WhatsApp Yazindua Kipengele Kipya cha Ku-forward Status kwa Marafiki

WhatsApp Yazindua Kipengele Kipya cha Ku-forward Status kwa Marafiki

Kampuni ya Meta, inayomiliki jukwaa maarufu la mawasiliano la WhatsApp, imeanza kutekeleza kipengele kipya kinachoruhusu watumiaji ku-forward Status kwa marafiki au kwenye Status zao wenyewe. Hili ni moja ya maboresho makubwa katika eneo la Status, linalokusudia kuongeza mwingiliano na urahisi wa kushirikiana maudhui kati ya watumiaji. Kwa kutumia kipengele hiki, mtumiaji anaweza kuchagua Status ya mtu mwingine iwe ni picha, video au maandishi na kuishiriki (forward) moja kwa moja kwa mtu mwingine au kuipost kwenye Status yake binafsi. Hii ni hatua inayofanana na mtindo wa kushirikiana Stories kwenye majukwaa mengine kama Instagram na Facebook. Mbali na kuongeza urahisi wa kushirikisha maudhui, WhatsApp pia imetoa chaguo la faragha, ambapo watumiaji wanaweza kuchagua kama wanataka status zao ziweze kushirikiwa na wengine au la. Hii inawapa watumiaji udhibiti kamili wa maudhui yao na jinsi yanavyosambazwa. Kipengele hiki kimeanza kusambazwa kwa baadhi ya watumiaji kupitia masasisho ya hivi karibuni, na kinatarajiwa kupatikana kwa wote katika siku zijazo. Watumiaji wa Android na iOS wanashauriwa kuhakikisha wanatumia toleo la kisasa la WhatsApp ili kufurahia huduma hii mpya.

Read More
 WhatsApp Yaanza Majaribio ya Live Photos kwa Watumiaji

WhatsApp Yaanza Majaribio ya Live Photos kwa Watumiaji

Kampuni ya WhatsApp imeanzisha majaribio ya kipengele kipya kinachoruhusu watumiaji kutuma picha zinazojongea, maarufu kama motion pictures au live photos. Hatua hii inalenga kuboresha mawasiliano kwa kuongeza uhalisia na hisia zaidi katika mazungumzo ya mtandaoni. Kulingana na ripoti kutoka vyanzo vya teknolojia, kipengele hiki kinajaribiwa kwa watumiaji wa toleo la beta la WhatsApp. Kinawawezesha watumiaji wa simu za iPhone kutuma picha za live photo moja kwa moja bila kubadilishwa kuwa picha tuli (still image). Kipengele hiki kitasaidia WhatsApp kushindana vyema na huduma nyingine kama iMessage ya Apple, ambayo tayari inaruhusu kutuma live photos, pamoja na Snapchat na Instagram ambazo zinatumia sana picha na video zenye mwendo. Ingawa bado haijafahamika rasmi lini kipengele hiki kitawekwa rasmi kwa watumiaji wote, inaonekana WhatsApp inaendelea kuwekeza katika kuboresha uzoefu wa mawasiliano kwa kutumia teknolojia za kisasa za kuona na kusikia. Watumiaji wengi wamepokea habari hii kwa shauku kubwa, wakitarajia kwamba kipengele hiki kitaongeza ubunifu na uhalisia katika kushiriki matukio yao ya kila siku kupitia moja ya majukwaa makubwa zaidi ya mawasiliano duniani.

Read More
 WhatsApp Kuleta Muhtasari wa Meseji Kupitia Teknolojia ya Akili Bandia

