Bien wa Sauti Sol amjibu Mchekeshaji Eric Omondi kwa kuwaponda wanamuziki wa Kenya

Bien wa Sauti Sol amjibu Mchekeshaji Eric Omondi kwa kuwaponda wanamuziki wa Kenya

Msanii wa Sauti Sol, Bien amemtolea uvivu mchekeshaji Eric Omondi kwa kukosoa wasanii wa kenya kutokana na kuzembea kuachia nyimbo. Kupitia ukurasa wake wa instagram bien amemtaka Omondi akome kuwashinikiza wasanii wa Kenya waachie muziki mzuri wakati uchekeshaji umemshinda. Mkali huyo wa ngoma ya “Inauma” amemtaka Omondi kuwekeza nguvu zake kwenye suala la kufufua tasnia ya ucheshi ambayo kwa mujibu wake imepoteza mwelekeo. Hata hivyo mashabiki wameonekana kumuunga mkono Bien huku wengine wakimtaka msanii huyo akubali ukweli muziki wa kenya umeshuka kwa kuwa wasanii hawatoi nyimbo nzuri ikilinganishwa na wasanii wa mataifa mengi. Kauli ya Bien imekuja mara baada ya Eric Omondi kushangazwa na hatua ya wasanii wa Kenya kushindwa kuingiza nyimbo nyingi kwenye chati ya muziki ya Apple Music ambayo imetawaliwa na wasanii wa Nigeria.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AWATAKA WASANII WA KENYA KUIMBA NYIMBO ZA KIINGEREZA

BIEN WA SAUTI SOL AWATAKA WASANII WA KENYA KUIMBA NYIMBO ZA KIINGEREZA

Mwanamuziki wa Sauti Sol, Bien ametoa changamoto kwa wasanii nchini kuanza kutumia lugha ya kiingereza kwenye nyimbo zao ili muziki wa Kenya uweze kufika mbali zaidi. Bien amesema licha ya wasanii wa Kenya kutoa muziki mzuri wengi wao wamekuwa wakitumia lugha ya Sheng kwenye nyimbo zao jambo analosema limewafanya wasanii kushindwa kutanua wigo wa muziki wao kimataifa. Katika hatua nyingine Bien amekiri kuwa hakuwa anajitambua kimuziki kabla ya wasanii wa kundi la Sauti Sol kuanza kufanya kazi zao kama wanamuziki wa kujitegemea. Hitmaker wa “Inauma” amesema amejifunza mambo mengi kama msanii huru ikiwemo kutayarisha na kuandilka nyimbo zake mwenyewe.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AFUNGUKA KUHUSU UCHAGUZI MKUU NCHINI KENYA

BIEN WA SAUTI SOL AFUNGUKA KUHUSU UCHAGUZI MKUU NCHINI KENYA

Mwana kikundi wa Sauti Sol, Bien amefunguka namna uchaguzi nchini Kenya ulivyoendeshwa. Katika mahojiano na Mungai Eve, Bien amesema mchakato mzima wa uchaguzi mkuu nchini ulikuwa wa haki na huru ambapo amewapongeza wakenya kwa kudumisha Amani kabla na hata baada ya uchaguzi. Hitmaker huyo “Inauma” amewataka wakenya kurejea kazini baada ya Rais mteule William Ruto kutangazwa na Tume huru ya uchaguzi IEBC hata kama kuna wale ambao hawakuridhishwa na matokeoa ya urais. Bien ametoa wito kwa serikali mpya itakayoingia mamlakani kuboresha sanaa nchini Kenya ili vijana waweze kupata ajira. Kuhusu mgogoro wao na muungano wa kisiasa wa Azimio la Umoja kutumia wimbo wao wa “Extravangaza bila ridhaa ya Sauti Sol, Bien amesema mawakili wao wanashughulikia suala hilo kuhakikisha wanapata haki.

Read More
 BIEN AFUNGUKA KUHUSU SAUTI SOL KUTOTUMBUIZA KWENYE MAJUKWAA YA KISIASA.

BIEN AFUNGUKA KUHUSU SAUTI SOL KUTOTUMBUIZA KWENYE MAJUKWAA YA KISIASA.

