Bahati Akanusha Kutumia Sakata la Mwanamke Aliyedai ni Mamake kuwa Kiki

Bahati Akanusha Kutumia Sakata la Mwanamke Aliyedai ni Mamake kuwa Kiki

Msanii wa muziki nchini Keny, Bahati, amekanusha madai kwamba anatumia sakata la mwanamke aliyejitokeza akidai ni mama yake mzazi kama mbinu ya kujipatia umaarufu mitandaoni. Bahati amesema tukio hilo limemshangaza kwa kuwa halikuwa sehemu ya mipango yake ya kujipatia kiki. Amefafanua kwamba mwanamke huyo amekuwa akimtafuta kwa zaidi ya miaka mitano, na hata aliwahi kuwasiliana na ndugu yake mkubwa bila mafanikio. Msanii huyo, ameeleza kuwa alimwona mwanamke huyo kwa mara ya kwanza kupitia video iliyosambaa mtandaoni, akisema kuwa ingawa baadhi ya mashabiki mitandaoni wanachukulia sakata hilo kama mzaha, kwake binafsi ni jambo lenye uzito. Hata hivyo amesisitiza kuwa hajawahi kupanga au kutumia hali hiyo kama njia ya kujipatia umaarufu, bali analichukulia kama tukio la maisha ambalo limemgusa kwa undani ikizingatiwa kuwa mama yake mzazi alifarikia miaka nyingi iliyopita.

Read More
 Bahati Aachwa na Maswali Mengi Baada ya Mwanamke Kujitokeza Akidai Kumzaa

Bahati Aachwa na Maswali Mengi Baada ya Mwanamke Kujitokeza Akidai Kumzaa

Staa wa muziki nchini Kenya, Bahati, amejikuta katika hali ya huzuni na mshtuko mkubwa baada ya mwanamke mmoja kujitokeza mtandaoni akidai kuwa ndiye mama yake halisi, licha ya mama mzazi wa Bahati kufariki miaka mingi iliyopita wakati akiwa bado mtoto mdogo. Katika video aliyochapisha mitandaoni, Bahati ameeleza kuwa kifo cha mama yake alikishuhudia akiwa na umri wa takriban miaka saba, na hata kuhudhuria mazishi yake. Amesema kuwa maisha yake yote amekuwa na kumbukumbu hiyo wazi, jambo linalomfanya kushindwa kuelewa madai ya mwanamke huyo. Bahati ameonesha kuchanganyikiwa na kutokuwa na uhakika kuhusu hatua anazopaswa kuchukua. Ameeleza kuwa hana mawasiliano na mwanamke huyo, na hata hajui pa kuanzia ili kuthibitisha madai hayo. Amehoji pia kama inawezekana kufanyika uthibitisho wa DNA baada ya kifo cha mama yake na kusisitiza kuwa kama kweli mama yake angekuwa hai, hilo lingekuwa jambo la furaha isiyo na kifani maishani mwake. Msanii huyo, ambaye mara nyingi huonekana mchangamfu na mwenye utani, amesema kuwa suala hilo limemgusa kwa kina na kumwacha katika hali ya huzuni na maswali mengi bila majibu.

Read More
 Mwanamke Ajitokeza Akidai Ni Mama Halisi wa Msanii Bahati 

Mwanamke Ajitokeza Akidai Ni Mama Halisi wa Msanii Bahati 

Mwanamke mmoja ameibuka akidai kuwa ndiye mama mzazi wa staa wa muziki nchini Kenya, Bahati. Mwanamke huyo anasema kuwa hajawahi kufariki, kinyume na imani iliyokuwa imeenea kwa miaka mingi, na kwamba mazingira ya umaskini aliyokumbana nayo zamani ndiyo yaliyosababisha kumpoteza mtoto wake. Anasema kuwa wakati huo alikabiliwa na changamoto ambazo zilimfanya ashindwe kumlea Bahati, na hivyo kumpoteza katika hali ambayo hakuwa na uwezo wa kuizuia. Sasa, anajitokeza hadharani akitaka kurudisha mahusiano ya kifamilia, na kuomba msamaha kwa yale anayoyaita maamuzi magumu ya maisha. Mwanamke huyo pia ameonyesha utayari wa kufanyiwa uchunguzi wa DNA ili kubaini kwa uhakika kama kweli yeye na Bahati wana uhusiano wa damu. Hatua yake imeibua mijadala mikali mtandaoni, baadhi ya watu wakitaka uchunguzi ufanyike ili kumaliza utata, huku wengine wakionesha mashaka kuhusu muda na mazingira ya kujitokeza kwake. Hadi sasa, Bahati mwenyewe bado hajatoa kauli yoyote kuhusu suala hilo. Mashabiki na wadau wa burudani wanangoja kwa makini kuona iwapo kutakuwa na majibu au hatua zitakazochukuliwa ili kupata ukweli wa tukio hili ambalo limevutia hisia za wengi.

