Weezdom Amkosoa Bahati kwa Kuvaa Mavazi ya Mkewe

Weezdom Amkosoa Bahati kwa Kuvaa Mavazi ya Mkewe

Msanii wa zamani wa muziki wa injili na meneja wa burudani, Weezdom, ameeleza masikitiko yake kuhusu mwenendo wa msanii Bahati, ambaye kwa sasa amegeukia maudhui yenye utata mtandaoni. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram, Weezdom amesema Bahati alikuwa mfano bora wa kuigwa, hasa kwa vijana na familia, na aliwahi kutumia kipaji chake kueneza neno la Mungu kupitia muziki. Lakini sasa anahisi kuwa Bahati amepoteza dira na kusahau msingi wa mafanikio yake. “Sometimes naangalia vitu my mentor, msee mwenye alinifunza Word ya God, vitu anafanya kwa mitandao namhurumia sana. Juu hakuna brand ilishawahi kuwa na influence kubwa kwa wazazi na watoto wadogo zaidi ya huyu jamaa bana!” aliandika Weezdom kwa hisia. Weezdom, ambaye aliwahi kuwa mshirika wa karibu wa Bahati katika huduma ya muziki wa injili, aliongeza kuwa Bahati anapaswa kutafakari upya nafasi yake kama kielelezo kwa vijana na kurejea kwenye msingi wa kiimani uliomuinua kimaisha. Kauli hiyo inakuja baada ya video na picha za Bahati kusambaa mitandaoni zikimwonyesha akiwa amevaa nguo za mkewe, jambo lililoibua maoni mseto kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake. Ujumbe wa Weezdom umechochea mijadala mikubwa mitandaoni, wengi wakijiuliza iwapo Bahati anapaswa kurejea kwenye muziki wa injili au kuendelea na mwelekeo wake wa sasa wa burudani mchanganyiko. Mpaka sasa, Bahati hajatoa tamko lolote rasmi kujibu maoni ya Weezdom, lakini mashabiki wengi wanaendelea kuonyesha maoni yao tofauti kuhusu suala hilo, baadhi wakimtetea na wengine wakimtaka arejee kwenye msingi uliompa umaarufu.

Read More
 Bahati Aingilia Kati Drama ya Mulamwah na Ruth, Atoa Wito wa Amani

Bahati Aingilia Kati Drama ya Mulamwah na Ruth, Atoa Wito wa Amani

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Bahati, ametoa wito wa amani na msamaha kwa wasanii wenzake Mulamwah na Ruth K, akiwataka kuweka tofauti zao binafsi mbali na mitandao ya kijamii kwa ajili ya mustakabali wa mtoto wao. Kupitia ujumbe wa kugusa moyo aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bahati alisema kuwa hajazoea kuingilia mambo ya watu binafsi, lakini hali inayoshuhudiwa kati ya Mulamwah na Ruth imemsikitisha sana kama mzazi na mwanajamii. “Siwezi kuingilia sana mambo ya watu binafsi, lakini sipendezwi kuona familia zikivunjika . Naomba umma tuwaombee vijana hawa wawili, na zaidi ya yote, Mungu arejeshe kile walichopoteza wakati wa sakata hili, aponye mioyo yao na amkinge mtoto asiye na hatia,” aliandika Bahati. Bahati, ambaye pia ni mzazi na mume wa Diana Marua, alisema kuwa ameshindwa kuwapata Mulamwah na Ruth kwa simu, na hivyo kuamua kuwafikia kwa njia ya umma ili kuwataka waepuke kulifanya suala hilo kuwa la hadhara. “Ombi langu kwa wazazi wenzangu Mulamwah na Ruth (kwa sababu siwezi kuwafikia kwa simu)… tafadhali acheni kuanika haya mitandaoni… ni jambo la kusikitisha lakini naamini litakuwa sawa kwa jina la Yesu .” aliongeza. Alihitimisha ujumbe wake kwa maandiko ya Biblia kutoka Yakobo 1:20, akisisitiza umuhimu wa kudhibiti hasira wakati wa migogoro ya kifamilia: “Hasira ya mwanadamu haizai haki ya Mungu,” aliandika Bahati Kauli ya Bahati imepokelewa kwa hisia kali na wafuasi wake, wengi wakimpongeza kwa kuonesha uelewa na huruma, huku wengine wakitumaini kwamba ujumbe huo utakuwa mwanzo wa mazungumzo ya suluhu kati ya wawili hao. Hali ya sintofahamu kati ya Mulamwah na Ruth K imekuwa gumzo mitandaoni hapo jana, huku kila mmoja akitoa maelezo yake kuhusu sababu za kutengana kwao, hali ambayo imewaacha mashabiki wakiwa na maoni tofauti.

