Mama Anayedai Kuwa Mzazi wa Bahati Akataa Matokeo ya DNA

Mama Anayedai Kuwa Mzazi wa Bahati Akataa Matokeo ya DNA

Mama anayedai kuwa mzazi wa msanii Bahati ameibuka na madai mapya akidai kuwa msanii huyo alihonga madaktari ili kubadilisha matokeo ya vipimo vya DNA. Kupitia video inayosambaa mitandaoni, mama huyo ameonyesha kutoridhishwa kwake na matokeo ya vipimo hivyo yaliyotolewa na maabara, ambayo yalionyesha kuwa hakuna uhusiano wa kibaiolojia kati yake na Bahati. Katika maelezo yake, mwanamama huyo amesema kuwa haamini matokeo ya vipimo vya DNA yalipangwa na kubadilishwa makusudi. Amedai kuwa Bahati ni mwanawe wa kumzaa na kwamba matokeo yaliyotolewa hayawakilishi ukweli. Aidha, amemtuhumu Bahati kwa madai ya kuwapa madaktari fedha ili kubadilisha majibu ya vipimo hivyo ili ionekane kuwa hawana uhusiano wa damu. Kisa hicho kimezua hisia tofauti miongoni mwa mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii, huku baadhi wakionyesha huruma kwa mwanamke huyo na wengine wakisema kuwa ni muhimu kuheshimu matokeo ya kisayansi ya vipimo vya DNA.

Read More
 Matokeo ya DNA Yathibitisha Judith Makokha Sio Mama Mzazi wa Bahati

Matokeo ya DNA Yathibitisha Judith Makokha Sio Mama Mzazi wa Bahati

Matokeo ya kipimo cha vinasaba kati ya mwanamuziki wa Kenya Bahati na mwanamke aliyedai kuwa mama yake mzazi Judith Makokha yametolewa rasmi, yakionyesha kuwa wawili hao hawana uhusiano wa damu. Kwa mujibu wa ripoti ya maabara, uwezekano wa Makokha kuwa mama mzazi wa Bahati ni asilimia sifuri. Ripoti hiyo inaeleza kuwa uchambuzi wa vinasaba uligundua kutokulingana kwa alama kadhaa za kijenetiki, zikiwemo loci D3S1358 na D1S1656, hali iliyowafanya wataalamu kufikia hitimisho kuwa Makokha hawezi kuwa mzazi wa kimaumbile wa msanii huyo. Ikumbukwe Judith Makokha alijitokeza hadharani akidai kuwa ndiye aliyemzaa Bahati na kumwacha katika makao ya watoto yatima mwaka 1993. Madai hayo yalipingwa na Bahati ambaye kwa muda mrefu amekuwa akieleza kuwa mama yake mzazi, Lucia Mueni, alifariki mwaka 1992. Kutokana na mvutano huo wa muda mrefu, pande husika zilikubaliana kufanyiwa kipimo cha DNA ili kubaini ukweli wa madai hayo. Matokeo yaliyotolewa sasa yanathibitisha kuwa hakuna uhusiano wa kimaumbile kati ya Bahati na Judith Makokha.

Read More
 Video ya Bahati Akifunzwa Kuvuta Cigar Yazua Gumzo Mtandaoni

Video ya Bahati Akifunzwa Kuvuta Cigar Yazua Gumzo Mtandaoni

Video inayomuonyesha msanii wa muziki kutoka Kenya, Bahati, akifunzwa namna ya kuvuta cigar imezua gumzo kubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kusambaa mtandaoni. Katika video hiyo ya nyuma ya pazia (behind the scenes) ya utayarishaji wa diss track yake inayojulikana kama “Lost for the Throne,” Bahati anaonekana akielekezwa jinsi ya kushika na kuvuta cigar wakati wakijiandaa kurekodi baadhi ya vipande vya video ya wimbo huo. Hatua hiyo imeibua mjadala miongoni mwa mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii, hasa kutokana na taswira ambayo Bahati amekuwa akiijenga kwa muda mrefu kama msanii mwenye maadili ya Kikristo. Wapo wanaodai kuwa tukio hilo linaenda kinyume na sura ambayo msanii huyo amekuwa akiionyesha kwa mashabiki wake. Hata hivyo, wengine wamejitokeza kumtetea wakisema kuwa ilikuwa ni sehemu tu ya uigizaji na ubunifu wa kisanii kwa ajili ya video ya wimbo huo, hivyo haipaswi kuchukuliwa kama tabia yake ya kawaida nje ya kazi ya muziki.

