Mama Anayedai Kuwa Mzazi wa Bahati Akataa Matokeo ya DNA
Mama anayedai kuwa mzazi wa msanii Bahati ameibuka na madai mapya akidai kuwa msanii huyo alihonga madaktari ili kubadilisha matokeo ya vipimo vya DNA. Kupitia video inayosambaa mitandaoni, mama huyo ameonyesha kutoridhishwa kwake na matokeo ya vipimo hivyo yaliyotolewa na maabara, ambayo yalionyesha kuwa hakuna uhusiano wa kibaiolojia kati yake na Bahati. Katika maelezo yake, mwanamama huyo amesema kuwa haamini matokeo ya vipimo vya DNA yalipangwa na kubadilishwa makusudi. Amedai kuwa Bahati ni mwanawe wa kumzaa na kwamba matokeo yaliyotolewa hayawakilishi ukweli. Aidha, amemtuhumu Bahati kwa madai ya kuwapa madaktari fedha ili kubadilisha majibu ya vipimo hivyo ili ionekane kuwa hawana uhusiano wa damu. Kisa hicho kimezua hisia tofauti miongoni mwa mashabiki na watumiaji wa mitandao ya kijamii, huku baadhi wakionyesha huruma kwa mwanamke huyo na wengine wakisema kuwa ni muhimu kuheshimu matokeo ya kisayansi ya vipimo vya DNA.
Read More