REMA NAMAKULA AFUNGUKA SABABU ZA KUTOANIKA NDOA YAKE MTANDAONI

REMA NAMAKULA AFUNGUKA SABABU ZA KUTOANIKA NDOA YAKE MTANDAONI

Msanii Rema Namakula has ameonyesha kuchukizwa na waganda kwa kuwa roho na roho mbaya. Katika mahojiano yake hivi karibuni Rema amesema siku hizi huwa haposti tena mume wake kwenye mitandao ya kijamii akieleza kuwa waganda wengi hawamtakii mema. Hitmaker huyo wa ngoma ya Gutujja amesema aliacha kuanika maisha yake ya mahusiano baada ya mashabiki wake kudai kuwa uhusiano wake na mumewe utaishia kwa kilio tu. “When I discovered that Ugandans are evil-hearted, I stopped showing them what makes me happy. At first, I thought if you are happy, you should just feel free. Let it all out because it’s normal but I realized it is not okay with some people,” she explained. Katika hatua nyingine ameeleza kuwa anaendelea kushirikiana na Eddy Kenzo kutoa matunzo kwa binti yao ambaye walizaa pamoja. Rema namakula amesema hawana utofauti wowote na eddy kenzo kwenye masuala ya kutoa malezi kwa mtoto wao kama wengi wanavyodhani. Utakumbuka Rema namakula aliachana na eddy kenzo mwaka wa 2019 ambapo aliingia kwenye mahusiano mengine na Hamsa Ssebunya

Read More
 REMA NAMAKULA MBIONI KUACHIA ALBUM YAKE MPYA

REMA NAMAKULA MBIONI KUACHIA ALBUM YAKE MPYA

Staa wa muziki nchini uganda Rema Namakula ametangaza ujio wa album yake mpya ambayo amekuwa akiifanyia kazi kwa muda mrefu. Kupitia ukurasa wake wa twitter Rema amedokeza kwamba yupo kwenye maandalizi ya mwisho ya kukamilisha album yake mpya ambayo itaingia sokoni mwaka huu wa 2022. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Katonotono” amesema amekuwa akitumia muda wake mwingi studio kuitayariasha album yake mpya  ambayo kwa mujibu wake amesema ni moto wa kuotea mbali, hivyo mashabiki zake wakae mkao wa kula kuipokea album yake hiyo. Utakumbuka tangu Rema Namakula ajifungue mtoto wake na Dr. Hamzah Sebunya amekuwa kimya kwenye masuala ya kuachia muziki kwa ajili ya kuishughulikia familia yake. Kazi ya mwisho kutoka kwa Rema Namakula ilikuwa ni ngoma iitwayo Akafe Che ambayo ndani kipindi cha miezi mitatu imefikisha zaidi ya views millioni 1.5 kwenye mtandao wa youtube.

Read More