Rayvanny Aandika Historia Juba, South Sudan kwa Kujaza Uwanja wa Taifa

Rayvanny Aandika Historia Juba, South Sudan kwa Kujaza Uwanja wa Taifa

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Rayvanny, ameandika historia mpya katika tasnia ya burudani barani Afrika baada ya kufanikisha tamasha kubwa lililovunja rekodi kwa kuhudhuriwa na zaidi ya watu 50,000 katika Uwanja wa Taifa wa Juba, South Sudan. Hili ndilo tamasha la kwanza katika taifa hilo lenye kiingilio rasmi kufikia kiwango hicho cha mahudhurio. Kutokana na mafanikio hayo ya kipekee, Rayvanny alitunukiwa Tuzo Maalum ya Heshima (Sold Out Plaque) kutoka kwa uongozi wa Juba National Stadium kama ishara ya kuthamini mchango wake katika muziki na kuvuka mipaka ya burudani ya Afrika Mashariki hadi Kati. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Rayvanny alieleza shukrani kwa taifa hilo kwa mapokezi ya kipekee na mafanikio hayo ya kihistoria. “Thanks a lot beautiful country South Sudan. Big thanks to Juba National Stadium for the Sold Out Plaque. Big thanks to all fans for the love and support,” Aliandika kwa hisia. Rayvanny pia alibainisha kuwa hilo ndilo tamasha la kwanza nchini South Sudan lenye kiingilio ambalo limeweza kuvutia hadhira ya zaidi ya watu elfu hamsini. Tamasha hilo linaashiria hatua kubwa kwa Rayvanny, ambaye ameendelea kujizolea sifa kama msanii wa kimataifa mwenye uwezo wa kuvutia mashabiki kwa kiwango kikubwa. Aidha, tukio hilo limedhihirisha jinsi muziki wa Bongo Fleva unavyozidi kupanuka na kukubalika katika nchi mbalimbali za Afrika, ukiwaunganisha watu kupitia ujumbe na burudani ya hali ya juu. Kwa mafanikio haya, Rayvanny amejiweka katika nafasi ya juu miongoni mwa wasanii wanaobadilisha sura ya muziki wa Afrika, akivunja rekodi, kuandika historia, na kuendeleza utambulisho wa sanaa ya Afrika Mashariki kwenye jukwaa la kimataifa. South Sudan, kwa hakika, haitamsahau hivi karibuni.

Read More
 Rayvanny Kutumbuiza Uwanja wa Taifa Juba, South Sudan

Rayvanny Kutumbuiza Uwanja wa Taifa Juba, South Sudan

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Rayvanny, anatarajia kutikisa jiji la Juba, South Sudan kwa onyesho kubwa litakalofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Juba (Juba National Stadium). Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Rayvanny amethibitisha taarifa hiyo kwa maneno mazito yaliyojaa kujiamini, akieleza kuwa yeye si msanii wa kumbi ndogo bali wa viwanja vikubwa. “Not Arena, we do stadiums! #JUBANATIONALSTADIUM I #GLOBALWAY!!! #SouthSudan NIAMINI MIMI HAPA PATAKUA HAKUNA PA KUKANYAGA,” ameandika Rayvanny. Kauli hiyo imezua gumzo kubwa mitandaoni, huku mashabiki wake wakionyesha shauku ya kumuona akiangusha burudani ya nguvu mbele ya maelfu ya mashabiki wa South Sudan. Onyesho hilo linaelezwa kuwa sehemu ya safari yake ya kimataifa ya muziki, inayolenga kufikisha sauti ya Bongo Fleva mbali zaidi kimataifa. Rayvanny, ambaye pia ni mmiliki wa lebo ya Next Level Music, anaendelea kudhihirisha kuwa yeye ni miongoni mwa wasanii wa Afrika wanaopiga hatua kubwa katika anga za kimataifa.

