Fik Fameica: Pallaso Ni Shabiki Tu, Si Mlezi Wangu Kimuziki

Fik Fameica: Pallaso Ni Shabiki Tu, Si Mlezi Wangu Kimuziki

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Fik Fameica amevunja ukimya na kukanusha vikali madai ya msanii mwenzake Pallaso, ambaye kwa muda mrefu amekuwa akidai kuwa alihusika pakubwa katika kukuza safari yake ya muziki. Hii ni baada ya Pallaso kudai kuwa alimtoa Fik Fameica kwenye mitaa ya Kawempe, na kumtambulisha kwenye muziki, na hata kumsaidia kifedha alipokuwa anaanza safari yake ya muziki. Hata hivyo, Fik Fameica kwenye mahojiano yake hivi karibuni ameyakana madai hayo akisema kwamba Pallaso hajawahi kutoa mchango wowote wa maana katika mafanikio yake. Alieleza kuwa Pallaso alikuwa tu shabiki kama walivyo mashabiki wake wengine. “Pallaso aliwadanganya. Hajawahi changia chochote katika safari yangu ya muziki. Alikuwa tu shabiki wangu, si zaidi ya hapo,” alisema Fameica katika mahojiano na runinga moja nchini Uganda. Fameica alisisitiza kuwa yeye ni msanii aliyejijenga mwenyewe (self-made), na kwamba mafanikio yake yalianza mara ya kwanza tu alipoingia studio. “Mimi ni msanii aliyejijenga. Mara ya kwanza niliingia studio, nilitoa kibao ‘Pistol’ ambacho kilipokelewa vizuri,” aliongeza. Fik Fameica alipata umaarufu mkubwa mwaka 2018 kupitia wimbo wake maarufu “Kutama”, na tangu wakati huo amekuwa akitoa nyimbo kali mfululizo na kumuweka katika nafasi ya juu kama mmoja wa wasanii bora zaidi katika tasnia ya muziki Afrika Mashariki.

Read More
 Pallaso Hatimaye Awapatanisha Green Daddy, Spice Diana na Manager Roger

Pallaso Hatimaye Awapatanisha Green Daddy, Spice Diana na Manager Roger

Katika tukio lililosubiriwa kwa muda mrefu kwenye tasnia ya muziki wa Uganda, msanii maarufu Pallaso ameongoza juhudi za upatanisho kati ya wasanii Green Daddy, Spice Diana, na Manager Roger, kufuatia uhasama uliochukua zaidi ya miaka miwili. Green Daddy amekuwa akimkosoa hadharani Spice Diana na meneja wake, Roger, mara kwa mara akiwaita wasio na maadili na hata kuwahusisha na ushetani. Madai haya yaliibua maswali mengi miongoni mwa mashabiki na wanamuziki wenzake, huku Spice Diana mara kadhaa akisema hajui chanzo cha chuki hiyo. Hata hivyo, hali hiyo sasa inaelekea kuwa historia, baada ya Pallaso kuingilia kati kwa nia ya kurejesha amani. Green Daddy juzi alikutana na Pallaso katika studio za Spice Diana, ambapo walikaa pamoja na kuzungumza kwa kina kuhusu tofauti zao. Katika mazungumzo hayo, Green Daddy alifunguka na kueleza chanzo cha malalamiko yake, akisema kuwa Manager Roger aliwahi kumtendea jambo baya sana, kiasi cha kuhatarisha maisha yake. Ingawa hakufafanua kwa undani, Green Daddy alionyesha kuwa yuko tayari kuweka tofauti zao kando. Kwa upande wake, Spice Diana aliahidi kuandaa kikao maalum kati ya Green Daddy na meneja wake ili waweze kuketi pamoja na kumaliza tofauti hizo moja kwa moja. Mpango huo ulipokelewa kwa mikono miwili na Green Daddy, aliyeonekana kutaka amani irejee. Upatanisho huu umepokelewa vyema na mashabiki pamoja na wadau wa muziki, ambao wamekuwa wakitaka kuona umoja na mshikamano miongoni mwa wanamuziki wa Uganda. Wengi wanaamini kuwa hatua hii inaweza kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na hata kazi za pamoja kati ya wasanii hao. Kwa sasa, macho yote yako kwa kikao cha mwisho kati ya Green Daddy na Manager Roger, ambapo wengi wanatarajia suluhu ya kudumu na fursa mpya za kisanii.