Read More
 Bahati Awataka Mashabiki Kuwa na Subira Kuhusu Matokeo ya DNA

Bahati Awataka Mashabiki Kuwa na Subira Kuhusu Matokeo ya DNA

Msanii nyota wa muziki, Bahati, amewataka mashabiki wake wawe na subira kufuatia shinikizo walilompa la kutaka atangaze matokeo ya vipimo vya DNA vinavyohusiana na mama mmoja aliyedai kuwa mzazi wake wa kumzaa. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Bahati amesema kuwa suala hilo ni nyeti na linahitaji muda kabla ya kuweka wazi matokeo hayo kwa umma. Amesema kuwa anafahamu hamu ya mashabiki wake kutaka kujua ukweli, lakini akawaomba faragha ya kushughulikia jambo hilo kwa utulivu. Kauli ya Bahati imekuja baada ya kushindwa kutimiza ahadi yake ya kutangaza matokeo hapo jana, licha ya kuthibitisha wiki chache zilizopita kuwa angefanya hivyo Machi 3, kufuatia kukamilika kwa mchakato wa vipimo kati yake na mama aliyedai kuwa mzazi wake wa kumzaa. Hali hii imezua mjadala mkubwa mitandaoni, huku mashabiki wakisubiri kwa hamu kuona mwelekeo wa matokeo hayo na namna yatakavyoweza kuathiri maisha yake binafsi na taswira yake katika muziki.

Read More
 Bahati Ashindwa Kujizuia Baada ya Kukutana na Mwanamke Aliyedai kuwa Mama yake Mzazi

Bahati Ashindwa Kujizuia Baada ya Kukutana na Mwanamke Aliyedai kuwa Mama yake Mzazi

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Bahati, ameshindwa kujizuia baada ya kukutana ana kwa ana na mwanamke aliyedai kuwa ndiye mama yake mzazi mwishoni mwaka 2025. Katika video inayoenea mtandaoni, Bahati ameonekana kuguswa sana na tukio la mwanamke huyo kumkumbatia kwa muda mrefu huku akilia kwa uchungu. Kwenye video hiyo, Mama huyo ameoneka akiomba Mungu msamaha kwa kile alichodai kuwa ni kumpoteza mwanawe kwa miaka mingi, akieleza maumivu aliyoyabeba moyoni kwa kipindi chote hicho. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Bahati amesema amechanganyikiwa na hajui aanzie wapi. Amekiri kuwa na maswali mengi kichwani mwake kuhusu maisha yake ya awali na ukweli wa madai ya mama huyo. Amesema hali hiyo si rahisi kuikubali mara moja, hasa ikizingatiwa historia yake ya kukulia katika mazingira ya changamoto tangu utotoni. Ikumbukwe mwanamke huyo alijitokeza mwishoni mwa mwaka jana akidai kuwa yeye ndiye mama halisi wa Bahati, akieleza kuwa amekuwa akimtafuta kwa muda mrefu bila mafanikio.

Read More
 Bahati na Diana Marua Wazua Tetesi Baada ya Kufuta Picha Zote Instagram

Bahati na Diana Marua Wazua Tetesi Baada ya Kufuta Picha Zote Instagram

Staa wa muziki Bahati na mkewe Diana Marua wamezua gumzo mitandaoni baada ya kubainika kuwa wameacha kufuatana (unfollow) kwenye mtandao wa Instagram. Hatua hiyo imewashangaza mashabiki wao wengi, hasa ikizingatiwa kuwa wawili hao wamekuwa wakionekana kama wanandoa wanaoheshimika zaidi kupitia mitandao ya kijamii. Kinachozidi kuzua maswali ni kwamba kila mmoja wao amefuta picha zote zilizokuwa kwenye kurasa zao za Instagram, huku ukurasa wa Diana Marua ukionekana kuwa mtupu kabisa bila hata picha moja. Hatua hii imewafanya mashabiki na wadau wa burudani kuanza kubashiri huenda kuna jambo zito linaendelea ndani ya ndoa yao. Kwa sasa, macho na masikio ya mashabiki yako kwa wawili hao wakisubiri kauli rasmi itakayoweka wazi ukweli wa kile kinachoendelea.