Read More
 Bahati Atangaza Ndoa na Diana Marua Mwaka 2026

Bahati Atangaza Ndoa na Diana Marua Mwaka 2026

Msanii nyota wa muziki nchini Kenya, Bahati, amewapa mashabiki wake habari ya kusisimua baada ya kuashiria kuwa hatimaye anapanga kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu, Diana Marua, mwaka ujao. Kupitia ujumbe wa hisia aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Bahati alifichua kuwa mwaka 2026 utakua wa kipekee kwao, kwani wataadhimisha miaka 10 ya kuwa pamoja. Katika chapisho lake, Bahati alimweleza Diana kuwa amekuwa mvumilivu kwa miaka yote, akiahidi kuwa wakati wao wa kusherehekea upendo wao kwa njia ya ndoa umefika. Akitumia hashtagi ya #SikuKuuYaBahati, Bahati alionekana kuelekeza maandalizi ya tukio kubwa ambalo linaweza kuwa harusi yao rasmi. “Mpenzi wangu mrembo @Diana_Marua, najua tumekuwa tukisubiri kwa muda mrefu ndoa yetu. Mwaka ujao tutatimiza miaka 10 pamoja. Najua inaonekana kama ni muda mrefu lakini usiali, #SikuKuuYaBahati itakuwa ya kipekee.” Bahati pia alielezea jinsi harusi ya msanii wa Bongo Fleva kutoka Tanzania, Juma Jux, ilivyomgusa na kumtia moyo kama mwanaume. Akitumia alama ya reli #JP2025, alikiri kuwa harusi hiyo ilimfundisha thamani ya kumpenda na kumheshimu mwanamke.  “#JP2025 imenifundisha jinsi mwanaume anavyopaswa kumthamini na kumuenzi yule anayempenda. Kaka yetu wa Afrika Mashariki, Jux, ametuheshimisha. Hongera sana kaka yangu @Juma_Jux na mrembo @its.priscy. Nathibitisha wazi kuwa mimi ndiye ninayefuata #BD2025.” Baada ya chapisho hilo, mashabiki walimiminika kwenye sehemu ya maoni wakionyesha furaha, wakitoa pongezi na pia kuomba kuhudhuria harusi hiyo. Wengi walieleza kuwa wamekuwa wakisubiri muda mrefu kuona Bahati akimvalisha Diana pete ya ndoa madhabahuni. Ikiwa mipango hiyo itatimia, basi mwaka 2025 huenda ukawa mwaka wa kihistoria kwa Bahati na Diana, na huenda pia tukashuhudia harusi mojawapo ya kifahari zaidi katika burudani ya Afrika Mashariki.

Read More
 Msanii Bahati Alazwa Hospitalini, Asema Ni Mara ya Kwanza Katika Miaka 33

Msanii Bahati Alazwa Hospitalini, Asema Ni Mara ya Kwanza Katika Miaka 33

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Bahati, amelazwa hospitalini baada ya kuugua ghafla, hali iliyomlazimu kuchukua mapumziko kutoka kwa shughuli za mitandao ya kijamii. Kupitia chapisho la hisia kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bahati alieleza kuwa kwa zaidi ya miaka 33 ya maisha yake hajawahi kulazwa hospitalini, lakini kwa sasa ameathirika kiafya kiasi cha kulazimika kupumzika ili kupona. “Kwa miaka 33 sijawahi kulala kwenye kitanda cha hospitali, lakini jioni hii nimejikuta humu. Nachukua mapumziko kutoka mitandao ya kijamii nikiomba uponyaji wa haraka. Afya njema ni baraka,” aliandika, akiambatanisha na alama ya kampeni ya #GoodHealthIsABlessing. Hata hivyo, msanii huyo hakufichua sababu kamili ya kulazwa kwake, lakini mashabiki wake na wafuasi wamejitokeza kwa wingi kumtakia nafuu ya haraka kupitia jumbe mbalimbali za faraja na maombi. Bahati, ambaye pia ni mume wa mwanamitandao maarufu Diana Marua, amekuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya muziki na shughuli za kijamii, na taarifa hizi zimezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa mashabiki wake. Wengi sasa wanasubiri taarifa zaidi kuhusu hali yake ya afya huku wakimtakia nafuu ya haraka na kurejea salama kwenye kazi yake ya muziki na huduma ya kijamii.

