Oga Obinna Awashauri Mabinti Wadogo Wajiepushe na Mimba Kabla ya Miaka 26

Oga Obinna Awashauri Mabinti Wadogo Wajiepushe na Mimba Kabla ya Miaka 26

Mtangazaji na mchekeshaji maarufu kutoka Kenya, Oga Obinna, ametoa ushauri kwa mabinti wadogo kuzingatia maisha yao binafsi na kujiepusha na kupata mimba kabla ya kufikisha umri wa miaka 26. Kupitia ujumbe wake alioutoa kwenye mitandao ya kijamii, Obinna alisisitiza kuwa umri wa kati ya miaka 20 hadi 26 ni kipindi muhimu sana kwa wanawake kujijenga kifedha, kielimu na kimaendeleo, badala ya kuharakisha kuanzisha familia au kuhamia kwa wanaume. “Huo ndio muda wenu wa ku-focus. Wakati wenu wa kujitengenezea maisha, siyo wa kulea watoto au kuhamia kwa wanaume,” alisema Obinna. Obinna aliongeza kuwa wanawake wengi hujikuta wakijutia maamuzi ya mapema ya kuanzisha familia bila kuwa tayari kiakili na kifedha, jambo ambalo humzuia mwanamke kufikia malengo yake ya maisha. Kauli yake imezua mijadala mitandaoni, huku baadhi wakiiunga mkono kama ujumbe wa kuhamasisha mabinti kupanga maisha yao kwa busara, ilhali wengine wakitafsiri kama mtazamo unaopuuza hali halisi ya maisha ya baadhi ya wanawake. Oga Obinna amekuwa akijulikana kwa maoni yake yenye utata lakini pia yenye lengo la kuamsha fikra, hususan kwa vijana wanaofuatilia mitindo ya maisha, mahusiano na maendeleo binafsi.

Read More
 Mwanamume wa Tanzania Aliyedai Kurogwa kwa Kuiba Mbuzi Akiri Kuigiza Tukio Lote

Mwanamume wa Tanzania Aliyedai Kurogwa kwa Kuiba Mbuzi Akiri Kuigiza Tukio Lote

Mwanamume mmoja kutoka Tanzania ambaye hivi majuzi alivuma mitandaoni kwa kudai kuwa alirogwa na kuanza kutoa sauti za wanyama baada ya kuiba mbuzi, sasa amefichua kuwa tukio hilo lote lilikuwa la kuigiza. Akizungumza katika mahojiano maalum na mtangazaji maarufu wa Kenya, Oga Obinna, mwanamume huyo alikiri kuwa alidanganya polisi na kuigiza sauti za mbuzi na mbwa kwa makusudi ili apate huruma na msaada wa nauli ya kuja Nairobi. Katika video iliyosambaa sana mtandaoni, mwanamume huyo alionekana akitoa sauti kama za mbuzi na mbwa, hali iliyozua mjadala mkubwa huku baadhi ya watu wakiamini kuwa alikuwa ameathiriwa na uchawi baada ya kuiba mbuzi. Hata hivyo, katika mahojiano hayo, alifichua kuwa hakurogwa na wala hakuhusishwa na wizi wa mifugo. Aliongeza kuwa kupitia huruma ya watu, alipata fedha za kutosha kumsafirisha hadi jijini Nairobi. “Niliamua kuigiza ili nipate msaada. Nilijua watu wangenihurumia wakifikiri nimerogwa,” alisema. Kauli yake imezua hisia mseto mitandaoni, baadhi wakimsifu kwa ujasiri wa kusema ukweli huku wengine wakimlaumu kwa kudanganya umma. Wengine wanahisi kuwa kitendo chake kinapotosha na kudhalilisha watu wanaopitia matatizo halisi ya afya ya akili au mateso ya kweli. Hadi sasa, mamlaka kutoka Tanzania na Kenya bado hazijatoa taarifa rasmi kuhusu tukio hilo na kukiri kwake.

Read More
 Stpd Boy Aomba Msamaha kwa Oga Obinna, Ataka Kurudi Rehab

Stpd Boy Aomba Msamaha kwa Oga Obinna, Ataka Kurudi Rehab

Rapper maarufu Stpd Boy ameibuka hadharani kuomba msamaha kwa mchekeshaji Oga Obinna, siku chache baada ya mvutano kati yao uliotikisa mitandao ya kijamii. Kupitia Instagram, Stpd Boy alionekana mwenye majuto makubwa huku akikiri kwamba amerejea kwenye ulevi na maisha yasiyo na mwelekeo. Katika ujumbe wake, aliomba arudishwe kwenye kituo cha rehab ili aweze kuendelea na safari ya kupona na kurekebisha maisha yake. “Nimeanguka tena kwenye mtego wa pombe. Nimekosea. Naomba Obinna anisamehe na anisaidie nirudi rehab. Sitaki kurudi kule nilikotoka,” alisema kwa hisia. Kauli hii imekuja baada ya msanii huyo hapo awali kumkashifu Oga Obinna, akidai kwamba alimtumia kwa ajili ya umaarufu wakati alipompeleka rehab kwa mara ya kwanza. Madai hayo yalizua mjadala mkali mtandaoni, huku baadhi ya watu wakimtuhumu Stpd Boy kwa kutoonyesha shukrani. Hata hivyo, kupitia video hii mpya, Stpd Boy ameonyesha kubadilika na kutambua mchango wa Obinna katika maisha yake, akisisitiza kuwa hana budi kuomba msaada tena ili aweze kujinasua kutoka kwenye mtego wa uraibu. Mpaka sasa, Oga Obinna bado hajatoa tamko lolote rasmi kuhusu msamaha huo wala ombi la kurejeshwa rehab.