Mwanakikundi wa Sauti Sol Bien amefunguka mara baada ya Diamond Platnumz kupewa nafasi ya kutumbuiza kwenye mkutano wa kisiasa wa mrengo wa Azimio la Umoja juzi kati. Kulingana na Hitmaker huyo “Inauma”,  sio wasanii wote wana haja ya kutumbuiza kwenye majukwaa ya kisiasa. “We don’t want to be in political forums” Amesema Bien. Bien ametoa kauli hiyo kufuatia hatua ya mchekeshaji Eric Omondi kuwatolea uvivu wasanii wa Kenya kwa kutotumbuiza kwenye hafla ya kisiasa ya Azimio la Umoja huko Kasarani.

Read More
 BIEN: SILALI CHUMBA KIMOJA NA MKE WANGU

BIEN: SILALI CHUMBA KIMOJA NA MKE WANGU

Msanii wa kundi la Sauti Sol Bien kwa mara nyingine tena ameibuka na kauli yenye utata kuhusu maisha yake na mkewe Mtangazaji Chikki. Akipiga stori na Mambo Mseto ya Radio Citizen Bien amesema licha ya mkewe kuwa Meneja wake, wanaposafiri kwa ajili ya show kila mmoja hulala chumba chake. “Katika ndoa yetu kuna mipaka pia, kwa mfano kama nimeitwa mahali niko na shoo, nakaa kwa chumba cha hoteli mimi peke yangu. Huwa sitaki hata muziki hapo ndani. Nataka tu kukaa peke yangu nijisikilize na kujitathmini kuhusu jinsi nitakavyoifanya hiyo shoo” alisema. “Kwa hiyo kama unaniita kama ajenti ama promota, huwezi nitengea chumba kimoja mimi na mke wangu, sitaki kulala na yeye kitanda kimoja hiyo siku, nataka kuenda kujisikilizia,” alisema Bien. Hittmaker huyo wa ngoma ya “Inauma” amefafanua kwamba wakienda kwa shoo na mke wake mambo ya uchumba yanabaki nyumbani na kule wanaenda kama msanii na Meneja wake na kwa hiyo kuna umuhimu wa kila mmoja kutengewa chumba chake binafsi mbali na mwingine.

Read More
 BIEN AWAPA SOMO VIJANA WALIO CHINI YA UMRI WA MIAKA 30

BIEN AWAPA SOMO VIJANA WALIO CHINI YA UMRI WA MIAKA 30

Mwimbaji mkuu wa Kundi la Sauti Sol nchini Kenya Bien amesema hashauri watu waliopo katika umri wa miaka ya ishirini kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwani ni kupotezeana muda. Bien amesema watu walio katika umri huo wanapaswa kujijali wenyewe na kusafiri kwa kuwa mtu aliyeko katika umri huo bado anajitafuta ajue kitu gani hasa anakihitaji. “Siwezi kumpa ushauri mtu mwenye umri wa miaka ishirini awe kwenye mahusiano, ni kupoteza muda, angalau fanya kazi, usafiri pia uwe na watu wengine huku na huko.” alisema Bien. Aidha aliongeza kwamba mtu akiwa katika umri huo hajitambui na mtu aliye naye pia hajitambui “Unadhani unafanya nini? Mnajaribu kusuluhisha mambo pamoja lakini mwisho wa siku yaani nadhani ni bora kuwa peke yako ikiwa uko katika miaka ya 20” alimaliza Mwanamuziki huyo.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AFUNGUKA KUHUSU KUPANGA UZAZI

BIEN WA SAUTI SOL AFUNGUKA KUHUSU KUPANGA UZAZI

Msanii kutoka kundi la Sauti Sol Bein Aim Baraza amesema kuwa yupo tayari kukata mshipa wa uzazi maarufu vascectomy punde atakapo pata watoto na mke wake Chiki Kuruka. Akizungumza kwenye kipindi cha Baldmen Session kwenye mtandao wa youtube Bein amesema kuwa kupanga uzazi barani Afrika ni swala ambalo limewachiwa wanawake. Bien amesema kuwa hawezi kumwachia mke wake mzigo huo pekee licha ya kuwa wanaume wengi wanaogopa kufanyiwa vasectomy. “Wanaume wengi hawako tayari kufanyiwa vasektomi lakini mimi niko tayari kuangalia vasektomi, nimechoka kuweka mzigo huu kwa vifaranga wetu, kwanza najua dawa mbalimbali za uzazi wa mpango zina madhara tofauti. “Amesema Bien kwenye kipindi anachoandaa. Lakini pia amefunguka kuwa mashabiki wamekuwa wakimshinikiza kupata mtoto na mke wake Chiki Kuruka licha ya kuwa kwenye ndoa kwa miezi 18 pekee. “Hata mimi Wakenya wameniangalia weird, I’ve stayed karibu for 18 months na sijafanya kitu lakini kila kitu na time yake,” alisema. “Sijawahi kuwa na hamu ya kuzaliana! Kwa hiyo haijawahi kunisumbua sana.” amesema

