Bahati Awahimiza Wanaume Kuachia Wake Zao Mali Ndoa Inapovunjika

Bahati Awahimiza Wanaume Kuachia Wake Zao Mali Ndoa Inapovunjika

Msanii wa muziki wa Kenya, Bahati, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kuwataka wanaume waachie wake zao mali na kila kitu iwapo wataachana au kupeana talaka. Akizungumza katika mahojiano yaliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Bahati amesisitiza kuwa amani ya moyo na kuanza upya ni jambo la maana zaidi kuliko kushikilia mali au vitu vya kidunia. Kwa mujibu wa msanii huyo, ni bora mwanaume aondoke mikono mitupu lakini akiwa na utulivu wa nafsi, kuliko kuingia kwenye malumbano yasiyoisha kuhusu mgawanyo wa mali. Bahati, ambaye mara nyingi huzungumza kwa ujasiri kuhusu masuala ya ndoa na mahusiano, amesema kuwa wanaume wanaojikuta wakipigania mali huishia kuchoshwa kiakili na kifedha. Hata hivyo amewashauri badala yake wajikite katika kujijenga upya na kusonga mbele. Kauli hiyo imezua maoni tofauti miongoni mwa mashabiki. Baadhi wamepongeza msanii huyo kwa kuhimiza amani na ukomavu, huku wengine wakisema wanaume nao wanastahili haki na si sahihi kuondoka bila chochote walichokifanyia kazi.

Read More
 Bahati Awatolea Uvivu Wasanii Wanaomtukana Diana B kwa Akaunti Bandia

Bahati Awatolea Uvivu Wasanii Wanaomtukana Diana B kwa Akaunti Bandia

Msanii wa Kenya Bahati ameibuka na kuwatolea uvivu wasanii wanaomtukana mkewe, Diana Marua, kupitia akaunti bandia, akisema wanapoteza muda badala ya kuangazia kazi zao. Kupitia Instagram, Bahati, ameonekana kuguswa na matusi anayopokea Diana, akiwashambulia wanaoendesha chuki hizo kwa kusema kwamba badala ya kutumia nguvu kumshusha Diana, wanapaswa kumuomba ushirikiano wa kimuziki. Bosi huyo wa EMB Records amesisitiza kuwa mafanikio ya mkewe hayawezi kuzimwa na chuki, akiwataka wapinzani wake kubadilisha mbinu. Hii inakuja baada ya Diana kuachia wimbo wake mpya “Bibi ya Tajiri” ambao umeibua gumzo mitandaoni na kupata mapokezi makubwa. Video ya wimbo huo tayari imepata zaidi ya views laki nane ndani ya siku tano pekee tangu kuachiwa, hali inayoonesha kupokelewa vizuri na mashabiki licha ya ukosoaji.

Read More
 Bahati Awajibu Wakosoaji Kuhusu Kuonyesha Utajiri

Bahati Awajibu Wakosoaji Kuhusu Kuonyesha Utajiri

Msanii kutoka Kenya, Bahati, ameibuka na kuwatolea uvivu wakosoaji wanaomshutumu kwa tabia yake ya kuonyesha mali na maisha ya kifahari kupitia mitandao ya kijamii. Kwa mujibu wa msanii huyo, hakuna tatizo lolote katika kuonyesha mafanikio kwani ameyapata kupitia juhudi kubwa na bidii aliyoweka kwa muda mrefu. Anasisitiza kuwa kila mtu ana uhuru wa kuishi maisha anayoyataka na kwamba mafanikio yake ni kielelezo cha kazi ngumu, uvumilivu na imani. Bahati ameendelea kusisitiza kuwa ataendelea kufurahia maisha na kutumia jukwaa lake kuonyesha baraka alizopewa na Mungu, sambamba na mipango ya miradi mikubwa ya muziki na biashara anayotarajia kuzindua siku za usoni. Katika sikiu za hivi karibuni, Bahati amekuwa gumzo baada ya kushiriki picha na video akionekana na fedha taslimu, magari ya kifahari na maisha ya kifamilia yenye mvuto.

