Octopizzo Akataa Dini ya Kikristo

Octopizzo Akataa Dini ya Kikristo

Rapa kutoka Kenya, Octopizzo, amezua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutoa kauli tata kuhusu dini, hususan Ukristo. Akizungumza kwa uwazi, Octopizzo amesema kuwa haamini katika dini ya Kikristo, akidai kuwa Ukristo kwa sasa umegeuzwa kuwa kitega uchumi na baadhi ya viongozi wa dini. Kwa mujibu wake, hali hiyo imemfanya kukosa imani na uhalisia wa dini hiyo. Msanii huyo amesema imani yake imejikita zaidi katika ufahamu na utambuzi wa ndani, maarufu kama consciousness, akieleza kuwa mtu anaweza kuishi maisha yenye mwelekeo bila ulazima wa kufungamana na dini rasmi. Aidha, Octopizzo amehoji kwa nini Ukristo una maelfu ya madhehebu ilhali waumini wote wanamwabudu Mungu mmoja. Ameeleza kushangazwa kwake na ukosefu wa umoja miongoni mwa Wakristo, akisema hali hiyo inaibua maswali kuhusu mshikamano na uhalisia wa imani hiyo. Hakuishia hapo, rapa huyo pia amekosoa mwenendo wa kidini nchini Kenya, akidai kuwa Wakristo ndio kundi linalohukumu watu zaidi katika jamii, jambo analosema linakwenda kinyume na mafundisho ya upendo na uvumilivu.

Read More
 Octopizzo Atoa Wito kwa Viongozi Kuwajibika kwa Matatizo ya Wafanyakazi

Octopizzo Atoa Wito kwa Viongozi Kuwajibika kwa Matatizo ya Wafanyakazi

Msanii wa muziki wa hip-hop kutoka Kenya, Octopizzo, ameikosoa vikali tabaka la wanasiasa nchini humo kwa kutoonyesha uwajibikaji katika matatizo yanayowakabili wananchi wa kawaida, hasa wafanyakazi wa sekta za umma. Kupitia taarifa aliyoandika kwenye ukurasa wake wa X, Octopizzo amehoji kwa nini viongozi waliochaguliwa kama wabunge, maseneta na wawakilishi wadi hawajawahi kuandamana kudai mishahara yao inapochelewa, ilhali watumishi wengine wa umma mara kwa mara hulazimika kufanya hivyo. Amebainisha kuwa kila mwaka, wataalamu muhimu kama madaktari, walimu na wahadhiri hulazimika kugoma au kuandamana kutokana na kucheleweshewa mishahara na mazingira duni ya kazi. Kwa mujibu wake, hawa ni watu wanaobeba mfumo wa afya na elimu wa taifa, na madai yao ni ya haki na muhimu kwa maendeleo ya taifa. Rapa huyo, amewataka viongozi kuchukua hatua za kweli kukabiliana na changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa Kenya, badala ya kujikita katika maslahi binafsi ambayo hayaleti mabadiliko kwa wananchi wanaowawakilisha. Octopizzo pia amewakumbusha viongozi wajibu wao wa kuhudumia umma, kulinda katiba na kuhakikisha huduma za serikali zinawanufaisha wananchi wote kwa usawa.

Read More
 Octopizzo Azuru Nyumbani kwa Odinga Kutoa Pole kwa Familia

Octopizzo Azuru Nyumbani kwa Odinga Kutoa Pole kwa Familia

Msanii wa hip hop nchini Kenya, Octopizzo, amezuru nyumbani kwa familia ya hayati Baba Raila Odinga ili kutoa heshima zake za mwisho na kushiriki majonzi pamoja nao. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Octopizzo amechapisha picha akiwa na familia ya Odinga na kueleza kuwa ilikuwa fahari kubwa kwake kuonyesha heshima kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Raila Odinga. Ametoa shukrani zake za dhati kwa Raila Junior na Mama Ida Odinga kwa mapokezi ya kifamilia na ukarimu waliomuonyesha wakati wa ziara hiyo. Octopizzo pia ametuma salamu za rambirambi akiwatakia familia hiyo faraja, nguvu na neema katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, huku akihimiza umoja na upendo miongoni mwa Wakenya wakati wa msiba huo.