Read More
 Bahati Ajigamba Kuwa Msanii Pekee Kenya Mwenye Nyimbo Tatu Zinazotrend YouTube

Bahati Ajigamba Kuwa Msanii Pekee Kenya Mwenye Nyimbo Tatu Zinazotrend YouTube

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo, Bahati, ameibuka tena mtandaoni akijigamba kuwa ndiye msanii pekee nchini Kenya mwenye nyimbo tatu zinazotamba kwenye orodha ya video kumi bora zaidi kwenye mtandao wa YouTube. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Bahati ameeleza kuwa anajivunia mafanikio hayo makubwa katika muziki wake, akisema ni heshima kubwa kwake kuona nyimbo tatu zake zikiwa zinatrend kwa wakati mmoja. Kauli yake imekuja muda mfupi baada ya nyimbo zake “First Love,” “Umenipendelea,” na “Bye Bye Baba” kuingia katika chati za ngoma zinazovuma nchini Kenya kwenye mtandao wa YouTube. Bahati ameendelea kuonyesha kuwa bado ana ushawishi mkubwa katika muziki wa kizazi kipya, huku mashabiki wake wakimpongeza kwa juhudi na uthabiti anaouonyesha licha ya changamoto na mijadala inayomzunguka mara kwa mara.

Read More
 Bahati Azima Tetesi za Baby Mama wake Kuvishwa Pete ya Uchumba

Bahati Azima Tetesi za Baby Mama wake Kuvishwa Pete ya Uchumba

Msanii wa muziki asiyeishiwa na matukio kila kuchao, Bahati, amezima tetesi zilizosambaa mtandaoni kuhusu baby mama wake, Yvette Obura, kuvishwa pete ya uchumba kupitia wimbo wake mpya uitwo First Love. Katika video ya wimbo huo, Yvette Obura na mwanaume anayedaiwa kuwa mchumba wake wameonekana kama video queen na video king, wakicheza nafasi za wapenzi wawili waliokuwa katika mahusiano ya kimapenzi yenye hisia kali. Hatua hiyo imewachanganya mashabiki wengi mtandaoni waliodhani kuwa Yvette amepata mchumba mpya, huku wengine wakihusisha tukio hilo na mbinu ya kuvutia hisia za mashabiki na kuongeza hamasa ya kutazamwa kwa video ya wimbo mpya wa Bahati, First Love. Kwa sasa, video ya wimbo huo imezidi kupata umaarufu mkubwa mtandaoni hasa Youtube ambapo ina zaidi ya watazamaji laki tatu ndani ya siku moja.Wachambuzi wa masuala ya burudani wamemsifu Bahati kwa ubunifu wa kipekee katika kutumia stori ya maisha halisi kuchochea mjadala wa muziki wake.

Read More
 Bahati Asema Hana Wivu Baada ya Baby Mama Wake Kuvishwa Pete

Bahati Asema Hana Wivu Baada ya Baby Mama Wake Kuvishwa Pete

Msanii wa muziki nchini Kenya Bahati ameamua kumpongeza mama mtoto wake, Yvette Obura, kwa uchumba wake mpya baada ya kupewa shinikizo na mashabiki wake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bahati ametoa ujumbe wa kumpongeza Yvette baada ya video kusambaa mtandaoni ikimuonyesha akivishwa pete ya uchumba na mwanaume mrefu, mwenye ngozi ya kahawia na sura ya kuvutia. Bahati amesema amekuwa akitagwa sana kwenye video hiyo na mashabiki zake, akionyesha kuridhishwa na uamuzi wa Yvette kumpata mwanaume wa ndoto zake. Ameongeza kuwa hana kinyongo na akamkaribisha mchumba huyo wa baby mama wake kwa chakula cha pamoja ili wajuane vyema. Ujumbe wake uliwavutia mashabiki wengi waliomsifu kwa ukomavu wa kiakili na ucheshi wake, huku wengine wakimpongeza kwa kudumisha urafiki mzuri na mama mtoto wake licha ya tofauti zao za zamani.

