Mike Sonko Ajitolea Kufadhili Tamasha la Vybz Kartel Nchini Kenya

Mike Sonko Ajitolea Kufadhili Tamasha la Vybz Kartel Nchini Kenya

Tajiri maarufu na aliyewahi kuwa Gavana wa Nairobi, Mike Sonko, ametangaza kuwa yuko tayari kufadhili tamasha kubwa la msanii nguli wa dancehall kutoka Jamaica, Vybz Kartel, nchini Kenya. Tangazo hilo limekuja muda mfupi baada ya Vybz Kartel kuonyesha nia ya kutumbuiza barani Afrika, akisema kuwa Kenya ni moja ya nchi anazopendelea kuzuru kwa ajili ya show maalum. Kupitia ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, Sonko alisema yuko tayari kushirikiana na wadau wa burudani kuhakikisha kuwa tamasha hilo linafanyika, licha ya gharama kubwa inayohusiana na kumleta Kartel. Kwa sasa, ada ya kumuweka jukwaani msanii huyo inakadiriwa kuwa kati ya Shilingi milioni 100 hadi 173 za Kenya. “Kama Vybz Kartel yuko tayari kuja Kenya, niko tayari kumfadhili. Tufanye hii show iwe ya kihistoria,” aliandika Sonko. Vybz Kartel, ambaye aliachiliwa kutoka gerezani mapema mwaka huu, ameendelea kudhihirisha ushawishi mkubwa katika tasnia ya muziki wa dancehall duniani. Nyimbo zake maarufu kama Fever, Summertime na Clarks zinaendelea kuvuma mitaani na kwenye redio nyingi humu nchini. Iwapo tamasha hilo litatimia, litakuwa moja ya maonyesho makubwa zaidi ya kimataifa kufanyika Kenya, na huenda likafungua milango kwa wasanii wengine wa kimataifa kuja kutumbuiza Afrika Mashariki.

Read More
 Vybz Kartel Asema Yuko Tayari Kutumbuiza Kenya, Atoa Wito kwa Waandaaji

Vybz Kartel Asema Yuko Tayari Kutumbuiza Kenya, Atoa Wito kwa Waandaaji

Msanii nguli wa muziki wa Dancehall kutoka Jamaica, Vybz Kartel, ameonyesha nia ya dhati kutua nchini Kenya kwa ajili ya kutumbuiza. Akiwa live kwenye Instagram, Kartel aliwapa mashabiki wake wa Kenya sababu ya kutabasamu baada ya kutoa wito kwa waandaaji wa matamasha nchini, akiwataka wamualike rasmi kwa tamasha kubwa. “Tell promoters Kartel is ready to come home,” alisema Kartel kwa sauti ya msisitizo huku akionekana mwenye shauku ya kuwa karibu na mashabiki wake wa Afrika, hususan Kenya. Kauli hiyo imeibua shangwe kubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa reggae na dancehall nchini Kenya, ambao wamekuwa wakimsubiri msanii huyo kwa muda mrefu. Katika ujumbe wake, Kartel alieleza mapenzi yake kwa Kenya, akiitaja kama “nyumbani”, jambo lililowasisimua wengi na kuongeza matumaini kuwa huenda onyesho lake nchini likawa karibu zaidi kuliko ilivyodhaniwa. Hadi sasa, mashabiki tayari wameanza kuwataja waandaaji wakubwa wa matamasha kama Shoke Shoke Festival, Koroga Festival, Blankets & Wine, na OktobaFest, wakiwataka wachukue hatua za haraka kuhakikisha Vybz Kartel anakuja nchini. Hii si mara ya kwanza msanii huyo kutuma ujumbe wenye mapenzi kwa bara la Afrika, lakini kutaja Kenya kwa jina na kuitambua kama nyumbani ni hatua ya kipekee inayodhihirisha ukubwa wa soko la muziki Afrika Mashariki na mapokezi mazuri anayopata kutoka kwa mashabiki wa eneo hili.

Read More
 Vybz Kartel na Mavado Waungana Tena Baada ya Miaka 17 ya Bifu la Gaza vs Gully

Vybz Kartel na Mavado Waungana Tena Baada ya Miaka 17 ya Bifu la Gaza vs Gully

Wasanii wawili maarufu wa dancehall kutoka Jamaica, Vybz Kartel na Mavado, wamezua gumzo kubwa baada ya kuungana tena rasmi kwa mara ya kwanza tangu bifu lao kali la mwaka 2008 maarufu kama “Gaza vs Gully”. Wawili hao, waliowahi kugawanya mashabiki wa muziki wa dancehall kwa kambi pinzani za Gaza (Kartel) na Gully (Mavado), sasa wameamua kuzikana tofauti zao na kushirikiana kwenye wimbo mpya unaotarajiwa kutikisa ulimwengu wa muziki. Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa, Vybz Kartel na Mavado wanashirikiana na DJ Khaled pamoja na gwiji mwingine wa dancehall, Bounty Killer, kwenye mradi huu mpya wa muziki. Ushirikiano huu si tu kwamba ni wa kihistoria, bali pia ni ujumbe mzito wa mshikamano na mabadiliko katika tasnia ya muziki wa Caribbean. Mashabiki duniani kote wamesema hawakuamini macho yao walipoona picha na video za wasanii hao wakirekodi pamoja. Wengi wamefurahia hatua hiyo wakisema imeleta matumaini mapya katika mwelekeo wa muziki wa dancehall. Wimbo huo mpya unatarajiwa kutolewa ndani ya wiki chache zijazo na tayari unahesabiwa kama moja ya collabo kubwa zaidi katika historia ya dancehall. Mashabiki wanasubiri kwa hamu kusikia ladha ya muziki huo ambao unawakutanisha tena magwiji waliowahi kuwa mahasimu wakubwa.