WhatsApp Kuleta Muhtasari wa Meseji Kupitia Teknolojia ya Akili Bandia

Kampuni ya Meta, inayomiliki WhatsApp, imetangaza kuwa inafanyia majaribio kipengele kipya cha akili bandia (AI) kitakachowezesha watumiaji wake kufupisha mazungumzo marefu kwenye meseji. Kwa kutumia teknolojia ya AI, WhatsApp itawaruhusu watumiaji kupata muhtasari wa haraka wa mazungumzo yao, jambo ambalo linalenga kusaidia wale wanaopokea ujumbe mwingi au ambao hawakuwahi kufuatilia kila ujumbe mmoja mmoja. Kipengele hiki kinatarajiwa kufanya kazi kwa kuchambua mazungumzo ya kundi au mtu binafsi, kisha kutoa muhtasari wa mambo muhimu yaliyojadiliwa, huku kikihifadhi usalama na faragha ya watumiaji kwa kutumia teknolojia ya usimbaji wa mwisho kwa mwisho (end-to-end encryption). Taarifa kutoka kwa baadhi ya watumiaji waliopata toleo la majaribio zinasema kuwa kipengele hicho kiko chini ya sehemu ya “Chat Summary,” ambapo AI inaweza kutoa dondoo fupi kuhusu mazungumzo yaliyopita. Hii ni moja kati ya hatua kadhaa ambazo Meta imeanza kuzitekeleza ili kuimarisha matumizi ya AI kwenye majukwaa yake, ikiwa ni pamoja na kuanzisha wasaidizi wa kidijitali ndani ya WhatsApp na Messenger. Hadi sasa, Meta haijatoa tarehe rasmi ya kuachia kipengele hicho kwa watumiaji wote, lakini matarajio ni kuwa kitakuwa sehemu ya masasisho yajayo ya WhatsApp mwaka huu

Read More
 Makundi WhatsApp Yapata Sehemu ya Status kwa Mara ya Kwanza

Makundi WhatsApp Yapata Sehemu ya Status kwa Mara ya Kwanza

Kampuni ya WhatsApp imeanza rasmi majaribio ya kipengele kipya kitakachowezesha makundi (Groups) kuwa na sehemu maalum ya Status, sawa na jinsi watumiaji wa kawaida wanavyoweka status binafsi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya karibu na majaribio hayo, mabadiliko haya yanalenga kuongeza mwingiliano wa kijamii ndani ya Groups, kwa kutoa nafasi kwa wanachama wa kundi kushiriki maudhui ya muda (status) yanayoonekana na members pekee wa group hilo. Kupitia kipengele hiki, kila Group kitakuwa na sehemu maalum ya Status, ambapo members wataweza kuchapisha status zao. Tofauti na status za kawaida, hizi hazitaonekana kwa watumiaji walio nje ya Group, hivyo kuongeza usiri na umakini wa mawasiliano ndani ya kundi. Aidha, WhatsApp imetoa uwezo kwa admin wa Group kudhibiti nani anaruhusiwa kuweka Status ama kutoa ruhusa kwa members wote, au kuweka kuwa admin tu ndiye anayeweza kuchapisha. Kipengele hiki kinatazamiwa kuongeza idadi ya views kwenye Status, kwa kuwa watumiaji sasa wataweza kushiriki status zao kwa watu wengi zaidi waliopo kwenye Group moja, hata kama si marafiki wa moja kwa moja kwenye akaunti zao binafsi. Hatua hii ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za WhatsApp kuboresha huduma zake kulingana na tabia na mahitaji ya watumiaji wake, na kuifanya kuwa zaidi ya jukwaa la ujumbe ikichukua nafasi ya kuwa sehemu ya kijamii inayotoa fursa za kushirikishana zaidi. Kwa sasa, kipengele hiki kiko katika hatua ya majaribio, na kinatarajiwa kuzinduliwa rasmi kwa watumiaji wote katika toleo lijalo la app hiyo baada ya tathmini ya awali kukamilika.