Read More
 BIEN ATOA YA MOYONI KUHUSU ERIC OMONDI KULETA MAGEUZI KWENYE MUZIKI KENYA

BIEN ATOA YA MOYONI KUHUSU ERIC OMONDI KULETA MAGEUZI KWENYE MUZIKI KENYA

Msanii wa Sauti Sol, Bien amedai kwamba anaunga mkono harakati za  mchekeshaji Eric Omondi kuleta mabadiliko kwenye tasnia ya muziki nchini. Katika mahojiano na Plug tv, Bien amesema kitu ambacho kinamfanya wakati mwingine kutofautiana kimawazo na Eric Omondi ni kutokana na mchekeshaji huyo kuingiza kiki nyingi kwenye masuala muhimu. Bien amesema licha ya kwamba wamekuwa wakitupia maneno makali mtandaoni na Eric Omondi, anaheshimu kila ambacho mchekeshaji huyo anakifanya kwa kuwa anajituma sana kwenye shughuli zinazomuingizia kipato. Katika hatua nyingine Bien amewataka wakenya waache kasumba ya kuwashambulia watengeneza maudhui na badala yake wawe mstari wa mbele kuunga mkono shughuli zao kwani kuwakosa kila mara ni ulimbukeni wa hali ya juu.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AZIDI KUMSHAMBULIA EZEKIEL MUTUA

BIEN WA SAUTI SOL AZIDI KUMSHAMBULIA EZEKIEL MUTUA

Msanii wa Sauti Sol bien amemtolea uvivu Mwenyekiti wa Chama cha Hakimiliki na Muziki nchini Ezekiel Mutua baada ya kudai kuwa alipewa mamlaka ya kutoa kibali kwa nyimbo zao kutumika kwenye shughuli za kibiashara. Katika mahojiano na Eve Mungai, Bien amesema ameshangazwa na hatua ya Mutua kutoa ruhusa ya wimbo wa “Extrangaza” kutumika kwenye shughuli za muungano wa Azimio la Umoja bila idhini yao ikizingatiwa kuwa walitumia kiasi cha shillingi millioni 2 za Kenya kutayarisha video ya wimbo huo. Aidha ameenda mbali zaidi na kusema kuwa Ezekiel Mutua hajui majukumu yake kwani alipewa wadhfa huo kuangazia maslahi ya wanasiasa. Hata hivyo amedokeza kuwa wanaendelea na mazungumzo na uongozi wa azimio la umoja kupata suluhu ya mgogoro uliobuka kati yao huku akitoa wito kwa mashabiki waendelea kusikiliza na kucheza nyimbo zao kwenye maeneo ya umma.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AKANUSHA KUWA KWENYE UGOMVI NA MUUNGANO WA KISIASA WA AZIMIO LA UMOJA

BIEN WA SAUTI SOL AKANUSHA KUWA KWENYE UGOMVI NA MUUNGANO WA KISIASA WA AZIMIO LA UMOJA

Msanii wa Sauti Sol, Bien amefunguka na kudai kuwa hana ugomvi wowote na muungano wa kisiasa wa Azimio la Umoja kama namna baadhi ya watu wanavyochukulia mtandaoni. Katika mahojiano na kituo kimoja cha redio nchini Bien amesema kile ambacho anakishinikiza kama kundi la Sauti Sol  malipo yao wimbo wa Extravangaza ambao ulitumiwa na muungano huo kwenye shughuli zao kisiasa bila ridhaa yao. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Mbwe Mbwe” amesema mawakili wapo kwenye mazungumzo na Uongozi wa Azimio la Umoja kutatua utata unaozingira wimbo wao  wa extra vangaza huku akidokeza kwamba huenda wakalipa shillingi billioni moja za kenya kwa kuharibiwa brand yao ya muziki. Kauli ya Bien imekuja mara baada ya Ezekiel Mutua kuitaka bendi ya Sauti Sol kuacha kushiriki vita vya mtandaoni na muungano wa Azimio la Umoja na badala yake watumie njia ya mazungumzo kutatua tofauti zao kudai haki yao kwani jambo hilo huenda likaathiri muziki wao. Utakumbuka baada ya Sauti Sol kutishia kuufungulia muungano wa Azimio la Umoja kesi kwa kuitumia wimbo wa Extravaganza kwenye kampeini zao bila ridhaa yao, walipoteza takriban subscribers 2,000 kwenye mtandao wa Youtube na kuifanya channel yao kushuka kutoka subscribers elfu 905 hadi 904.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AUCHANA MUUNGANO WA KISIASA NCHINI KENYA AZIMIO LA UMOJA

