Spice Diana Aeleza Sababu za Kukataa Kubadili Maumbile kwa Upasuaji

Spice Diana Aeleza Sababu za Kukataa Kubadili Maumbile kwa Upasuaji

Staa wa muziki kutoka Uganda, Spice Diana, ameweka wazi msimamo wake kuhusu wimbi la wasanii na wanawake wengi kugeukia upasuaji wa urembo au butt lift ili kubadilisha maumbile yao. Msanii huyo ambaye anafanya poa na single yake iitwayo “Award” amesema kuwa sababu kubwa inayomzuia ni hofu ya maumivu, akieleza kwamba hataki kitu chochote kinachoweza kuumiza mwili wake. Licha ya msimamo wake binafsi, mrembo huyo amesisitiza kuwa kila mtu ana uhuru wa kufanya maamuzi kuhusu mwili wake. Anaamini kuwa dunia ya sasa inaruhusu watu kuamua wanachotaka kufanya, iwe ni upasuaji, butt lift au mabadiliko mengine ya kimaumbile, na kwamba haifai mtu yeyote kulaumiwa au kukosolewa kwa uamuzi huo. Kauli ya Spice Diana inakuja wakati mjadala kuhusu upasuaji wa urembo unaendelea kushika kasi barani Afrika, huku baadhi wakiona ni njia ya kujiamini na wengine wakihofia madhara ya kiafya pamoja na viwango visivyo halisi vya urembo.

Read More
 Spice Diana Amshambulia Sheebah, Adai Analipa Wanablogu Kumchafua

Spice Diana Amshambulia Sheebah, Adai Analipa Wanablogu Kumchafua

Msanii nyota wa muziki nchini Uganda, Spice Diana, ameendeleza mashambulizi ya maneno dhidi ya msanii mwenzake Sheebah Karungi, akimtuhumu kuwalipa wanablogu na baadhi ya watu kutoka kwenye timu yake ili kusambaza taarifa za kumchafua mtandaoni. Akizungumza katika mahojiano na kituo cha runinga nchini Uganda, Spice Diana alisema kuwa Sheebah mara nyingi hujikita kumzungumzia kila anapopata nafasi, jambo ambalo kwa upande wake anadai halimsumbui. Spice Diana amesema kuwa hatua ya kum-unfollow Sheebah kwenye Instagram ilitokana na kile alichokiona kama tabia za kimaslahi binafsi na zisizo za ukweli. Alieleza kuwa badala ya kushughulikia masuala yao binafsi kwa njia ya moja kwa moja, Sheebah alichagua kuchapisha ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, hali iliyomfanya apoteze imani naye. Kwa upande wake, Sheebah Karungi, kupitia mkutano na wanahabari uliofanyika wiki iliyopita, alikanusha madai ya kumshambulia Spice Diana au kulipa wanablogu waandike habari mbaya kumhusu, akieleza kuwa hana sababu yoyote ya kufanya hivyo. Mvutano kati ya wasanii hawa wawili umeendelea kushika kasi kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya mzozo huo

Read More
 Jowy Landa Apinga Kauli ya Spice Diana Kuhusu Mafanikio Bila Kuwa na Hit songs

