Rayvanny amtambulisha msanii mpya ndani ya lebo ya Next Level Music.

Rayvanny amtambulisha msanii mpya ndani ya lebo ya Next Level Music.

Mkurugenzi wa Lebo ya Next Level Music na msanii wa Bongofleva, Rayvanny, amemtambulisha msanii mpya atakayekuwa chini ya usimamizi wa lebo hiyo baada ya kutemana na msanii wake wa kwanza Mac Voice. Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Rayvanny ameposti video ikimwonyesha akiwa kwenye maandalizi ya picha (photoshoot) na msanii huyo mpya anayejulikana kwa jina la Kuss Love. Katika ujumbe wake, Chui amemkaribisha rasmi Kuss Love kwenye familia ya Next Level Music, hatua inayozua matumaini mapya kwa mashabiki wa lebo hiyo. Kutambulishwa kwa Kuss Love kunakuja wakati ambapo aliyekuwa msanii wa kwanza wa lebo hiyo, Mac Voice, kutemana na Rayvanny kwa madai ya kudhulumiwa kifedha licha ya juhudi zake na mikataba waliyosaini awali.

Read More
 Rayvanny afichua mkakati wa kukuza vipaji vipya kupitia lebo yake

Rayvanny afichua mkakati wa kukuza vipaji vipya kupitia lebo yake

Msanii na bosi wa lebo ya Next Level Music, Rayvanny, ametangaza rasmi mipango ya kumrudisha msanii wake Mac Voice ambaye kwa muda mrefu amekuwa kimya kimuziki. Kupitia maelezo yake, Rayvanny amesema maandalizi ya kurejea kwa Mac Voice yako katika hatua za mwisho, akiwataka mashabiki kukaa mkao wa kula kupokea kazi mpya kutoka kwa msanii huyo muda wowote kuanzia sasa. Mbali na mpango wa kumrudisha Mac Voice, Rayvanny pia amefichua kuwa Next Level Music ipo mbioni kumtambulisha msanii mpya. Hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa lebo hiyo kuendelea kukuza vipaji vipya, kupanua wigo wa muziki wake na kuimarisha nafasi yake katika soko la muziki Afrika Mashariki.

Read More
 Rayvanny Azima Vugu Vugu Linalodai Kususia Muziki wa Bongo Fleva kwa Show kali Kigoma

Rayvanny Azima Vugu Vugu Linalodai Kususia Muziki wa Bongo Fleva kwa Show kali Kigoma

Msanii wa Bongo Fleva Rayvanny amepiga show kali mjini Kigoma, kitendo kilichoonekana kuvunja kabisa wimbi la baadhi ya Watanzania waliodai kususia nyimbo na burudani za wasanii wa Bongo Fleva wanaodaiwa kujihusisha na masuala ya kisiasa. Kupitia mitandao ya kijamii, Rayvanny amewashukuru watu wa Kigoma hasa vijana wa Gen Z kwa upendo mkubwa waliomuonesha, akisema sapoti hiyo ndiyo nguvu yake kubwa katika safari ya muziki. Amesema mapokezi aliyopata Kigoma ni uthibitisho kuwa muziki wake unaendelea kupendwa na kuungwa mkono na Watanzania wengi, bila kujali mijadala inayozuka mitandaoni. Msanii huyo pia amejivunia mafanikio ya wimbo wake “Mama Tetema”, akibainisha kuwa hadi sasa hakuna msanii aliyefikia rekodi ya wimbo huo, uliotikisa Afrika Mashariki na kuvuka mipaka ya kimataifa. Kwa mujibu wa Rayvanny, mafanikio ya “Mama Tetema” bado yanabaki kuwa historia muhimu katika muziki wa Bongo Fleva. Rayvanny alikuwa miongoni mwa wasanii waliotoa burudani katika tamasha la Pilau Day, lililoandaliwa na Mbunge Baba Levo, ambapo maelfu ya wananchi walijitokeza kushuhudia burudani hiyo huku wakifurahia muziki na chakula.

Read More
 Rayvanny Awashukuru Gen Z kwa Sapoti Kubwa Tiktok

Rayvanny Awashukuru Gen Z kwa Sapoti Kubwa Tiktok

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Rayvanny, ameibuka kifua mbele akidai kuwa kwa sasa hakuna msanii anayemfikia, baada ya wimbo wake mpya “Toto” kufanikisha rekodi kubwa kwenye mtandao wa TikTok. Wimbo huo umefanikiwa kufikisha jumla ya posti milioni 1 TikTok, hatua iliyomfanya kuwa msanii pekee kutoka Tanzania aliyefikia rekodi hiyo kwa mwaka huu. Kupitia Instastory yake, Rayvanny hakusita kujitapa, akisisitiza kuwa hakuna msanii anayeweza kufikia idadi hiyo ya posti TikTok kwa mwaka 2025. Hitmaker huyo wa Mama Tetema, ameongeza kuwa mafanikio hayo ni ya kipekee zaidi kutokana na ukweli kuwa wimbo huo ulitoka nje ya kipindi cha kawaida cha kutoa nyimbo. Rayvanny pia amewashukuru mashabiki wake, hususan Gen Z, kwa sapoti kubwa waliyoonyesha tangu kuachiwa kwa wimbo huo.

