioko nje. Alishauri mabinti wajifunze kujipenda na kutosema kila kitu mtandaoni, kwani baadhi ya watu hutumia taarifa hizo kuwadhulumu. Nyota Ndogo amemalizia kwa kuwaombea wasichana walioko ughaibuni, akisisitiza kuwa wanahitaji ulinzi wa Mungu dhidi ya udanganyifu wa mapenzi na hali ngumu za kazi. Kauli yake imeibua hisia mbalimbali mitandaoni, wengi wakikiri kuguswa na ujumbe huo wa uhalisia.

Read More
 Nyota Ndogo: Bora Kuolewa na Mwanaume Aliyetalikiwa Kuliko Aliyefiwa

Nyota Ndogo: Bora Kuolewa na Mwanaume Aliyetalikiwa Kuliko Aliyefiwa

Msanii wa muziki kutoka Pwani, Nyota Ndogo, ametoa mtazamo wake kuhusu ndoa na uhusiano. Kupitia ujumbe aliouchapisha, alisema kuwa kwake binafsi, anaona ni bora mwanamke aolewe na mwanaume ambaye ameachana na mke wake kwa talaka, kuliko mwanaume ambaye amempoteza mke kwa kifo. Kwa mujibu wake, mwanaume ambaye ameachana na mke wake mara nyingi huwa tayari kuanza ukurasa mpya, tofauti na yule aliyefiwa na mke, ambaye kumbukumbu na mapenzi ya mke aliyefariki hubaki moyoni na mara nyingi huathiri ndoa mpya. Baadhi ya mashabiki walikubaliana naye wakisema ni vigumu kushindana na kumbukumbu ya mke aliyefariki, huku wengine wakimkosoa wakidai kuwa kifo hakimaanishi mtu amekwama katika maisha ya ndoa, kwani anaweza kumpenda na kumheshimu mke mpya bila matatizo. Nyota Ndogo mara kwa mara hutoa maoni ya moja kwa moja kuhusu masuala ya ndoa na mahusiano, na amesema huwa anazungumza kile anachoamini bila kuficha hisia zake.

Read More
 Nyota Ndogo Amwaga Hisia Kuhusu Uzee na Shinikizo la Mitandao ya Kijamii

Nyota Ndogo Amwaga Hisia Kuhusu Uzee na Shinikizo la Mitandao ya Kijamii

Msanii maarufu wa muziki kutoka Pwani ya Kenya, Nyota Ndogo, ameibua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii baada ya kueleza hisia zake kuhusu namna watu wanavyomzungumzia kutokana na mwonekano wake wa sasa. Kupitia chapisho la hisia kwenye Instagram, Nyota Ndogo aliweka wazi kuwa baadhi ya watu humtusi au kumshusha hadhi kwa sababu ya uzee, hali ya kawaida inayomkumba kila mwanadamu. “Nikisema tujipostini bila filter hamtaki. Nikijipost kazeeka. Kwani uzee dhambi?” aliandika kwa uchungu lakini pia kwa msimamo thabiti. Kauli hiyo imeonekana kama wito kwa jamii kuacha kuweka shinikizo lisilo la haki kwa watu maarufu, hasa wanawake, kuonekana vijana milele kwa kutumia vichujio au kuficha umri wao. Mashabiki wengi walimpongeza kwa ujasiri wake na kumwita mfano bora wa kujikubali. Wengi waliungana naye kwa kusema kuwa tasnia ya burudani na mitandao ya kijamii imejaa vigezo visivyo halisi vya urembo, na kwamba uzee haupaswi kuwa jambo la aibu. Katika enzi ambayo mitandao ya kijamii imejaa shinikizo la kuonekana vijana milele, ujumbe wa Nyota Ndogo unakuja kama ukumbusho kwamba uzee si udhaifu wala dhambi, bali ni sehemu ya safari ya maisha inayoleta busara, hadhi na uzuri wa kipekee.