Read More
 Bahati Amchana Mariga, Asema Binti Yake Ni Maarufu Zaidi

Bahati Amchana Mariga, Asema Binti Yake Ni Maarufu Zaidi

Mwanamuziki Bahati amemchana bila huruma Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka Nchini (FKF), McDonald Mariga, akidai kwamba hana jina kubwa la kutumiwa kama chanzo cha kiki. Bahati amesema anamuheshimu Mariga kama gwiji wa soka, lakini akashangazwa na madai kwamba anatafuta umaarufu kupitia jina lake. Amesisitiza kuwa hata binti yake wa mwisho, Malaika, ana umaarufu mkubwa zaidi ukilinganisha na Mariga. Msanii huyo pia ameongeza kuwa kulikuwa na hujuma nyingi dhidi yake kufanikisha mchakato wa kutoa ahadi yake ya shillingi millioni moja kwa Hatambee stars. Kwa mujibu wa maneno yake, waliopanga wanajua ukweli. Kauli hizo zimezua gumzo kubwa, huku baadhi ya mashabiki wakimtetea kwa kusema ana haki ya kulinda heshima yake, na wengine wakimtaka aendelee kuheshimu wachezaji waliowahi kuitumikia Kenya.

Read More
 Bahati Amchana Fred Arocho Kufuatia Sakata la Mchango kwa Harambee Stars

Bahati Amchana Fred Arocho Kufuatia Sakata la Mchango kwa Harambee Stars

Msanii aliyegeukia siasa, Bahati, amemtolea uvivu bila huruma mtangazaji wa Radio 47, Fred Arocho, kufuatia kauli za kumkosoa kwa kuchelewa kutimiza ahadi yake ya kutoa shilingi milioni moja kwa Harambee Stars. Kupitia Instagram, Bahati amejigamba kuwa ana uwezo mkubwa kifedha na hata akitaka anaweza kumpigia mmiliki wa Radio 47 sasa hivi na kununua kituo hicho. Amesema pia yuko tayari kumweka mke wake, Diana Marua, kama boss wa kituo hicho cha redio ambacho Arocho hufanyia kazi, akisisitiza kwamba pesa kwake si tatizo. Haikuishia hapo amejinasibu kuhusu utajiri wake, kwa kusema kwamba kwa wiki moja hutumia shilingi milioni tatu, na hata baada ya mwaka mmoja bila kutoa wimbo mpya bado anaendelea kustawi kifedha. Hitmaker huyo wa Pete yangu, amefafanua kuwa kuchelewa kutoa mchango wake hakumaanishi hana nia ya kusaidia. Ameeleza kwamba alikuwa amejiandaa kwa muda wa wiki nzima kuandaa sherehe kubwa ya kuzaliwa kwa mtoto wake, hafla ambayo hakutaka kuiahirisha kwa ajili ya kutoa mchango huo. Hata hivyo, Bahati amelalamika kwamba hata pale alipokuwa tayari kuwasilisha mchango wake kwa timu ya taifa, hakukuwa na mtu aliyejitokeza rasmi kupokea, akimlaumu kiungo wa zamani wa Harambee Stars McDonald Mariga kwa kutopokea simu zake. Kauli ya Bahati inakuja wiki moja baada ya, Arocho kueleza kutoridhishwa na ahadi ya msanii huyo kwa timu ya taifa akisema kwamba mashabiki na wachezaji wa Harambee Stars walikuwa wakisubiri kwa matumaini makubwa msaada huo, na kuchelewa kwake kumeonekana kama njia ya kujitafutia kiki.

Read More
 Diana Bahati Aonyesha Utajiri wake Wakati Mumewe Akikumbwa na Kashfa

Diana Bahati Aonyesha Utajiri wake Wakati Mumewe Akikumbwa na Kashfa

Mke wa msanii Bahati, Diana Marua maarufu kama Diana B, amewajibu kimkakati wanaozidi kumbeza mume wake Bahati ambaye anahusishwa na kashfa ya kushindwa kutimiza ahadi yake ya kutoa KSh1 milioni kwa timu ya taifa, Harambee Stars. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diana alionekana akijivunia shopping ya mwezi mmoja iliyogharimu takribani KSh160,000. Bidhaa alizonunua zilijumuisha vyakula, bidhaa za nyumbani na mahitaji mengine ya familia yake. Hata hivyo, kilichowashangaza wengi ni pale alipoweka wazi wingi wa pesa taslimu alizokuwa nazo nyumbani. Diana alionekana akishika mirundo ya noti za KSh1,000, ambazo alidai zinafikia jumla ya KSh2 milioni. Wakati mashabiki wengine wakivutiwa na maisha ya kifahari anayoyaonesha, wengi walishangaa hatua yake ya kuonyesha kiasi kikubwa cha fedha hadharani, hasa ikizingatiwa kwamba Bahati anatupiwa lawama kwa kukosa kutimiza ahadi yake ya kifedha kwa wachezaji wa Harambee Stars baada ya ushindi wao mkubwa kwenye mashindano ya CHAN 2024. Mashabiki mtandaoni wamehoji uhalisia wa pesa hizo, wengine wakisema huenda ilikuwa njia ya Diana kutafuta kiki na kutetea hadhi ya kifamilia wakati jina la Bahati linatikiswa na shinikizo la mashabiki na wanamichezo.