Read More
 Rayvanny na Nora Fatehi Washukuru Mashabiki Baada ya Kushinda Tuzo ya Video Bora ya Mwaka

Rayvanny na Nora Fatehi Washukuru Mashabiki Baada ya Kushinda Tuzo ya Video Bora ya Mwaka

Msanii wa Bongo Fleva Rayvanny na nyota wa kimataifa Nora Fatehi wamewafikia mashabiki wao kwa ujumbe wa shukrani baada ya ushindi mkubwa kwenye EAEA Awards, ambako wimbo wao “Oh Mama Tetema” umeibuka mshindi wa Video Bora ya Mwaka. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rayvanny amepakia video ya Nora Fatehi akitoa shukurani kwa mashabiki wote waliounga mkono kazi hiyo. Katika video hiyo, Nora amewashukuru kwa upendo na sapoti waliyoonyesha tangu kutolewa kwa wimbo huo ambao umeendelea kufanya vizuri kimataifa. Mbali na ushindi wa “Oh Mama Tetema”, Nora Fatehi pia aliibuka kidedea kwa kutwaa tuzo ya Best Video kupitia wimbo wake “Snakes” aliomshirikisha staa wa Marekani, Jason Derulo. Tuzo hizo mbili zimeongeza uthibitisho wa nafasi yake kama mmoja wa wasanii wa kimataifa wanaoendelea kutamba kwa mafanikio makubwa kwenye muziki na video.

Read More
 Rayvanny Afichua Mpango wa Kufanya EP na Wasanii Chipukizi

Rayvanny Afichua Mpango wa Kufanya EP na Wasanii Chipukizi

Mwanamuziki nyota wa Tanzania, Rayvanny, ametangaza mpango mpya wa kuibua vipaji kwa kutengeneza EP maalum akiwashirikisha wasanii chipukizi kutoka mitaani. Kupitia mitandao ya kijamii, Rayvanny amesema lengo ni kuwapa nafasi vijana wenye uwezo mkubwa lakini wasio na majukwaa ya kujitangaza. Ameongeza kuwa safari yake ya mafanikio ilisaidiwa na watu waliomuamini, hivyo hana budi kuwarudishia fadhila kwa kuinua kizazi kipya cha wasanii. Msanii huyo wa ngoma ya Songi Songi, amewahimiza mashabiki kuendelea kupendekeza majina ya madogo wakali wanaowafahamu ili wapate nafasi ya kuonyesha uwezo wao kupitia mradi huo mpya wa muziki. Kauli yake imekuja mara baada ya mashabiki kupendekeza majina ya wasanii mbalimbali chipukizi alipotangaza nia ya kufanya kazi na kijana mmoja aliyeonyesha kipaji chake mwezi Juni mwaka huu kupitia mitandao ya kijamii

Read More
 Rayvanny Ajivunia Mafanikio ya Tamasha la Dubai

Rayvanny Ajivunia Mafanikio ya Tamasha la Dubai

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Rayvanny, ameendelea kuthibitisha umahiri wake baada ya kupiga show ya nguvu jijini Dubai, tukio lililohudhuriwa na maelfu ya mashabiki kutoka mataifa mbalimbali. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rayvanny ameonyesha furaha na kujivunia mafanikio hayo akisema kuwa mpaka sasa nchini Tanzania hakuna msanii mwenye onyesho kali kama alilolifanya juzi kati Dubai Rayvanny ameongeza kuwa ngoma yake “Mama Tetema”, aliyomshirikisha nyota wa kimataifa Nora Fatehi, ndiyo wimbo bora zaidi Tanzania kwa mwaka huu, na hakuna msanii mwingine aliyetoa wimbo uliofikia kiwango hicho cha umaarufu. Kauli hiyo imezua mjadala mtandaoni, baadhi ya mashabiki wakimtaja kama mmoja wa wasanii wachache wanaoendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania kimataifa. Wengine wamesema Rayvanny amepiga hatua kubwa tangu alipotoka kwenye lebo ya WCB inayomilikiwa na Diamond Platinumz.