Read More
 WhatsApp Yaboresha Njia ya Kuonyesha Replies

WhatsApp Yaboresha Njia ya Kuonyesha Replies

Kampuni ya Meta kupitia jukwaa la WhatsApp inafanya majaribio ya kuongeza mtindo mpya wa kuonyesha majibu yote yaliyotolewa kwenye meseji ambayo mtu amejibu. Hii ina maana kwamba badala ya kuona jibu moja tu, sasa mtumiaji ataweza kuona muktadha mzima wa mazungumzo yaliyotangulia yanayohusiana na meseji hiyo. Kipengele hiki kinatarajiwa kusaidia watumiaji kuelewa kwa urahisi zaidi muktadha wa majibu hasa katika mazungumzo ya vikundi ambapo mazungumzo yanaweza kuwa mengi na kuchanganyika. Hii itapunguza kuchanganyikiwa na kuifanya mazungumzo yawe wazi na rahisi kufuatilia. Hadi sasa, WhatsApp bado inajaribu mtindo huu na imetolewa kwa baadhi ya watumiaji wa toleo la majaribio (beta). Haijatangazwa rasmi lini kipengele hiki kitawekwa kwa watumiaji wote. Mtumiaji anayetaka kujaribu awali anaweza kujiunga na programu ya WhatsApp Beta kupitia duka la programu la simu yake.

Read More
 Marekani Yapiga Marufuku WhatsApp Katika Vifaa vya Serikali

Marekani Yapiga Marufuku WhatsApp Katika Vifaa vya Serikali

Baraza la Wawakilishi la Marekani limetoa amri ya kupiga marufuku matumizi ya programu ya WhatsApp kwenye vifaa vyote vinavyomilikiwa na serikali, likieleza kuwa hatua hiyo inalenga kulinda usalama wa kitaifa, data nyeti, na mawasiliano ya ndani ya serikali. Katika taarifa rasmi iliyotolewa jana, Baraza hilo lilieleza kuwa uamuzi huo umetokana na wasiwasi unaoongezeka kuhusu namna programu hiyo ya ujumbe, inayomilikiwa na kampuni ya Meta, inavyoshughulikia usalama wa taarifa za watumiaji, hasa kwenye mazingira ya kazi za serikali. “Katika nyakati ambapo vitisho vya kiusalama na mashambulizi ya kimtandao vinaongezeka kwa kasi, ni muhimu kwa taasisi za serikali kuchukua tahadhari za hali ya juu kulinda taarifa na mawasiliano ya ndani,” ilisema sehemu ya taarifa ya Baraza hilo. Wataalamu wa usalama wa mitandao wamekuwa wakielezea hofu juu ya matumizi ya programu zinazotegemea mitandao ya kimataifa, wakitahadharisha kuwa huenda mawasiliano ya siri yakavujishwa au kufuatiliwa na wahusika wa nje. Ingawa WhatsApp hutumia teknolojia ya usimbaji wa hali ya juu (end-to-end encryption), Baraza la Wawakilishi limeeleza kuwa haitoshi kuhakikisha usalama kamili katika muktadha wa shughuli za kiserikali. Marufuku hiyo itaanza kutekelezwa mara moja, na wafanyakazi wa serikali wametakiwa kuondoa programu hiyo kutoka kwa simu, tableti na vifaa vingine rasmi vya kazi. Aidha, watakaokaidi agizo hilo watakabiliwa na hatua kali za kinidhamu. WhatsApp na kampuni mama Meta bado hawajatoa tamko rasmi kuhusu hatua hiyo ya Marekani, lakini wachambuzi wanaamini huenda uamuzi huu ukaibua mjadala mpana kuhusu faragha na usalama wa kidijitali, hasa miongoni mwa taasisi za serikali kote duniani. Kwa sasa, Marekani inaungana na mataifa mengine kama India na Ufaransa ambayo tayari yamechukua hatua mbalimbali za kudhibiti matumizi ya programu za mawasiliano katika sekta nyeti za serikali.