Read More
 Nyota Ndogo Alalamikia Ukosefu wa Mwitikio kwa Muziki wa Kenya

Nyota Ndogo Alalamikia Ukosefu wa Mwitikio kwa Muziki wa Kenya

Mwanamuziki maarufu wa Kenya, Nyota Ndogo, amezua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutoa kauli yenye uzito kuhusu hali ya muziki wa Kenya katika vyombo vya habari vya ndani. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Nyota Ndogo alilalamikia ukosefu wa msaada kwa wasanii wa humu nchini, hasa katika vipindi vya redio na televisheni. “Mgeni akiingia Kenya, ni ngumu kujua kama ameingia Kenya kwa sababu redio na TV za Kenya hazisupport mziki wa ndani,” alisema kwa uchungu msanii huyo ambaye amekuwa kwenye tasnia kwa zaidi ya muongo mmoja. Kauli hiyo imeibua hisia mseto kutoka kwa mashabiki na wadau wa muziki, wengi wakikubaliana naye kwamba muziki wa Kenya haupewi nafasi ya kutosha kwenye majukwaa ya kitaifa. Wengine walihisi kuwa wasanii pia wana jukumu la kuboresha kazi zao ili zilingane na viwango vya kimataifa. Nyota Ndogo aliongeza kuwa redio na runinga nyingi hupendelea kucheza muziki wa mataifa ya nje kama Nigeria, Afrika Kusini, na Tanzania, hali inayodhoofisha ukuaji wa tasnia ya muziki ya Kenya na kuwakatisha tamaa wasanii chipukizi. “Hatuna uhaba wa vipaji. Tunachohitaji ni jukwaa la kuonekana na kusikika. Bila hayo, muziki wa Kenya utaendelea kudidimia,” alisisitiza. Wasanii wengine wamejitokeza kuunga mkono kauli ya Nyota Ndogo, wakitoa wito kwa serikali na wadau wa burudani kuwekeza zaidi katika kukuza muziki wa ndani kwa kuweka sera madhubuti zitakazolazimisha vyombo vya habari kutoa angalau asilimia fulani ya muda wao kwa muziki wa Kenya. Kwa sasa, mjadala huu unaendelea kushika kasi, na wengi wanatumai kuwa sauti ya Nyota Ndogo itafungua macho ya wale walio kwenye nafasi za maamuzi ili kuchukua hatua madhubuti kwa manufaa ya wasanii wa Kenya.

Read More
 Nyota Ndogo athibitisha kulipwa pesa zake baada ya kutapeliwa

Nyota Ndogo athibitisha kulipwa pesa zake baada ya kutapeliwa

Msanii mkongwe nchini Nyota ndogo amethibitisha kulipwa pesa zake siku moja baada ya kudai kuporwa na watu waliotumia vyumba vya kulala katika hoteli yake na kisha kutoroka. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Nyota ndogo ameshindwa kuficha furaha yake kwa walioshea video clip akiwa anatoa malalamiko yake ambapo amedai kuwa watu hao walimlipa pesa ya huduma aliyowapa huku wakiomba radhi kwa jaribio la kutaka kumdhulumu jasho lake. Sanjari na hilo, Msanii huyo amekiri kosa la kuwahudumia watu hao kabla ya malipo huku akiahidi kutorudia makosa yake kwani amejifunza kutoamini watu asiowafahamu. “Thank you so much my people. Video ya kilio imefika mbali sana jamaa wamelipa na yakutoa.nilikua na number zao but sikueka nilikua na majina Yao but sikueka niliwaurumia juu najua mungewavamia sana,” “…wameomba pia samahani pia ahsante kwa wote walioshare video ya kiliochangu nyie nyote mumechangia mimi kulipwa. MUNGU awabariki.mumesimama na mimi…pia makosa yetu ni kuwacha waingie kabla kulipa hio kosa sitaikwepa nimekubali pia imenifunza,” Ameandika.

Read More
 Nyota Ndogo aporwa maelfu ya pesa

Nyota Ndogo aporwa maelfu ya pesa

Msanii mkongwe kwenye muziki Nyota Ndogo amejipata akiwa kwenye huzuni mkubwa katika kipindi hiki cha sikukuu baada ya watu waliokuwa wamekodisha vyumba vya kulala katika hoteli yake kushindwa kulipia gharama ya huduma aliyowapa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” amesikitishwa na kitendo cha watu hao wanane kudanganya mhudumu wa vyumba hivyo kuwa walimtumia pesa kwa laini yake binafsi kabla ya kutoroka na kuzima simu zao. Mwanamuziki huyo mwenye makaazi yake Pwani ya Kenya hajaweka wazi ni muda gani watu hao waliishi kwenye vyumba hivyo ila amesisitiza kuwa watakuwa wa mwisho kumfanya vitendo vya kitapeli. Hata hivyo watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii wameonekana kumhurumia kwa utapeli aliofanyiwa huku wakimtaka kuripoti kisa hicho kwa polisi lakini pia wakamshauri kuanzisha mfumo wa watu kulipia kwanza huduma kabla ya kuwapa vyumba vya kulala.

Read More
 Nyota Ndogo akataa zawadi ya bei ghali kutoka kwa mume wake Henning Nielsen

Nyota Ndogo akataa zawadi ya bei ghali kutoka kwa mume wake Henning Nielsen

Mwanamuziki mkongwe nchini Nyota Ndogo amewashangaza mashabiki baada ya kukataa zawadi ya bei ghali kutoka kwa mpenzi wake mwenye asili ya kizungu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema hana haja na toleo jipya la simu aina ya iphone 14 ambayo  mume wake Henning Nielsen alikuwa amepanga kumzawadi huku akisema kuwa tayari ana simu aina ya iphone 11 ambayo kwa mujibu wake amerithika nayo. Hitmaker huyo wa ‘Watu na Viatu” amemtaka mume wake kumnunulia shamba na kumjengea hoteli ya kifahari kwani itawasaidia kama kitega uchumi kipindi ambacho mume wake huyo atastaafu. Hata hivyo mume wake amesisitiza kuwa atamnunulia simu ya iphone 14  huku akiridhia ombi  la kumnunulia shamba na kumjenga hoteli.

