Familia ya Betty Bayo Yaomba Uchunguzi Maalum Kuhusu Kifo Chake cha Ghafla

Familia ya Betty Bayo Yaomba Uchunguzi Maalum Kuhusu Kifo Chake cha Ghafla

Familia ya mwimbaji wa injili marehemu Betty Bayo imewasilisha ombi rasmi kwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) ikiitaka ianzishe uchunguzi maalum kuhusu mazingira ya kifo chake cha ghafla. Mama mzazi wa marehemu ndiye aliyeongoza hatua hiyo, akisema familia imeachwa na maswali mengi bila majibu. Kwa mujibu wa familia, Betty hakuwa na historia yoyote ya ugonjwa ulioweza kuhatarisha maisha yake. Wanasema hawakuwahi kuonyeshwa rekodi zozote za kitabibu kueleza kilichomsibu, wala hawakupatiwa ripoti ya uchunguzi wa mwili (postmortem) ili kufahamu sababu kamili ya kifo. Familia pia imeeleza wasiwasi kuhusu mazishi ya haraka ya msanii huyo, wakidai kuwa kasi ya maandalizi na mazishi inaweza kuwa ilificha ukweli muhimu ambao ungeisaidia familia na mamlaka kuelewa kilichotokea. Wakizungumza baada ya kuwasilisha ombi lao, familia imetoa wito kwa mamlaka husika, ikiwemo ODPP na vyombo vya usalama, kuharakisha uchunguzi ili ukweli ujulikane na haki kutendeka. Wamesema hatua hiyo si tu kwa ajili ya marehemu, bali pia kwa ajili ya umma ambao unahitaji uwazi, hasa kwa kifo cha ghafla cha mtu maarufu katika tasnia ya muziki wa injili.

Read More
 Betty Bayo Azikwa Nyumbani kwake Kiambu

Betty Bayo Azikwa Nyumbani kwake Kiambu

Mwimbaji nyota wa Injili nchini Kenya, Betty Bayo, amezikwa leo nyumbani kwake, Mugumo Estate katika kaunti ya Kiambu. Maelfu ya waombolezaji, wakiwemo viongozi wa kidini, wasanii wenzake, na mashabiki waaminifu, walijitokeza kwa wingi kushiriki ibada ya mazishi iliyofanyika katika uga wa Ndumberi kutoa heshima zao za mwisho. Waliohudhuria mazishi hayo wakiwemo viongozi wa kisiasa walimtaja marehemu Betty Bayo kama mtu aliyekuwa na mchango mkubwa na chanya kwa taifa kupitia muziki wake. Wasanii wenzake walisema kwamba Bayo alikuwa mfano wa kuigwa na alileta mapinduzi katika sekta ya muziki wa Injili. Betty Bayo atakumbukwa kwa nyimbo zake zilizojenga na kutoa matumaini kwa Wakenya wengi, na kifo chake kimeacha pengo kubwa katika tasnia ya sanaa na injili nchini Kenya. Mwanamuziki huyo alifariki mapema mwezi huu baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa damu aina ya leukemia, ambao alikuwa akipambana nao kwa muda kabla ya kifo chake.

Read More
 Familia Ya Msanii Betty Bayo Yafunguka Kuhusu Chanzo Cha Kifo Chake

Familia Ya Msanii Betty Bayo Yafunguka Kuhusu Chanzo Cha Kifo Chake

Familia ya aliyekuwa mwimbaji wa injili Betty Bayo imevunja ukimya na kufunguka kuhusu chanzo cha kifo chake kilichotikisa mashabiki na wadau wa muziki wa injili nchini Kenya. Kupitia taarifa rasmi kwa vyombo vya habari, familia imethibitisha kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa damu aina ya leukemia, ambao alikuwa akipambana nao kwa muda kabla ya hali yake kuzorota wiki iliyopita. Kwa mujibu wa familia, Betty Bayo alilazwa katika High Dependency Unit (HDU) ya Hospitali ya Kenyatta baada ya kuanza kuugua ghafla, lakini juhudi za madaktari kumwokoa hazikufaulu. Familia imeongeza kuwa marehemu alipigana kwa ujasiri na ugonjwa huo hadi dakika za mwisho, huku wakiomba umma kuheshimu faragha yao wakati huu wa majonzi. Hata hivyo wamesema mipango ya mazishi inaendelea, na mwili wa marehemu umehamishwa kutoka Hospitali ya Kenyatta hadi KU Referral Funeral Home.

Read More
 Msanii wa Injili Betty Bayo Aaga Dunia

Msanii wa Injili Betty Bayo Aaga Dunia

Msanii wa muziki wa injili nchini Kenya, Betty Bayo, ameaga dunia akiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Kenyatta, Nairobi. Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na watu wa karibu naye, Betty Bayo alikuwa akipokea matibabu kwa muda kabla ya hali yake kuzorota na kufariki dunia akiwa hospitalini. Betty Bayo alijulikana kwa sauti yake yenye mvuto na nyimbo zilizogusa maisha ya wengi, nyimbo zake maarufu Maneno na Siyabonga, zilimpatia umaarufu mkubwa katika muziki wa injili nchini Kenya. Mbali na taaluma yake ya muziki, marehemu pia alikuwa mke wa zamani wa mchungaji Victor Kanyari, na wawili hao walikuwa wamejulikana sana kutokana na ndoa yao iliyokuwa ikifuatiliwa kwa karibu na vyombo vya habari. Habari za kifo chake zimetikisa tasnia ya muziki wa injili na kuibua majonzi miongoni mwa mashabiki na viongozi wa dini huku wengi wakituma salamu za rambirambi kwa familia yake.

Read More