Jowy Landa Apinga Kauli ya Spice Diana Kuhusu Mafanikio Bila Kuwa na Hit songs

Mwanamuziki chipukizi kutoka Uganda, Jowy Landa, amejitokeza hadharani kupinga kauli ya Spice Diana kwamba mtu anaweza kufanikiwa katika muziki bila kuwa na nyimbo kali (hit songs). Kupitia mahojiano aliyofanya hivi karibuni na kituo cha redio, Jowy Landa alisema kuwa mafanikio ya kweli katika muziki hayawezi kupimwa kwa umaarufu wa mtu mtandaoni au mwonekano wa kisanaa pekee, bali kwa uwezo wa kutoa kazi zinazogusa mashabiki na kudumu kwenye chati. “Ni vigumu kusema umefanikiwa kama hauna hata wimbo mmoja ambao watu wanaweza kuuita hit. Mafanikio katika muziki yanatokana na impact unayoacha kwa wasikilizaji. Nyimbo kali huonyesha ubunifu na uwezo halisi wa msanii,” alisema Jowy. Kauli hiyo imeonekana kumlenga moja kwa moja Spice Diana, ambaye hivi majuzi alijinasibu kwamba amefanikiwa katika tasnia ya muziki licha ya kutoachia nyimbo nyingi zilizotamba. Mashabiki kwenye mitandao ya kijamii wamegawanyika, baadhi wakimuunga mkono Jowy kwa kusema kuwa muziki mzuri ndio unaojenga jina la msanii, huku wengine wakimtetea Spice Diana wakidai kuwa mafanikio ni pana zaidi na si lazima yaambatane na hit songs pekee.

Read More
 Spice Diana Afunguka Kuhusu Uzazi na Nia ya Kuwa na Watoto Wengi

Spice Diana Afunguka Kuhusu Uzazi na Nia ya Kuwa na Watoto Wengi

Mwanamuziki nyota kutoka Uganda, Spice Diana, amefunguka kwa mara ya kwanza kwa undani kuhusu suala la uzazi, akieleza kuwa ni jambo alilo wazi nalo kwa moyo wote na analiangalia kwa uzito mkubwa. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Spice Diana alisema kuwa anapenda sana watoto, na kama isingekuwa muziki aliouanza tangu akiwa na umri mdogo, tayari angekuwa na zaidi ya watoto kumi na wawili. “Familia ni kitu kizuri sana. Kama nisingekuwa maarufu mapema, ningekuwa na watoto zaidi ya kumi na wawili. Nampenda sana watoto. Uzuri wa kuwa na watoto mapema niliuona kupitia mama yangu aliyenizaa akiwa na miaka kumi na nne. Tulikua pamoja, na ilikuwa ni safari nzuri,” alisema Spice Diana kwa hisia. Spice Diana alieleza kuwa mafanikio yake ya mapema katika muziki ndiyo yaliyochangia kuchelewesha ndoto yake ya kuwa mama. Akiwa amewekeza muda mwingi katika kazi yake ya sanaa, amekuwa akiahirisha suala hilo kwa muda mrefu. Licha ya hilo, anasema sasa analichukulia uzazi kama jambo la heshima na baraka, na anatarajia kuwa mama wa watoto wengi katika miaka ijayo. “Kuzaa ni baraka, na sasa naliangalia kwa uzito mkubwa. Ni kitu ninachotarajia kwa furaha na moyo mweupe,” aliongeza. Katika kizazi chake cha muziki, Spice Diana anabaki kuwa mmoja wa wasanii wachache wa kike ambao bado hawajaanzisha familia. Wenzake kama Sheebah Karungi, Cindy Sanyu, na Vinka tayari wameingia kwenye maisha ya kuwa mama, hali inayoonesha mabadiliko ya kijamii na kipekee kwa wanamuziki wa kike katika ukanda huo. Mashabiki wake sasa wanafuatilia kwa shauku na matumaini, wakisubiri kuona ni lini Spice Diana atachukua hatua hiyo muhimu ya maisha. Hata hivyo, msanii huyo amesema hawezi kuweka muda maalum kwa sasa, lakini uzazi ni sehemu ya mipango yake ya baadaye.