Read More
 Bahati Ampongeza Jux Kwa Kuiwakilisha Afrika Kimuziki, Azua Tetesi za Wimbo Mpya

Bahati Ampongeza Jux Kwa Kuiwakilisha Afrika Kimuziki, Azua Tetesi za Wimbo Mpya

Staa wa muziki nchini Kenya, Bahati, amempongeza nyota wa Bongo Fleva Jux kwa mafanikio makubwa anayoyapata kimuziki, akisema kuwa ushindi wake ni baraka kwa Afrika na pia chanzo cha shinikizo kwa wasanii wengine kufanya kazi kwa bidii zaidi. Kupitia mitandao ya kijamii, Bahati ameeleza kufurahishwa na jinsi Jux anavyopeperusha bendera ya Afrika katika anga ya kimataifa, akibainisha kuwa mafanikio hayo yanaweka viwango vipya kwenye tasnia ya muziki wa Afrika Mashariki. Hata hivyo, kilichozua gumzo zaidi ni video aliyoposti Bahati akiwa pamoja na Jux katika mazingira yanayofanana na ya harusi. Katika video hiyo, wawili hao wanaonekana wakiwa wamepambika vizuri, hali iliyowafanya mashabiki wengi kuamini kuwa huenda walikuwa wakishoot video ya wimbo wao mpya. Tetesi hizo zilipata nguvu zaidi baada ya caption ya Bahati iliyoambatana na video hiyo, ambapo aliandika maneno yaliyoashiria mashabiki waendelee kusubiri, jambo lililowafanya wengi kuamini kuwa ngoma mpya iko njiani.

Read More
 Bahati Awaomba Mashabiki Ushauri wa Mabadiliko Mwaka wa 2026

Bahati Awaomba Mashabiki Ushauri wa Mabadiliko Mwaka wa 2026

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Bahati, amewashangaza mashabiki wake baada ya kuwaomba hadharani wamsaidie kwa kumpa ushauri wa mambo anayopaswa kubadilisha au kuboresha kuelekea mwaka wa 2026. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Bahati amesema kuwa mwaka mpya unampa nafasi ya kujipima upya kama msanii, mume na baba, huku akisisitiza kuwa maoni ya mashabiki wake yana mchango mkubwa katika safari yake. Msanii huyo, amesema kuwa yuko tayari kusikiliza ukosoaji wa kujenga, iwe ni kuhusu muziki wake, tabia, mawasiliano na mashabiki, au mwelekeo wa maisha kwa ujumla. Bahati amesema atayapitia maoni yote na kuyazingatia kwa makini, akisisitiza kuwa yuko tayari kubadilika pale inapobidi kwa ajili ya familia yake, mashabiki na mustakabali wake kama msanii.

Read More
 Bahati Asema Ana Fedha za Kutosha Kukaa Mwaka Mzima Bila Kufanya Kazi

Bahati Asema Ana Fedha za Kutosha Kukaa Mwaka Mzima Bila Kufanya Kazi

Staa wa muziki kutoka nchini Kenya, Bahati, ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kudai kuwa ana fedha za kutosha kumwezesha kukaa bila kufanya kazi kwa kipindi chote cha mwaka 2026. Kupitia mitandao ya kijamii, Bahati amejigamba kuwa ana fedha za kutosha na kuambatanisha kauli hiyo na kuonesha magari yake ya kifahari aina ya Mercedes-Benz G-Wagon pamoja na Range Rover, huku akisisitiza kuwa mafanikio yake ya kifedha yanamruhusu kuchukua mapumziko marefu bila kuathiri maisha yake. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya msanii huyo kushambuliwa vikali na baadhi ya Wakenya mtandaoni, kufuatia madai yake kuwa yeye ndiye msanii pekee mwenye mafanikio makubwa kuwahi kutokea nchini Kenya. Kauli hiyo iliwakera wengi waliodai kuwa ni ya kujikweza na kuwadharau wasanii wengine waliotoa mchango mkubwa katika tasnia ya muziki.