Read More
 Pallaso Aweka Wazi Msimamo Wake Kuhusu Siasa

Pallaso Aweka Wazi Msimamo Wake Kuhusu Siasa

Msanii maarufu wa muziki nchini Uganda, Pius Mayanja almaarufu Pallaso, amesema kwa sasa hana mpango wa kujiingiza kwenye masuala ya siasa, akisisitiza kuwa bado anajikita kikamilifu katika taaluma yake ya muziki. Akizungumza katika mahojiano ya hivi karibuni, Pallaso alieleza kuwa hajatimiza malengo aliyojiwekea katika muziki, na hivyo anataka kuyakamilisha kabla ya kufikiria kuchukua jukumu lolote jipya katika maisha yake ya kitaaluma.  “Sihitaji kuingia kwenye siasa kwa sasa. Niko katika harakati za kutimiza ndoto yangu ya muziki, na nataka kuikamilisha kikamilifu kabla ya kufikiria jambo lolote jingine.” Ingawa hajajitosa rasmi katika siasa, Pallaso alisema anaendelea kutumia muziki wake kama chombo cha kuwasilisha ujumbe wa kijamii na kisiasa. Anaamini kuwa muziki ni jukwaa lenye nguvu kubwa la kufikisha ujumbe, na ndilo eneo analolielewa vyema. “Siasa ni wito. Binafsi bado sijaupata. Nikihisi moyoni kwamba ni wakati wa kuingia katika siasa, nitafanya hivyo. Lakini kwa sasa, ninaendelea kuwasilisha ujumbe wangu kupitia muziki.” Kauli ya Pallaso inajiri wakati ambapo baadhi ya wasanii nchini Uganda wameanza kujitosa katika siasa, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi. Miongoni mwao ni Big Eye na Nina Roz, ambao tayari wametangaza nia ya kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa. Ingawa Pallaso hana pingamizi kwa wasanii kuingia katika siasa, amesema ataingia katika ulingo huo pale tu atakapohisi kwa dhati kuwa ni wito wake wa kweli kulitumikia taifa. Kwa sasa, anabaki kuwa mmoja wa wasanii wanaotumia kazi zao kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Read More
 Chameleone adokeza mpango wa kubuni bendi ya muziki ya familia

Chameleone adokeza mpango wa kubuni bendi ya muziki ya familia

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amefichua mpango wa kuunda bendi ya familia itakayojumuisha ndugu zake, Pallaso na Weasel. Katika mahojiano hivi karibuni, Chameleone ameeleza kuwa watatu hao bado wapo kwenye mazungumzo kwa ajili ya kufikia makubaliano. Bendi hiyo huenda ikazinduliwa hivi karibuni katika hafla itakayofanyika jijini Kampala, katika uwanja wa Namboole. “Tunapanga kuanzisha bendi ya familia na tutatoa mweelekeo hivi karibuni. Uzinduzi huo unahitaji ukumbi mkubwa ambao hauko tayari kwa sasa. Tunataka eneo ambalo linaweza kuchukua zaidi ya watu 40, 000,” alisema. Jose Chameleone ameweka wazi hayo kwenye mkao na waandishi wa habari wakati akielezea mipango yake juu  tamasha lake “Gwanga Mujje” litakalofanyika huko Lugogo Cricket Oval mwezi Februari mwaka huu.

Read More
 Pallaso arejesha akaunti yake ya Facebook kutoka kwa wadukuzi

Pallaso arejesha akaunti yake ya Facebook kutoka kwa wadukuzi

Staa wa muziki kutoka Uganda Pallaso amefanikiwa kurejesha akaunti ya Facebook kutoka kwa wadukuzi. kupitia ukurasa wake wa Insagram Pallaso ameshindwa kuficha furaha yake kwa kuupongeza uongozi wake kwa kumsaidia kuirejesha chaneli yake ya youtube yenye subscribers laki saba. “Ni mwaka mmoja na nusu tangu nipoteze ukurasa wangu wa Facebook. Asante Mungu, imerudi,” inasomeka sehemu ya ujumbe ambayo Pallaso amechapisha kwenye Instastory yake. Kaunti hiyo hajakuwa hewani kwa kipindi cha miezi 18 baada ya kudukuliwa na watu wasiojulikana. Hata hivyo amewataka mashabiki kuwa makini na matapeli wanaoweza kutumia jina lake kuwalaghai.