Read More
 Bahati Ashindwa Kutimiza Ahadi ya Ksh 1 Milioni kwa Harambee Stars

Bahati Ashindwa Kutimiza Ahadi ya Ksh 1 Milioni kwa Harambee Stars

Staa wa muziki, Bahati, amejipata kwenye lawama baada ya kushindwa kutimiza ahadi yake ya kutoa shilingi milioni moja kwa wachezaji wa Harambee Stars kufuatia ushindi wao dhidi ya Morocco kwenye michuano ya CHAN 2024. Katika mahojiano, baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa wamefichua kuwa fedha walizopokea zilikuwa zawadi kutoka kwa Rais William Ruto, na siyo kutoka kwa Bahati kama ilivyokuwa imetangazwa awali. Wiki iliyopita, msanii mwenzake Willy Paul alimkosoa vikali Bahati akimtaka atimize ahadi yake kwa timu hiyo, hatua iliyomlazimu Bahati kujitokeza na kujitetea. Alidai kuwa hakuweza kukamilisha ahadi hiyo kwa sababu sheria za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) zilimzuia kufika kambini kuonana moja kwa moja na wachezaji. Hata hivyo, mashabiki na wadau wa soka wameendelea kumtupia lawama wakimtaka awe na uwazi na uadilifu katika kutoa ahadi zake, hasa pale zinapohusiana na masuala ya taifa.

Read More
 Weezdom Amkosoa Bahati kwa Kuvaa Mavazi ya Mkewe

Weezdom Amkosoa Bahati kwa Kuvaa Mavazi ya Mkewe

Msanii wa zamani wa muziki wa injili na meneja wa burudani, Weezdom, ameeleza masikitiko yake kuhusu mwenendo wa msanii Bahati, ambaye kwa sasa amegeukia maudhui yenye utata mtandaoni. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram, Weezdom amesema Bahati alikuwa mfano bora wa kuigwa, hasa kwa vijana na familia, na aliwahi kutumia kipaji chake kueneza neno la Mungu kupitia muziki. Lakini sasa anahisi kuwa Bahati amepoteza dira na kusahau msingi wa mafanikio yake. “Sometimes naangalia vitu my mentor, msee mwenye alinifunza Word ya God, vitu anafanya kwa mitandao namhurumia sana. Juu hakuna brand ilishawahi kuwa na influence kubwa kwa wazazi na watoto wadogo zaidi ya huyu jamaa bana!” aliandika Weezdom kwa hisia. Weezdom, ambaye aliwahi kuwa mshirika wa karibu wa Bahati katika huduma ya muziki wa injili, aliongeza kuwa Bahati anapaswa kutafakari upya nafasi yake kama kielelezo kwa vijana na kurejea kwenye msingi wa kiimani uliomuinua kimaisha. Kauli hiyo inakuja baada ya video na picha za Bahati kusambaa mitandaoni zikimwonyesha akiwa amevaa nguo za mkewe, jambo lililoibua maoni mseto kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake. Ujumbe wa Weezdom umechochea mijadala mikubwa mitandaoni, wengi wakijiuliza iwapo Bahati anapaswa kurejea kwenye muziki wa injili au kuendelea na mwelekeo wake wa sasa wa burudani mchanganyiko. Mpaka sasa, Bahati hajatoa tamko lolote rasmi kujibu maoni ya Weezdom, lakini mashabiki wengi wanaendelea kuonyesha maoni yao tofauti kuhusu suala hilo, baadhi wakimtetea na wengine wakimtaka arejee kwenye msingi uliompa umaarufu.