Read More
 Bahati Akiri Kudanganya kuhusu Kunyoa Nywele

Bahati Akiri Kudanganya kuhusu Kunyoa Nywele

Msanii mashuhuri wa muziki nchini Kenya, Kevin Bahati, maarufu kama Bahati, amefichua kuwa hakuwahi kunyoa nywele zake aina ya rasta kama ilivyodhaniwa awali. Kupitia chapisho katika ukurasa wake rasmi wa Instagram, Bahati alieleza kuwa picha zilizokuwa zikimuonesha akiwa hana nywele zilihaririwa kwa makusudi, kama sehemu ya mkakati wa kisanaa. Katika ujumbe wake, Bahati aliandika: “Nimechoka kujificha pia editor anasema amechokaaaa kunibadilisha vichwa.” Kauli hiyo imekuwa gumzo mitandaoni, ikiwa ni mara ya kwanza kwa msanii huyo kufichua ukweli kuhusu mabadiliko hayo ya muonekano yaliyozua mijadala miongoni mwa mashabiki na wafuasi wake. Bahati alifafanua kuwa hatua ya kuhariri picha hizo ilikuwa sehemu ya mbinu ya ubunifu ili kuvutia hisia na kuanzisha mwelekeo mpya katika kazi zake za muziki. Amedokeza kuwa hakuwahi kuwa na nia ya kuwadanganya mashabiki wake, bali alitumia mbinu hiyo kama njia ya kuwasilisha maudhui kwa mtazamo tofauti. “Ilikuwa ni njia ya kuwasiliana kisanii. Sikunyowa rasta, ila nilitaka kuanzisha sura mpya ya ubunifu,” alisema kupitia mitandao ya kijamii. Taarifa hiyo imepokelewa kwa hisia mseto. Wakati baadhi ya mashabiki wameonyesha kuelewa na kupongeza ubunifu wa Bahati, wengine wameeleza kusikitishwa na kile walichokiona kuwa ni udanganyifu wa makusudi. Hata hivyo, mjadala huu unaashiria athari kubwa aliyo nayo Bahati katika tasnia ya burudani nchini. Kwa mara nyingine, Bahati ameweza kuvuta hisia za umma kupitia mitandao ya kijamii, akitumia mbinu isiyo ya kawaida kufikisha ujumbe wake. Anaendelea kudhihirisha kuwa katika ulimwengu wa kisasa wa burudani, ubunifu hauishii kwenye muziki pekee, bali pia katika namna ya kujieleza na kuwasiliana na mashabiki.

Read More
 Bahati Awashukuru Mashabiki kwa Kumpongeza kwa Muonekano Mpya Licha ya Video Kuzua Maswali

Bahati Awashukuru Mashabiki kwa Kumpongeza kwa Muonekano Mpya Licha ya Video Kuzua Maswali