Read More
 WhatsApp Yafanya Maboresho Makubwa kwa Mwonekano wa WhatsApp Web

WhatsApp Yafanya Maboresho Makubwa kwa Mwonekano wa WhatsApp Web

WhatsApp imezindua rasmi maboresho mapya ya muonekano wa WhatsApp Web kwa watumiaji wote wanaotumia huduma hiyo kupitia kivinjari cha kompyuta. Maboresho haya yanakusudia kurahisisha matumizi na kufanya uzoefu wa mtumiaji kuwa bora zaidi. Mabadiliko haya ni sehemu ya juhudi za WhatsApp za kuendana na mahitaji ya watumiaji wanaoongeza kutumia huduma ya WhatsApp Web kwa mawasiliano yao ya kila siku. Kwenye toleo jipya la WhatsApp Web, watumiaji wataona muundo ulioboreshwa unaowezesha kupata ujumbe, mazungumzo, na vipengele vingine kwa urahisi zaidi. Mbali na kuboresha muonekano, WhatsApp pia imeongeza kasi na ufanisi wa matumizi, huku ikihakikisha kwamba huduma hiyo inaendeshwa kwa usalama na faragha inayostahili. Watumiaji wa WhatsApp Web sasa wanashauriwa kusasisha kivinjari chao na kufungua tena WhatsApp Web ili kufurahia maboresho haya mapya. Maboresho haya ni hatua nyingine katika mfululizo wa masasisho yanayolenga kuongeza ubora wa huduma za WhatsApp kwa kila aina ya mtumiaji, iwe ni kupitia simu au kompyuta.

Read More
 WhatsApp Imeanza Kuweka Matangazo Sehemu ya Status

WhatsApp Imeanza Kuweka Matangazo Sehemu ya Status

WhatsApp, mojawapo ya huduma maarufu za ujumbe duniani, imetangaza kuanza kuweka matangazo katika sehemu yake ya Status. Hatua hii inalenga kuwapa wateja na biashara fursa zaidi ya kufikia watumiaji wake milioni bilioni kila mwezi kupitia njia hii mpya ya matangazo. Sehemu ya Status ya WhatsApp ni sehemu ambapo watumiaji huweza kushiriki picha, video, na ujumbe unaoisha baada ya masaa 24, sawa na Stories kwenye Instagram au Facebook. Kwa sasa, matangazo haya yataonekana kati ya Status za marafiki na familia, na yatakuwa na alama ya “Ad” ili kutofautisha na maudhui ya kawaida. WhatsApp imeeleza kuwa matangazo haya hayatatumia mazungumzo binafsi ya watumiaji kwa ajili ya kulenga matangazo, hivyo kuhakikisha faragha inahifadhiwa. Kampuni inatarajia kuwa njia hii mpya itasaidia kuongeza mapato na kuimarisha huduma bila malipo kwa watumiaji wake. Watumiaji wanashauriwa kufuatilia mabadiliko haya na kutoa maoni yao ili kuboresha uzoefu wa matumizi ya WhatsApp.

Read More
 Simu Kongwe Zaondolewa WhatsApp Kufuatia Mabadiliko ya Mfumo

Simu Kongwe Zaondolewa WhatsApp Kufuatia Mabadiliko ya Mfumo

Kampuni mama ya WhatsApp, Meta, imetangaza kushusha rasmi kiwango cha chini cha mfumo wa simu unaohitajika ili kuendelea kutumia huduma ya WhatsApp. Kwa sasa, watumiaji wa programu hiyo wanapaswa kuwa na simu zilizo na Android 5 au zaidi, au iOS 15.1 na kuendelea. Simu zinazotumia matoleo ya zamani ya mifumo hiyo ya uendeshaji hazitaweza tena kufikia WhatsApp kuanzia mwezi huu. Hatua hii inalenga kuboresha usalama na utendaji wa programu hiyo, lakini pia inaathiri maelfu ya watumiaji wa simu kongwe. Kwa upande wa iPhone, simu zinazotumia iOS 12.5.6, kama vile iPhone 5s na iPhone 6, zimeanza kuzuiliwa kutumia WhatsApp. Watumiaji wa simu hizo watalazimika kubadilisha simu na kutumia vifaa vinavyowezesha kusasisha hadi mifumo ya kisasa ili kuendelea kuwasiliana kupitia WhatsApp. Meta imeshauri watumiaji kukagua toleo la mfumo wa simu zao kupitia sehemu ya Settings > About Phone au Settings > General > About, na kusasisha mara moja iwapo inawezekana.