Read More
 Dufla Diligon Amlalamikia Mulamwah kwa Kumblock Instagram

Dufla Diligon Amlalamikia Mulamwah kwa Kumblock Instagram

Msanii wa muziki wa Kenya, Dufla Diligon, amezua mjadala mtandaoni baada ya kufichua kuwa amefungiwa (blocked) na mchekeshaji maarufu Mulamwah kwenye mtandao wa Instagram. Kupitia Instastory yake, Dufla alisimulia tukio hilo kwa mshangao na utani, akisema kuwa aligundua amefungiwa wakati alipokuwa akitafuta akaunti ya Mulamwah akiwa katika mazungumzo na msanii Lyanii.  “Jana tulikuwa na mazungumzo na @officialiyanii, halafu nikaamua kutafuta akaunti ya Mulamwah kwenye IG. Nilishangaa kuona nimefungiwa. Kumbe mimi na Obinna tuko kwa listi moja!” aliandika Dufla. Katika ujumbe wake, Dufla hakusita kuonyesha mshangao wake na hata kumtaka Mulamwah “kupunguza hisia”, akionekana kutofahamu chanzo cha hatua hiyo ya mchekeshaji huyo.  “Punguza feelings buda!!!” aliongeza, kwa mtindo wa utani lakini uliobeba ujumbe mzito. Hadi sasa, Mulamwah hajatoa majibu yoyote hadharani kuhusu hatua hiyo, wala kueleza sababu ya kuwazima Dufla na Obinna kwenye ukurasa wake wa Instagram. Hata hivyo, mashabiki wa pande zote wameendelea kutoa maoni tofauti, wengine wakisisitiza haja ya kuwepo kwa mawasiliano ya moja kwa moja kati ya wahusika badala ya kupeana block mitandaoni.

Read More
 Oga Obinna Aahidi Kumsaidia Stoopid Boy Kurudi Shuleni na Kujenga Maisha Yake Upya

Oga Obinna Aahidi Kumsaidia Stoopid Boy Kurudi Shuleni na Kujenga Maisha Yake Upya

Mtangazaji na mchekeshaji maarufu nchini Kenya, Oga Obinna, ameonyesha moyo wa kipekee wa utu na msaada kwa msanii Stoopid Boy kwa kuahidi kumsimamia katika safari yake mpya ya maisha baada ya kutoka kwenye kituo cha urekebishaji tabia (rehab). Kupitia ujumbe alioutoa hadharani, Obinna alisema kuwa ameweka nia ya kumrudisha Stoopid Boy shuleni, kumsaidia kujiunga na mazoezi ya gym, na kuhakikisha anapata msaada anaohitaji kupona kikamilifu na kujijenga upya kimaisha. “Huu si mwisho wa safari yake, bali ni mwanzo mpya. Nitahakikisha anarudi shuleni, anaingia gym, na anapata mwongozo wa kujijenga tena,” alisema Obinna kwa msisitizo, akionyesha dhamira ya dhati ya kusaidia kijana huyo kurejea kwenye njia sahihi. Stoopid Boy, ambaye amewahi kuwa maarufu kwa mitindo ya kipekee ya uimbaji na burudani mtandaoni, alikumbwa na changamoto za uraibu zilizomlazimu kuingia kwenye rehab. Hatua ya Obinna kumsaidia imetajwa na wengi kuwa mfano bora wa jamii kuunga mkono vijana walioanguka ili waweze kuinuka tena. Mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii wamepongeza uamuzi wa Obinna, wakimtaja kuwa kiongozi wa kipekee ambaye anatumia jukwaa lake kusaidia badala ya kuhukumu. Wengine wamesisitiza kuwa msaada wa aina hii ni muhimu hasa kwa wasanii chipukizi wanaopitia changamoto za maisha. Kwa sasa, macho ya wengi yako kwa Stoopid Boy kuona jinsi atakavyochukua nafasi hii mpya kuandika ukurasa mpya wa maisha yake, chini ya uangalizi na usaidizi wa Oga Obinna.

Read More
 MCHEKESHAJI OGA OBINNA AZUA GUMZO MTANDAONI

MCHEKESHAJI OGA OBINNA AZUA GUMZO MTANDAONI

Mchekeshaji kutoka nchini Kenya Oga Obinna amezua gumzo mtandaoni mara baada ya kutoa kauli kuwa wanawake waliochora tattoo na kutoboa miili yao kwa kuweka vipini kwenye pua sio wife material. Kauli hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa Wakenya kwenye mitandao ya kijamii huku wengi wakisema kuwa hayupo sahihi ikizingatiwa kuwa kila mwanamke ana haki ya kuolewa kwani tattoo na vipini ni urembo tu wa nje na sio tabia. Moja ya wadau kutoka Twitter anasema “yote inategemea kile unachotaka. ukimpenda kwa kutoboa na tattoo zake basi utamuoa. wakati mwingine huhitaji kuangalia mambo kama hayo,mwanamke anaweza kuwa na tattoo na akawa mama bora kwa watoto na familia yake”.

Read More