Read More
 Pallaso anyosha maelezo kuhusu ugomvi wake na Ivien Karma.

Pallaso anyosha maelezo kuhusu ugomvi wake na Ivien Karma.

Mwanamuziki nyota nchini Uganda Pallaso amekiri kuwa hajutii kitendo cha kujiondoa kwenye uongozi wa Karma Ivien. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Pallaso amesema hatua hiyo ya kutengana na Karma haitaathiri shughuli zake za muziki siku za mbeleni kwani meneja huyo wa muziki alimtelekeza kipindi cha korona, jambo ambalo lilimfanya kugharamia muziki wake kama msamii wa kujitegemea. Hitmaker huyo wa “Malamu” amedai kuwa baada ya msala wa Korona kuisha, aliamua kuugura uongozi wa Karma Ivien na kuendelea kujisamamia kimuziki kutokana na kitendo chake cha kusitisha kufadhili baadhi ya kazi zake. Kauli ya Pallaso imekuja mara baada ya Ivien Karma kujinasibu kuwa yeye ndiye alimkingia kifua hadi akatusua kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda ambapo alienda mbali zaidi na kuhoji kuwa kuna kipindi Pallaso atakuja kujutia kuondoka kwenye usimamizi wake.

Read More
 PALLASO AMKANA KWEUPE IVAN KARMA

PALLASO AMKANA KWEUPE IVAN KARMA

Siku chache baada ya Ivan Karma kutishia kumfungulia mashtaka Pallaso kwa kuvunja mkataba wao wa miaka mitano ghafla, msanii huyo ameamua kutia neno juu ya  tuhuma za meneja huyo wa muziki kutoka Uganda. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni msanii huyo amesema hana muda wa kuzungumzia shtuma za ivan karma kwa kuwa anatumia jina lake kutafuta umaarufu mtandaoni. Pallaso alisaini na uongozi wa Ivan Karma  mwaka wa 2019 na tangu kipindi hicho ameachia nyimbo kali ambazo zimeacha alama kwenye tasnia ya muziki nchini uganda.

Read More
 PALLASO AKWEPA KESI YA KUVUNJA MKATABA NA MENEJA IVAN KARMA

PALLASO AKWEPA KESI YA KUVUNJA MKATABA NA MENEJA IVAN KARMA

Msanii Pallaso ameripotiwa kudinda kutii amri ya mahakama baaada ya meneja wake wa zamani Ivan Karma kumfungilia mashtaka kwa madai ya kukiuka mkataba wa miaka mitano wa kufanya kazi pamoja. Kulingana na wakili wa Ivan Karma, Pallaso amekuwa akikwepa kutia saini stakabadhi muhimu kwa kudai kuwa ameshikika na majukumu yake ya kikazi. Pallaso anaidaiwa kusaini mkataba unaompa Ivan Karma haki ya kuandaa shows na kutangaza kazi zake za muziki maeneo mbali mbali duniani. Jukumu la pallaso lilikuwa tu kuimba hadi pale alipoanza kufanya shows zake mwenyewe mara baada ya kutofautia kimawazo na Ivan Karma kutokana na masuala ya fedha. Mpaka sasa Pallaso ameandaa shows 90 bila uwepo wa Ivan Karma jambo ambalo limemfanya meneja wake huyo wa zamani kumtaka awajibikie shows hizo alizofanya bila idhini yake.

Read More
 PALLASO AKANUSHA KUTENGANA NA MENEJA WAKE IVIEN KARMA

PALLASO AKANUSHA KUTENGANA NA MENEJA WAKE IVIEN KARMA

Mwanamuziki Pallaso Mayanja amekanusha madai ya kutengana na meneja wake, Kama Ivien. Katika mahojiano, Pallaso amesema bado ana uhusiano mzuri wa kufanya kazi na Karma Ivien licha ya kutomtaja katika wimbo wake mpya “True Love”. Pallaso amesema alizidiwa na mzuka akiwa studio, hivyo akasahau kumpa shavu meneja wake. “Nitakapoacha kufanya naye kazi, nitaweka wazi kwenye kurasa zangu za mitandao ya kijamii. Bila tamko rasmi kutoka kwangu, usiamini uvumi huo,” Pallaso amebainisha. Ikumbukwe mapema wiki iliyopita ripoti zilidai kuwa wawili hao waliingia kwenye ugomvi kutokana na masuala yanayofungamana na pesa.