Read More
 Spice Diana Mbio Kuwabariki Mashabiki na Albamu Mpya

Spice Diana Mbio Kuwabariki Mashabiki na Albamu Mpya

Msanii nyota wa muziki wa Uganda, Spice Diana, ameweka wazi kuwa yuko mbioni kukamilisha albamu yake ya kwanza ya studio, akiahidi mashabiki wake kuwa itazinduliwa kabla ya mwisho wa mwaka huu. Spice Diana, ambaye amekuwa kwenye tasnia ya muziki kwa zaidi ya miaka kumi, amesema huu ndio mradi wake mkubwa zaidi, na anaamini utakuwa wa kipekee kuliko kazi zake zote za awali. Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini Uganda, msanii huyo alieleza kuwa albamu hiyo ina nyimbo nyingi, lakini sasa anapitia changamoto ya kuchagua ni zipi ataweka rasmi kwenye albamu hiyo.  “Nafanya kazi ya albamu. Kuna nyimbo nyingi sana hadi napata shida kuchagua. Lakini nitahakikisha albamu itatoka kabla ya mwaka kuisha. Ni kazi bora kabisa kutoka kwangu kwa sababu nimewekeza muda na nguvu nyingi,” alisema Spice Diana. Albamu hiyo inakuja katika kipindi ambacho wasanii wengi wa Uganda wameanza kuelekeza nguvu zao kwenye utayarishaji wa albamu kamili, tofauti na zamani ambapo walikuwa wakizingatia zaidi nyimbo za mtu mmoja mmoja. Spice Diana ataungana na orodha ya wasanii wengine wa Uganda waliokwisha toa albamu, akiwemo Sheebah, Juliana Kanyomozi, Azawi, Bebe Cool, Eddy Kenzo, Navio, A Pass na wengine. Mashabiki wake wanaisubiri kwa hamu kazi hiyo mpya, ambayo inatarajiwa kuonyesha ubunifu na mwelekeo mpya katika muziki wa Spice Diana.

Read More
 Spice Diana Asimulia Maisha Magumu ya Utotoni, Amsifu Mama kwa Kujitolea

Spice Diana Asimulia Maisha Magumu ya Utotoni, Amsifu Mama kwa Kujitolea

Mwanamuziki maarufu kutoka Uganda, Spice Diana, ameweka wazi safari yake ya maisha ya utotoni iliyojaa changamoto, akimsifia mama yake kwa kujitoa muhanga ili kuwapatia yeye na dada yake maisha bora. Kupitia mahojiano ya hivi karibuni, Spice Diana alisimulia namna mama yake alivyolazimika kuacha familia yake vijijini Kiboga na kwenda jijini Kampala kufanya kazi kama msaidizi wa nyumbani ili kuwahudumia. Kwa mujibu wa Spice Diana, wazazi wake walitengana akiwa na umri wa miaka mitatu. Hali hiyo ilimlazimu mama yake kuwapeleka kwa bibi yao mkoani Kiboga, kisha kurudi mji mkuu wa Kampala kuanza maisha ya kuhangaika kama mfanyakazi wa ndani katika familia mbalimbali. Lengo lake kuu lilikuwa kuhakikisha watoto wake hawakosekani katika masuala ya msingi kama elimu na makazi bora. Baada ya miezi kadhaa ya kufanya kazi kwa bidii, mama yake aliweza kuwarudisha watoto wake mjini na kuanza maisha mapya nao. Akiwa Kampala, mama yao alipata mume mwingine aliyewapokea watoto wake kwa moyo wa baba wa kambo, na aliwapatia huduma zote muhimu, zikiwemo ada za shule, chakula na malezi ya upendo. Hata hivyo, penzi hilo halikudumu, kwani baada ya muda kulizuka migogoro ya kifamilia na mwanaume huyo akaondoka kwenye maisha yao kabisa. Spice Diana amesema kuwa licha ya changamoto zote, ana mshukuru mama yake kwa moyo wake wa kujitolea na uvumilivu usio na mipaka. Amedai mafanikio yake ya leo ni matokeo ya maelekezo na maadili aliyopata kutoka kwa mama yake. Ametumia fursa hiyo kuhimiza vijana kuwaheshimu wazazi wao, hasa wale waliopitia maisha magumu kwa ajili ya kuwalea.

