Nyota Ndogo Awaonyesha Upendo Madereva kwa Kuwapikia Chakula Siku ya Valentine’s
Mwanamuziki na mfanyabiashara kutoka Kenya, Nyota Ndogo, ameamua kuwaonyesha upendo madereva wa bajaji, boda boda na magari kwa kuwapikia chakula maalum kama ishara ya kuthamini mchango wao katika jamii kwenye siku ya wapendanao duniani. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Nyota Ndogo ameposti video ikionesha namna alivyowapikia pilau na kuwagawia madereva hao huku akisindikiza na maua kama zawadi ya Valentine. Msanii huyo amesema aliamua kusherekea siku ya wapendao na madereva kutokana na umuhimu wao kwenye jamii hasa ikizingatiwa kuwa wamekuwa mstari wa mbele kuwahakikishia abiria usalama wa wao barabarani. Katika tukio hilo, madereva walipokea chakula kwa furaha huku wakimpongeza kwa moyo wake wa kujali jamii. Wengi wameeleza kuwa kitendo hicho kimewapa hamasa na kuwafanya wajihisi kuthaminiwa. Hatua ya Nyota Ndogo imepongezwa na mashabiki wake mitandaoni, wakisema kuwa amedhihirisha maana halisi ya mapenzi kwa kuonesha kuwa Valentine si kwa wapenzi pekee, bali ni siku ya kusambaza upendo kwa kila anayestahili.
Read More