Read More
 PALLASO AGUSWA NA MASAIBU YA EDDY DEE, AMLIPIA KODI YA STUDIO

PALLASO AGUSWA NA MASAIBU YA EDDY DEE, AMLIPIA KODI YA STUDIO

Mwanamuziki kutoka Uganda Pallaso ameamua kuwa na moyo wa ukarimu kwa aliyekuwa prodyuza wake Eddy Dee. Msanii huyo ametoa shillingi millioni moja za Uganda kwa prodyuza huyo ili aweze kukamilisha deni la kodi analodaiwa la shillingi millioni 4. Eddy Dee ambaye amehusika pakubwa kutayarisha nyimbo za pallaso ameweka wazi taarifa hiyo kwa mashabiki zake kupitia mitandao yake ya kijamii ambapo amemwagia sifa mwimbaji huyo kwa kuwa na moyo wa kusaidia. Hata hivyo masaibu ya prodyuza huyo hajaisha kwa kuwa bado mwenye nyumba anasisitiza kwamba atamruhusu kwenye mjengo wake atapokamilisha pesi zote za kodi. Utakumbuka juzi kati prodyuza Eddy Dee alifungiwa studio yake baada ya kukosa kulipa kodi kwa takriban miezi 7 ambapo alienda mbali zaidi na kutoa wito kwa wasanii wote aliofanya nao kazi kipindi cha nyuma wamsaidie kulipa kodi.

Read More
 PALLASO AWEKA WAZI KIASI CHA FEDHA ANACHOTOZA KWENYE SHOO ZAKE

PALLASO AWEKA WAZI KIASI CHA FEDHA ANACHOTOZA KWENYE SHOO ZAKE

Msanii nyota kutoka Uganda Pallaso ameamua kutaja kiasi cha pesa anacholipisha kwenye show zake iwapo utahitaji kufanya nae kazi Katika mahojiano yake hivi karibuni Pallaso amesema analipisha kati ya shillingi millioni 15 hadi 20 za Uganda. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Malamu” amesema amechukua hatua hiyo kutokana na bidii anayoweka kila siku kwenye shughuli zake za muziki kwani amekuwa akiwekeza pesa nyingi kutoa muziki mzuri. Utakumbuka Pallaso katika siku za hivi karibuni amekuwa akipokea shows nyingi kutoka kwa mapromota lakini pia ni  moja kati ya wasanii ghali nchini Uganda wanaolipwa mkwanja mrefu kwenye maonesho ya muziki kutokana na muziki wake kupendwa na wengi.

Read More
 PALLASO ASITISHA TAMASHA LAKE KISA JERAHA LA GOTI

PALLASO ASITISHA TAMASHA LAKE KISA JERAHA LA GOTI

Msanii nyota kutoka Uganda Pallaso amelazimika kusitisha tamasha lake la muziki mara baada ya kuzidiwa na maumivu makali ya goti. Pallaso ambaye juzi kati alifanyiwa upasuaji wa goti anasema anahitaji muda wa kutosha kuuguza majeraha aliyoyapata kwenye moja ya performance yake wiki kadhaa zilizopita kabla ya kurejea rasmi kwenye majukwaa ya muziki. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Mpa Love” amesema kwa sasa ameanza mazungumzo na uongozi wake kwa ajili ya kuja na tarehe nyingine ambayo ataanza kufanya tamasha lake la muziki ambalo lilipaswa kufanyika Juni 1 na 2 mwaka huu. Hata hivyo Pallaso amesema hatoweza kuwapa mashabiki zake thamani ya pesa zao katika hali yake ya sasa ikizingatiwa kuwa amekuwa akitumbuiza kwenye shoo zake akiwa katika kiti cha magurudumu.

Read More