Read More
 Wakazi Akosoa Mikataba Kandamizi kwa Wasanii Tanzania, Atumia Kisa cha Harmonize Kuonyesha Unyonyaji

Wakazi Akosoa Mikataba Kandamizi kwa Wasanii Tanzania, Atumia Kisa cha Harmonize Kuonyesha Unyonyaji

Msanii wa Hip Hop nchini Tanzania, Wakazi, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kukosoa vikali aina ya mikataba wanayopewa wasanii wachanga na baadhi ya lebo kubwa za muziki nchini humo. Kupitia chapisho lake kwenye mtandao wa Instagram, Wakazi alisema kuwa mikataba mingi inalenga kuwanufaisha wamiliki wa lebo huku wasanii wakibaki bila mamlaka ya kazi zao hata zile walizozifadhili kwa pesa zao wenyewe. Katika maelezo yake, Wakazi alimtaja msanii Harmonize, akifichua kuwa licha ya yeye kugharamia baadhi ya kazi zake binafsi wakati akiwa chini ya lebo ya Wasafi (WCB), bado alilazimika kulipa kiasi kikubwa cha fedha ili aweze kuchukua catalog ya nyimbo alizotoa akiwa na lebo hiyo.  “Kumbuka Harmonize alikuwa anagharamia baadhi ya kazi zake kutoka mfukoni, lakini Wasafi walitaka alipie hela ili achukue catalog yake (wakati wao hata hawaku-invest on),” aliandika Wakazi. Wakazi aliongeza kuwa hali kama hiyo si ya kipekee, bali ni changamoto ambayo imekuwa ikiwakumba wasanii wengi chipukizi nchini Tanzania. Alisema kuwa kwa kutokuelewa masuala ya kisheria, wengi wao husaini mikataba kwa pupa, hali inayowaacha wakinyonywa kwa muda mrefu bila njia rahisi ya kujinasua. Wakazi ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wasanii kuhakikisha wanapata ushauri wa kisheria kabla ya kuingia kwenye mikataba, ili kulinda kazi na haki zao. Pia amezitaka lebo za muziki kuwa na uwazi na kuweka mbele maslahi ya wasanii badala ya kutazama faida pekee. “Muziki ni biashara, lakini isiwe biashara ya kumnyonya msanii aliyetoa jasho lake. Tunahitaji mabadiliko ya kweli kwenye mfumo huu,” alisema. Kauli hiyo imeungwa mkono na baadhi ya mashabiki na wadau wa sanaa, huku wengine wakitaka kuanzishwe taasisi huru zitakazosaidia wasanii kusoma na kuelewa mikataba kabla ya kuisaini. Suala la mikataba kandamizi limekuwa likirudiwa mara kwa mara katika mijadala ya burudani nchini Tanzania. Wasanii kama Harmonize, Rayvanny, na wengine waliowahi kujitoa katika lebo kubwa wameelezea wazi namna walivyolazimika kulipa fedha nyingi ili kurejesha uhuru wa kazi zao.

Read More
 Rayvanny mbioni kuachia Flowers III EP

Rayvanny mbioni kuachia Flowers III EP

Staa wa muziki wa BongoFleva Rayvanny ametangaza ujio wa EP yake mpya ambayo ana mpango wa kuachia hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bosi huyo wa Next Level Music amethibitisha taarifa hiyo kwa kusema kuwa mwaka huu 2023 ataachia EP ya ‘Flowers III’. ‘Flowers III’ itaifuata EP yake ya ‘Flowers II’ aliyoiachia Februari 10, mwaka 2022 iliyokuwa imebeba nyimbo tisa huku ikiwa na kolabo sita tuu za wasanii kama Marioo, Zuchu na wengine wengi. Kama wewe ni mmoja kati ya watu waliofurahia mtiririko wa EP za ‘Flowers’ kutoka kwa Rayvanny basi yaandae masikio yako kwa ajili ya muendelezo wa EP hizo.