Read More
 Rapa Octopizzo Aomboleza Kifo cha Meneja Wake Ongaya Vick

Rapa Octopizzo Aomboleza Kifo cha Meneja Wake Ongaya Vick

Msanii wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Octopizzo, ameingia katika majonzi kufuatia kifo cha meneja wake na rafiki wa muda mrefu, Ongaya Vick, anayefahamika pia kwa jina la Cheeks Zone. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Octopizzo ameeleza huzuni yake kuu akitangaza msiba huo, akisema Ongaya hakuwa tu meneja bali pia alikuwa mtu aliyemwamini na kumtia moyo tangu mwanzo wa safari yake ya muziki. Kwa mujibu wa Octopizzo, Ongaya ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuona uwezo wake wakati wengi walikuwa na mashaka kama muziki wa rap ungeweza kumtoa kisanaa. Amesema tangu mwaka 2009, Ongaya amekuwa nguzo kuu ya ubunifu nyuma ya chapa ya Octopizzo, akisaidia kuijenga hadi kufikia mafanikio ya kimataifa. Rapa huyo ameeleza kuwa imani na maono ya marehemu yalimsaidia si tu katika taaluma yake ya muziki, bali pia kumfanya kuwa mtu bora zaidi maishani. Kwa sasa, marafiki na jamaa wanakusanyika katika makazi ya familia ya Ongaya eneo la Woodley, Nairobi, kwa maandalizi ya mazishi. Marehemu anatarajiwa kuzikwa nyumbani kwake Kakamega, ambako familia itamkumbuka kama mtu mwenye moyo wa upendo, ubunifu, na uongozi.

Read More
 Octopizzo Aipeperusha Bendera ya Kenya Grammy 2026

Octopizzo Aipeperusha Bendera ya Kenya Grammy 2026

Msanii wa hip hop kutoka Kenya, Octopizzo, ameweka historia mpya baada ya kutangazwa kuwa miongoni mwa wasanii walioteuliwa kwa hatua ya kujadiliwa katika mchakato wa Tuzo za Grammy za 2026. Octopizzo amethibitisha habari hiyo njema kupitia ukurasa wake wa Instagram, akieleza kuwa anahisi heshima kubwa kuona kazi zake zikifikia hatua hiyo. Wimbo wake “Kadi” umechaguliwa kwa vipengele viwili, Song of the Year na Best Global Music Performance, wakati kazi yake nyingine “June 25th” ikichaguliwa kwa Best African Music Performance. Rapa huyo ameeleza kuwa hatua hiyo ni ushahidi wa namna muziki wa Afrika unavyopata nafasi kwenye jukwaa la kimataifa,huku akiwashukuru wanachama wa jopo la wapiga kura wa Grammy kwa kuthamini kazi kutoka bara hilo. Hata hivyo Octopizzo amesema kuwa lengo lake ni kupeleka simulizi za Kiafrika hadi kwenye jukwaa la dunia kupitia muziki wake.

Read More
 Kimeumana! Diss Track Yawafanya Marapa Octopizzo na Kayvo Washikane Mashati

Kimeumana! Diss Track Yawafanya Marapa Octopizzo na Kayvo Washikane Mashati

Rap ya Kenya imewaka moto tena baada ya marapa Octopizzo na Kayvo KForce kujipata wakirushiana maneno makali kiasi cha karibu kuzichapa kwa makonde. Chanzo cha mvutano huu kilikuwa diss track ya Kayvo, iliyolenga moja kwa moja kuhoji uhalali wa Octopizzo katika kiwanda cha hip hop. Baada ya Diss hiyo, wawili hao walikutana uso kwa uso, hali ikawa tete. Octopizzo alionekana kumwonya Kayvo akome, akimtaka aache kuingilia maisha yake ya muziki kwa kuachia “diss tracks za kijinga” na badala yake ajikite kuboresha sanaa yake. Kayvo hakusita kujibu, akimtuhumu Octopizzo kwa kudhoofisha jina lake. Alidai kuwa kauli za rapa huyo kwenye Iko Nini Podcast, kwamba hatoki Kibera, zilimchafua hadharani. Octopizzo naye hakusalia kimya; alirudisha moto kwa kudai Kayvo amekuwa akijipendekeza kama mwana wa Kibera ilhali hajakulia wala kuishi humo. Kayvo alipuuza hoja hizo akisisitiza kwamba hazina mashiko. Kauli hizo zilimkera zaidi Octopizzo, ambaye alimtaka Kayvo aonyeshe makazi yake Kibera kama anadai ni mwenyeji. Aidha, alimshutumu kwa kutumia jina la Kibera kwa manufaa binafsi. Mzozo huo uliwafikisha pabaya kiasi cha kushikana mashati na kuanza kurushiana makonde, lakini hali hiyo ilidhibitiwa na watu wa karibu waliowaingilia kati. Kwa kumbukumbu, wawili hao waliwahi kuwa marafiki na hata kuachia wimbo wa pamoja uitwao “Voice of Kibera” mwaka 2011, kabla ya nyota ya Octopizzo kung’aa na kupelekea tofauti za kimawazo na kimaisha.