Mwanamuziki wa Kenya, Bahati, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuwashukuru mashabiki wake kwa pongezi walizompa kuhusu muonekano wake mpya bila nywele. Kupitia video aliyochapisha kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, Bahati alidai kuwa alinyoa rasta zake kufuatia kichapo cha timu yake ya Arsenal mikononi mwa PSG, katika mechi ya hivi karibuni ya UEFA Champions League. Katika ujumbe wake kwa mashabiki, Bahati alisema: “Nimeanza kujipenda zaidi bila nywele. Nimejifunza kuwa upendo wa kweli huanza na wewe mwenyewe.” Hata hivyo, kilichozua utata ni ubora wa video hiyo, ambayo inaonyesha mabadiliko ya haraka ya uhariri (transition), huku dreadlocks zake zikiendelea kuonekana kwa vipindi tofauti ndani ya video hiyo. Baadhi ya mashabiki walihoji iwapo alinyoa kweli au kama ilikuwa ni kiki ya mitandao. Katika sehemu ya maoni, baadhi ya mashabiki walitoa pongezi wakisema muonekano wake mpya unampendeza na unampa sura ya “umakini mpya”, huku wengine wakitilia shaka ukweli wa madai yake. “Bahati hata kama ni kiki, umetuburudisha. Ila tuambie ukweli – hizo rasta bado zipo ama?” aliandika mmoja wa mashabiki. Muimbaji huyo, anayejulikana kwa kubadili mitindo ya maisha hadharani, ameendelea kuvutia vichwa vya habari kwa sababu mbalimbali kuanzia maisha ya ndoa, siasa, hadi mitindo ya uvaaji. Sasa, inaonekana hata nywele zimeingia kwenye orodha ya vitu vinavyoleta mjadala. Hadi sasa, Bahati hajatoa kauli rasmi kuhusu video hiyo au kama kweli alinyoa, lakini haijazuia mashabiki wake kuendelea kutoa maoni mseto kati ya wanaomsifu na wanaohoji ukweli wa mabadiliko yake

Read More
 Willy Paul akosolewa kwa kutumia Kshs millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake

Willy Paul akosolewa kwa kutumia Kshs millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake

Staa wa muziki nchini Kenya Willy Paul anazidi kupata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki mbali mbali wa muziki baada ya msanii huyo kuweka wazi kuwa alitumia kiasi cha shillingi millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake mpya ‘Keki’ aliyomshirikisha Bahati. Kupitia post aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram akijinadi kutumia kiasi hicho cha fedha kwenye uandaaji wa video ya ngoma hiyo, baadhi ya mashabiki walioachia maoni yao kwenye chapisho hilo wameonekana kutofurahia viwango alivyoonesha kwenye nyimbo alizoziachia rasmi Januari 31 ambazo ni Keki pamoja na Paah. Kulingana na kauli za mashabiki, licha ya Willy Paul kutumia nguvu nyingi kutangaza ujio wa kazi hizo, alifeli kwenye suala la uandishi wa nyimbo wakihoji kuwa msanii ameishiwa na ubunifu wa kutoa nyimbo za kuvutia. Aidha wamempa changamoto kuwatafuta waandishi wazuri wa nyimbo na kuwalipa ili waweze kumuandikia nyimbo ambazo zina maudhui ya kuburudisha jamii sambamba na kuelimisha. Katika hatua nyingine wamemshauri kubadilisha prodyuza anayetayarisha kazi zake za muziki kutokana na kukosa ubunifu wa kuandaa nyimbo zinazoendana na nyakati zilizopo. Willy Paul ambaye yupo mbioni kuandaa tamasha lake muziki mnamo Februari 14 mwaka huu amepokea ukosoaji mkubwa sio tu kutoka kwa mashabiki bali pia kutoka kwa maprodyuza wa muziki nchini, wa hivi punde akiwa ni prodyuza Vinc on The Beat ambaye ameonekana kutoridhishwa na kiwango cha msanii huyo baada ya kuachia nyimbo mbili kwa pamoja alizomshirikisha msanii Bahati ambaye ni hasimu wake wa muda mrefu kwenye muziki.

Read More
 Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Wakati bado Bahati anaendelea kufanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Nowe Sweety,’ ameonyesha kuwa hataki kulaza damu kuhusu muziki,ameonekana ujio wa kazi yake mpya na msanii wa BongoFleva Harmonize. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bahati amepost picha akiwa na Harmonize na kuandika ‘2023 are You Ready for Us??? Brother  @Harmonize_tz ‘ na Harmonize akajibu kwa kuandika ‘SEND IT BRO I HAVE ONLY ONE WATSP NUMBER LOVE YOU NO MARA WAA !!! GETO BOYS ‘. Iwapo Bahati atafanikiwa kuachia wimbo wake na Harmonize atakuwa ameongeza orodha ya wasanii wa Bongoflava aliofanya nao kazi ikizingatiwa kuwa ana kazi ya pamoja na  Rayvanny, Mbosso na Aslay.