Read More
 Spice Diana Afichua Siri Nzito ya Uchawi Miongoni mwa Wasanii Uganda

Spice Diana Afichua Siri Nzito ya Uchawi Miongoni mwa Wasanii Uganda

Msanii maarufu wa Uganda, Spice Diana, ametikisa tasnia ya burudani kwa madai mazito ya kuwepo kwa uchawi miongoni mwa wanamuziki. Katika mahojiano a Galaxy TV, msanii huyo wa “Source Management” alieleza kuwa baadhi ya wasanii hutumia nguvu za giza kwa lengo la kudhoofisha na kuvuruga mafanikio ya wenzao. “Watu wanafanya kazi kwa bidii gizani kuhakikisha wanaharibu kazi za wenzao. Tuwe wakweli – haya mambo yapo,” alisema Spice Diana kwa msisitizo Licha ya kuwa na imani kwamba uchawi upo katika sekta ya muziki, Spice Diana anasema hajawahi kuathirika moja kwa moja na uchawi huo. Anaamini kuwa nguvu ya maombi kutoka kwa mashabiki wake na imani yake kwa Mungu ndiyo ngao yake. “Labda mtu alijaribu kuniroga lakini akashindwa. Mungu amenilinda kupitia maombi ya mashabiki wangu wengi,” alisema. Hata hivyo, msanii huyo aliongeza kuwa si kila changamoto inayompata msanii ina uhusiano na uchawi. Alisisitiza kuwa matatizo ya kawaida ya kibinadamu pia huwapata wasanii kama watu wengine. “Wakati mwingine tunapitia matatizo ya kawaida kama binadamu wengine, lakini tunadhani tumerogwa. Ndio maana sitaki kila tatizo ninalopitia niunganishe na uchawi,” alieleza. Kauli ya Spice Diana imezua mijadala mikali katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, huku baadhi wakimsifu kwa ujasiri wake wa kusema ukweli, na wengine wakihofia kuwa madai hayo yanaweza kuongeza hofu na chuki miongoni mwa wasanii. Hili si tukio la kwanza kwa madai ya aina hiyo kusikika. Wasanii wengine kama Zanie Brown na Grace Nakimera pia wamewahi kuelezea masaibu waliyopitia kutokana na kile walichodai kuwa ni hujuma za kishirikina kutoka kwa wenzao katika muziki.

Read More
 Jowy Landa Atoa Majibu Mazito kwa Wakosoaji Wake

Jowy Landa Atoa Majibu Mazito kwa Wakosoaji Wake

Msanii wa muziki kutoka Uganda, Jowy Landa, ameibuka na kujibu ukosoaji anaoupata kutoka kwa baadhi ya mashabiki na wadau wa tasnia ya burudani, akisema kwamba hawamsumbui kwani anaamini wanachukizwa na mafanikio yake. Kwenye mahojiano na runinga moja nchini Uganda, Jowy alisema kwamba hafuatilii wala kubeba kwa uzito maoni ya wanaomsema vibaya.  “Mimi hukosolewa kwa sababu mimi ni bora. Watu huwa hawaendi kinyume na wasio na mvuto. Wanaonizungumzia ni kwa sababu wamekasirishwa na ukuaji wangu wa kimuziki,” alisema kwa msisitizo. Kauli hiyo imezua maoni mseto kutoka kwa mashabiki, hasa ikizingatiwa historia yake ya kutoa kauli kali dhidi ya wasanii wenzake. Mapema mwaka huu, alizua mjadala mkubwa baada ya kumkosoa vikali Spice Diana, akimtuhumu kuwa na kiwango duni cha sauti na kudai kwamba kazi zake hazina ubunifu wa kweli. Kauli hiyo iliwakasirisha baadhi ya mashabiki wa Spice Diana, lakini upande wa msanii huyo haukujibu hadharani, jambo lililowafanya wengi kusifu utulivu wa timu ya Spice katika kukabiliana na mivutano ya kisanii. Hata hivyo, Jowy sasa anaonekana kukerwa na ukosoaji wa watu dhidi yake, jambo ambalo limeibua maswali kutoka kwa baadhi ya wachambuzi wa burudani: Je, msanii anayependa kukosoa wenzake hastahili pia kukosolewa? Wadadisi wa masuala ya muziki wanasema hali kama hizi huibua mjadala kuhusu ukomavu wa wasanii, uwezo wa kujifunza kupitia maoni ya wengine, na uhusiano wa kweli kati ya ubunifu na ukosoaji wa wazi.