Read More
 Rayvanny atajwa kuwania tuzo kubwa za Kilatini

Rayvanny atajwa kuwania tuzo kubwa za Kilatini

Boss wa lebo ya ‘Next Level Music’, msanii Rayvanny kufuatia ametajwa kwenye tuzo kubwa za Kilatini ziitwazo “Lo Nuestro Awards”. Waandaaji wa tuzo hizo kupitia kurasa zao za mitandao ya Kijamii Premiolonuestro wametangaza majina ya wasanii waliochaguliwa kuwania mwaka huu kupitia vipengele mbalimbali. Majina ya wanamuziki wakubwa Dunianii yamehusu sana akiwemo pia Mtanzania pekee Rayvanny akiiwakilisha vyema Afrika Mashariki kwa ujumla. Rayvanny amechaguliwa kuwania kwenye Kipengele cha Wimbo Bora wa Mwaka “Song of the Year (Urbun pop)” kupitia wimbo wake “Mother tremble” ambao ni Mama Tetema akiwa na Maluma. Tuzo hizo za 35 mwaka huu, zinatarajiwa kutolewa Februari 24 ndani ya Miami-Dade Arena, huko Miami, Florida nchini Marekani.

Read More
 Rayvanny na Otile Brown waingia studio kurekodi kolabo yao

Rayvanny na Otile Brown waingia studio kurekodi kolabo yao

Wanamuziki nyota wanaoiwakilisha vyema Afrika Mashariki, wasanii Rayvanny na Otile Brown wameingia studio na wameonekana kwenye upishi wa kazi mpya. Wawili hao wanatajwa kuingia studio usiku wa kuamkia leo katika studio za Next Level Music zilizopo Mbezi Beach jijini Dar es salaam, zilizo chini ya msanii Rayvanny. Hata hivyo, bado haijafamika kuwa hii itakuwa ni kazi ya nani, tarajia kuipata kazi hiyo kutoka kwa wawili hao siku za usoni.

Read More
 Harmonize na Rayvanny watupiana maneno makali mtandaoni

Harmonize na Rayvanny watupiana maneno makali mtandaoni

Msanii wa Bongofleva, Rayvanny ametapika nyongo kumuhusu Harmonize, ni vita ya maneno ambayo ilianzia kwenye insta story kufuatia Harmonize kuwataka wasanii kuacha kuimba nyimbo za kutukuza pombe kwani zinaharibu Jamii. Tamko hili lilimgusa Rayvanny ambaye aliibuka na kumjibu Harmonize kwamba, asiongee chochote kuhusu nyimbo za pombe kwani hajawahi kufanya nyimbo za aina hiyo na zikafanya vizuri. Rayvanny hakuishia hapo, ni kama alikuwa amekaa na kitu rohoni kwa muda mrefu sana kuhusu Harmonize. Kupitia insta story yake usiku wa kuamkia leo ameongea mengi ikiwemo kumchana Harmonize kuwa ana roho mbaya, mbinafsi kwa kutaka kumfunga Jela kufuatia lile sakata la mtoto wa Kajala, Paula. Mmiliki huyo wa Next Level Music, aliendelea kutema nyongo kwa kusema amemsaidia Harmonize kimuziki ikiwemo kumuandikia verse nzima kwenye wimbo wa “Paranawe” na “Happy Birthday” lakini pia alifunguka kwamba, ameilipa lebo ya WCB shillingi milioni 53 za Kenya lakini hakuwahi kufungua mdomo wake kuongea.

Read More
 Rayvanny adokeza ujio wa kolabo nyingine na Abigail Chams

Rayvanny adokeza ujio wa kolabo nyingine na Abigail Chams

Bosi wa Label ya Next Level Music (NLM), Msanii Rayvanny ameingia tena studio kufanya kazi na Abigail Chams ikiwa ni baada ya mwaka mmoja. Rayvanny aliwahi kumshirikisha Abigail Chams katika wimbo wake ‘Stay’ unaopatikana kwenye EP yake, New Chui iliyotoka Oktoba mwaka 2021. Hatua hiyo inakuja baada ya hivi karibuni Abigail Chams kufanya nyimbo mbili na Harmonize, ambazo ni Closer na Leave Me Alone. Kwa sasa Rayvanny anafanya vizuri na wimbo wake ‘Nitongoze’ akimshirikisha Diamond Platnumz ukiwa ni wimbo wa nane kufanya pamoja.

