SHILOLE AUMIZWA NA MAUJI YA MAKE UP ARTIST TANZANIA

SHILOLE AUMIZWA NA MAUJI YA MAKE UP ARTIST TANZANIA

Msanii wa muziki na mjasiriamali nchini Tanzania Shilole amelizwa na tukio la mauaji ya mrembo maarufu wa shughuli za urembo (Make up artist) aliyeuawa kwa kupigwa risasi saba kichwani. Kupitia waraka mrefu aliouandika kupitia ukurasa wake wa Instagram Shilole amesema kuwa ndoa siyo jela, na mtu akishindwa na masuala ya ndoa anapaswa kuondoka kwani ndoa za siku hizi siyo kama za zamani ambazo mtu anaweza vumilia. Hitmaker huyo wa “Pindua Meza” amesema kuwa kama mwanaume hamjali mke wake na anampiga kila wakati ni vyema mwanamke achane nae kwani anaweza kumsababishia matatizo. Mwanamke huyo aitwaye Swalha aliuawa kwa kupigwa na risasi na mumewe usiku wa kumkia Jumapili ya Mei 29 mwaka 2022. Tukio hilo limetokea nyumbani kwa wanandoa hao huko Buswelu nchini Tanzania huku chanzo kikielezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Read More
 NYOTA NDOGO AFUNGUKA SABABU ZA UKIMYA WAKE KWENYE MUZIKI

NYOTA NDOGO AFUNGUKA SABABU ZA UKIMYA WAKE KWENYE MUZIKI

Msanii mkongwe kwenye muziki, Nyota Ndogo ameweka wazi kwamba kwa sasa hana uwezo wa kutayarisha muziki mpya licha ya mashabiki wengi kumshawishi sana arudi studioni. Nyota Ndogo amebainisha kuwa kwa sasa anasimamamia Hoteli yake huku akiwasihi mashabiki wake kupromoti biashara yake hiyo. “Naona mashabiki wanasema nitoe nyimbo sasa mwenyewe nilisahau kuimba, njooni hotelini kwangu munipromoti chakula napika vizuri sana,” Nyota Ndogo ameandika kupitia Instagram. Mwanamuziki huyo kutoka eneo la Pwani amedokeza kuwa ana mpango wa kufanya media tour hivi karibuni huku akitoa ombi kwa vyombo vya habari kutomhoji kwa Kiingereza kwani hana uwezo wa kuzungumza lugha hiyo kwa ufasaha. “I was thinking nifanye media tour lakini naomba kuojiwa kwa kingereza tu. Uwa nakiongea vizuri kimoyo moyo lakini nikifungua mdogo balaa.but the more nakiongea nikama mazoezi vile imagine umefungua radio nyota anaongea kingereza simtakufa na vicheko but me I don’t care nitakazana”, Amefichua hilo kupitia Instagram.

Read More
 NYOTA NDOGO: NDOA SIO JELA, UKISHINDWA ONDOKA TU

NYOTA NDOGO: NDOA SIO JELA, UKISHINDWA ONDOKA TU

Msanii mkongwe kwenye tasnia ya muziki nchini Nyota Ndogo amefunguka kuhusu visa vya mauji ambavyo vimeongezeka miongoni mwa wana ndoa katika siku za hivi karibuni. Kupitia waraka mrefu aliouandika kupitia ukurasa wake wa Instagram Nyota Ndogo amesema kuwa ndoa siyo jela, na mtu akishindwa na masuala ya ndoa anapaswa kuondoka kwani ndoa za siku hizi siyo kama za zamani ambazo mtu anaweza vumilia. “Wanawake tunavumilia kweli lakini lakini musikubali kuendeshewa ndoa zenu na wazazi wenu. Kweli ndoa nikuvumiliana lakini uvumilivu hio ulikua wakatii wao. Kitambo ilikua hakuna mauwaji ya mke kamuua mume ama mume kamuua mke. Kitambo hapakua na watu sijui kuchomwa na mume mauwaji mpaka Sasa yameingia kwa watoto MUNGU wangu twaelekea wapi?” amesema Nyota Ndogo. Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” amesema kuwa kama mwanaume hamjali mke wake na anampiga kila wakati ni vyema mwanamke achane nae kwani anaweza kumsababishia matatizo. “Huwezi kumpiga mke wako Kisha useme unampenda. Vile vile mke pia uwezi kumpiga mume useme unampenda nyinyi mumechokana na nyinyi ndio munajua mulipofikishana. Talaka hairuhusiwi katika dini lakini kwa kikazi hiki unaletewa mwanao maiti ama nimzima lakini Hana viungo vingine vya mwili. Ukinichoka umenichoka hata kuekwe vikao vya nyumba kumi hio ndio haiwezi kua.” amesisitiza Nyota Ndogo. Nyoa Ndogo ameongeza kuwa “Ifike Mahali tuseme Tosha I will not kill my wife nitamrudisha kwao mzima kama nilivyomchukua atapata mume mwengine na wewe pia utapata mke vile vile kwa mke. INATOSHA JAMANI INATOSHA MAUWAJI YAMEZINI MPAKA HATUOGOPI TENA SIMBA TINAOGOPA MWANADAMU”