Read More
 Octopizzo Awataka Wakenya Wapunguze Hasira kwa George Ruto

Octopizzo Awataka Wakenya Wapunguze Hasira kwa George Ruto

Msanii maarufu wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Octopizzo, amewataka Wakenya wapunguze hasira zao dhidi ya George Ruto, mwanawe Rais William Ruto, kufuatia uzinduzi wa matatu maarufu inayofahamika kama Nganya mwishoni mwa wiki hii. Kupitia mitandao ya kijamii, Octopizzo amewakosoa Wakenya wanaomshambulia George kutokana na hali ya kiuchumi inayokumba taifa, akisisitiza kuwa “dhambi za mzee si za mtoi.” akimaanisha kuwa makosa au historia ya mzazi haifai kuhamishiwa kwa watoto wao. “Dhambi za mzee si za mtoi,” aliandika msanii huyo, akisisitiza kuwa George ana haki ya kuishi maisha anayopenda bila kulaumiwa kwa sababu ya hadhi ya baba yake Octopizzo pia ameelezea kuwa ni jambo la kawaida kwa mtoto wa bilionea kuishi maisha ya kifahari, akionekana kushangazwa na jinsi baadhi ya Wakenya wanavyomshinikiza George kutafuta kazi ilhali baba yake ana uwezo mkubwa wa kifedha.  “Babake ni billionaire alafu mnataka George afanye kazi gani? Aanze kuuza mandazi?” aliandika kwa kejeli, akilenga kuonyesha kuwa ni kawaida kwa watoto wa viongozi matajiri kuwa na maisha ya kifahari. Uzinduzi wa Nganya ya George Ruto ulifanyika kwa mbwembwe kubwa jijini Nairobi, huku baadhi ya Wakenya wakilalamikia matumizi ya kifahari wakati taifa linapitia changamoto za kiuchumi.

Read More
 Siasa si Majina, ni Maendeleo – Ujumbe wa Octopizzo kwa Wakenya

Siasa si Majina, ni Maendeleo – Ujumbe wa Octopizzo kwa Wakenya

Msanii maarufu wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Octopizzo, ameibua mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii baada ya kuchapisha ujumbe mzito katika mtandao wa X (zamani Twitter), akiwataka Wakenya wawe makini na hali ya kisiasa nchini. Kupitia ujumbe huo, Octopizzo amewataka raia kukataa kile alichokiita usahaulifu wa kisiasa, akieleza kuwa upinzani unaojitokeza hivi sasa si mpya kwa kweli, bali unaundwa na viongozi waliowahi kushika nyadhifa serikalini kwa muda mrefu bila kuleta maendeleo ya maana kwa taifa. “Wakenya hawapaswi kusahau historia ya kisiasa. Huu unaoitwa upinzani mpya ni mkusanyiko wa viongozi waliokataliwa, au waliodumu serikalini kwa zaidi ya miaka ishirini bila kuwa na mafanikio yoyote ya kushikika. Wanaonekana kutamani madaraka, si mageuzi ya kweli,” ameandika msanii huyo. Octopizzo ameendelea kwa kutoa wito kwa wananchi kuwa waangalifu na kutanguliza maendeleo ya taifa badala ya kushabikia watu binafsi au vyama. “Tuwe waangalifu na tujitolee kwa maendeleo, si kwa kushabikia watu au majina. Kama taifa, tunastahili uongozi unaowajali wananchi si wakati wa uchaguzi pekee, bali kila siku.” Ameongeza kwa msisitizo. Ujumbe huu umepokelewa kwa hisia tofauti mitandaoni, baadhi ya wananchi wakimsifu kwa kutoa kauli yenye busara na ujasiri,huku wengine wakitumia fursa hiyo kujiuliza maswali kuhusu mwelekeo wa kisiasa nchini. Hii si mara ya kwanza kwa Octopizzo kutoa maoni kuhusu masuala ya kijamii na kisiasa, kwani amekuwa akitumia majukwaa yake ya mitandao ya kijamii kuhamasisha umma kuhusu haki, uwajibikaji, na maendeleo ya vijana nchini.