Read More
 Rayvanny adokeza mpango wa kuachia Chuchumaa REMIX

Rayvanny adokeza mpango wa kuachia Chuchumaa REMIX

Staa wa muziki kutoka nchini Tanzania Rayvanny ameonesha kushangazwa na ngoma yake iitwayo “Chuchumaa” iliyotoka miaka mitatu iliyopita kuwa bado inafanya vizuri sehemu mbalimbali dunini Kupitia ukurasa wake wa Twitter RayVanny amewahakikishia mashabiki wake kuachia toleo jipya la wimbo huo, huku akiwa bado anajiuliza msanii yupi atakuwa sahihi kumshirikisha. Itakumbukwa, wimbo wa Chuchumaa ulitoka rasmi Oktoba 5, mwaka 2019 Rayvanny akiwa chini ya uongozi wake wa awali, lebo ya ‘WCB’ na ulitayarishwa na producer Gachib

Read More
 Rayvanny aachia rasmi Unplugged Session EP

Rayvanny aachia rasmi Unplugged Session EP

Hatimaye msanii wa bongofleva Rayvanny amekata kiu ya mashabiki zake na Ep mpya inayokwenda kwa jina la Unplugged Session. Rayvanny ameamua kuwa surprise mashabiki zake kwa kuachia Extended Playlist hiyo mpya yenye jumla ya mikwaju 8 ya moto huku ikiwa na kolabo moja pekee kutoka msanii aitwaye Fari. Unplugged Session EP ina nyimbo kama Mama, Vacation, I Love You, Mwamba, Mtoto na nyingine nyingi. Hata hivyo Rayvanny kupitia mitandao yake ya kijamii amesema ameachia Unplugged Session EP kama zawadi ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka mpya. EP hiyo kwa sasa inapatikana exclusive kwenye Digital Platforms zote za kusambaza muziki duniani ikiwemo Boomplay.

Read More
 Rayvanny ashinda tuzo ya Diafa, Dubai

Rayvanny ashinda tuzo ya Diafa, Dubai

Mwimbaji wa Bongofleva toka Next Level Music (NLM), Rayvanny ameshinda tuzo za Diafa kutokea Dubai usiku wa kuamkia leo. Rayvanny anakuwa msanii wa kwanza kutoka ukanda wa Afrika Mashariki kupokea Tuzo hiyo ambayo hutolewa kuwaheshimisha watu mashuhuri mbali mbali toka falme za Kiarabu na hata Kimataifa kufuatia mafanikio na mchango wao kwa mwaka mzima katika Kusaidia na kuboresha Jamii. Tuzo za kwanza zilifanyika 2017. Kwenye Tuzo za mwaka huu ambazo zilitolewa Novemba 4, zilijumuisha ‘honorees’ kutoka mataifa 18 ikiwemo Ufaransa, Tanzania, Pakistan, India, Tunisia, Saudi Arabia na mengine. Washindi huchaguliwa na kamati maalum yenye uweledi kwenye nyanja tofauti kama Muziki, Sanaa, Utamaduni, Biashara, Kazi za Kijamii na kadhalika.

Read More
 Rayvanny awashukuru mashabiki kwa kushinda tuzo ya Zikomo nchini Zambia

Rayvanny awashukuru mashabiki kwa kushinda tuzo ya Zikomo nchini Zambia

Msanii wa Bongofleva Rayvanny amewashukuru mashabiki wake baada ya album yake “Sound from Africa” kushinda tuzo za Zikomo nchini Zambia kama Album Bora ya Mwaka. Boss huyo wa lebo ya NLM Rayvanny aliachia rasmi album yake “Sound from Africa” Februari Mosi, 2021 ikiwa ndio album yake ya kwanza katika safari yake ya muziki. Ina jumla ya nyimbo 23 alizowashirikisha wasanii 20 kutoka Tanzania na nchi nyingine za Afrika. Itakumbukwa, Album ya “Sound from Africa” iliweka rekodi Afrika Mashariki kwa kufikisha wasikilizaji zaidi ya Milioni 100 ndani ya wiki moja pekee tangu itoke. Ikijumuisha wasikilizaji kutoka mitandao ya Audiomack, Boomplay, iTunes, Spotify, YouTube, Boomplay na Apple Music.

Read More