Read More
 Bahati Alalamikia Chuki na Wivu Kutoka kwa Wasanii wa Nyimbo za Injili

Bahati Alalamikia Chuki na Wivu Kutoka kwa Wasanii wa Nyimbo za Injili

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Bahati, ameshindwa kuvumilia ukosoaji anaoupata mtandaoni baada ya kuonekana akilia hadharani akielezea machungu anayopitia kutokana na chuki na wivu kutoka kwa baadhi ya wasanii wenzake, hasa wale wa muziki wa Injili. Kupitia video aliyoshiriki kwenye mitandao ya kijamii, Bahati ameonekana mwenye majonzi akisema kwamba kama Mungu angekuwa binadamu, huenda maisha yake yasingekuwa salama kutokana na chuki na husuda za watu. Ameeleza kuwa mara nyingi amekuwa akihukumiwa kwa maamuzi yake ya kisanii na maisha yake binafsi, huku wengi wakisahau kwamba yeye ni binadamu wa kawaida anayekosea kama wengine. Bahati ambaye amepata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki, ameongeza kuwa kila anapojaribu kuinuka, baadhi ya watu wamekuwa wakitamani ashindwe, jambo ambalo limekuwa likimuumiza zaidi akiona baadhi ya wasanii wa Injili wakiendelea kumuombea mabaya badala ya kumtakia heri. Hata hivyo ameahidi kuachia wimbo wake mpya wa kumshukuru Mungu kwa mafanikio aliyoyapata, akisema ni ushuhuda wa jinsi Mungu amemuinua licha ya changamoto na maneno ya watu. Bahati ameeleza kuwa hajawahi kujiona mkamilifu, lakini anaamini baraka zake zinatoka kwa Mungu. Amesema watu wengi hawajui machozi na maumivu aliyopitia ili kufika alipo sasa, na ndiyo sababu ameamua kutumia muziki wake mpya kama sala ya shukrani. Kauli ya Bahati inakuja muda mfupi baada ya kuomba mashabiki zake msamaha kutokana na miendo yake inayokwenda kinyume na maadili ya jamii kwa kujihusisha na maudhui yanayohamasisha ngono.

Read More
 Bahati Aomba Msamaha Hadharani Baada ya Ukosoaji Mkubwa wa Mashabiki

Bahati Aomba Msamaha Hadharani Baada ya Ukosoaji Mkubwa wa Mashabiki

Msanii wa muziki mwenye utata kutoka Kenya, Bahati, amelazimika kuomba msamaha hadharani kufuatia wimbi la ukosoaji alilopokea kutokana na maudhui yake mapya tangu arejee kwenye muziki. Kupitia video aliyoipakia kwenye mitandao ya kijamii, Bahati ameeleza kuwa amepokea simu na jumbe nyingi kutoka kwa marafiki wa karibu, mashabiki, wachungaji, na hata watu wasiowajua, wakionesha kutoridhishwa na mwelekeo wa kazi zake za hivi karibuni. Amesema hakutaka kujibu kwa hasira au hisia kwa kuwa anawaheshimu wote, na badala yake aliamua kuzungumza nao moja kwa moja kutoka moyoni. Bahati amesema kuwa anatambua amewaudhi baadhi ya watu kutokana na mienendo na maudhui ya muziki wake wa sasa, hasa baada ya kurejea na wimbo wake mpya Set It. Ameeleza kuwa lengo lake halikuwa kuwakera, bali kuonyesha ubunifu wake kama msanii anayekua na kubadilika. Msanii huyo ameongeza kuwa anatambua umuhimu wa mashabiki wake, familia, na washirika wake wa karibu, akiwashukuru kwa kumuunga mkono kwa kipindi cha miaka 10 kwenye muziki. Kwa mujibu wake, mafanikio yake yamechangiwa zaidi na upendo na uvumilivu wa mashabiki wake kuliko uwezo binafsi wa uimbaji. Bahati pia ametumia nafasi hiyo kuomba radhi kwa wote aliowakera, akisema yeye ni binadamu anayejifunza kila siku. Amesisitiza kuwa anakubali kurekebishwa lakini pia anahitaji maombi na msaada wa wale wanaomuamini. Aidha, ameahidi kutorudia makosa ya kutayarisha maudhui yanayokwenda kinyume na maadili ya jamii, akisema anajitathmini upya ili kuhakikisha kazi zake za baadaye zinabeba ujumbe chanya na wenye manufaa kwa mashabiki wake. Kauli yake inakuja mara baada ya kuachia wimbo wenye utata uitwao Set It, ambao umeonekana kuhamasisha ngono na kuibua mjadala mkali mitandaoni. Mbali na hilo, Bahati pia alichapisha misururu ya video zinazomuonyesha akiwa amevalia chupi na nyingine akinywa mvinyo alioshea miguu ya mkewe, Diana Marua, jambo lililowakera mashabiki wengi waliomkosoa kwa kupoteza maadili aliyojulikana nayo awali.