Read More
 Octopizzo awaasa wasanii wakubwa Afrika Mashariki kuwasaidia watu wenye uhitaji kwenye jamii

Octopizzo awaasa wasanii wakubwa Afrika Mashariki kuwasaidia watu wenye uhitaji kwenye jamii

Rapa Octopizzo amewahimiza wasanii wakubwa Afrika Mashariki kuhakikisha wanaisaidia jamii kwa kuwawezesha watu wenye uhitaji. Akizungumza katika mahojiano na Wasafi, Octo ameeleza kuwa hapendi kila kitu kuhusu msanii Diamond ila anafarajika na namna ambavyo ametengeneza fursa za ajira kwa vijana. Octopizzo pia amewatolea uvivu wasanii ambao hutumia kiki kutangaza muziki wao kwa kusema kwamba wana njaa ya maskini. Rapa huyo amewataka wasanii nchini Kenya kuzingatia suala la kutayarisha muziki mzuri badala ya kiki ambazo hazina msingi wowote. Hata hivyo amesema kwamba haihitaji kuimba Kiingereza ili utoboe kimataifa, kwani kuna ngoma nyingi sana zimekuwa kubwa dunia nzima na hazijaimbwa kwa Kiingereza.

Read More
 Rapa kutoka Kenya Octopizzo aachia rasmi album yake mpya

Rapa kutoka Kenya Octopizzo aachia rasmi album yake mpya

Rapa kutoka nchini Kenya Octopizzo ameachia rasmi album yake mpya inayokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki zake. Album hiyo inayokwenda kwa jina la Lamu Nights  ina jumla ya ngoma 10 za moto ambazo amewashirikisha wakali kama Wendy Kay, Jivu, Tito Wagithomo, Coaster Ojwang, Okella Max na Burklyn Boyz. Album hiyo ina nyimbo kama No Signal, Bad Vibes, Want It, Vacation, Moaning, Achupa na na inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mtandao wa Youtube. Lamu Nights ni Album ya saba kwa mtu mzima Octipozzo, baada ya Fuego iliyotoka mwaka wa 2021 ikiwa na jumla ya mikwaju 12 ya moto.

Read More
 OCTOPIZZO AMTAKA RUTO AHALALISHE BANGI

OCTOPIZZO AMTAKA RUTO AHALALISHE BANGI

Msanii wa Hip Hop nchini Kenya, Octopizzo amemtaka Rais mteule William Ruto kuihalalisha bangi pindi tu atakapokula kiapo cha kuingia ofisini kama Rais wa tano wa Kenya. Katika video ambayo imesambazwa mitandaoni, Octopizzo anamuelezea Ruto kwamba hata kama ataona kuhalalisha bangi ni jambo gumu basi aifanye isiwe kama ni hatia kwa mtu anayepatikana naye bali liwe tu ni jambo la kawaida. “Najua wewe ni mkristo na kwa hiyo hili gumzo huenda litakuwa gumu kidogo kwako lakini unajua bangi ni moja ya dawa ambazo ni takatifu zaidi duniani. Na amabcho nakuomba hata si kuhalalisha matumizi yake bali ni kuiweka bangi isiwe kama hatia kwa mtu anayepatikana nayo,” alisema Octopizzo. “Juzi nilikuona ulikutana na seneta wa Delaware, huko mtu anaruhusiwa kutembea na bangi gramu 3 kwa kujivinjari tu ilmradi mtu ako na miaka 21. Hii ni biashara ya mabilioni na tunajua kuna watu serikalini wenye wanafanya biashara hiyo,” Staa huyo alisema.

Read More
 OCTOPIZZO AWEKA WAZI VIGEZO VYA KUFANYA NAYE KOLABO

OCTOPIZZO AWEKA WAZI VIGEZO VYA KUFANYA NAYE KOLABO

Rapa Octopizzo  amefunguka kuhusiana na swala la yeye kutofanya kolabo na wasanii wenzake hususani wa nje. Kupitia Mambo Mseto ya Radio Citizen Octopizzo amesema hatokuja kufanya kolabo na mtu ambaye ana faida kwake kwa kuwa anafanya muziki kama biashara. Haikushia hapo ameenda mbali zaidi na kusema kwamba ikitokea amefanya kolabo na msanii yeyote ni lazima awe na Master Recording za muziki wake kwani hapendi suala la kufaidisha lebo za muziki. Mbali na hayo ameonyosha maelezo kuhusu kufanya wimbo wa pamoja na Khaligraph Jones kwa kusema watafanya kazi na rapa huyo muda sahihi ukifika kwa kuwa hawana ugomvi kama walimwengu wanavyodai mtandaoni.

Read More