Read More
 Bahati Aingilia Kati Drama ya Mulamwah na Ruth, Atoa Wito wa Amani

Bahati Aingilia Kati Drama ya Mulamwah na Ruth, Atoa Wito wa Amani

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Bahati, ametoa wito wa amani na msamaha kwa wasanii wenzake Mulamwah na Ruth K, akiwataka kuweka tofauti zao binafsi mbali na mitandao ya kijamii kwa ajili ya mustakabali wa mtoto wao. Kupitia ujumbe wa kugusa moyo aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bahati alisema kuwa hajazoea kuingilia mambo ya watu binafsi, lakini hali inayoshuhudiwa kati ya Mulamwah na Ruth imemsikitisha sana kama mzazi na mwanajamii. “Siwezi kuingilia sana mambo ya watu binafsi, lakini sipendezwi kuona familia zikivunjika . Naomba umma tuwaombee vijana hawa wawili, na zaidi ya yote, Mungu arejeshe kile walichopoteza wakati wa sakata hili, aponye mioyo yao na amkinge mtoto asiye na hatia,” aliandika Bahati. Bahati, ambaye pia ni mzazi na mume wa Diana Marua, alisema kuwa ameshindwa kuwapata Mulamwah na Ruth kwa simu, na hivyo kuamua kuwafikia kwa njia ya umma ili kuwataka waepuke kulifanya suala hilo kuwa la hadhara. “Ombi langu kwa wazazi wenzangu Mulamwah na Ruth (kwa sababu siwezi kuwafikia kwa simu)… tafadhali acheni kuanika haya mitandaoni… ni jambo la kusikitisha lakini naamini litakuwa sawa kwa jina la Yesu .” aliongeza. Alihitimisha ujumbe wake kwa maandiko ya Biblia kutoka Yakobo 1:20, akisisitiza umuhimu wa kudhibiti hasira wakati wa migogoro ya kifamilia: “Hasira ya mwanadamu haizai haki ya Mungu,” aliandika Bahati Kauli ya Bahati imepokelewa kwa hisia kali na wafuasi wake, wengi wakimpongeza kwa kuonesha uelewa na huruma, huku wengine wakitumaini kwamba ujumbe huo utakuwa mwanzo wa mazungumzo ya suluhu kati ya wawili hao. Hali ya sintofahamu kati ya Mulamwah na Ruth K imekuwa gumzo mitandaoni hapo jana, huku kila mmoja akitoa maelezo yake kuhusu sababu za kutengana kwao, hali ambayo imewaacha mashabiki wakiwa na maoni tofauti.

Read More
 Bahati Atangaza Ndoa na Diana Marua Mwaka 2026

Bahati Atangaza Ndoa na Diana Marua Mwaka 2026

Msanii nyota wa muziki nchini Kenya, Bahati, amewapa mashabiki wake habari ya kusisimua baada ya kuashiria kuwa hatimaye anapanga kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu, Diana Marua, mwaka ujao. Kupitia ujumbe wa hisia aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Bahati alifichua kuwa mwaka 2026 utakua wa kipekee kwao, kwani wataadhimisha miaka 10 ya kuwa pamoja. Katika chapisho lake, Bahati alimweleza Diana kuwa amekuwa mvumilivu kwa miaka yote, akiahidi kuwa wakati wao wa kusherehekea upendo wao kwa njia ya ndoa umefika. Akitumia hashtagi ya #SikuKuuYaBahati, Bahati alionekana kuelekeza maandalizi ya tukio kubwa ambalo linaweza kuwa harusi yao rasmi. “Mpenzi wangu mrembo @Diana_Marua, najua tumekuwa tukisubiri kwa muda mrefu ndoa yetu. Mwaka ujao tutatimiza miaka 10 pamoja. Najua inaonekana kama ni muda mrefu lakini usiali, #SikuKuuYaBahati itakuwa ya kipekee.” Bahati pia alielezea jinsi harusi ya msanii wa Bongo Fleva kutoka Tanzania, Juma Jux, ilivyomgusa na kumtia moyo kama mwanaume. Akitumia alama ya reli #JP2025, alikiri kuwa harusi hiyo ilimfundisha thamani ya kumpenda na kumheshimu mwanamke.  “#JP2025 imenifundisha jinsi mwanaume anavyopaswa kumthamini na kumuenzi yule anayempenda. Kaka yetu wa Afrika Mashariki, Jux, ametuheshimisha. Hongera sana kaka yangu @Juma_Jux na mrembo @its.priscy. Nathibitisha wazi kuwa mimi ndiye ninayefuata #BD2025.” Baada ya chapisho hilo, mashabiki walimiminika kwenye sehemu ya maoni wakionyesha furaha, wakitoa pongezi na pia kuomba kuhudhuria harusi hiyo. Wengi walieleza kuwa wamekuwa wakisubiri muda mrefu kuona Bahati akimvalisha Diana pete ya ndoa madhabahuni. Ikiwa mipango hiyo itatimia, basi mwaka 2025 huenda ukawa mwaka wa kihistoria kwa Bahati na Diana, na huenda pia tukashuhudia harusi mojawapo ya kifahari zaidi katika burudani ya Afrika Mashariki.