Read More
 Bahati Ajitangaza Msanii Mwenye Mafanikio Zaidi Kenya

Bahati Ajitangaza Msanii Mwenye Mafanikio Zaidi Kenya

Msanii nyota wa muziki nchini Kenya, Bahati, ametangaza kuwa yeye ndiye msanii mwenye mafanikio makubwa zaidi kuwahi kutokea nchini humo. Bahati ametoa kauli hiyo alipokuwa akiwatakia mashabiki wake sikukuu njema ya Krismasi, akiwa pamoja na mke wake Diana B na watoto wao, akisema safari yake ya muziki imejaa baraka, mafanikio na ushindi mkubwa unaoonekana wazi kupitia maisha na kazi zake. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya msanii huyo kujizawadia gari la kifahari aina ya Range Rover, kama sehemu ya kusherehekea kutimiza miaka 33 tangu kuzaliwa kwake. Kupitia mitandao ya kijamii, Bahati alishiriki picha na video za gari hilo, akisema ni zawadi ya kujithamini na kuthamini juhudi zake binafsi.

Read More
 Bahati Ajizawadia Range Rover Mpya Kusherehekea Miaka 33 ya Kuzaliwa

Bahati Ajizawadia Range Rover Mpya Kusherehekea Miaka 33 ya Kuzaliwa

Staa wa muziki kutoka Kenya, Bahati, amejizawadia gari jipya aina ya Range Rover kama sehemu ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 33. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bahati ameposti picha na ujumbe mzito wa shukrani, akitafakari safari yake ya maisha iliyojaa changamoto na baraka. Bahati ameeleza kuwa anajivunia kuwa na umri wa miaka 33, akiwa baba na mtu aliyebarikiwa kwa njia nyingi. Msanii huyo alikumbuka alikokulia katika makao ya watoto ya ABC Kenya Children’s Home yaliyoko Mathare Slums, ambako aliota siku moja kufikia mafanikio kama anayoyaishi kwa sasa ikiwemo kuwa baba ya familia ya watoto wanne. Bahati amehitimisha ujumbe wake kwa kusema kuwa anajiona mwenye baraka nyingi na mwenye furaha kubwa, akimshukuru Mungu kwa kumfikisha hatua hiyo muhimu ya maisha yake. Hatua ya Bahati kujizawadia Range Rover imepokelewa kwa hisia mseto mitandaoni, huku mashabiki na wadau wa tasnia ya burudani wakimpongeza kwa juhudi, uvumilivu na mafanikio yake, wakimtaja kama mfano wa kuigwa kwa vijana wengi waliokulia katika mazingira magumu lakini wakaendelea kuamini ndoto zao

Read More
 Bahati Akanusha Kutumia Sakata la Mwanamke Aliyedai ni Mamake kuwa Kiki

Bahati Akanusha Kutumia Sakata la Mwanamke Aliyedai ni Mamake kuwa Kiki

Msanii wa muziki nchini Keny, Bahati, amekanusha madai kwamba anatumia sakata la mwanamke aliyejitokeza akidai ni mama yake mzazi kama mbinu ya kujipatia umaarufu mitandaoni. Bahati amesema tukio hilo limemshangaza kwa kuwa halikuwa sehemu ya mipango yake ya kujipatia kiki. Amefafanua kwamba mwanamke huyo amekuwa akimtafuta kwa zaidi ya miaka mitano, na hata aliwahi kuwasiliana na ndugu yake mkubwa bila mafanikio. Msanii huyo, ameeleza kuwa alimwona mwanamke huyo kwa mara ya kwanza kupitia video iliyosambaa mtandaoni, akisema kuwa ingawa baadhi ya mashabiki mitandaoni wanachukulia sakata hilo kama mzaha, kwake binafsi ni jambo lenye uzito. Hata hivyo amesisitiza kuwa hajawahi kupanga au kutumia hali hiyo kama njia ya kujipatia umaarufu, bali analichukulia kama tukio la maisha ambalo limemgusa kwa undani ikizingatiwa kuwa mama yake mzazi alifarikia miaka nyingi iliyopita.

Read More