Read More
 NYOTA NDOGO AMSHAMBULIA MWANABLOGU ALIYEMZUSHIA TAARIFA ZA UONGO

NYOTA NDOGO AMSHAMBULIA MWANABLOGU ALIYEMZUSHIA TAARIFA ZA UONGO

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Nyota Ndogo amechukizwa na kitendo cha mwanablogu mmoja  kuchapisha taarifa za uongo dhidi yake. Mwanablogu huyo alichapisha taarifa akisema kwamba Nyota Ndogo  alidai kwenye moja ya interview kuwa asipoimba jina lake litazidi kuzungumziwa nchini ikizangatiwa kuwa ni msanii mkongwe ambaye ameacha alama kwenye tasnia ya muziki nchini. Sasa kupitia instagram page yake Nyota Ndogo ameibuka na kukanusha madai yaliyoibuliwa na blogger huyo kwa kusema kwamba hajawahi jigamba kuwa yeye ni bora kuliko msanii yeyote kwani hapendi kabisa kujisifu kwenye maisha yake. Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” amesema kama watu wamechoshwa na muziki wake wa sasa ni afadhali waanze kusapoti biashara yake ya vyakula ya Nyota Ndogo jikoni ambayo makao yake yapo mjini voi, kaunti ya Taita Taveta.

Read More
 NYOTA NDOGO AELEZA ANAVYOITWA SURA MBAYA NA WANAUME MITANDAONI

NYOTA NDOGO AELEZA ANAVYOITWA SURA MBAYA NA WANAUME MITANDAONI

Msanii mkongwe kwenye muziki  nchini Nyota Ndogo, amefunguka namna ambavyo amekua akishambuliwa kwa maneno ya kejeli mtandaoni na baadhi ya wanaume kwa kumuita sura mbaya. Nyota Ndogo kupitia ukurasa wake wa Instagram amefunguka namna amekuwa akipokea kejeli haswa kutoka kwa wanaume, baada ya kufikisha umri wa miaka 40 mwaka huu. “Sasa kuitwa mazee na sura Mbaya nishazoea munaweza mukatafuta maneno makali mengine yakuniita na wengi wao uwa wanaume mybe I look much better at 40 kushinda your galfriend mwenye ako 25.hatukatai uzee uzee ni sunna ni hatizeeki kizembe hatujitupi wall yangu ikikusinya ni block” amesema Nyota Ndogo. Hata hivyo Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” amesema kwamba amezoea kuitwa sura mbaya na hivyo wanaomshambulia wanapaswa kutafuta maneno mengine ya kumuita huku akieleza kwamba yeye ni mrembo kuliko wapenzi wao wa miaka 25.

Read More
 NYOTA NDOGO AINGIA UBIA WA KUFANYA KAZI NA KAMPUNI YA JOY MILLERS LIMITED.

NYOTA NDOGO AINGIA UBIA WA KUFANYA KAZI NA KAMPUNI YA JOY MILLERS LIMITED.

Staa wa muziki nchini Nyota Ndogo amelamba dili nono la kuwa balozi wa unga wa ugali wa Raha Premium. Nyota Ndogo ametengaza habari hiyo njema kwa mashabiki zake kupitia ukurasa wake wa instagram huku akieleza kuwa ana furaha kujiunga na familia ya Raha Premium. Lakini pia ameishikuru uongozi wa kampuni ya Joy Miller Limited kwa kutambua nguvu yake na kuhamua kumpatia dili hilo ambalo litamjengea heshima. Nyota Ndogo sasa atatakiwa kutangaza bidhaa za Raha Premium kwa mashabiki zake kupitia mitandao ya kijamii kwa lengo la kuongeza mauzo ya unga hiyo ya ugali. Hitmaker huyo wa “Watu na Viatu” anajunga na msanii Bahati pamoja mke wake Diana Marua ambao pia waliingia ubia wa kufanya kazi na kampuni ya Joy millers limited mwezi Agosti mwaka huu. Ikumbukwe nyota ndogo ni mmoja kati ya wasaani ambao wamewekeza kwenye biashara kuuza vyakula na amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kutangaza mgahawa wake ambao ameupa jina la  Nyota Ndogo jikoni.

Read More