Read More
 SHILOLE AUMIZWA NA MAUJI YA MAKE UP ARTIST TANZANIA

SHILOLE AUMIZWA NA MAUJI YA MAKE UP ARTIST TANZANIA

Msanii wa muziki na mjasiriamali nchini Tanzania Shilole amelizwa na tukio la mauaji ya mrembo maarufu wa shughuli za urembo (Make up artist) aliyeuawa kwa kupigwa risasi saba kichwani. Kupitia waraka mrefu aliouandika kupitia ukurasa wake wa Instagram Shilole amesema kuwa ndoa siyo jela, na mtu akishindwa na masuala ya ndoa anapaswa kuondoka kwani ndoa za siku hizi siyo kama za zamani ambazo mtu anaweza vumilia. Hitmaker huyo wa “Pindua Meza” amesema kuwa kama mwanaume hamjali mke wake na anampiga kila wakati ni vyema mwanamke achane nae kwani anaweza kumsababishia matatizo. Mwanamke huyo aitwaye Swalha aliuawa kwa kupigwa na risasi na mumewe usiku wa kumkia Jumapili ya Mei 29 mwaka 2022. Tukio hilo limetokea nyumbani kwa wanandoa hao huko Buswelu nchini Tanzania huku chanzo kikielezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Read More
 NYOTA NDOGO AFUNGUKA SABABU ZA UKIMYA WAKE KWENYE MUZIKI

NYOTA NDOGO AFUNGUKA SABABU ZA UKIMYA WAKE KWENYE MUZIKI

Msanii mkongwe kwenye muziki, Nyota Ndogo ameweka wazi kwamba kwa sasa hana uwezo wa kutayarisha muziki mpya licha ya mashabiki wengi kumshawishi sana arudi studioni. Nyota Ndogo amebainisha kuwa kwa sasa anasimamamia Hoteli yake huku akiwasihi mashabiki wake kupromoti biashara yake hiyo. “Naona mashabiki wanasema nitoe nyimbo sasa mwenyewe nilisahau kuimba, njooni hotelini kwangu munipromoti chakula napika vizuri sana,” Nyota Ndogo ameandika kupitia Instagram. Mwanamuziki huyo kutoka eneo la Pwani amedokeza kuwa ana mpango wa kufanya media tour hivi karibuni huku akitoa ombi kwa vyombo vya habari kutomhoji kwa Kiingereza kwani hana uwezo wa kuzungumza lugha hiyo kwa ufasaha. “I was thinking nifanye media tour lakini naomba kuojiwa kwa kingereza tu. Uwa nakiongea vizuri kimoyo moyo lakini nikifungua mdogo balaa.but the more nakiongea nikama mazoezi vile imagine umefungua radio nyota anaongea kingereza simtakufa na vicheko but me I don’t care nitakazana”, Amefichua hilo kupitia Instagram.

Read More
 NYOTA NDOGO: NDOA SIO JELA, UKISHINDWA ONDOKA TU

NYOTA NDOGO: NDOA SIO JELA, UKISHINDWA ONDOKA TU

Msanii mkongwe kwenye tasnia ya muziki nchini Nyota Ndogo amefunguka kuhusu visa vya mauji ambavyo vimeongezeka miongoni mwa wana ndoa katika siku za hivi karibuni. Kupitia waraka mrefu aliouandika kupitia ukurasa wake wa Instagram Nyota Ndogo amesema kuwa ndoa siyo jela, na mtu akishindwa na masuala ya ndoa anapaswa kuondoka kwani ndoa za siku hizi siyo kama za zamani ambazo mtu anaweza vumilia. “Wanawake tunavumilia kweli lakini lakini musikubali kuendeshewa ndoa zenu na wazazi wenu. Kweli ndoa nikuvumiliana lakini uvumilivu hio ulikua wakatii wao. Kitambo ilikua hakuna mauwaji ya mke kamuua mume ama mume kamuua mke. Kitambo hapakua na watu sijui kuchomwa na mume mauwaji mpaka Sasa yameingia kwa watoto MUNGU wangu twaelekea wapi?” amesema Nyota Ndogo. Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” amesema kuwa kama mwanaume hamjali mke wake na anampiga kila wakati ni vyema mwanamke achane nae kwani anaweza kumsababishia matatizo. “Huwezi kumpiga mke wako Kisha useme unampenda. Vile vile mke pia uwezi kumpiga mume useme unampenda nyinyi mumechokana na nyinyi ndio munajua mulipofikishana. Talaka hairuhusiwi katika dini lakini kwa kikazi hiki unaletewa mwanao maiti ama nimzima lakini Hana viungo vingine vya mwili. Ukinichoka umenichoka hata kuekwe vikao vya nyumba kumi hio ndio haiwezi kua.” amesisitiza Nyota Ndogo. Nyoa Ndogo ameongeza kuwa “Ifike Mahali tuseme Tosha I will not kill my wife nitamrudisha kwao mzima kama nilivyomchukua atapata mume mwengine na wewe pia utapata mke vile vile kwa mke. INATOSHA JAMANI INATOSHA MAUWAJI YAMEZINI MPAKA HATUOGOPI TENA SIMBA TINAOGOPA MWANADAMU”

Read More