WIZKID MBIONI KUACHIA ALBUM MPYA

WIZKID MBIONI KUACHIA ALBUM MPYA

Album ijayo ya Wizkid itakuwa ya moto sana. Amethibitishia meneja wa zamani wa Chris Brown, Mike G kupitia ukurasa wake wa Twitter  kwenye picha ambayo amepozi na mkali huyo kutoka nchini Nigeria. Mwezi Oktoba mwaka wa 2021 wakati akiwa kwenye ziara yake ya muziki ‘Made In Lagos’ Wizkid alitangaza kuwa Album yake ya Tano itaitwa “More Love, Less Ego” na itatoka mapema mwaka huu. Mike G kwa sasa anafanya kazi na mastaa wa dunia akiwemo Wizkid, Burna Boy, Young Thug na The Kid Laroi.

Read More
 WIZKID ATAJWA KUWANIA TUZO ZA BILLBOARD MWAKA HUU

WIZKID ATAJWA KUWANIA TUZO ZA BILLBOARD MWAKA HUU

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria Wizkid anaendelea kuchana mbuga Kimataifa mara baada ya kutangazwa kuwania tuzo za Billboard Music Awards kwenye kipengele cha Top R&B Song kupitia REMIX ya wimbo wake ‘Essence’ aliyomshirikisha Justin Bieber pamoja na Tems. Wizkid ambaye ni mshindi wa tuzo tatu za Billboard kupitia wimbo wa Drake ‘One Dance’ kolabo ambayo ilibeba tuzo hizo 3 usiku wa Mei 21, mwaka 2017. Hii inakuwa mara yake ya 8 kuingia kwenye nominations za tuzo hizo maarufu nchini Marekani. Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa Mei 16, huko Marekani, na mwaka huu wasanii The Weeknd, Doja Cat na Justin Bieber wakiongoza kuwa na nominations nyingi zaidi.

Read More
 WIZKID AWAPONGEZA BLACK COFFEE NA ANGELIQUE KIDJO KUSHINDA GRAMMY

WIZKID AWAPONGEZA BLACK COFFEE NA ANGELIQUE KIDJO KUSHINDA GRAMMY

Staa wa muziki kutoka Nigeria Wizkid amewapongeza Waafrika wenzake Angelique Kidjo kutoka Benin na Black Coffee kutoka Afrika Kusini ambao waliibuka washindi kwenye tuzo za 64 za Grammy, ambao alikua akichuana nao kwenye vipengele tofauti tofauti. Wizkid ametoa pongezi hizo kwa wasanii hao kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram huku Wanigeria wakiwa bado na dukuduku kuwa msanii wao (Wizkid) ndio alistahili zaidi kupewa tuzo hizo. “Hongereni sana kwa kuendelea kuling’arisha bara la Afrika. Muziki wa Afrika unakua”, Ameandika WizKid. Ikumbukwe, Wizkid alitajwa kuwania vipengele viwili kwenye tuzo za grammy kupitia vipengele vya Best Global Music Perfomance na ngoma yake ya Essence) na Best Global Music Album na album yake Made In Lagos: Deluxe Edition).

Read More
 STAA WA MUZIKI KUTOKA NIGERIA WIZKID AFIKISHA STREAMS MILIONI 100 BOOMPLAY

STAA WA MUZIKI KUTOKA NIGERIA WIZKID AFIKISHA STREAMS MILIONI 100 BOOMPLAY

Nyota wa muziki kutoka Nigeria Wizkid anaendelea kugonga vichwa vya habari kwa upande wa idadi ya watu wanaofutilia mziki wake kwenye digital platforms mbali mbali za kustream muziki duniani. Wizkid amefanikiwa kufikisha jumla ya STREAMS Milioni 100 kwenye App namba moja ya kusikiliza na kupakua muziki mtandaoni ya Boomplay Music, Hivyo amejiunga rasmi na Golden Club baada ya kupata idadi hiyo ya streams. Lakini pia anaungana na wakali wengine kutoka Nigeria waliofikisha idadi hiyo ya streams kupitia Boomplay ambao ni Davido, Omah Lay na Fire Boy. Utakumbuka wasanii Joeboy na Burna Boy tayari wana streams zaidi ya Milioni 200.