Read More
 Vybz Kartel avunja ukimya baada ya kufutwa kwa onyesho lake nchini Trinidad

Vybz Kartel avunja ukimya baada ya kufutwa kwa onyesho lake nchini Trinidad

Msanii nguli wa muziki wa dancehall kutoka Jamaica, Vybz Kartel, amevunja ukimya kufuatia kufutwa kwa onyesho lake lililokuwa limepangwa kufanyika leo katika One Caribbean Festival nchini Trinidad. Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, msanii huyo mashuhuri wa dancehall alieleza kuwa licha ya kutoa ushauri mara kadhaa kwa waandaaji wa tamasha hilo kuhusu hatua muhimu zinazopaswa kuchukuliwa, matatizo hayo hayakutatuliwa kwa wakati. Kartel alifichua kuwa alitoa onyo mapema ili kuhakikisha kuwa kila kitu kinaenda sawa, lakini ushauri wake haukufanyiwa kazi ipasavyo. Msanii huyo pia aliwaomba radhi watu wa Trinidad na mashabiki wake waliokuwa wakisubiri kwa hamu kumpa sapoti jukwaani. “Nimesikitishwa sana na jinsi mambo yalivyokwenda. Mashabiki wangu walistahili burudani, na ninawaahidi kuwa nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kuwa hali kama hii haitajirudia,” alisema Vybz Kartel. Mashabiki wengi wameeleza masikitiko yao kwenye mitandao ya kijamii huku wakimtaka msanii huyo kupanga upya onyesho hilo mara tu matatizo yaliyopo yatakapotatuliwa.

Read More
 Vybz Kartel Atangaza Ziara ya Dunia “Worl’ Boss Tour”

Vybz Kartel Atangaza Ziara ya Dunia “Worl’ Boss Tour”

Msanii mashuhuri wa muziki wa dancehall kutoka Jamaica, Vybz Kartel, ametangaza kuanza kwa ziara yake ya kimataifa inayojulikana kama Worl’ Boss Tour, ikiwa ni mara ya kwanza kwa msanii huyo kufanya maonyesho ya kimataifa baada ya miaka 20. Ziara hiyo ya maonyesho 15 itaanza rasmi Mei 24 mjini Georgetown, Guyana, na itaendelea katika miji mikubwa kama Atlanta, London, Paris, Kingston na hatimaye Birmingham, Uingereza mwezi Septemba. Tangazo hili linakuja wiki chache baada ya Kartel kufanikisha maonyesho mawili yaliyosheheni mashabiki katika ukumbi wa Barclays Center, New York,  hatua iliyozua hisia kubwa katika tasnia ya muziki. Vybz Kartel, ambaye pia amepata uteuzi wa tuzo ya Grammy na kuonekana kwenye jalada la jarida maarufu la Billboard, anaendelea kufufua kazi yake ya muziki baada ya kuachiliwa kutoka gerezani mapema mwaka huu. Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, msanii huyo amesema ziara hiyo inalenga kuunganisha mashabiki wake duniani kote na kusherehekea mafanikio ya muziki wa dancehall. “Nilisimama hapa nikiwa na ndoto; leo picha yangu ndiyo inasafiri kwenye ndoto hizo. Ni baraka isiyoelezeka.” Aliandika Instagram. Ziara ya Worl’ Boss Tour inatazamiwa kuwa mojawapo ya matukio makubwa ya muziki wa Karibea mwaka huu, ikimrejesha rasmi Kartel katika jukwaa la kimataifa kwa kishindo.

Read More
 Vybz Kartel amposa mrembo wa Kituruki Sidem Ozturk

Vybz Kartel amposa mrembo wa Kituruki Sidem Ozturk

Mkali wa Dancehall mwenye umaarufu mkubwa duniani Vybz Kartel ambaye kwa sasa anaendelea kusotea gerezani, amemposa mrembo Mturuki Sidem Ozturk. Kwa mujibu wa Radio ya Nation Wide, posa hilo lilifanyika wakati wa ziara iliyoidhinishwa gerezani humo, ambapo Vybz Kartel anatumikia kifungo cha maisha jela kwa mauaji ya Clive “Lizard” Williams. Sidem Ozturk ambaye ameajiriwa huko London, Uingereza kama mfanyakazi wa kijamii, amekatiza taaluma yake na kuhamia Kingston, Jamaica ili kuwa karibu na nyota huyo wa Dancehall. Licha ya changamoto wanazokabiliana nazo kutokana na Kartel kulala nyuma ya nyondo, Ozturk hajakata tamaa katika penzi lao.

Read More