Read More
 Rayvanny Atoa Onyo Kali Kwa Anaendesha Akaunti Feki Facebook kwa Jina Lake

Rayvanny Atoa Onyo Kali Kwa Anaendesha Akaunti Feki Facebook kwa Jina Lake

Msanii wa Bongo Fleva, Rayvanny, ametoa onyo kali kwa mtu anayejifanya yeye kwenye ukurasa wa Facebook ulioidhinishwa (verified), wenye wafuasi zaidi ya milioni 3.4, baada ya akaunti hiyo feki kutumia jina lake kuposti picha na video za matukio ya kusikitisha yanayoendelea nchini Tanzania. Kupitia instastory zake, Rayvanny alionekana mwenye hasira akimtahadharisha mtu huyo kuacha mara moja kutumia jina na taswira yake kwa njia za udanganyifu. Rayvanny amewataka mashabiki wake kuwa makini na kuripoti ukurasa huo kwa mamlaka husika za mtandao wa Facebook, akisisitiza kuwa yeye hana uhusiano wowote na maudhui hayo yanayosambazwa. Akaunti hiyo feki inadaiwa imekuwa ikichapisha maudhui yanayohusiana na matukio ya vifo, ikiwemo picha za miili ya watu waliopoteza maisha kwenye maandamano ya kupinga uchaguzi uliokamilika nchini Tanzania, jambo ambalo limezua taharuki miongoni mwa mashabiki na wafuasi wa msanii huyo.

Read More
 Rayvanny Afunguka Kuhusu Kusemwa Vibaya na Mbosso

Rayvanny Afunguka Kuhusu Kusemwa Vibaya na Mbosso

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Rayvanny, amefunguka kuhusu maumivu aliyopitia kutokana na kile alichokiita usaliti kutoka kwa msanii mwenzake Mbosso. Kwenye mahojiano na waadishi wa habari, Rayvanny amesema aliumizwa sana baada ya kusikia kuwa Mbosso alimsema vibaya kwa Diamond Platinumz wakati alipokuwa akiondoka kwenye lebo ya WCB Wasafi. Hitmaker huyo wa “Mama Tetema” amefafanua kuwa, licha ya tofauti zilizojitokeza, yeye ndiye aliyepigania Mbosso kusainiwa kwenye lebo hiyo. Lakini pia amekiri kwamba yeye ndiye aliyemuunganisha Baba Levo na Diamond, jambo lililomsaidia kupata nafasi ya ajira ndani ya WCB. Kwa mujibu wa Bosi huyo wa Next Level, jambo la kushangaza ni kwamba licha ya mchango wake mkubwa kwa wasanii hao wawili, wamekuwa wakimzungumzia vibaya badala ya kumshukuru.

Read More
 Rayvanny Aandika Historia Juba, South Sudan kwa Kujaza Uwanja wa Taifa

Rayvanny Aandika Historia Juba, South Sudan kwa Kujaza Uwanja wa Taifa

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Rayvanny, ameandika historia mpya katika tasnia ya burudani barani Afrika baada ya kufanikisha tamasha kubwa lililovunja rekodi kwa kuhudhuriwa na zaidi ya watu 50,000 katika Uwanja wa Taifa wa Juba, South Sudan. Hili ndilo tamasha la kwanza katika taifa hilo lenye kiingilio rasmi kufikia kiwango hicho cha mahudhurio. Kutokana na mafanikio hayo ya kipekee, Rayvanny alitunukiwa Tuzo Maalum ya Heshima (Sold Out Plaque) kutoka kwa uongozi wa Juba National Stadium kama ishara ya kuthamini mchango wake katika muziki na kuvuka mipaka ya burudani ya Afrika Mashariki hadi Kati. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Rayvanny alieleza shukrani kwa taifa hilo kwa mapokezi ya kipekee na mafanikio hayo ya kihistoria. “Thanks a lot beautiful country South Sudan. Big thanks to Juba National Stadium for the Sold Out Plaque. Big thanks to all fans for the love and support,” Aliandika kwa hisia. Rayvanny pia alibainisha kuwa hilo ndilo tamasha la kwanza nchini South Sudan lenye kiingilio ambalo limeweza kuvutia hadhira ya zaidi ya watu elfu hamsini. Tamasha hilo linaashiria hatua kubwa kwa Rayvanny, ambaye ameendelea kujizolea sifa kama msanii wa kimataifa mwenye uwezo wa kuvutia mashabiki kwa kiwango kikubwa. Aidha, tukio hilo limedhihirisha jinsi muziki wa Bongo Fleva unavyozidi kupanuka na kukubalika katika nchi mbalimbali za Afrika, ukiwaunganisha watu kupitia ujumbe na burudani ya hali ya juu. Kwa mafanikio haya, Rayvanny amejiweka katika nafasi ya juu miongoni mwa wasanii wanaobadilisha sura ya muziki wa Afrika, akivunja rekodi, kuandika historia, na kuendeleza utambulisho wa sanaa ya Afrika Mashariki kwenye jukwaa la kimataifa. South Sudan, kwa hakika, haitamsahau hivi karibuni.