Read More
 Pallaso Hatimaye Awapatanisha Green Daddy, Spice Diana na Manager Roger

Pallaso Hatimaye Awapatanisha Green Daddy, Spice Diana na Manager Roger

Katika tukio lililosubiriwa kwa muda mrefu kwenye tasnia ya muziki wa Uganda, msanii maarufu Pallaso ameongoza juhudi za upatanisho kati ya wasanii Green Daddy, Spice Diana, na Manager Roger, kufuatia uhasama uliochukua zaidi ya miaka miwili. Green Daddy amekuwa akimkosoa hadharani Spice Diana na meneja wake, Roger, mara kwa mara akiwaita wasio na maadili na hata kuwahusisha na ushetani. Madai haya yaliibua maswali mengi miongoni mwa mashabiki na wanamuziki wenzake, huku Spice Diana mara kadhaa akisema hajui chanzo cha chuki hiyo. Hata hivyo, hali hiyo sasa inaelekea kuwa historia, baada ya Pallaso kuingilia kati kwa nia ya kurejesha amani. Green Daddy juzi alikutana na Pallaso katika studio za Spice Diana, ambapo walikaa pamoja na kuzungumza kwa kina kuhusu tofauti zao. Katika mazungumzo hayo, Green Daddy alifunguka na kueleza chanzo cha malalamiko yake, akisema kuwa Manager Roger aliwahi kumtendea jambo baya sana, kiasi cha kuhatarisha maisha yake. Ingawa hakufafanua kwa undani, Green Daddy alionyesha kuwa yuko tayari kuweka tofauti zao kando. Kwa upande wake, Spice Diana aliahidi kuandaa kikao maalum kati ya Green Daddy na meneja wake ili waweze kuketi pamoja na kumaliza tofauti hizo moja kwa moja. Mpango huo ulipokelewa kwa mikono miwili na Green Daddy, aliyeonekana kutaka amani irejee. Upatanisho huu umepokelewa vyema na mashabiki pamoja na wadau wa muziki, ambao wamekuwa wakitaka kuona umoja na mshikamano miongoni mwa wanamuziki wa Uganda. Wengi wanaamini kuwa hatua hii inaweza kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano na hata kazi za pamoja kati ya wasanii hao. Kwa sasa, macho yote yako kwa kikao cha mwisho kati ya Green Daddy na Manager Roger, ambapo wengi wanatarajia suluhu ya kudumu na fursa mpya za kisanii.

Read More
 Halima Namakula Awaasa Wasanii wa Kike: “Msikimbilie Kujifungua, Jengeni Kwanza Ndoto Zenu”

Halima Namakula Awaasa Wasanii wa Kike: “Msikimbilie Kujifungua, Jengeni Kwanza Ndoto Zenu”