Read More
 WhatsApp Yaanza Kupatikana Rasmi kwa Watumiaji wa iPad

WhatsApp Yaanza Kupatikana Rasmi kwa Watumiaji wa iPad

Baada ya kusubiri kwa zaidi ya miaka 15, hatimaye kampuni ya Meta imezindua rasmi toleo la WhatsApp kwa iPad. Kwa muda mrefu, watumiaji wa iPad walikosa njia ya moja kwa moja kutumia WhatsApp, tofauti na watumiaji wa simu na kompyuta ambao walikuwa na app kamili au toleo la WhatsApp Web. Kwa mujibu wa taarifa ya WhatsApp wiki hii, toleo la iPad sasa linapatikana kupitia App Store na linatumia mfumo wa multi-device linking. Watumiaji wanaweza kuunganisha iPad yao na akaunti ya WhatsApp kutoka kwenye simu kwa kuskani QR code, hivyo kuwezesha kusoma na kutuma ujumbe, picha, video, na hata kupiga simu za sauti na video bila hitaji la kuweka laini ya simu kwenye iPad. Uzinduzi huu ni hatua muhimu kwa Meta, kwani washindani kama Telegram na Signal tayari walikuwa na matoleo ya iPad. WhatsApp sasa inapanua wigo wake wa matumizi, na hatua hii inatarajiwa kuongeza idadi ya watumiaji, hasa miongoni mwa waliokuwa wakitegemea njia zisizo rasmi kutumia huduma hiyo kwenye iPad.

Read More
 WhatsApp Kuanza Kuruhusu Watumiaji Kushiriki Status za Wengine (Repost)

WhatsApp Kuanza Kuruhusu Watumiaji Kushiriki Status za Wengine (Repost)

WhatsApp imeanzisha rasmi majaribio ya kipengele kipya kinachowezesha watumiaji kushiriki (repost) Status za wengine moja kwa moja kwenye Status zao binafsi, bila kulazimika kuomba au kupakua maudhui hayo. Kipengele hiki kwa sasa kinapatikana kwa watumiaji wa toleo la majaribio (beta) kwa Android na iOS, na kinatarajiwa kubadilisha namna watumiaji wanavyoshirikiana kwenye jukwaa hilo. Kwa kutumia kipengele hiki, mtumiaji atakuwa na uwezo wa kubofya kitufe cha “Repost” chini ya Status ya rafiki, na kuiweka kwenye Status yake papo hapo. Hii ni habari njema kwa wapenzi wa memes, vichekesho, na ujumbe wa haraka, kwani itaondoa hatua za kuomba au kudownload maudhui ya mtu mwingine. WhatsApp imeweka pia mipangilio ya faragha, ambayo inamruhusu mtumiaji kuchagua nani anaweza kushiriki Status zake.  Hili linahakikisha kuwa faragha inazingatiwa licha ya kipengele hiki kipya kuongeza mwingiliano kati ya watumiaji. Wachambuzi wa teknolojia wanaamini kipengele hiki kitafanya WhatsApp kuwa karibu zaidi na majukwaa ya kijamii kama Instagram Stories au Facebook Stories, huku ikibaki kuwa salama na ya binafsi zaidi. Kipengele hicho kinatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika usambazaji wa maudhui mtandaoni pindi kitakapoanza kutumika kwa wote. Kwa sasa, bado hakuna tarehe rasmi ya uzinduzi wa kipengele hiki kwa watumiaji wote duniani, lakini kwa jinsi majaribio yanavyoendelea vizuri, huenda kikaanza kutumika rasmi katika miezi michache ijayo.

Read More
 Whatsapp imeanza kuzuia Screenshots na Screen-Record

Whatsapp imeanza kuzuia Screenshots na Screen-Record

WhatsApp imeweka mabadiliko kwa kuweka uwezo wa kuzuia mtu asiweze kupiga screenshot katika picha au video ambayo mtu ametuma kwa kutumia option ya “View Once”.  Lakini pia inazuia mtu asiweze ku-screen record! Mabadiliko haya yameanza rasmi na kwa watumiaji wote ambao wanatumia toleo jipya (updated) app. Mtu akipiga screenshot au kurekodi screen picha haionekana na anapewa ujumbe kuwa WhatsApp imezuia screenshot/screen-record. Ikumbukwe bado watu wataweza kutumia simu nyingine kurekodi au kupiga picha hivyo sio mabadiliko ambayo yanaweka uhakika na usalama.

Read More