Read More
 DAVIDO NA WIZKID WAZIKA TOFAUTI ZAO BAADA YA KUKUTANA CLUB LAGOS  NA KUKUMBATIANA

DAVIDO NA WIZKID WAZIKA TOFAUTI ZAO BAADA YA KUKUTANA CLUB LAGOS NA KUKUMBATIANA

Wanamuziki wa Nigeria Davido na WizKid ni kama wamemaliza tofauti zao ,mara baada ya kukutana kwenye moja ya club huko jijini Lagos nigeria na kukumbatiana huku wakionekana kuwa na furaha kila mmoja. Wanamuziki hao mara kadhaa wametajwa kuwa kwenye ugomvi, na katika hili wanaongeza idadi ya wanamuziki waliopatana ndani ya mwaka huu baada ya Burna Boy kutangaza kumaliza tofauti zake na Davido. Hata hivyo mashabiki wa muziki nchini Nigeria wameonekana kufurahia hatua ya Davido na Wizkid kumaliza ugomvi wao huku wakiwataka wawili hao kuachia  ngoma ya pamoja.

Read More
 WIZKID AMZAWADI GARI MENEJA WAKE SUNDAY ARE

WIZKID AMZAWADI GARI MENEJA WAKE SUNDAY ARE

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria Wizkid ameufunga mwaka 2021 kwa kujiongezea baraka, amemfanyia surprise meneja wake wa muda mrefu Sunday Are kwa kumpatia zawadi ya gari mpya aina ya Prado. Meneja huyo ameshare video kwenye Instagram kuionesha gari hiyo, Toyota Land Cruiser SUV na kumshukuru Hitmaker huyo wa Essence. Thamani ya gari hiyo ni kati ya shilingi milioni 6.9 hadi milioni 10 za Kenya kulingana na mahali na jinsi ilivyonunuliwa. Hii si mara ya kwanza Sunday anapewa zawadi ya gharama na staa huyo. Mwaka 2019 Wizkid alimpa zawadi saa ya Richard Mille.

Read More
 ESSENCE YA WIZKID YAFIKISHA MAUZO YA PLATINUM MAREKANI

ESSENCE YA WIZKID YAFIKISHA MAUZO YA PLATINUM MAREKANI

Ngoma ya Wizkid akiwa amemshiriki Tems, Essence imefanikiwa kufikisha kiwango cha mauzo ya platinum nchini Marekani. Essence imefanikiwa kuuza jumla ya nakala milioni 1 katika nchini hiyo tangu kuachiwa kwake Oktoba 29, mwaka wa 2020. Lakini pia wimbo huo ulifikisha mauzo ya Gold Septemba 2, mwaka wa 2021 kwa kuuza jumla ya nakala laki 5  nchini Marekani. Wimbo wa Essence  ambao ni wimbo wa nne kwenye album ya ‘Made In Lagos’ iliyotoka Novemba mwaka wa 2020, unakuwa wimbo wa kwanza kutoka Nigeria kuingia kwenye rekodi hiyo nchini Marekani.

Read More
 “MADE IN LAGOS” YAFIKISHA ZAIDI YA STREAMS BILLIONI MOJA

“MADE IN LAGOS” YAFIKISHA ZAIDI YA STREAMS BILLIONI MOJA

Album ya msanii WizKid kutoka Nigeria, “Made in Lagos” Deluxe Edition iliyotoka Agosti 27 mwaka huu yenye hitsong kama Essence Remix, imefanikiwa kufikisha jumla ya streams Bilioni Moja. Made in Lagos” imefikisha jumla ya streams hizo ikiwa ni mjumuisho wa streams zote za (Deluxe Edition) katika Platform mbalimbali za muziki duniani kama Apple Music (millioni 322.75), Spotify (millioni 229.33), Youtube (millioni 227.82), Audiomack (millioni 178.25), Boomplay (millioni 40.17) na Pandora (millioni 20.1) WizKid ambaye kwa sasa yupo nchini Marekani kwenye ziara yake ya kimuziki ya “Made In Lagos Tour”, aliyoianza Septemba 10 mwaka huu, anaendelea pia kufanya vizuri kwa kupata idadi kubwa ya mashabiki kwenye show zake.

Read More