BIEN WA SAUTI SOL AUCHANA MUUNGANO WA KISIASA NCHINI KENYA AZIMIO LA UMOJA

Mwanakikundi wa Sauti Sol, Bien ameamua kurusha jiwe gizani kwenda kwa uongozi wa Azimio la Umoja unaongozwa na Raila Odinga baada ya bendi hiyo kupoteza jumla ya subscribers 2.000 kwenye mtandao wa youtube ndani ya kipindi cha masaa 48. Kupitia Mtandao wa Instagram Bien, ameandika ujumbe wa kimafumbo ambao umetafsiriwa na wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii kuwa bendi hiyo inaegemea upande wa mrengo wa Kenya Kwanza unaongozwa na Naibu wa Rais Dakta William Ruto wakati huu taifa inajiandaa kwa uchaguzi mkuu wa Agosti 9. “Time will reveal. Wale wanashuka washuke saa hii. Stage yao imefika.” Ameandika Instagram. Chapisho hilo kutoka kwa Bien imeibua hisia mbali mbali miongoni mwa wakenya kwenye mitandao ya kijamii, ambapo wengi wamewataka wasaani hao bendi hiyo kujitenga na masuala ya siasa na badala yake wawekeze nguvu zao kwenye suala la kutoa muziki mzuri. Channel ya Youtube ya Sauti Sol ambayo ilikuwa na subscribers elfu 903 kwa sasa ina jumla ya subscribers elfu 903. Jumatatu wiki hii bendi ya Sauti Sol ilitishia kuushtaki Muungano wa Azimio la Umoja kwa kutumia wimbo wao “Extravaganza” bila ridhaa yao kwenye kampeni zao ambapo siku hiyo walikuwa wakimtambulisha Mgombea mwenza wa Raila Odinga, Bi. Martha Karua. Utakumbuka mwaka wa 2021 Sauti Sol walikuwa baadhi ya wasanii Kenya waliojitokeza hadharani na kupinga mchakato wa kuifanyia katiba marekebisho kupitia Mpango wa Maridhiano BBI ambao ulikuwa unaongozwa na kinara wa ODM Raila Odinga.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AKIRI KUWAHI KUTAKA KUIVUNJA NDOA YAKE NA MKEWE CHIKI KISA MSONGO WA MAWAZO

BIEN WA SAUTI SOL AKIRI KUWAHI KUTAKA KUIVUNJA NDOA YAKE NA MKEWE CHIKI KISA MSONGO WA MAWAZO

Mwanakikundi wa bendi ya Sauti Sol, Bien Barasa ameendelea kutoa ushuhuda wa ndani kuhusu maisha yake, amefunguka kwamba aliwahi kutaka kuivunja ndoa yake. Kwenye podcast ya Bald Box msanii huyo amesema kwamba mwaka wake wa kwanza kwenye ndoa nusra ampe talaka mke wake Chiki kuruka baada ya kupitia wakati mgumu kipindi cha korona. Hitmaker huyo wa ngoma ya “MbweMbwe” amesema alipatwa na msongo wa mawazo kipindi cha korona baada ya shughuli za kimuziki za bendi ya Sauti Sol kusambaratika lakini alikuja akapata afueni alipopata ushauri nasaha kutoka kwa mwanasaikolojia. Utakumbuka Bien Aime Barasa na mkewe Chiki Kuruka ambaye ni dancer, mwalimu wa mazoezi ya mwili na mtangazaji wa redio walifunga ndoa miaka miwili iliyopita.

Read More