Spice Diana Afichua Siri Nzito ya Uchawi Miongoni mwa Wasanii Uganda

Spice Diana Afichua Siri Nzito ya Uchawi Miongoni mwa Wasanii Uganda

Msanii maarufu wa Uganda, Spice Diana, ametikisa tasnia ya burudani kwa madai mazito ya kuwepo kwa uchawi miongoni mwa wanamuziki. Katika mahojiano a Galaxy TV, msanii huyo wa “Source Management” alieleza kuwa baadhi ya wasanii hutumia nguvu za giza kwa lengo la kudhoofisha na kuvuruga mafanikio ya wenzao. “Watu wanafanya kazi kwa bidii gizani kuhakikisha wanaharibu kazi za wenzao. Tuwe wakweli – haya mambo yapo,” alisema Spice Diana kwa msisitizo Licha ya kuwa na imani kwamba uchawi upo katika sekta ya muziki, Spice Diana anasema hajawahi kuathirika moja kwa moja na uchawi huo. Anaamini kuwa nguvu ya maombi kutoka kwa mashabiki wake na imani yake kwa Mungu ndiyo ngao yake. “Labda mtu alijaribu kuniroga lakini akashindwa. Mungu amenilinda kupitia maombi ya mashabiki wangu wengi,” alisema. Hata hivyo, msanii huyo aliongeza kuwa si kila changamoto inayompata msanii ina uhusiano na uchawi. Alisisitiza kuwa matatizo ya kawaida ya kibinadamu pia huwapata wasanii kama watu wengine. “Wakati mwingine tunapitia matatizo ya kawaida kama binadamu wengine, lakini tunadhani tumerogwa. Ndio maana sitaki kila tatizo ninalopitia niunganishe na uchawi,” alieleza. Kauli ya Spice Diana imezua mijadala mikali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, huku baadhi wakimsifu kwa ujasiri wake wa kusema ukweli, na wengine wakihofia kuwa madai hayo yanaweza kuongeza hofu na chuki miongoni mwa wasanii. Hili si tukio la kwanza kwa madai ya aina hiyo kusikika. Wasanii wengine kama Zanie Brown na Grace Nakimera pia wamewahi kuelezea masaibu waliyopitia kutokana na kile walichodai kuwa ni hujuma za kishirikina kutoka kwa wenzao katika muziki.

Read More
 Meneja wa Spice Diana atuhumiwa kumtishia mtu maisha Uganda

Meneja wa Spice Diana atuhumiwa kumtishia mtu maisha Uganda

Mcheza densi kutoka Uganda Ritah amejitokeza na kumshutumu meneja wa msanii Spice Diana, Roger Lubega kwa kumtishia maisha. Ritah anasema Roger na timu yake wamekuwa wakimtumia jumbe za vitisho kuwa watamtoa uhai kutokana na matamshi yake dhidi ya tamasha la Spice Diana lililofanyika juzi kati huko Lugogo Cricket Oval. Ritah alidai enesho la Spice Diana halikuwa na mvuto, jambo ambalo lilimkasirisha Roger Lubega. “Marafiki zangu, nina hofia maisha yangu. Kama kuna jambo lolote litanitokea, mnajua wa kuwalaumu. Wale jamaa ni hatari kama mnavyofahamu, huko nyuma wamekuwa wakihusishwa na mauaji. Siwezi kuchukua vitisho vyao kwa wepesi,” alisema. Julai mwaka jana, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Henry Nsamba, aliuawa nyumbani kwa Spice Diana eneo la Makindye na tangu kipindi hicho familia ya mwenda zake hajawahi pata haki.

Read More
 ROGER LUBEGA AMJIBU GRAVITY OMUTUJJU, ADAI ANATUMIA JINA LA SPICE DIANA KUTAFUTA KIKI

ROGER LUBEGA AMJIBU GRAVITY OMUTUJJU, ADAI ANATUMIA JINA LA SPICE DIANA KUTAFUTA KIKI

Meneja wa Spice Diana, Roger Lubega amemjibu Gravity Omutujju kuonekana kumshambulia katika siku za hivi karibuni kwa kudai kwamba ni mnafiki na hajawahi watakiwa wasanii wengine mema kwenye muziki wao. Katika mahojiano yake Roger Lubega amesema hana ugomvi wowote na Omutujju huku akidai kuwa rapa huyo anatumia jina la msanii wake Spice Diana kutengeneza matukio ya kuzungumziwa mtandaoni kama njia ya kuitangaza tamasha lake litakalofanyika Cricket Oval Lugogo, Oktoba mosi mwaka huu. Kwa upande rapa Gravity Omutujju amepuzilia mbali madai ya lubega kwa kusema kwamba mambo yote aliyozungumza juu meneja huyo ni ya kweli huku akisema kwamba hawezi kutumia jina lake kutafuta kiki kwa kuwa yeye ni msanii mkubwa. Hata hivyo amesema amefanya matamasha makubwa ambayo yamepata mapokezi mazuri kutoka kwa mashabiki bila kutumia kiki huku akitishia kusitisha tamasha lake iwapo watu wataendelea kudai kwamba anatengeza matukio kwa ajili ya kutangaza tamasha hilo. Utakumbuka mwaka wa 2019 Gravity Omutujju aliwadanganya mashabiki zake kuwa alipigwa risasi tumboni lakini ilikuja ikabainika alitumia njia hiyo kwa ajili ya kutangaza show yake aliyoifanya katika ukumbi wa Cricket Oval Lugogo, nchini Uganda.

Read More