CAROL KATRUE AMKIA KIFUA MIRACLE BABY KWA KUKIMBIA UJA UZITO

CAROL KATRUE AMKIA KIFUA MIRACLE BABY KWA KUKIMBIA UJA UZITO

Msanii wa Mugithi Carol Katrue amemkingia kifua mume wake Peter Miracle Baby kwenye sakata la kumpa uja uzito mrembo aitwaye Tash Baby. Kwenye mahojiano na Mungai Eve Katrue amekataa ombi la Tash Baby kutaka mume wake kufanya vipimo vya DNA kuthibitisha kama alizaa nae mtoto kwa kusema kuwa uja uzito wa mrembo huyo sio wa Miracle Baby bali ni wa jamaa aitwaye Lorenzo. Katika hatua nyingine amekanusha tuhuma za Peter Miracle Baby kumtelekeza baba yake mzazi kwa kusema kuwa wazazi wa mume wake huyo wanaisha maisha mazuri, hivyo stori za mwanaume aliyejitokeza juzi kati mtandaoni na kudai ni baba mzazi wa Peter Miracle Baby hazina ukweli wowote. Carol Katrue amesema stori za Baba Mzazi wa msanii huyo kuishi maisha ya taabu zilitungwa na ukurasa mmoja wa udaku kwenye mtandao wa Facebook kwa lengo la kujitafutia umaarufu.

Read More
 BABA MZAZI WA PETER MIRACLE BABY ALIA KUPITIA MAISHA MAGUMU, AOMBA MSAADA WA KIFEDHA

BABA MZAZI WA PETER MIRACLE BABY ALIA KUPITIA MAISHA MAGUMU, AOMBA MSAADA WA KIFEDHA

Wakati msanii Peter Miracle Baby anaendelea kufanya vizuri kwenye muziki wa Mugithi, kumbe Baba yake mzazi hana makazi na anapitia maisha magumu sana mtaani. Kupitia video ambayo inasambaa mtandaoni Mzee David Ndolo maarufu Notorious, ameonekana mtaani akiomba msaada kwa kijana wake huyo ambaye hawana mahusiano mazuri. Mzee huyo amesema kuwa hafurahishwi kabisa na maisha anayoishi mtaani ambapo amemtaka Miracle Baby kuingilia kati na kumtoa kwenye maisha ya uchochole. “Niaje wathii, mi ndio baba Miracle Baby, anaitangwa Willy Mpole, nimemzalia hapa Mlango Mkubwa…Anaitangwa Miracle Baby Wilson … Mimi naitangwa David Ndolo … Mi ndio baba yake nimemzaa … siezi kubali hiyo maisha ju ni ya shida nay a kuteseka na kusononeka Zaidi,” alisema. Miracle Baby hata hivyo amejibu tuhuma hizo kwa kejeli kwa kuandika “Niseme Nini mimi willy mpole na msee mwingine asiniulize kuhusu babangu tena kwani coz sikujizaa mm na amjuae baba ya mtoto ni mama so io swali si yangu kujibu “

Read More
 PETER MIRACLE BABY AKANUSHA MADAI YA KUWA NA WANAWAKE WENGI

PETER MIRACLE BABY AKANUSHA MADAI YA KUWA NA WANAWAKE WENGI

Msanii wa Sailors Gang Peter Miracle Baby kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusu tuhuma zilizokuwa zikimuanda za kuwatelekeza wanawake aliozaa nao. Katika mahojiano na Mungai Eve, Miracle Baby amekanusha madai ya kuwa na wanawake wengi kwa kusema kwamba wanawake wote waliokuwa wanadai amepata nao watoto kwenye mitandao ya kijamii walikuwa wanatumia jina lake kujitafutia umaarufu mtandaoni. Katika hatua nyingine amewajibu walimwengu waliokuwa wanadai kuwa amekaliwa sana na mke wake Carol Katrue kwa kusema kwamba madai hayo hayana msingi wowote kwa kuwa ni mapenzi ya dhati aliyonayo kwa mke wake ndio yamewafanya watu kuanza kumzungumzia vibaya. Utakumbuka kipindi cha nyuma wanawake mbali mbali  walijitokeza mtandaoni wakidai kwamba wana ujazito wa Peter Miracle Baby jambo ambalo lilipelekea mke wake Carol Katrue kurushiana maneno makali na baadhi ya wanawake hao kama njia ya kumkingia kifua mume wake.

Read More