
Mwanamama Kim Kardashian ameripotiwa kuongeza pesa zaidi kwenye ulinzi lakini pia kuimarisha usalama wa watoto wake kufuatia Kanye West kuanika hadharani Jina la shule ambayo watoto wanasoma.
Kanye West alijikuta akifunguka hadharani na kutaja Jina la shule hiyo kwenye mfululizo wa post zake kwenye mitandao ya kijamii wakati akipambana kuwajibu wakosoaji wake kwenye sakata la βWhite Lives Matterβ ambalo lilishika vichwa vya habari kwa kuwakera watu weusi duniani kote.