Read More
 Rayvanny Kutumbuiza Uwanja wa Taifa Juba, South Sudan

Rayvanny Kutumbuiza Uwanja wa Taifa Juba, South Sudan

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Rayvanny, anatarajia kutikisa jiji la Juba, South Sudan kwa onyesho kubwa litakalofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Juba (Juba National Stadium). Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Rayvanny amethibitisha taarifa hiyo kwa maneno mazito yaliyojaa kujiamini, akieleza kuwa yeye si msanii wa kumbi ndogo bali wa viwanja vikubwa. “Not Arena, we do stadiums! #JUBANATIONALSTADIUM I #GLOBALWAY!!! #SouthSudan NIAMINI MIMI HAPA PATAKUA HAKUNA PA KUKANYAGA,” ameandika Rayvanny. Kauli hiyo imezua gumzo kubwa mitandaoni, huku mashabiki wake wakionyesha shauku ya kumuona akiangusha burudani ya nguvu mbele ya maelfu ya mashabiki wa South Sudan. Onyesho hilo linaelezwa kuwa sehemu ya safari yake ya kimataifa ya muziki, inayolenga kufikisha sauti ya Bongo Fleva mbali zaidi kimataifa. Rayvanny, ambaye pia ni mmiliki wa lebo ya Next Level Music, anaendelea kudhihirisha kuwa yeye ni miongoni mwa wasanii wa Afrika wanaopiga hatua kubwa katika anga za kimataifa.

Read More
 Wakazi Akosoa Mikataba Kandamizi kwa Wasanii Tanzania, Atumia Kisa cha Harmonize Kuonyesha Unyonyaji

Wakazi Akosoa Mikataba Kandamizi kwa Wasanii Tanzania, Atumia Kisa cha Harmonize Kuonyesha Unyonyaji

Msanii wa Hip Hop nchini Tanzania, Wakazi, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kukosoa vikali aina ya mikataba wanayopewa wasanii wachanga na baadhi ya lebo kubwa za muziki nchini humo. Kupitia chapisho lake kwenye mtandao wa Instagram, Wakazi alisema kuwa mikataba mingi inalenga kuwanufaisha wamiliki wa lebo huku wasanii wakibaki bila mamlaka ya kazi zao hata zile walizozifadhili kwa pesa zao wenyewe. Katika maelezo yake, Wakazi alimtaja msanii Harmonize, akifichua kuwa licha ya yeye kugharamia baadhi ya kazi zake binafsi wakati akiwa chini ya lebo ya Wasafi (WCB), bado alilazimika kulipa kiasi kikubwa cha fedha ili aweze kuchukua catalog ya nyimbo alizotoa akiwa na lebo hiyo.  “Kumbuka Harmonize alikuwa anagharamia baadhi ya kazi zake kutoka mfukoni, lakini Wasafi walitaka alipie hela ili achukue catalog yake (wakati wao hata hawaku-invest on),” aliandika Wakazi. Wakazi aliongeza kuwa hali kama hiyo si ya kipekee, bali ni changamoto ambayo imekuwa ikiwakumba wasanii wengi chipukizi nchini Tanzania. Alisema kuwa kwa kutokuelewa masuala ya kisheria, wengi wao husaini mikataba kwa pupa, hali inayowaacha wakinyonywa kwa muda mrefu bila njia rahisi ya kujinasua. Wakazi ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wasanii kuhakikisha wanapata ushauri wa kisheria kabla ya kuingia kwenye mikataba, ili kulinda kazi na haki zao. Pia amezitaka lebo za muziki kuwa na uwazi na kuweka mbele maslahi ya wasanii badala ya kutazama faida pekee. “Muziki ni biashara, lakini isiwe biashara ya kumnyonya msanii aliyetoa jasho lake. Tunahitaji mabadiliko ya kweli kwenye mfumo huu,” alisema. Kauli hiyo imeungwa mkono na baadhi ya mashabiki na wadau wa sanaa, huku wengine wakitaka kuanzishwe taasisi huru zitakazosaidia wasanii kusoma na kuelewa mikataba kabla ya kuisaini. Suala la mikataba kandamizi limekuwa likirudiwa mara kwa mara katika mijadala ya burudani nchini Tanzania. Wasanii kama Harmonize, Rayvanny, na wengine waliowahi kujitoa katika lebo kubwa wameelezea wazi namna walivyolazimika kulipa fedha nyingi ili kurejesha uhuru wa kazi zao.

Read More