Read More
 Bahati Asema Mashabiki Wanatamani Maisha Yake na Diana Marua

Bahati Asema Mashabiki Wanatamani Maisha Yake na Diana Marua

Mwanamuziki mwenye utata nchini Kenya, Bahati, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kudai kuwa mashabiki wake wanatamani maisha anayoyaishi na mke wake, Diana Marua. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bahati amepakia video akiwa na mkewe Diana wakifurahia mvinyo (wine) huku wakipigana mabusu hadharani licha ya maneno ya watu. Katika video hiyo mpya, Bahati amesema kuwa alikuwa anasoma maoni ya mashabiki kuhusu ukosoaji wa video yake ya awali, akisisitiza kuwa wengi wanatamani maisha yao ya kifahari na kimahaba. Kauli yake imejiri saa chache baada ya mwanamuziki huyo kukosolewa vikali mitandaoni kwa kuchapisha video nyingine akiwa amevaa chupi, hatua iliyozua mjadala mkubwa kuhusu mienendo yake ya kisanii na maisha binafsi.

Read More
 Bahati Aadhimisha Miaka 9 ya Ndoa, Aahidi Zawadi Tisa kwa Mkewe

Bahati Aadhimisha Miaka 9 ya Ndoa, Aahidi Zawadi Tisa kwa Mkewe

Msanii wa muziki nchini Kenya, Bahati, anaadhimisha miaka 9 ya ndoa yake na mkewe Diana Marua, akifichua kuwa anapanga kutoa zawadi tisa kuashiria kila mwaka wa mapenzi yao. Kupitia mitandao ya kijamii, Bahati ameeleza furaha yake kwa kufikisha miaka tisa katika ndoa, akisema kuwa safari yao imekuwa ya baraka na mafanikio. Msanii huyo, ameomba mashabiki wake kupendekeza aina ya zawadi anayopaswa kumpa mke wake mwaka huu, akisisitiza kuwa zawadi zote tisa tayari ameziandaa kwa ajili ya mke wake huyo. Bahati amekuwa na utamaduni wa kutoa zawadi kila mwaka kulingana na muda wao wa kudumu kwenye ndoa, jambo ambalo limekuwa likiwavutia mashabiki wake wengi mtandaoni.

Read More
 Bahati Ajitangaza Msanii Namba Moja Afrika Mashariki

Bahati Ajitangaza Msanii Namba Moja Afrika Mashariki

Staa wa muziki kutoka Kenya, Bahati, amejitangaza kuwa msanii namba moja nchini humo na Afrika Mashariki kwa ujumla baada ya wimbo wake wa kuomboleza kifo cha Raila Odinga kushika nafasi ya kwanza kwenye YouTube Trending Tab. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bahati amesema kuwa nyimbo zake mbili kushika nafasi ya kwanza na ya pili kwa wakati mmoja ni uthibitisho kuwa muziki wake unapendwa na Wakenya. Msanii huyo amewataka wasanii wenzake wa Kenya kuchangamkia nafasi zilizobaki kwenye orodha ya nyimbo zinazotrend Youtube, ambazo kwa sasa nyingi zinashikiliwa na wasanii kutoka Tanzania. Hata hivyo Bahati amesisitiza kuwa ataendelea kujiweka kileleni kwenye tasnia ya muziki nchini Kenya, akiwatahadharisha wasanii wenzake waliopanga kuachia nyimbo wiki ijayo kuahirisha mipango yao kwa kuwa naye pia anatarajia kuachia wimbo mwingine mpya ambao ni moto wa kuotea mbali Wimbo wake “Bye Bye Baba”, ambao unamuenzi hayati Raila Odinga, umevutia zaidi ya milioni moja ya watazamaji ndani ya siku moja tangu uachiwe rasmi. Wakati huo huo, wimbo wake mwingine wenye utata “Seti” umevuka views milioni mbili ndani ya wiki mbili kwenye mtandao wa Youtube

Read More
 Bahati Atangaza Kuachia Wimbo wa Kuomboleza Raila Odinga

Bahati Atangaza Kuachia Wimbo wa Kuomboleza Raila Odinga

Mwanamuziki kutoka Kenya, Bahati, ametangaza kuwa ataachia wimbo maalum wa kuomboleza kifo cha kiongozi wa ODM, Raila Odinga, mchana wa leo. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Bahati amesema kuwa wimbo huo ni njia yake ya kumuenzi kiongozi huyo ambaye, kwa mujibu wake, amekuwa nguzo muhimu katika siasa za Kenya na amegusa maisha ya wengi. Amesema kifo cha Raila kimeacha pengo kubwa ambalo halitasahaulika. Bahati anajiunga na wasanii wengine waliotoa nyimbo za kuomboleza, akiwemo Akothee, Prince Indah, na Embarambamba, ambao kwa nyimbo zao wameonyesha upendo na heshima zao kwa marehemu kiongozi huyo. Ikumbukwe kwamba mwaka wa 2022, wakati wa uchaguzi mkuu, Bahati alikuwa karibu sana na Raila Odinga baada ya kutangaza kugombea ubunge wa Mathare kupitia mrengo wa Azimio la Umoja One Kenya. Uhusiano wao wa kisiasa na wa kibinadamu ulionekana wazi kupitia matukio waliyoshiriki pamoja.

Read More