Read More
 Diana B ashindwa kuficha hisia zake kwa mume wake Bahati

Diana B ashindwa kuficha hisia zake kwa mume wake Bahati

Mwanamitandao aliyegeukia muziki nchini Diana B ameamua kuwapa somo wanawake wa Kenya jinsi ya kuwaonyesha upendo wapenzi zao. Mama huyo wa watoto watatu ameshea video hii kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa anamlisha mume wake Bahati ambaye kwa sasa anaumwa. Kwenye posti yake hiyo ameandika ujumbe mzito wa mahaba kwenda kwa mume wake huyo ambaye alionekana kudeka na kitendo hicho huku akimhakikishia kumpenda kwa shida na raha. “In Sickness and in Good Health, Mapenzi Tight kama kifuniko ya gas “, Aliandika. Hata hivyo watumiaji wa mitandao ya kijamii wameonekana kukoshwa na upendo wa wawili hao huku wengi wakiahapa kufuta nyayo zao kwa ajili ya kuboresha mahusiano yao. “Mapenzi wewe any time I pass through dee and bahaa…. I feel I need a man in my life… 2023 wewe lazima mr right akuwe nimechokaa kuangalia ya wenyewe,” Mtumiaji mmoja wa mitandao ya kijamii aliandika.

Read More
 Weezdom akiri kupatwa na msongo wa mawazo kisa Bahati

Weezdom akiri kupatwa na msongo wa mawazo kisa Bahati

Msanii Weezdom amefunguka kupatwa na msongo wa mawazo baada ya kuachana na aliyekuwa bosi wake chini ya label ya EMB Records, Bahati. Kwenye mahojiano na Podcast ya EMM, amesema tangu uhusiano wake na Bahati kuingiwa na ukungu, ilikuwa vigumu kwake kujikimu kimaisha jambo lilimpelekea kuchukua maamuzi magumu na kuanza kubugua pombe kupindukia kama njia ya kukimbia changomoto za maisha. Msanii huyo amesema ulevi ulimfanya kupoteza mweelekeo kiasi cha kusahau kufanya muziki. Hata hivyo amesema anamshukuru mwenyezi Mungu kwa kumtoa kwenye tatizo la ulevi baada ya wasamaria wema kujitokeza na kumsaidia kuondokana na matumizi ya pombe.

Read More
 Bahati akoshwa na wimbo wa Dullah Makabila, “Pita Huku”

Bahati akoshwa na wimbo wa Dullah Makabila, “Pita Huku”

Mwimbaji nyota wa muziki toka Kenya, Bahati ameonyesha kukoshwa na ubunifu alioutumia staa wa Singeli nchini, msanii Dulla Makabila kwenye video ya wimbo wake mpya Pita Huku ulioibua mijadala juu ya mengi kufuatia yaliyo zungumziwa kwenye wimbo huo. Akiacha koment kwenye video hiyo katika mtandao wa YouTube, ujumbe wa Bahati unasomeka, “Huu ni Ubunifu Kaka Yangu. Hongera kwa Muziki mzuri”. Mbali na Bahati pia na wengine wengi wameacha komenti zao wakiusifia ubunifu uliofanywa kwenye kazi hiyo. Wimbo wa “Pita Huku” ambao umetoka Jumatatu ya wiki hii umefanikiwa kupata mapokezi makubwa kutoka kwa wadau mbalimbali wa muziki pamoja na mashabiki kwa ujumla.

Read More
 Bahati adai wakosoaji wake mtandaoni wanampa nguvu ya kutia bidii kimuziki

Bahati adai wakosoaji wake mtandaoni wanampa nguvu ya kutia bidii kimuziki

Mwanamuziki kutoka Kenya Bahati amedai kwamba hana muda wa kuwajibu wanaomkosoa mtandaoni. Hitmaker huyo wa Adhiambo amewaambia watesi wake kuwa chuki anayoipata kwenye mitandao ya kijamii inampa changamoto ya kutia bidii kwenye kazi zake za muziki. “Guys thank you so much for your support. Like we wouldn’t be here without you without your love, without your criticism, negativity, we take them in”, Aliandika Instagram. Bahati alisema hayo alipokuwa akizindua tuzo ya Golden Plaque aliyotunukiwa na mtandao wa YouTube kwa ajili ya kupata wafutialiaji (Subscribers) milioni moja. Bahati na mke wake Diana B wamekuwa wakikosolewa mitandaoni mwaka mzima kwa matukio ambayo wamekuwa wakijihusisha nayo na hawajaathirika kwa namna yeyote kwenye shughuli zao.

Read More