OCTOPIZZO AKIRI KUCHOSHWA NA WANAOMKOSOA MTANDAONI

OCTOPIZZO AKIRI KUCHOSHWA NA WANAOMKOSOA MTANDAONI

Rapa Octopizzo amefunguka sababu za kutowajibu wanaomkosoa kwenye mitandao ya kijamii tofauti na ilivyokuwa awali. Akipiga stori na presenter Ali Octopizzo amesema aliamua kuweka kando kila kitu kwa ajili ya afya yake ya akili lakini pia kujihusisha na mambo ambayo yataamuingizia hela kwani alikuja kugundua kuwa alikuwa anapoteza muda wake mwingi kupishana na watu wasiokuwa na malengo maishani. Octopizzo ambaye anafanya vizuri na ngoma mpya “Tom Mboya” amesema kwamba anapenda sana watu wanapomkosoa mtandaoni kwa kuwa inampa changamoto ya kurekebisha baadhi ya vitu ambavyo haviendi sawa kwenye muziki wake. Utakumbuka Octopizzo amekuwa kwenye tour yake tangu mwezi Machi Mwaka huu ambapo amekuwa akihubiri amani na kuwahamasisha vijana wajitokeze kwa wingi kuwachagua viongozi watakaowafaa kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu.

Read More
 TECNO YAMTAMBULISHA OCTOPIZZO KAMA BALOZI WA SIMU ZAO ZA SPARK 9 SERIES

TECNO YAMTAMBULISHA OCTOPIZZO KAMA BALOZI WA SIMU ZAO ZA SPARK 9 SERIES

Rapa Octopizzo ametangazwa kuwa balozi wa simu mpya ya Mkononi kutoka kampuni ya Tecno Kenya inayokwenda  kwa jina la Tecno Spark 9 Series itakayouzwa katika maduka yote ya simu nchini. Akizungumza na waandishi habari leo jijini Nairobi, Mkurugenzi wa Techno, Peter Shi amesema kuwa wanatarajia  jamii itafaidika kwa kupata elimu kuhusu bidhaa za kampuni hiyo kupitia kwa balozi Octopizzo kwani wameamua kuileta simu ya Techno Spark 9 series  ili waweze kuwasaidia wananchi wa hali ya chini kumiliki simu janja . Kwa upande wake Rapa Octopizzo ameishukuru kampuni Techno kwa kumwamini na kutambua kuwa ana vigezo stahili kuwa balozi wao na kuahidi kuwa hatowaangusha katika kuitangaza kampuni hiyo sambamba na bidhaa zake zinazozalishwa na kampuni hiyo ambayo utengeneza simu, Kompyuta na vifaa vingine vya teknolojia Octopizzo sasa atatakiwa kutangaza bidhaa za Techno Spark 9 Series kwa mashabiki zake kupitia mitandao yake ya kijamii kwa lengo la kuiongezea kampuni hiyo mauzo.

Read More
 OCTOPIZZO ADOKEZO UJIO WA KOLABO NA NYASHINSKI, ZIARA YAKE YA KIMUZI PAMOJA NA ALBUM MPYA

OCTOPIZZO ADOKEZO UJIO WA KOLABO NA NYASHINSKI, ZIARA YAKE YA KIMUZI PAMOJA NA ALBUM MPYA

Mkali wa muziki wa Hiphop nchini Octopizzo ametangaza ujio wa wimbo wake mpya aliyomshirikisha na lejendari wa muziki Nyashinski Octopizzo amethibitisha taarifa hiyo njema kwa mashabiki zake Kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kushare picha akiwa na  Nyashinski  ambapo  amewataka mashabiki wakae mkao wa kula kupokea collabo yao ambayo kwa mujibu wake itakuwa moto wa kuotea mbali. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Motivation” hajeweka wazi ni lini hasa ngoma hiyo itaingia sokoni ila itakuwa wimbo wake wa kwanza kufanya na  Nyashinski tangu aanze safari yake ya muziki. Mbali na hayo, Octopizzo ametangaza kuja na ziara ya kimuziki iitwayo live music tour samba na kuachia album mpya ambayo hajataja Siku Rasmi ya kuachia Album hiyo lakini ameweka baadhi ya picha zikimuonesha akiwa kwenye maandalizi ya Album yake Mpya. Hii  inaenda kuwa Album ya 7 kwa mtu mzima Octopizzo, baada ya  Fuego”  iliyotoka mwaka wa 2021 ikiwa na jumla ya mikwaju 12 ya moto.

Read More