Read More
 Msanii Bahati Alazwa Hospitalini, Asema Ni Mara ya Kwanza Katika Miaka 33

Msanii Bahati Alazwa Hospitalini, Asema Ni Mara ya Kwanza Katika Miaka 33

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Bahati, amelazwa hospitalini baada ya kuugua ghafla, hali iliyomlazimu kuchukua mapumziko kutoka kwa shughuli za mitandao ya kijamii. Kupitia chapisho la hisia kwenye ukurasa wake wa Instagram, Bahati alieleza kuwa kwa zaidi ya miaka 33 ya maisha yake hajawahi kulazwa hospitalini, lakini kwa sasa ameathirika kiafya kiasi cha kulazimika kupumzika ili kupona. “Kwa miaka 33 sijawahi kulala kwenye kitanda cha hospitali, lakini jioni hii nimejikuta humu. Nachukua mapumziko kutoka mitandao ya kijamii nikiomba uponyaji wa haraka. Afya njema ni baraka,” aliandika, akiambatanisha na alama ya kampeni ya #GoodHealthIsABlessing. Hata hivyo, msanii huyo hakufichua sababu kamili ya kulazwa kwake, lakini mashabiki wake na wafuasi wamejitokeza kwa wingi kumtakia nafuu ya haraka kupitia jumbe mbalimbali za faraja na maombi. Bahati, ambaye pia ni mume wa mwanamitandao maarufu Diana Marua, amekuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya muziki na shughuli za kijamii, na taarifa hizi zimezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa mashabiki wake. Wengi sasa wanasubiri taarifa zaidi kuhusu hali yake ya afya huku wakimtakia nafuu ya haraka na kurejea salama kwenye kazi yake ya muziki na huduma ya kijamii.

Read More
 Bahati Akiri Kudanganya kuhusu Kunyoa Nywele

Bahati Akiri Kudanganya kuhusu Kunyoa Nywele

Msanii mashuhuri wa muziki nchini Kenya, Kevin Bahati, maarufu kama Bahati, amefichua kuwa hakuwahi kunyoa nywele zake aina ya rasta kama ilivyodhaniwa awali. Kupitia chapisho katika ukurasa wake rasmi wa Instagram, Bahati alieleza kuwa picha zilizokuwa zikimuonesha akiwa hana nywele zilihaririwa kwa makusudi, kama sehemu ya mkakati wa kisanaa. Katika ujumbe wake, Bahati aliandika: “Nimechoka kujificha pia editor anasema amechokaaaa kunibadilisha vichwa.” Kauli hiyo imekuwa gumzo mitandaoni, ikiwa ni mara ya kwanza kwa msanii huyo kufichua ukweli kuhusu mabadiliko hayo ya muonekano yaliyozua mijadala miongoni mwa mashabiki na wafuasi wake. Bahati alifafanua kuwa hatua ya kuhariri picha hizo ilikuwa sehemu ya mbinu ya ubunifu ili kuvutia hisia na kuanzisha mwelekeo mpya katika kazi zake za muziki. Amedokeza kuwa hakuwahi kuwa na nia ya kuwadanganya mashabiki wake, bali alitumia mbinu hiyo kama njia ya kuwasilisha maudhui kwa mtazamo tofauti. “Ilikuwa ni njia ya kuwasiliana kisanii. Sikunyowa rasta, ila nilitaka kuanzisha sura mpya ya ubunifu,” alisema kupitia mitandao ya kijamii. Taarifa hiyo imepokelewa kwa hisia mseto. Wakati baadhi ya mashabiki wameonyesha kuelewa na kupongeza ubunifu wa Bahati, wengine wameeleza kusikitishwa na kile walichokiona kuwa ni udanganyifu wa makusudi. Hata hivyo, mjadala huu unaashiria athari kubwa aliyo nayo Bahati katika tasnia ya burudani nchini. Kwa mara nyingine, Bahati ameweza kuvuta hisia za umma kupitia mitandao ya kijamii, akitumia mbinu isiyo ya kawaida kufikisha ujumbe wake. Anaendelea kudhihirisha kuwa katika ulimwengu wa kisasa wa burudani, ubunifu hauishii kwenye muziki pekee, bali pia katika namna ya kujieleza na kuwasiliana na mashabiki.

Read More