Mwanamuziki mkongwe na anayeheshimika sana katika tasnia ya burudani nchini Uganda, Halima Namakula, ameendelea kudhihirisha hekima yake kwa kutoa ushauri mzito kwa wasanii wa kike wa kizazi kipya. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Namakula aliwahimiza wasanii wa kike kutokukimbilia suala la kuanzisha familia mapema, badala yake wajikite kwenye masuala yakukuza taaluma zao za muziki na kufurahia maisha yao wakiwa wangali wachanga. “Hamstahili kuharakisha kujifungua. Jengeni kwanza kazi zenu, mfurahie maisha yenu. Uzazi una wakati wake, na utakapofika, mtakuwa mmejiandaa vya kutosha,” alisema Namakula kwa msisitizo. Katika ushauri wake, Namakula alimtaja msanii maarufu Spice Diana, ambaye amekuwa akikumbwa na shinikizo la mashabiki wanaomtaka kuwa mama, akisema hapaswi kuogopa shinikizo hizo, kwani bado ana muda mrefu wa kuwa mama. Alipendekeza Diana afikirie kuwa na familia baada ya kufikisha miaka thelathini. “Diana ana muda mwingi. Aendelee na kazi yake, apate mafanikio zaidi, na afikirie kuwa mama akifikisha miaka thelathini.” Namakula alieleza kuwa msingi thabiti wa kazi ya muziki unaweza kuwa nguzo imara kwa maisha bora ya watoto siku za mbeleni. Alisisitiza kuwa mafanikio ya sasa yatawasaidia wasanii hao kuwapa watoto wao maisha yenye usalama, uthabiti na fursa. Kwa mujibu wake, uzazi ni baraka, lakini unahitaji maandalizi ya kiakili, kifedha, na kimazingira. Hivyo basi, kujijenga kwanza ni njia bora ya kuwajibika kama mzazi katika siku za usoni. Kwa miaka mingi, Halima Namakula amekuwa mlezi, mshauri, na mfano kwa wasanii wengi wa kike katika ukanda wa Afrika Mashariki. Anaamini kuwa mafanikio hayaji kwa bahati, bali kwa mipango thabiti, nidhamu, na subira.

Read More
 Rapa Gravity Omutujju akiri kumchukia Spice Diana na meneja wake Rodger Lubega

Rapa Gravity Omutujju akiri kumchukia Spice Diana na meneja wake Rodger Lubega

Rapa Gravity Omutujju na Spice Diana walikuwa marafiki wakubwa sana kwa muda mrefu hadi alipokosana kutokana na sababu ambazo hawakuweka wazi. Wakati wa mahojiano hivi karibuni, Gravity amefichua kwamba anachukia uongozi wa Spice Diana kiasi kwamba hakutaka kusikia chochote kuhusu tamasha la mrembo huyo lililokamilika hivi karibuni. “Sikusikia kuhusu tamasha lake. Sikujua chochote kuhusu yeye pamoja na meneja wake. Siwapendi,” alisema kwenye mahojiano na Galaxy TV. Rapa huyo ameendelea kumlaani meneja wa Spice Diana, Rodger Lubega kwa madai ya kuwa mtu mbaya ambaye amekuwa akihujumu shughuli za watu.

Read More
 Meneja wa Spice Diana atuhumiwa kumtishia mtu maisha Uganda

Meneja wa Spice Diana atuhumiwa kumtishia mtu maisha Uganda

Mcheza densi kutoka Uganda Ritah amejitokeza na kumshutumu meneja wa msanii Spice Diana, Roger Lubega kwa kumtishia maisha. Ritah anasema Roger na timu yake wamekuwa wakimtumia jumbe za vitisho kuwa watamtoa uhai kutokana na matamshi yake dhidi ya tamasha la Spice Diana lililofanyika juzi kati huko Lugogo Cricket Oval. Ritah alidai enesho la Spice Diana halikuwa na mvuto, jambo ambalo lilimkasirisha Roger Lubega. “Marafiki zangu, nina hofia maisha yangu. Kama kuna jambo lolote litanitokea, mnajua wa kuwalaumu. Wale jamaa ni hatari kama mnavyofahamu, huko nyuma wamekuwa wakihusishwa na mauaji. Siwezi kuchukua vitisho vyao kwa wepesi,” alisema. Julai mwaka jana, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Henry Nsamba, aliuawa nyumbani kwa Spice Diana eneo la Makindye na tangu kipindi hicho familia ya mwenda zake hajawahi pata haki.

Read More